Stress za hitaji la ndoa sio kwa wanawake tu bali hata kwetu sisi wanaume

BOMBAY

JF-Expert Member
Apr 16, 2014
4,682
3,392
Habari wana JF,

Natumai mko poa, na mishemishe za kulikimbiza tonge la kila siku zinaendelea vizuri.

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza,

Nikiwa ninamaanisha kuwa suala la kuchelewa kuolewa si la wanawake tu bali hata kwa wanaume tunaojitambua pia tunalo janga la kuchelewa kuoa, suala ambalo wengi wetu tunapofikia umri flani huwa linatuumiza vichwa kila kukicha.

Kumekuwa na mijadala mingi humu ihusuyo kuchelewa kufunga ndoa ambayo kwa namna moja au nyingine ni wanawake pekee ndio wamekuwa wakihusishwa na kadhia hii hatimae wanaonekana kuwa na stress za hitaji la ndoa bila mafanikio.

Binafsi napingana na dhana hii kwa kusema kuwa suala hili la stress za ndoa si kwa KE pekee bali hata kwa ME licha ya kutofautiana kwa namna moja au nyingine kati yetu.

Sitaki kuamini kuwa kama kuna asiependa kuitwa "Mume wangu"katika uhalisia wenyewe na yule ampendae kwa dhati wakiwa ndani ya ndoa.

Nina mifano mingi ya wanaume wengi nami nikiwemo ambao wameshachoshwa na maisha ya ubachelor, yaani ni wahitaji wa kweli wa ndoa lakini mpaka sasa bado hawajafanikiwa kuingia katika taasisi hii nyeti kutokana na sababu mbalimbali ambazo zimekuwa ni kikwazo katika kufanikisha jambo hili.

Sababu kuu ambayo kwakiasi kikubwa nimeisikia ikilalamikiwa sana na vijana wengi wa kiume ni UGUMU WA MAISHA ikifuatiwa na HOFU YA MAUMIVU YA MAPENZI ambavyo chimbuko lake ni USALITI, KERO NA CHANGAMOTO MBALIMBALI zinazojitokeza katika ndoa ambavyo vimekuwa ni gumzo kwa wanandoa kila kukicha.

Ugumu wa maisha ndio sababu kubwa inayochangia vijana wengi kujiweka mbali na suala la ndoa na, wengi tunajifariji tu lakini ukweli utabaki palepale.

Nina rafiki yangu hivi juzi kati amepatwa na kijihoma cha siku nne akiwa kitanda hajiwezi, anasema umuhimu wa kuwa na mke ndo ameuona kwa jinsi alivyokuwa mpweke, nia ya kuoa anayo lakini kipato ndo kinachompa stress.

Bila kuwachosha ningependa kuwasilisha mada hii kwenu wana Bodi ili kama mtakubaliana na mtazamo wangu kwa pa1 tuungane kuipinga dhana hii yakuhusisha wanawake pekee katika suala hili ijapokuwa wao ni wahanga zaidi kuliko sisi.

Naomba kuwasilisha.

AHSANTENI

 
Ni kweli mkuu uoga ni tatizo kubwa miongoni mwetu team bachelor
ikiwa maisha magumu, kamwe hayatakuwa mepesi, ni suala la maamuzi ya kukubalina na maisha ukikomaa kitu kinaeleweka....
 
BOMBAY uko sawa kabisa mkuu suala la kutamani sana kuwa ndani ya ndoa lipo kwa jinsia zote mbili,mimi pia ni shuhuda wa hilo kuna mkaka ni alikuwa haishi kupata stress kufikiria atamuoa nani mpaka mwishowe amempata na ana furaha isiyo na kifani stress zote kwishnei,kwa ufupi hakuna asiyetamani kuitwa mume/mke wangu na kujenga familia yake iliyojaa upendo sema swali huwa ni unaijenga na mtu wa aina ipi?je atachangia furaha ndani yandoa yenu au ni stress tupu??????????
 
Last edited by a moderator:
raha za ndoa kama hizi hapa chini
10686801_324291981084272_2296098317517548943_n.jpg
 
Tuombe dua tukosee mambo mengine lakin si kuoa/kuolewa na pasua kicho ni sheeeedaaaah!
BOMBAY uko sawa kabisa mkuu suala la kutamani sana kuwa ndani ya ndoa lipo kwa jinsia zote mbili,mimi pia ni shuhuda wa hilo kuna mkaka ni alikuwa haishi kupata stress kufikiria atamuoa nani mpaka mwishowe amempata na ana furaha isiyo na kifani stress zote kwishnei,kwa ufupi hakuna asiyetamani kuitwa mume/mke wangu na kujenga familia yake iliyojaa upendo sema swali huwa ni unaijenga na mtu wa aina ipi?je atachangia furaha ndani yandoa yenu au ni stress tupu??????????
 
Last edited by a moderator:
Aisee,yaani ni kweli asilimia 100% japokuwa wanawake wanakuwa na feelings nyingi sana,lakn wanaume ndio wanaoamua ndoa,coz wao ndio wenye nguvu kubwa kwenye jambo hili japokuwa na wanawake pia wana part yao kwenye maamuzi,lkn wanaume wana-play part kubwa zaidi.....
 
Habari wana JF

Natumai mko poa, na mishemishe za kulikimbiza tonge la kila cku
zinaendelea vizuri.

Kama kichwa cha habari kinavyo jieleza, nikiwa ninamaanisha kuwa suala
la kuchelewa kuolewa si la wanawake tu bali hata kwa wanaume
tunaojitambua pia tunalo janga la kuchelewa kuoa,suala ambalo wengi wetu
tunapofikia umri flan huwa linatuumiza vichwa kila kukicha.

Kumekuwa na mijadala mingi humu ihusuyo kuchelewa kufunga ndoa ambayo
kwa namna moja au nyingine ni wanawake pekee ndio wamekuwa wakihusishwa
na kadhia hii hatimae wanaonekana kuwa na stress za hitaji la ndoa bila
mafanikio.

Binafsi napingana na dhana hii kwakusema kuwa suala hili la stress za
ndoa si kwa KE pekee bali hata kwa ME licha ya kutofautiana kwa namna
moja au nyingine kati yetu.

Sitaki kuamini kuwa kama kuna asiependa kuitwa "Mume wangu"katika
uhalisia wenyewe na yule ampendae kwa dhati wakiwa ndani ya ndoa.

Nina mifano mingi ya wanaume wengi nami nikiwemo ambao wamesha choshwa
na maisha ya ubachelor, yaani ni wahitaji wa kweli wa ndoa lakini mpaka
sasa bado hawajafanikiwa kuingia katika taasisi hii nyeti kutokana na
sababu mbalimbali ambazo zimekuwa ni kikwazo katika kufanikisha jambo
hili.

Sababu kuu ambayo kwakiasi kikubwa nimeisikia ikilalamikiwa sana na
vijana wengi wa kiume ni UGUMU WA MAISHA ikifuatiwa na HOFU YA MAUMIVU
YA MAPENZI ambavyo chimbuko lake ni USALITI, KERO NA CHANGAMOTO
MBALIMBALI zinazojitokeza ktk ndoa ambavyo vimekuwa ni gumzo kwa
wanandoa kila kukicha.

Ugumu wa maisha ndio sababu kubwa inayochangia vijana wengi kujiweka
mbali na suala la ndoa na, Wengi tunajifariji tu lakin ukweli utabaki
palepale.

Nina rafiki yangu hivi juzi kati amepatwa na kijihoma cha cku nne akiwa
kitanda hajiwezi,anasema umuhimu wa kuwa na mke ndo ameuona kwa jinsi
alivyokuwa mpweke, nia yakuoa anayo lakini kipato ndo kinachompa stress.

Bila kuwachosha ningependa kuwasilisha mada hii kwenu wana Bodi ili kama
mtakubaliana na mtazamo wangu kwa pa1 tuungane kuipinga dhana hii
yakuhusisha wanawake pekee ktk suala hili ijapokuwa wao ni wahanga zaidi
kuliko sisi.

Naomba kuwasilisha.

AHSANTENI

100% ukweli mtupu baeleze yaan ungekuwa karibu ningekutoa out.dah wametuchosha na kuolewa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom