'Street codes' za kukusaidia uishi vizuri na watu mtaani kwako katika mji wowote Tanzania

Mkuu Vipi kuhusu kwenda kujitambulisha kwa wale wapenda shiriki yaan wabobezi katika kada ya uchawi ,wanga na ulozi waliopo mtaani kwangu maana hayo yote nimekwisha kuyafanya lakini walozi na wachaw Bado wanaendelea kuniletea sintofaham kubwa sana hapa mtaani kwangu kwa mtogole.
 
8. Epuka nyendo zako zote kuwa wazi sana machoni kwa kila mtu. Miche miche zako nyingi zisiwe zinatabirika. Kwa mfano, unapenda nini zaidi, hupendi nini, unatoka saa ngapi, unarudi nyumbani saa ngapi, unafanya kazi gani, una biashara gani, una mipango gani ya kimaisha, una miliki nini nk.
Well said mkuu, uwe undefined!
 
Hiyo namba 6 tunaita Intelligent Service kwajili ya maisha yako binafsi ni muhimu kuwa nayo kwenye mambo mengi hasa wazee wa mishe mishe kibao.
 
Kujenga mazoea na mhuni uko sawa japo utegemee yote ,

Niliibiwa kiti mmoja akasaidia tukakipata bila kuumizana nikasema hapa fresh, mwisho wa siku huyuhuyu akaiba kuku akanaimbia mshkaji wangu nipoze chochote kuku wetu mzee kasema niuze nipate nauli ya kwenda kijijin kusalimia
chupuchupu nile pingu uzuri busara za mwenye kuku zilisaidia
 
Namba moja naitumia sana kitaa kwa vile mimi ni mtu wa salamu na utani wa hapa na pale, ila kuna nyumba jirani na ninapoishi ina watu wa ajabu (mostly wanawake)

Nilianza kuwasalimia kila ninapopita hapo asubuhi ila wakawa wanaitikia kwa taabu sana yaani kinyonge kama hawataki vile... nikaendelea kuwasoma pasipo kujua tatizo ni nini!

Mara ya mwisho nikasalimia (walikuwa wanawake watatu) kibarazani, wote wakakaa kimya kama vile hawajasikia salamu yangu.
Kuanzia siku hiyo nikajiapiza kutowasalimia tena.. yaani mpaka kesho napita kama siwaoni vile.
 
jifunze mchezo wowote au hata kuwa mshabiki. mchezo wa draft ni moja ya njia bora sana ya kuweza kuishi mji wowote. kama huuwezi basi hudhuria vibanda umiza na bishana mpira.
 
Mtoa mada salute kwako!,umeandika vitu muhimu japo kwa wengine vipo baadhi tunapishana navyo,mfano Mimi kukaa vijiweni kumenishinda kabisa sio kama nadharau ila asilimia 90 ya vijiwe huwa wanaongelea nonsense,stori za mademu na nyingine nyingi,ukiwaingizia siasa kidogo wengi wapo empty hawana facts ila ushabiki,ukiwaingizia soka ni hivyohivyo na kelele nyingi,swala la kuzoeana na wahuni nakubali asilimia zote,kusalimia nakubali japo huwa namsoma mtu kama anaitikia kinyonge huwa namind my business.Alafu kingine ukitaka kuzoeana na watu sana watataka wakujue kila kitu, kuanzia kula yako,ratiba zako zipoje,unatoka na mademu gani etc..,kwenye maisha usiruhusu uwe rafiki wa kila mtu hapo haujengi heshima ila unabomoa kuishi na waswahili kazi sana mkuu.
 
Wewe unaniongelea mimi kabisa, yaani sina stori za kukaa maskani hapa mtaani lakini nnaekutana nae namsalimi na nkimkuta njiani nampa lift. Ila tabia ya kukopa hapa mtaani sina maana sioni wa kunikopesha isipokua wao ndo huja kunikupa. Hili kuhusu vijana me nna marafiki wawili tu na namba zao nnazo, mmoja ni muhuni na anaendesha kerry n mwengine sio mlevi lakini anavuta bangi balaa. Hao ndo hunipa stori zote za mtaa kwa hiyo nashkuru naishi kwa amani sana
 
Back
Top Bottom