Antetokounmpo
JF-Expert Member
- Feb 5, 2020
- 1,242
- 1,996
Kwahyo huyo manzi wa karatu, yuko msoma hadi Leo mkuu??Inaendelea
Siku zilivyokua sinasonga nilianza kuzoea mazingira ya Arusha, kama kawaida yangu kupiga misele ndo ilikua jadi yangu nahisi mitaa ya Arusha ambayo cjafika ni michache mpk loliondo nilitimba huko ndani ndani Arashi kote huko nilifika.
Pale nilipokua nimepanga tulikua wapangaji kumi, mmoja tu ndo alikua anaishi na familia yake, tuliyobaki sisi ni ma Bachelor...kuna mpangaj mmoja alikua ni binti wa kinyaturu cku moja alimpokea rafiki ake wakike ni Muiraq ( ndo hao hao wambulu tu )..huyo rafiki ake alikua ni mrembo kweli mweupe alafu mwembamba.
Huyo muiraq nilijikuta tu nimeanza nae mahusiano ( cjui hata yalianzaje hayo mahusiano )....kuna siku alinambia niende nae kwao ( karatu ) akawasalimie ndugu zake alafu turud cku hyo hyo.
Sijui kwanini nilikubali kilahisi vile....kazini niliomba ka likizo ka siku 4 ( kwa mwaka likizo jumla ziko 28 )....basi nilipewa kishingo upande hyo likizo na karani.Jumapili mapema tu tulikua kisongo tukapanda gari ( hice ) mpk karatu...tulipokelewa vizur na mzee wake, Mama yake alikwisha fariki tokw zamani ko alikua anaish na Mzee wake na ndugu zake wengine.
Siku nilikula vizur sana ( kwenye kupika nawa appreciate sana ) tulivyomaliza kula tukapiga story na hyo familia waliniuliza me mwenyej wap nikawaambia natokea Mara Tarime ( nilidanganya wilaya )...jioni ilifika tukashindwa kurud Matevesi gar zilikosa ko ilibid nilale pale ( ukweni ).
Kesho yake mapema tu tuliamua kusepa zetu,.....huyo Manzi niliona amechukua mabegi yake ya nguo me nikajua labda ameamua kuchukua tu kwenda nayo kwa huyo mnyaturu.Sikumuuliza kwanini achukue yale mabeg yake maana niliona hayanihusu.
Ile tumefika pale tunapoishi badala aingize yale mabegi chumba anachokaa.Yeye akayaingiza mageton kwangu....nilimuuliza "kwani loyce hayupo"....alijibu yupo nikamwambia mbn mabeg tena kwangu akasema kwanzia muda ule yeye ni mke wangu maana mpaka kwao nilishaenda na wananijua.
Pozi liliniisha kwa kweli mke tena usawa ule jamani,nilimwambia mbn hakunambia na mbona ni mapema hvyo asee me kuwa mume wake.Alijibu ndo ishakua tena alianza kupiga na usafi kabisa.
Hii ndoa nayo ilkua ni ya kibabe sana nilifikiria huyu mtu nitamtorokaje maana hizo pigo za kuishi na mwanamke nilikua ctaki kabisa...yani cku hyo nililala nae bila kumgusa kabisa.
Kwa vile likizo yangu ilibakisha siku mbili niliamua kwenda kwa wale washkaji zangu walionipokea kuwaambia hilo tukio...Walicheka sana wakanambia kuwa nilifanya makosa makubwa kwenda kwao na huyo manzi walinambia ni kawaida ya wasichana wa kule kujilengesha kwa wanaume ili waolewe hata bila mahari.
Niliamua kuishi nae hivyo hivyo nilikubaliana na hari.Uzur wake alkua hakai home alkua anafanya kazi mgahawa mmoja hivi uko kisongo karibu na sokoni kwa hyo alikua akitoka asubui anarud saa moja usiku.
Ila huyu manzi nilimuona ana msaada sana, me hua ni mvivu kwenye vikaz vya home ko alikua akivifanya yeye.
Nilikua nikipata mchepuko nilikua nampeleka kwa wale jamaa walio nipokea maana funguo za mlango wao nilkua najua wanapozitunzia.
Huyu mke nilikuona naona yupo serious na mimi alikua ana nambia kuwa anataka niombe likizo hata ya wiki mbili ili twende nae musoma akawaone Wazazi wangu.Nilimwambia labda mwezi December ndo nitachukua lkizo ili niende nae musoma.Lakin yeye alikataa akataka nimuongezee nauli alafu ni mdairekti ( direct ) aende mwenyewe.
Mwez September katikati Mama angu alikua anarud kwake yeye mwenyew lakin wagonjwa mmoja alienda dodoma na mwingine alienda Mwanza ( wa kike ndo yupo dodoma )...Mama nilimwambia kuwa nimepata mchumba, kabla hajarud musoma nili mwambie huyo wife aende morombo akawasalimie.
Mama anamkubali sana huyo mwanamke cjui kisa ni mweupe na kipindi cha nyuma ndo nimepewa taarifa za kuja Arusha Mama alinambia kuwa nikiona sana nimeshindwa kujizuia na wanawake nitafute mmoja niweke ndani kama mke.Ko nadhan alifurahi kwa hilo.
Mama aliondoka nae kwenda musoma yupo mpaka leo hii.Kipindi hayupo nilijinafas kuna msajili laini ( sim card's ) wa voda na yeye ni pisi kali ya kimbulu niliitafuna kimasihara tu, ila sio mageton kwangu ni kwa washkaji.
Kiwandani nilifanya kazi kwanzia mwez wa 07 mwez wa 11...
Bado na kama visa viwili au vitatu ni hitimishe Uzi wangu
Nitarejea