Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 45
~BAADA YA WIKI MOJA~
Nilikuwa mzima wa afya na safari ya kurudi kwetu Tanzania ilikuwa imeshafika sikuweza kuwaona wale watu tena pale wodini tayari Gervas wangu alikuwa pembeni yangu mzima tena tukicheka naye na kupiga stori kwenye gari huku tukielekea uwanja wa ndege wa zambia.
Hapakuwa mbali sana kwani ndani ya nusu saa tulikuwa tayari tunaingia ndani ya uwanja wa ndege huku tukielekea kupanda ndege ile ile iliyotuleta.
Furaha kwangu ilikuwa kubwa sana na hata Grvas naye alifurahi sana kwa upendo niliokuwa nimemuonesha wa kujitolea figo yangu ya upande mmoja na kumpatia.
‘’Levina huyu ni nani?’’
Ilikuwa ni sauti ya gervas akitaka kujua ni nani yule Mama tuliyeongozana naye mpaka Zambia.
‘’huyu ni mfanyakazi pale 'airport' dar na ametoa msaada mkubwa mpaka wewe kufika hapa...’’
‘’Ahsante sana Mama. Nakushukuru sana kwa msaada wako ulioutoa...!’’
‘’Hata nawewe nakushukuru mwanangu pole sana na naimani umeshapona kabisa’’
Nilipenda sana ukarimu wa yule Mama na hata tulipofika uwanja wa ndege Gervas alimuomba sana twende naye mpaka nyumbani kwetu.
Tuliingia Dar alfajiri sana kwenye saa kumi na mbili,
Siku hiyo hiyo tulipofika tuliandaa sherehe kubwa sana huku ‘Jammy’ akisaidiana na yule Mama kutengeneza vyakula tofauti tofauti,majirani walikuwa ni wengi sana pamoja na bosi wake Gervas wote walikuwapo katika kumpa pole Gervas.
~ BAADA YA MWEZI ~
Maisha ya pale nyumbani yaliendelea kuwa mazuri japo sio sana na tuliamua kuiuza ile nyumba ya kina Gervas tuliokuwa tumeipangisha hivyo pesa yote tukaiingiza katika miradi mbali mbali tuliokuwa nayo,yule Mama aliacha kazi ya usafi 'Airport' hivyo tukawanaye akisimamia baadhi ya miradi tuliokuwa nayo, Sikuamini hata siku moja kama yule Mama angebadilika kiasi kile labda ni kutokana na maisha, alikuwa mtu mtakatifu sana na alininyenyekea kwa kila kitu hivyo alitufanyia mengi mema.
Siku moja Gervas alivyorudi toka ofisini.
‘’Levina mke wangu’’
‘’surprise......!!!’’
‘’Otea ni kitu gani kizuri nataka kukwambia kimetokea ofisini leo...?’’
‘’Wewe niambie tu mimi siwezi kujua ni kitu gani mpenzi wangu’’
‘’Haya fumba macho nikupe kitu’’
Nikafumba macho kujua ni kitu gani ameniwekea mkononi mwangu. Haraka haraka nikafungua macho nakushuhudia bahasha ya kaki mikononi mwangu.
‘’Wewe niambie tu kunanini Gervas’’
‘’Haya nimekuruhusu ifungue mwenyewe uone ni kitu gani hicho’’
Nikafungua taratibu huku moyo ukinienda mbio akilini mwangu nilijua tu itakuwa kaongezewa labda cheo tena.
‘’Mungu wangu nini tena hiki?’’
Nilijikuta mwili unanyong'onyea kila nilipokuwa naendelea kusoma mpaka nikaamua kuacha kusoma.
‘’Kwahiyo Gervas ndicho unachofurahia hiki?.. Haya endelea kufurahia..! Endelea tu’’
Nilikuwa na hasira sana mpaka nikatoka zangu nje huku mishipa ya shingoni ikiwa imenitoka na mchozi ulikuwa ukinilenga lenga.
‘’Gervas sitaki unifuate nasema rudi ndani, rudi Gervas’’
Kiukweli nilimpenda sana mpenzi wangu Gervas na nilikuwa tayari kufunga naye ndoa kwani nimetoka naye mbali kwa shida na raha, na ile barua aliyonipa ilikuwa inamhusu yeye mwenyewe kuwa meneja Mkuu na siyo msaidizi tena na hata hivyo nusu ya wafanyakazi wa ofisi yao inahamia Mtwara na Gervas anatakiwa akasimamie tawi la Mtwara hivyo mshahara na cheo vimeongezeka mara mbili ya ilivyokuwa.
Amani ilinipotea kabisa mwilini mwangu huku nikiwa sijiamini kabisa kwani ni muda mrefu sijakaa na Gervas mbali.
Nikarudi ndani kuendelea na shughuli zangu za kawaida lakini Gervas alikuwa chumbani nikamfuata kumchungulia anafanyaje lakini nilipoingia chumbani nilimkuta kakaa tu kwenye Laptop yake anafanya kazini kasimama mlangoni nakumuangalia kwa huruma huku mchozi ukinitoka na kusisimka taratibu nikamfuata na kukaa pembeni yake kisha nikachukuwa mikono yangu na kupenyeza mabegani mwake huku nikimpapasa kwa kuitelezesha ile mikono yangu kwenye mabega yake,
‘’Gervas mme wangu.. Nakupenda sana...!’’
‘’Nalijua hilo na hata mimi nakupenda tena sana Levina’’
Nikamzunguka kwa nyuma na kumkumbatia kwa furaha huku nikijitahidi kujisahaulisha yaliyotokea lakini kabla sijamkumbatia mara nikajisikia vibaya nikakimbia moja kwa moja mpaka chooni huku Gervas akinifuata kwa spidi nyuma nyuma na nilipofika nikatazamana na sinki la pale karibu na choo nikaanza kutapika na nilitapika sana bila kujua ni kwanini, Kwani nilishikwa na kichefu chefu ghafla.
‘’Pole Levina, Nini tena lakini umekula?’’
‘’Sijui Gervas ila nahisi kama kizungungu zungu’’
Haraka haraka Gervas akanipakiza kwenye gari kutokea nyumbani kurasini mpaka hospitalini 'Ocean road' na tulipofika tu moja kwa moja akanipeleka kwa Dokta wake akanipokea na kuniingiza kwenye kachumba kisha.
‘’Wewe nisubiri hapo nje’’
Yule Dokta alimwambia Gervas kisha nikamwangalia akitoa vitu kama vichuma chuma vilivyounganishwa na waya kisha akaviweka tumboni mwangu huku akivisikilizia kisha akavitoa na kunishika shika tumboni, na baada ya hapo akachomoa kimrija kisha akanipa akaniambia nikidumbukize kwenyesehemu zangu za siri, Nikafanya hivyo baada ya muda nikampatia akakiweka kwa juu huku akikiangalia mara mbili tu na kuniambia.
‘’Hongera Levina..’’
Nilikuwa kama sijiamini amini huku nikidhani kama ni ndoto naota lakini ilikuwa ni ukweli mtupu.
‘’Embu niambie ukweli Dokta nini tena?’’
‘’Unamimba na ina wiki kama tatu mpaka sasa’’
Hapo hapo nikatoka spidi mpaka nje kwa Gervas na kwenda kwania ya kumwambia lakini nikiwa natoka Dokta akaniita
‘’Levina? Levina?’’
~BAADA YA WIKI MOJA~
Nilikuwa mzima wa afya na safari ya kurudi kwetu Tanzania ilikuwa imeshafika sikuweza kuwaona wale watu tena pale wodini tayari Gervas wangu alikuwa pembeni yangu mzima tena tukicheka naye na kupiga stori kwenye gari huku tukielekea uwanja wa ndege wa zambia.
Hapakuwa mbali sana kwani ndani ya nusu saa tulikuwa tayari tunaingia ndani ya uwanja wa ndege huku tukielekea kupanda ndege ile ile iliyotuleta.
Furaha kwangu ilikuwa kubwa sana na hata Grvas naye alifurahi sana kwa upendo niliokuwa nimemuonesha wa kujitolea figo yangu ya upande mmoja na kumpatia.
‘’Levina huyu ni nani?’’
Ilikuwa ni sauti ya gervas akitaka kujua ni nani yule Mama tuliyeongozana naye mpaka Zambia.
‘’huyu ni mfanyakazi pale 'airport' dar na ametoa msaada mkubwa mpaka wewe kufika hapa...’’
‘’Ahsante sana Mama. Nakushukuru sana kwa msaada wako ulioutoa...!’’
‘’Hata nawewe nakushukuru mwanangu pole sana na naimani umeshapona kabisa’’
Nilipenda sana ukarimu wa yule Mama na hata tulipofika uwanja wa ndege Gervas alimuomba sana twende naye mpaka nyumbani kwetu.
Tuliingia Dar alfajiri sana kwenye saa kumi na mbili,
Siku hiyo hiyo tulipofika tuliandaa sherehe kubwa sana huku ‘Jammy’ akisaidiana na yule Mama kutengeneza vyakula tofauti tofauti,majirani walikuwa ni wengi sana pamoja na bosi wake Gervas wote walikuwapo katika kumpa pole Gervas.
~ BAADA YA MWEZI ~
Maisha ya pale nyumbani yaliendelea kuwa mazuri japo sio sana na tuliamua kuiuza ile nyumba ya kina Gervas tuliokuwa tumeipangisha hivyo pesa yote tukaiingiza katika miradi mbali mbali tuliokuwa nayo,yule Mama aliacha kazi ya usafi 'Airport' hivyo tukawanaye akisimamia baadhi ya miradi tuliokuwa nayo, Sikuamini hata siku moja kama yule Mama angebadilika kiasi kile labda ni kutokana na maisha, alikuwa mtu mtakatifu sana na alininyenyekea kwa kila kitu hivyo alitufanyia mengi mema.
Siku moja Gervas alivyorudi toka ofisini.
‘’Levina mke wangu’’
‘’surprise......!!!’’
‘’Otea ni kitu gani kizuri nataka kukwambia kimetokea ofisini leo...?’’
‘’Wewe niambie tu mimi siwezi kujua ni kitu gani mpenzi wangu’’
‘’Haya fumba macho nikupe kitu’’
Nikafumba macho kujua ni kitu gani ameniwekea mkononi mwangu. Haraka haraka nikafungua macho nakushuhudia bahasha ya kaki mikononi mwangu.
‘’Wewe niambie tu kunanini Gervas’’
‘’Haya nimekuruhusu ifungue mwenyewe uone ni kitu gani hicho’’
Nikafungua taratibu huku moyo ukinienda mbio akilini mwangu nilijua tu itakuwa kaongezewa labda cheo tena.
‘’Mungu wangu nini tena hiki?’’
Nilijikuta mwili unanyong'onyea kila nilipokuwa naendelea kusoma mpaka nikaamua kuacha kusoma.
‘’Kwahiyo Gervas ndicho unachofurahia hiki?.. Haya endelea kufurahia..! Endelea tu’’
Nilikuwa na hasira sana mpaka nikatoka zangu nje huku mishipa ya shingoni ikiwa imenitoka na mchozi ulikuwa ukinilenga lenga.
‘’Gervas sitaki unifuate nasema rudi ndani, rudi Gervas’’
Kiukweli nilimpenda sana mpenzi wangu Gervas na nilikuwa tayari kufunga naye ndoa kwani nimetoka naye mbali kwa shida na raha, na ile barua aliyonipa ilikuwa inamhusu yeye mwenyewe kuwa meneja Mkuu na siyo msaidizi tena na hata hivyo nusu ya wafanyakazi wa ofisi yao inahamia Mtwara na Gervas anatakiwa akasimamie tawi la Mtwara hivyo mshahara na cheo vimeongezeka mara mbili ya ilivyokuwa.
Amani ilinipotea kabisa mwilini mwangu huku nikiwa sijiamini kabisa kwani ni muda mrefu sijakaa na Gervas mbali.
Nikarudi ndani kuendelea na shughuli zangu za kawaida lakini Gervas alikuwa chumbani nikamfuata kumchungulia anafanyaje lakini nilipoingia chumbani nilimkuta kakaa tu kwenye Laptop yake anafanya kazini kasimama mlangoni nakumuangalia kwa huruma huku mchozi ukinitoka na kusisimka taratibu nikamfuata na kukaa pembeni yake kisha nikachukuwa mikono yangu na kupenyeza mabegani mwake huku nikimpapasa kwa kuitelezesha ile mikono yangu kwenye mabega yake,
‘’Gervas mme wangu.. Nakupenda sana...!’’
‘’Nalijua hilo na hata mimi nakupenda tena sana Levina’’
Nikamzunguka kwa nyuma na kumkumbatia kwa furaha huku nikijitahidi kujisahaulisha yaliyotokea lakini kabla sijamkumbatia mara nikajisikia vibaya nikakimbia moja kwa moja mpaka chooni huku Gervas akinifuata kwa spidi nyuma nyuma na nilipofika nikatazamana na sinki la pale karibu na choo nikaanza kutapika na nilitapika sana bila kujua ni kwanini, Kwani nilishikwa na kichefu chefu ghafla.
‘’Pole Levina, Nini tena lakini umekula?’’
‘’Sijui Gervas ila nahisi kama kizungungu zungu’’
Haraka haraka Gervas akanipakiza kwenye gari kutokea nyumbani kurasini mpaka hospitalini 'Ocean road' na tulipofika tu moja kwa moja akanipeleka kwa Dokta wake akanipokea na kuniingiza kwenye kachumba kisha.
‘’Wewe nisubiri hapo nje’’
Yule Dokta alimwambia Gervas kisha nikamwangalia akitoa vitu kama vichuma chuma vilivyounganishwa na waya kisha akaviweka tumboni mwangu huku akivisikilizia kisha akavitoa na kunishika shika tumboni, na baada ya hapo akachomoa kimrija kisha akanipa akaniambia nikidumbukize kwenyesehemu zangu za siri, Nikafanya hivyo baada ya muda nikampatia akakiweka kwa juu huku akikiangalia mara mbili tu na kuniambia.
‘’Hongera Levina..’’
Nilikuwa kama sijiamini amini huku nikidhani kama ni ndoto naota lakini ilikuwa ni ukweli mtupu.
‘’Embu niambie ukweli Dokta nini tena?’’
‘’Unamimba na ina wiki kama tatu mpaka sasa’’
Hapo hapo nikatoka spidi mpaka nje kwa Gervas na kwenda kwania ya kumwambia lakini nikiwa natoka Dokta akaniita
‘’Levina? Levina?’’