Story: Safari ya kutafuta mali za Mjerumani katika msitu wa Nyumbanitu - Njombe

๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€ mkuu si hata hujasogea kwenda chooni kma hivyio.
IMG_20201025_221424.jpg
hali ilivyooo..!
 
DISCLAIMER: Nianze kwa kusema hii story sio ya kwangu, ni ya member Mbwichichi ambae amesimulia hii story ndani ya story

๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡

https://www.jamiiforums.com/threads...-macho-yangu-katika-msitu-wa-nairoto.1808580/

Hivyo nimeona nisaidie kuweka hapa iwe peke yake ili irahisishe usomaji na ufuatiliaji maana imeleta shida sana kwa wasomaji mbalimbali
Kwa ruhusa yako mkuu Mbwichichi naomba niandike hii story kwa hapa kama itakupendeza
Ukwaju Citizen B Naki 12 Joannah na wengine wote karibuni


Mimi miweke hapa hapa habari yangu kuhusu machimbo haya na actually siyo machimbo ni harakati za kusaka mali alizoacha mjerumani wakati wanaondoka kutuachia nchi

kuna kitu tunafumbwa sana tunafichwa ukweli,wakoloni walipanga kila kilichotokea kwenye makoloni yao na hata yanayotokea sasa yalipangwa na wanajua nini kitafatia baada hata ya miaka kumi kuhusu nchi hizi masikini za afrika

kwamba walijipanga kuondoka ni KWELI,na uhuru hatukupigania,ni wao walipanga sasa watatutawala kwa namna nyingine ili waende wakajenge nchi zao huku wakiendelea kututawala kwa mbali na kuchuma mali zao...viongozi wote wanaokuwa madarakani ni vibaraka wao,hakuna hata mmoja mzalendo wa kweli na nchi yake

nina ushuhuda wa kusema haya,moja kati ya makubaliano yao ilikua ni kuacha mali zao salama na jukumu la serikali ni kuzilinda na kuwaruhusu wakija zichukua hata baada ya miaka mia,haya yapo kimkataba na kila raisi anayeingia madarakani anaambiwa hizi siri....na waliacha mali kweli za kutosha

story yangu sasa inabase kwenye hizi mali,hapa ni madini waliyoacha kwenye misitu ya nyumbanitu huko njombe,safari ya kuzifata hizo mali zilifanya nipoteze ndugu zangu watatu na mimi kunusurika chupu chupu ila kubaki na ulemavu...sitasahau hii safari ya machozi,jasho na damu.

ngoja nikaoge nakuja...

Baada ya kubembelezwa saaaana huko DM kwa kutumiwa hadi wadada kuniahidi tunu basi nimebadili mawazo sasa nitasimulia habari ya safari yetu ya kutafuta mali (RUPIA) humo msitu wa NYUMBANITU

(achaneni na utani wa hapo juu) sasa twende taratibu,matukio mengi nitafupisha tu kufanya story kueleweka

Kwa wasiojua...Nyumbanitu iko Njombe wilaya ya wangingโ€™ombe kuna mahala panaitwa Mdandu huko,ni msitu wenye habari za kutisha sana wenyeji wa huko hakuna sehemu wanapaheshimu kama hapo

Huu msitu cha kwanza uko na wanyama wasio wa kawaida kabisa na wanapatikana huko tu,kuna kuku fulani weusi tiii na midomo myekundu,hawa wanaishi humo na hakuna anayewahudumia kwa chakula wala matunzo...pia kuna ngโ€™ombe n.k wote hawa ni kwa ajili ya matambiko ya makabila mbalimbali ya mkoa wa Njombe,zamani ikiwa wilaya ya Iringa,,haswa wabena na wakinga.

Kuna ukoo kule unaitwa wa akina Mkongwa,hawa ndio wamiliki halisi wa huo msitu na inasemekana wao wakifa huwa wanageuka kuwa nyoka na wanaishi huko kwenye huo msitu...kwa waliofika kutalii kuna wazee wako nje huwa wanatoa maelekezo ya namna ya kuingia humo na mila za humo,kama una roho nyepesi unaweza ishia tu kufika mlangoni ukarudi zako ulikotoka...unapigwa mkwara mlangoni na moja kati ya issue unapaswa kujipanga ni kwamba kama mwanamke usiende ukiwa kwenye HEDHI sababu mizimu humo ikisikia tu harufu ya damu wote mlioongozana na huyo mnapotea na hamuwezi onekana hadi wazee wa mila wafanye yao...

achana na hayo...

kilichotutia tamaa sisi kuhusu humo ndani ni story za uwepo wa RUPIA za mjerumani bwanaaa...na hakika zipo na zilikuepo,tulichogundua wale wazungu washenzi sana,hii ya kujenga hofu watu wasiende humo kwa kujiamini ndio imefanikiwa kuziacha mali zao salama mule msituni...wazungu akili nyingi sana,humo wamepandikiza uchawi mkali sana na unalindwa na hao wazee wa mila bila wao kujua wanalinda mali za watu....

ilikua 2001 mwezi wa 12 sasa tukiwa na jamaa zangu tukapanga mkakati wa kuingia mule bila kufata sheria zao za kichawi...maana ukifata protocal kuna maeneo huruhusiwi kufika na ndio inasemekana yana mali

kuna mapango makubwa inasemekana yakitumika wakati wa vita...kwa story tulizopata ni kwamba hizi mali zimefichwa kwenye masanduku makubwa yananingโ€™inia kwenye mapango/mahandaki yaliyoko ndani kabisaaaa wanakosemaga ndio anakaa mzee mwenye msitu,ingawa kikweli huko sababu ya giza na kutisha basi kumekua makazi salama ya nyoka wakubwa wa kila aina na hao kuku wa kichawi ndio chakula chao...

tukiwa tumejipanga,plan ilikua ni kazi ya usiku mmoja tu tunamaliza tunarudi na mali na utajiri wetu...kulikua na habari kwamba soko ya rupia ni uhakika...

nikirudi naanzia sasa kwenye safari yenyewe kuingia msituni nyumbanitu



plan yetu kuingia mwezi wa 12 ilikua sababu ile ni miezi ya kula mavuno kwa wakazi wa Njombe wanajua huu ni msimu wa mvua na watu wengi ndio huwa wanaenda kutambika huko malori kwa magari ya kifahari...hata hao kuku huwa wengi na habari ni kwamba hata mali ndio inakua nyingi,inasemekana huwa inakuja mali na kupotea na ishara ni hao kuku kuwa wengi na kupungua

tulikua watano,1.mimi ,2.mobu (marehemu) ,huyu alikua mkinga alikua ana mishe za kupasua mbao kwa msumeno wa mkono shimoni (waliokaa njombe wanajua hii style ya kupasua mbao) 3.usungilo (marehemu) naye alikua na mishe za kupasua mbao,kwao ni bulongwa makete huko 4.mangi(alitoka mzima) huyu tulifanikiwa kutoka naye ila baada ya kutoka alikaa kama wiki moja akaanza onesha dalili za kuwa kichaa,na akawa kichaa kweli akaondokaga pale njombe hadi leo sijui habari zake (mungu amrehemu huko aliko) 5.mwaikambo (marehemu) jamaa wa mbeya alikua naye kaja kuhangaika na maisha tu Njombe.

Nirudi kwangu mimi kwanza kidogo,by then mimi nilikua mwajiriwa kiwanda cha chai,ajira siyo ya kitaalamu lakini kipato cha kuweza kuwanyanyasa hao jamaa zangu wote kiuchumi...wanangu sana,tunakutana kijiweni tunawa washkaji haswaa...kwenye hii safari mimi ndio nilikua master planer,sababu labda ya kuwa na kauli...mangi ndio alikua kama mwenye maono yote na alikua na njaa sana na hii mali...kwahiyo kupona kwangu mimi ilikua sababu sikua mstari wa mbele kuingia ndani kabisa ya pango kwenye hayo masanduku..

usiku tar 22/12 tukiwa na kila kitu cha kuingia kufungua masanduku tukaenda mdandu...fika tukiwa tushapiga mitungi yetu wanangu wako mbele mbele tukaingilia upande mwingine kabisa wa msitu ambako hata hakuna watu...hakuna kibaya hapo,tunakata majani kwa mapanga na miti midogo kupata njia...tumetembea zaidi ya masaa mawili msituni ili kuja unganisha na njia ya kule wanakoingilia watalii...na sababu tayari tulikua ndani hatukuonekana na wale wazee kule nje pamoja na walinzi wa msitu


wazee...mule ndani ni giza totoro,tochi zetu za mawe zile za kuitwa KURUNZI.,,,betri tatu tatu,tukafika tukaipata ile sasa njia ya ndani kabisa kwenda mapangoni...humu mchana kunatisha saanaaa,sasa imagine usiku inakuaje,hakuna story hapo na kama ni kuitana ni kwa sauti za chini sana,hofu ilikua kubwa na mvua sasa ikawa imeanza kupiga...baridi ni kali sana msituni

tumeendaaaa tukafika sasa kwenye mlango wa pango hapo ndio visa vilipoanzia...kule ndani usiku wanyama ndio wanakua active sababu ya ratiba labda za utalii so usiku pango ndio zinakua na fujo...tukaanza liingia pango bila uoga,mwendo kama wa dakika 30 hivi...huko ni kusikia tu sauti za wadudu na wanyama wadogo..tukamaliza hiyo zone ya zile pango za kitalii sasa tukawa kwenye mwisho ambako watu huwaga hawaruhusiwi kusogea zaidi ya hapo kwa imani kwamba watapotea hawatorudi.

na ndio habari ya vifo vya ndugu zangu watatu,kichaa cha mangi na ulemavu wangu inaanzia hapa...

ulemavu wangu wala usiwape wazo...ni kwamba niliumwa na nyoka huko nikafanikiwa kwa kudra za mungu tu kuokolewa kwa kukatwa mguu wa kushoto..



nimerudi wadau,tusameheane...nimeandika habari yangu baada ya kusoma story mama ya huu uzi ukanifurahisha na kati ya vitu nimesuffer ni kutafuta mwendelezo kama hivi mnavyosuffer nyie

ila all in all nipo hapa...

....kati ya makosa tuliyofanya (haya nilikuja gundua baada ya mchakato kuisha na kupona kabisa,kuanza kuwaza ilikuaje hadi tukafanya tukio lile),lilikua ni kuchukulia lile tukio kama kitu rahisi tu,hatukufanya uchunguzi wa kutosha labda sababu ya ile haraka ya kufanikiwa na habari za kufata mkumbo kwamba kuna watu waliofanikiwa walivyoingia humo ndani,kule Njombe kulikua na tajiri aliyeitwa Mwanzinga(marehemu kafa 2017/18 kama sijakosea) huyu ni moja ya watu wanaodaiwa kutajirika baada ya kufanikiwa kuzama humo na kutoka na mali...story kama hizi ndio zilituchanganya na kujikuta tumebamia mapango ya watu bila kujipanga...pia baadae nilikuja ambiwa kwamba ile mali haisakwi kwa makundi,yaani unatakiwa kuwa man alone,peke yako ukifanikiwa kuzama ukatoka basi umetoboa,kosa letu lilikua kwenda kikundi...tuachane na hayo

sikumbuki masaa exactly lakini siyo chini ya saa sita hivi tukawa ndio huko pango kubwa...kutembea kwenda mbele ndio ilikua mtihani sababu nje mvua ilikua inanyesha na hilo pango ndio iliku njia ya maji yanaingia halafu yanapotelea huko ndani ndani yanatokea upande wa pili wa msitu kwenye miteremko kuunda mikondo ya maji

maji yalikua mengi na yanaenda kwa kasi sana so tulikua tunatembea kwa kujishikilia pembeni kwa tahadhari sana,giza ni kubwa bila zile tochi hufanyi kitu chochote kule...ukiongea sauti kidogo tu inakua multiplied sababu ya mwangwi,lile pango linaenda linashuka chini...ni kama shimoni,umbali wa kama viwanja viwili vya mpira ndio mauzauza yakipoanza

sisi kwetu kule huwa wanasema ukisikia hofu sana ghafla kwa kitu ambacho ulianza fanya kwa ujasiri basi acha mara moja...mimi hofu ikaanza kuniingia,lbda sababu sikua na moto sana kuhusu hizi rupia kuliko wenzangu(ikumbukwe nilikua na kibarua) nilikuaga naambiwa kuhusu nywele kusimama sikuwahi experience kabla,,,mara nikahisi mapigo ya moyo yako kazi sana hofu ni kubwa na nywele zinawasha sana ndio nywele kusimama huko...kutetemeka sababu ya baridi kukazidi ,sikumwambia mtu yeyote..kwa kadri ya ramani ya mangi alisema tumefika hayo maeneo yenye masanduku,kwa maelezo yake tulitakiwa fika kwenye korongo liko ndani ya pango...kwamba kwenye korongo juu kumeunganishwa minyororo mirefuuuuu imefungwa juu kabisa imeshuka chini huko ndio imeungwa kiustadi kwenye mashanduku imara kabisa,kwa uhandisi ule hayawezi anguka leo wala kesho...ni kweli binafsi niliona sasa sijui huwa ni wenge au nini,sababu humo ni kuchafu na kuna mizizi sana huwezi confirm kuwa ni kweli ni minyororo au ni mizizi,jamaa pia alituambia kuhusu beacon,ni kweli tuliona beacon zikiwa na maelezo ya lugha hatuifahamu kwa maelezo ya mangi hizo ni code wameandikiana wao siku wakija wanazitumia kufata mali....na zile zimeandikwa katika namna ukizitumia bila kujua ndio zinakupoteza zaidi (wazungu washenzi sana)...yaani unaweza kuta mshale umeenda kusini mita 2 kumbe wanamaanisha aendee kusini ya nchi,unakuta ni songea huko au vyovyote na mali haipo hapo unapodhani wewe,ni anayeweza chukua zile mali ni lazima awe na taarifa za kutosha sanaaaa...sababu hata wao huwa wanakuja na wanarudi patupu sometimes wakikosea maelezo.

nimeongea kuhusu mangi(huyu bwana kumbe yeye alikua keshawahi kuja fanya jaribio ila hakuweza mwenyewe ndio maana akaamua kutafuta kampani)

sasa ndio akatuambia tukiwa hapo kwamba...huko chini kushuka lazima watu washushwe kwa kamba(tulibeba kwa urefu wanaotosha sana,kama marufu kule njombe zinaitwa TANTAN) nani anashuka ikawa sasa wajitolee wawili akiwemo mangi mbeba maono...alikua pamoja na usungilo,mobu na mwaikambo wawashikilie kamba na mimi nikawa tu pending nimewashikia vitu pamoja na kucheki cheki usalama tu...wakajifunga kikomando tayari kushuka,kushuka kwenyewe hujui unashuka wapi...unafata tu mizizi maana huwezi jua kama ni ndio mnyororo au nini kisa msongamano wa taka.

jamaa wakaanza kushuka chini...kimya kikatawala pale sababu ya hofu tu.

dakika kama tano za kushuka kwa tahadhari ndio ikatokea shida,kikweli huwa sijui ni nini hasa kilitikea sababu mimi ni ghafla sana nikaona mwanga mkali mno,mkali saaaana kama radi kutoka kule shimoni ni kama zikanipoteza fahamu kwa muda,mwanga uliambatana na sauti za kilio kule chini as if mtu kakamatwa ghafla na mnyama mkali,nadhani alikua usungilo sababu baadaye mangi alifanikiwa kutoka(nitasema baadae tulikutana vipi)

nilichoweza kufanya haraka kwa muda ule ilikua ni kulala chini haraka sana,kule chini sauti jamaa ilikua inazidi kupungua ikimaanisha keshazidiwa nguvu...sikujua chochote kuhusu wenzangu washika kamba pale juu sababu kila mtu nadhani alianza kujitetea kivyake..

nikaanza kukimbia nikiwa na ule upofu wa kupigwa na mwanga mkali ghafla ukiwa gizani....kimbia bila mwelekeo,nikajigonga vibaya kichwani kwenye sehemu ya juu ya pango,na kilichoniokoa ni kwamba nilikua naelekea mbele zaidi ambako ni jirani kutoka nje kuliko kule tulikotoka...wenzangu hapo sijui wameelekea wapi...ile kujigonga ikanimaliza nguvu kabisa nikajikuta nimelala hapo hapo damu zinanitoka(ile fact ya damu nadhani ndio inaaply hapa) ghafla mbele yangu,ule upande niliowaacha jamaa sasa nikaona bonge ya nyoka ila siyo wa kumeza,mkubwa kwa hawa nyoka tumewazoea ila siyo chatu..kujivutavuta nadhani nikamkanyaga ndio akanigonga,akili hapa ndio zikaja baada ya kujua kifo ndio kimefika,chap nikatoa kiatu nikafungua kamba za viatu vyote viwili,nikafunga juu ya goti na chini ya goti sababu alinigonga kwenye hii nyama ya nyuma ya mguu...nikajikamua kamua kizushi nikawa napambana sasa kuelekea nje ,ambacho sikujua(labda ni mungu tu) kwamba kumbe tulikua nje kabisa hata ya msitu ambako sasa ni karibu na barabara kabisa watu ambako watu wanapita..tena karibia na kijijini...cha mwisho nakumbuka niliweza fanya ni kupiga kelele ya mwito kule njombe inaitwa ngoro....nikapiga za vilio kama mara tano hivi pumzi ikakata sikuelewa kilichofata baada ya hapo aiseee...hadi siku nazinduka nikiwa hospitali ya kibena....mguu ukiwa na hali mbaya sana umeharibika lakini pia ngozi yangu karibia mwili mzima ikiwa na upele fulani wa kuwasha sana...

nikaanza matibabu huku nikiwa sijui nimefikaje,sijui kuhusu jamaa zangu na hapo nimetulia sijauliza mtu yoyote sababu hakuna hata aliyeniuliza kulikoni

nitarudi sasa na habari ya matibabu yang na kuujua ukweli kuhusu vifo vya jamaa zangu na yule mwengine aliyegeuka mwehu...kisha mtazamo wangu kuhusu hizi mali za wachawi wazungu...

mnisamehe kwa mpangilio mbovu,naandika haraka sana niendane na muda kupambania kombe watoto wapate chochote kitu...

INAENDELEA.......

nimerudi tena sasa baada ya kushiba sasa...


pale kibena hospital kumbe nililetwa na wanakijiji tu,kwamba imezoeleka wao wakisikia kelele toka kule msituni basi huwa wanajua lazima ni watu waliopotea pangoni sasa kuonekana kwao huwa kwa style hiyo,na baada ya hapo wengi huwa wanapata kichaa kiasi cha kushindwa kabisa elezea nini waliona kule pangoni...(mimi sikupata nitasema kwanini pia)

....nikiwa bado nauguza kidonda,hapo tayari wafanyakazi wenzangu na ndugu wameshafika,ndugu zangu ni wa njombe na wanajua habari kuhusu msitu,baada ya kuambiwa niliokotwa kule chap wakajua cha kufanya,walikuja na dawa kadhaa na MTAALAMU fulani tokea kijijini kuja kunitoa mkosi na laana zinazopatikana huko(hii huduma ndio aliikosa mangi kwa maelezo ya baadaye) ndio maana aliishia kuwa kichaa...baadae niliambiwa mambo ya mule hayapaswi simuliwa kwahiyo ukifanikiwa kutoka mzima ni aidha ufanyiwe UTAALAMU au uwe kichaa usiwe na kumbukumbu kabisa...

mguu uliendelea kutibiwa na na kuharibika kadri siku zinasonga na ule upele ukawa unazidi na nabadilika kuwa wa kijani mguu wote sasa...madaktari wakashauri unatakiwa kukatwa ili kuoza kusiendelee(hii issue ya matibabu siyo concern yangu haswa)...kwa kifupi ndio wakakata mguu ila with time nilifanikiwa kupata operesheni ya kipande bandia huwezi jua kabisa kuwa sina mguu.

nilikaa pale mwezi mzima ingawa siku za mwanzo zilikua ngumu,kumbukizi ya matukio haikua inakuja full yaani unakumbuka tu habari hadi kipindi fulani halafu hukumbuki nini kilifatia aidha unaishia kusinzia au kupata mawenge...wenge linakuja sababu ile sauti na mwanga vinakua vinaflash upya kichwani,yaani siku za mwanzo ilikua nikifika ile hatua ya mwanga na sauti ya jamaa kule chini kila kitu kinapotea hadi baadae sana ndio ikawa naweza kumbuka kila kitu na kusimulia kama hivi...

sasa turudi kuhusu wale jamaa zangu...hii habari ya jamaa kwakweli sijuagi nini kiliwapata kule,wale wawili wa chini ni mangi alifanikiwa kupata miili yao wengine haikuwahi patikana pamoja na kwamba zilifanyika mila kibao lakini wanachodai ni kwamba mtu akipotelea huko shimoni huwa ni sadaka kwa hiyo wanaita mizimu na hata msihangaike kutafuta ila ukitaka tu mabaki yake ndio kuna mahala wazee huwa wanaenda fata napo ni mifupa na hawaziki kikawaida inazikwa kimila ili kutosambaza wanachoita โ€œtegoโ€

mangi ndani ya ile wiki alifika hospitali na hata alikua na uwezo wa kuongea baada ya kuanza changanyikiwa na nilimuelewa mwanzoni ila kadri siku zinasonga akaacha hata kuwa anatimba kunipa gwala...natoka mimi keshakua chizi

kwa upande wake anasema alichoona kule chini ilikua ni ajabu(mangi alifanikiwa kupanda sababu anasema kwa bahati nzuri kamba yake yule jamaa wa juu alipata akili ya kuifunga kwenye mti kwa juu) kwa hiyo wakati yeye kapigwa mwanga na kuachia kamba bado mangi ilimshika sababu na yeye alikua kajifunga kiunoni akafanikiwa kupanda juu kwa kujivuta kwa ile kamba,anasema yeye alifanikiwa kutoka na pia aliokotwa na wanakijiji na ndio aliyewapa habari hadi ndugu zangu ndio kufanikiwa kunifanyizia dawa...sijui kwa mangi ziligoma labda sababu ya kuwa na damu tofauti na ya wabena,lakini sababu yeye alishawahi kuzama akatoka mzima naona akapuuza.

anasema alipigwa mwanga mkali na aliona kila kitu kule chini,kwa maelezo yake ni aliona masanduku makubwa sana yanaelea lakini sasa huko chini kuna majoka balaa,nyoka ni wengi sana(nahisi ndio hii wanayoita huku uraiani mizimu ya akina MKONGWA)...sasa huwa wanasema ukifika hatua ya kuona hawa ndio lazima ufe au uwe chizi...anasema struggle yake kutoka shimoni haikua rahisi alichoona kuhusu wake jamaa ni kwamba waliyeshuka naye alikamatwa na moja kati ya hao nyoka na kushushwa huko,pia ule mshtuko ulimvuta na aliyekua kamshikia kamba akaangukia humo,sijui kilimtokea nini yule watatu ila naye ilikuja thibitika kwamba alikufa na wazee wa mila...

nitakuja tena..
Aisee Pole na changamoto Mkuu japo ni muda sana umepita ,ila Hongera na kupambana
uliongelea swala la kuwa na taarifa sahihi juu ya kazi hizi kwenye eneo mlilokuwa mnaelekea,na nikweli bahati mbaya hamkuwa na taarifa sahihi na pili Hamkuwana uelewa deep juu ya Field husika,pia kuna swala la siku za kuingia saiti ninyi nahisi kabisa mlikuwa hamjui siku sahihi na na kwenye site huwa wanaingia watu 2 tu na wakizidi inakuwa na Hasira huwa inapungza yenyewe waliozidi na ndiyo maan amlibaki 2.
 
Aisee Pole na changamoto Mkuu japo ni muda sana umepita ,ila Hongera na kupambana
uliongelea swala la kuwa na taarifa sahihi juu ya kazi hizi kwenye eneo mlilokuwa mnaelekea,na nikweli bahati mbaya hamkuwa na taarifa sahihi na pili Hamkuwana uelewa deep juu ya Field husika,pia kuna swala la siku za kuingia saiti ninyi nahisi kabisa mlikuwa hamjui siku sahihi na na kwenye site huwa wanaingia watu 2 tu na wakizidi inakuwa na Hasira huwa inapungza yenyewe waliozidi na ndiyo maan amlibaki 2.
mbona jamaa keshakuambia Story si yake bali amecopy na kuPaste kutoka kwa Mbwichichi ili kuturahisishia, hayoa Mapango na mengineyo niya imani za kimizimu na amesema kulikuwa na masanduku yanayoning'inia, kwa hiyo anayetumbukia haijulikani anakoenda labda anaangukia miamba na kukwama hatimaye kufa
tunaambiawa majoka ya Ginimbi
1606029499927.png
 
mbona jamaa keshakuambia Story si yake bali amecopy na kuPaste kutoka kwa Mbwichichi ili kuturahisishia, hayoa Mapango na mengineyo niya imani za kimizimu na amesema kulikuwa na masanduku yanayoning'inia, kwa hiyo anayetumbukia haijulikani anakoenda labda anaangukia miamba na kukwama hatimaye kufa
tunaambiawa majoka ya Ginimbi
View attachment 1632075
Yamejaa mahela tu humo.
 
mbona jamaa keshakuambia Story si yake bali amecopy na kuPaste kutoka kwa Mbwichichi ili kuturahisishia, hayoa Mapango na mengineyo niya imani za kimizimu na amesema kulikuwa na masanduku yanayoning'inia, kwa hiyo anayetumbukia haijulikani anakoenda labda anaangukia miamba na kukwama hatimaye kufa
tunaambiawa majoka ya Ginimbi
View attachment 1632075
Duh
 
mbona jamaa keshakuambia Story si yake bali amecopy na kuPaste kutoka kwa Mbwichichi ili kuturahisishia, hayoa Mapango na mengineyo niya imani za kimizimu na amesema kulikuwa na masanduku yanayoning'inia, kwa hiyo anayetumbukia haijulikani anakoenda labda anaangukia miamba na kukwama hatimaye kufa
tunaambiawa majoka ya Ginimbi
View attachment 1632075
Yaaani navuta picha upo shimoni unatafuta masanduku ghfla unaiona hii minyoka walah dadeq naweza nikapaaa
 
Nyoka wale na kuku wale ni wale wote walioenda na kupotea kule ndiyo wanakuwa walinzi na Hata aliyekuwa chizi alirudi kule na laiti kama hata leo akapata wakuingia nae kwa usahii lazima atawaona wote aliokuwa nao Kabla.
 
mbona jamaa keshakuambia Story si yake bali amecopy na kuPaste kutoka kwa Mbwichichi ili kuturahisishia, hayoa Mapango na mengineyo niya imani za kimizimu na amesema kulikuwa na masanduku yanayoning'inia, kwa hiyo anayetumbukia haijulikani anakoenda labda anaangukia miamba na kukwama hatimaye kufa
tunaambiawa majoka ya Ginimbi
View attachment 1632075
yes ni kweli ila nimejibu katika kutoa elimu kwa anayesoma hapo
 
Hapo ni kuyavamia tu hayo mapango, tunaenda na siraha zetu na mbuzi mmoja wa kumtanguliza chini kama chambo. Shida ni ule mwanga ulitoka wapi au kuna volikeno, ila pangekuwa na joto. Sasa tunaanzia wapi ,vitendea kazi vipo nahitaji nguvu kazi shuguri ianze mara moja au mpo tayari kufa masikini nyinyi

Kwa urozi mshana yupo tutaambatana nae, yy atafanya matambiko ya kimira mm na wengine tutakuwa na Ak 47 mkononi kwa ajiri ya hao majoka na wapuuzi wengine watakao jaribu kudhoofisha mpango wetu.
 
Back
Top Bottom