Stori ya kusisimua - Taxi

Taxi - (155)

ILIPOISHIA

Walipoingia tu sebuleni Bob aliufungua ule mlango wa ufunguo kisha akauchomoa ule ufunguo na kuuweka mfukoni, wale watu wakashtuka na kugeuka haraka kumtazama kwa mshangao, na hapo wakakutana na mtutu ukiwaelekea, lakini ni kama walikuwa wamejiandaa kwa jambo hilo. Walijigawa na kuruka juu huku wakiachia mapigo ya haraka kumwelekea Bob lakini mapigo yao hayakutimiza wajibu wake ingawa walifanikiwa kuidondosha bastola ya Bob iliyokuwa mkononi huku Bob akifanikiwa kuyakwepa mapigo hayo na kujiweka sawa.

Kabla hawajafanya jambo jingine lolote walishtukia wakimwona Tunu akiibuka toka kusikojulikana na kuruka juu huku akijipindua hewani akiwa ametanua miguu yake na kuutanguliza mguu wake wa kushoto usiokuwa na jeraha, ukifuatiwa na mguu wa kulia. Mwanamume mmoja aliyekuwa karibu na Tunu akafanya jitihada za kujikinga na shambulizi hilo huku akiwa tayari amechomoa bastola yake.

Tunu alikiwa bado hewani aliachia pigo moja matata lililomfanya mwanamume yule na kumfanya apepesuke na kugonga kichwa chake kwenye ukuta. Bastola iliyokuwa mkononi mwake ilimtoka na kuanguka kando. Kabla Tunu hajatua sakafuni akampa pigo jingine la judo ambalo lilitua ubavuni mwake na kumlegeza kabisa. Pigo lililofuata lilimlazimisha yule mwanamume kuanguka sakafuni akiwa hana fahamu.

Wakati hayo yakiendelea yule mwanamume wa pili alijikuta akikabiliwa na Bob aliyeachia pigo maridadi lakini yule mwanamume aliliona na kuinua mkono wake juu kulikinga huku mkono wake wa pili ukijiandaa kubonyeza kitufe cha bastola yake. Bob hakuruhusu mkono huo ufanikiwe kuifyatua ile bastola. Aliruka akampiga kichwa kikavu kilichompa kisurisuri na kufanya ateremke sakafuni bila ubishi na kupoteza kabisa fahamu.

ENDELEA...

Tunu aliwatazama wale wanaume kwa makini akiwa haamini kabisa kama waliweza kugundua yalipo maficho yake. Moyo wake ulimdunda sana ingawa hakujua au kupata kuhisi hofu katika moyo wake, lakini kitu fulani kilimpanda moyoni na kumtia hasira na kichefuchefu. Mlango wake wa hisia ya sita ulimtanabaisha kuwa wale wanaume hawakuwa peke yao, bali kulikuwa na mtu au watu wengine waliokuwa wameambatana nao na huenda walikuwa sehemu fulani jirani na eneo lile wakijiandaa kuvamia. Sasa Tunu aliamua kupambana na yeyote.

Kwa kusaidiana na Bob, waliwaburuza wale wanaume hadi kwenye chumba kidogo cha maliwato ya jumuia, wakawafungia humo baada ya kuwapekua na kuwakuta wakiwa na chupa ndogo ya dawa ya kusababisha usingizi aina ya Chloroform, bastola mbili, simu na vifaa maalumu vya mawasiliano. Kisha waliwavua nguo wakiwaacha na boksa na kuwafunga pingu miguuni kwa pamoja, mmoja mguu wa kushoto na mwingine mguu wa kulia.

Tunu na Bob walivichukua vile vifaa vya mawasiliano na kuvivaa ili kufuatilia mawasiliano yoyote kati ya wale wanaume na wenzao, hata hivyo walishangaa kuona kuwa tayari mawasiliano yalikuwa yamekatwa. Wakaamua kuviacha vile vifaa na kuweka mtego ili kuwanasa endapo wangejaribu kufuatilia au kuingia mle ndani. Tunu alimtaka Bob atangulie kutoka nje na apande kwenye mti mkubwa uliokuwa sehemu ya mbele ya ile nyumba, ili aweze kumwona kila mtu ambaye angejaribu kuingia mle ndani kupitia mbele. Bob akatoka nje na kukwea mti mmoja kwa tahadhari.

Wakati huo Tunu alikuwa akiandaa mtego kwa yeyote ambaye angefanikiwa kuingia mle ndani, alichukua chupa fulani iliyofanana na chupa ya manukato, akaziba pua na mdomo wake kwa kitambaa maalumu na kuyapulizia yale manukato yote kwa tahadhari kubwa eneo la sebuleni kwenye mlango mkubwa wa kuingilia na jikoni kulikokuwa na mlango mwingine wa kuingilia ndani.

Baada ya muda mfupi eneo lote la jikoni na sebuleni likajaa harufu nzuri ya marashi. Tunu aliporidhika akachukua begi lake lenye vifaa vyake vya kazi na kutoka haraka, aliizunguka ile nyumba, kisha kwa kutumia mbinu yake ya kijasusi aliupanda mti mmoja mkubwa uliokuwa kando ya ukuta uliokuwa ukiizunguka ile nyumba.

Alitafuta sehemu nzuri juu ya tawi moja kubwa la ule mti lililokuwa na majani mengi na kujibanza, ilikuwa ni sehemu ambayo aliweza kumwona kila mtu aliyekaribia au kupita jirani na nyumba ile kwa kupitia eneo la nyuma. Mara simu yake ikaanza kuita kwa kutetema, aliitoa na kuitazama kwa makini huku akikunja sura yake, akaliona jina la Tom na kushusha pumzi huku akiuma midomo yake. Aliipokea ile simu haraka, “Niambie, Tom!” aliongea kwa sauti ndogo yenye tahadhari.

“Vipi kwema huko, mbona kama unaongea kwa tahadhari kubwa sana!” Tom aliuliza kwa wasiwasi baada ya kuhisi kuwa mambo hayakuwa shwari kwa upande wa Tunu.

“Mambo si shwari, watu wa Mr. Oduya wamevamia hapa, hata sijui wamepafahamu vipi...” Tunu alisema kwa sauti ya chini iliyobeba kila aina ya tahadhari.

What!” Tom aling’aka kwa mshtuko mkubwa. “Lakini wote mko salama?”

“Usijali! Tumewadhibiti kirahisi mno, ila tumeweka mtego kuwanasa wengine watakaokuja,” Tunu alisema na kusita kidogo. “Na wewe nipe ripoti!”

“Huku mambo yamekwenda kama tulivyopanga, tayari ujumbe umeshawafikia IGP Solomon Zirro na Naibu Kamishna Mamboleo, muda wowote kuanzia sasa moto utawaka. Kuhusu Kamishna Omalla na Mr. Oduya ni kama tulivyokubaliana, tusubiri kwanza,” Tom alisema na kumfanya Tunu aachie tabasamu pana la ushindi.

“Okay, tuwasiliane...” Tunu alisema na kukata simu, muda huohuo akawaona wanaume wawili waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki wakipita jirani na ile nyumba, Tunu aliweza kumtambua mtu aliyekuwa akiendesha ile pikipiki licha ya kuwa alikuwa amevaa mavazi yaliyomficha, miwani mikubwa ya jua iliyofunika macho yake na chapeo (helmet) kichwani. Alikuwa Spoiler.

Ile pikipiki ilipita mbele ya ile nyumba pasipo kusimama, hata hivyo wale watu walitupa macho yao kuangalia kwenye ile nyumba katika namna ya kuyachunguza mazingira ya ile nyumba, pikipiki ikaelekea mbele zaidi ikipita kwenye njia nyembamba iliyopita katikati ya vichaka vidogovidogo. Tunu alijua kuwa wale watu walikuwa wakitafuta namna ya kuingia ndani kwa kusoma mazingira. Hakuwa na shaka yoyote kuwa walikwishagundua kuwa wenzao walioingia ndani walikuwa kwenye hatari, huenda ndiyo maana waliamua kuwazima vifaa vya mawasiliano.

“Bob, unanikopi?” Tunu aliwasiliana na Bob ili kumpa taarifa.

“Nakukopi, nadhani na wewe umeona nilichokiona. Ndege wawili wanaruka jirani na kiota, au siyo?” Bob alisema kwa sauti ya chini yenye kila aina ya tahadhari.

“Yap! Basi endelea kufuatilia huko mbele na inabidi tuongeze umakini zaidi,” Tunu alisema huku akitazama upande ilikoishia ile pikipiki, hakusikia tena muungurumo wake.

“Usijali, endapo wakiingia tu kwenye kiota basi watakuwa asusa...”

“Na lazima wawe asusa!” Tunu akadakia kisha akageuza shingo yake kutazama huku na huko kwa makini. “Lazima wanase kwani kila kitu kipo kama tulivyopanga.”

“Basi vema...” Bob alisema na kusita kidogo. “Namwona ndege mmoja akirejea taratibu,” Bob alisema kwa tahadhari.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali Mweweso Songa Heri esiankiki mnadhimu mkuu wa jf red apple the-sniper MR KUO dan oseko Jackal kuku mweus mtugani wa wapi huyo chiqutitta ndukulusudicho ADK aggyd BAHARI J

NB: Litro 👩
 
Taxi - (156)

Okay! Nakukopi, endelea kufuatilia na ninaomba uzidishe umakini!” Tunu alisema na mara akamwona Spoiler akitembea kwa tahadhari akipita eneo la nyuma ya ile nyumba. Eneo alilopita lilikuwa kama mita ishirini na tano tu kutoka ilipo nyumba ile. Hakuwa na pikipiki, hivyo Tunu aliweza kubaini kuwa waliiacha pikipiki yao sehemu na kuamua kurudi kwa miguu wakiwa wamejigawa, mmoja akielekea upande wa nyuma ya ile nyumba na mwingine upande wa mbele kisha wakakutanie ndani.

Tunu aliweza kugundua kuwa Spoiler alikuwa amevaa kitu fulani sikioni kwake na alikuwa akiwasiliana na mwenzake katika kujuzana kinachoendelea.

Tunu alimtazama Spoiler kwa makini wakati akiisogelea ile nyumba, kisha kwa kutumia mbinu ya hali ya juu ya kikomando, alikwea ukuta na kurukia ndani pasipo kutoa kishindo, kisha alijibanza kwenye banda moja lililojengwa kwa ajili ya kufugia kuku kule nyuma, jirani na ule mti ambao Tunu alijificha. Kabla ya kufanya mjongeo wowote alitulia palepale akayatembeza macho yake kupeleleza mandhari ya ile nyumba, alipogundua kuwa kajificha mahala salama akawasiliana na mwenzake.

Muda mfupi tangu Spoiler awasiliane na mwenzake Tunu alimwona mwanamume mwingine akitumia mbinu ileile ya kikomando kuingia ndani ya uzio wa nyumba bila kishindo kisha akakimbilia kwenye mti mmoja mkubwa wa kivuli na kujificha. Hapo Tunu akagundua kuwa alikuwa anacheza na watu hatari wenye uzoefu mkubwa wa masuala ya kihalifu.

Wale watu waliendelea kujificha kwa muda mrefu huku wakionekana kuyasoma mazingira katika namna ya kujiridhisha na hali ya usalama wa eneo lile. Walistaajabu kuona hali ikiwa shwari kabisa. Hatimaye Spoiler akaondoka pale kwenye banda na kusogea upande wa kulia akiambaa na maua kuizunguka ile nyumba katika namna ya kupata uhakika wa hali ya usalama wa eneo lile, huku akifanya mjongeo makini wa utulivu akitoka eneo moja na kuhamia eneo jingine akiifuata baraza ndogo ya nyuma ya nyumba kwa tahadhari.

Wakati huo yule mwanamume mwingine aliendelea kujibanza palepale akiwa makini zaidi, bastola yake ilikuwa imetulia vyema kwenye kiganja cha mkono wake wa kushoto akiwa tayari kumlinda mwenzake endapo jambo lolote baya lingemtokea.

Kwa tahadhari Spoiler alifika katika baraza ya ile sehemu ya nyuma ya nyumba na kuanza kupanda ngazi chache za varandani kuelekea mlango wa nyuma. Alipoufikia ule mlango wa jikoni alianza kuchunguza, akashika kitasa na kukinyonga lakini mlango haukufunguka, hivyo akatumia pini maalumu kutengulia vitasa cha mlango na kuzama ndani haraka huku akiurudisha mlango. Alikuwa na kila aina ya tahadhari. Kisu mkononi na macho yakiwa yanazunguka huku na kule.

Alisimama pale jikoni na kwa namna ya ajabu akakumbana na harufu nzuri ya marashi. Alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu, lilikuwa kosa kubwa kwani alianza kuhisi akili yake ikiwa nzito na mwili ukimlegea, kabla hajajua afanye nini alidondoka sakafuni na mara usingizi mzito ukameza na kumteka kabisa.

Dakika mbili baadaye yule mwanamume mwingine alionekana akijaribu kuwasiliana na Spoiler bila mafanikio, upesi akafanya namna kuingia ndani lakini kwa tahadhari kubwa, bastola yake iliendelea kutulia vyema kwenye kiganja cha mkono wake wa kushoto akiwa tayari kwa lolote. Aliufungua mlango na kuusukuma huku akiyatupa macho yake kutazama ndani, akamwona Spoiler akiwa sakafuni amemezwa na usingizi mzito.

Yule mwanamume alishtuka sana, akakunja uso wake na macho yake aliyakodoa kwa hofu. Alishafahamu kuwa mambo yalikuwa yameenda kombo. Alitaka kugeuka ili arudi alikotoka lakini alikuwa amechelewa, kwani muda huohuo alihisi ubaridi wa bomba lililomgusa kisogoni. Ulikuwa ni mtutu wa bastola ndogo ya Tunu aina ya Glock 19M.

“Don’t try to do anything stupid, sitasita kukuua. Ingia mwenyewe ndani kimyakimya,” sauti kali ya Tunu ilimwamuru. Yule mwanamume alimfahamu vyema Tunu hivyo aliona hakutakiwa kufanya jambo lolote kwa pupa isipokuwa kutii amri hiyo kisha atafute namna ya kujiokoa. Alipoingia tu ndani ule mlango ukafungwa haraka. Yule mwanamume aliruka juu na kujiviringisha, akatua sakafuni nyuma ya jokofu kubwa huku akigeuka tayari kwa mapambano, bastola yake ikiwa tayari kwa lolote.

Alishangaa kuona akiwa peke yake na muda huohuo mwili wake ukianza kulegea baada ya kuvuta harufu nzuri ya marashi, hakuchukua muda akadondoka sakafuni huku akimezwa na usingizi mzito. Usingizi ambao usingemtoka hadi baada ya saa ishirini na nne.

* * * * *

Naibu Kamishna Mamboleo alikuwa ametulia tuli kwenye kiti chake ndani ya ofisini yake kubwa, alikuwa akiitazama video fupi ya mauaji ya kutisha kwenye runinga maalumu ya ofisini kwake. Alikuwa anaiangalia video ile kwa mara ya tatu kabla hajabaini kuwa haikuwa na kasoro yoyote bali ilikuwa na picha halisi ambazo hazikuchezewa.

Hata sauti alizokuwa amezisikia ndani ya ile CD aliamini kabisa kuwa zilikuwa ni sauti halisi za wahusika, kwani seti ile ya runinga aliyoitumia kuangalia na kusikiliza ilikuwa ni moja ya runinga zenye uwezo mkubwa wa kubaini kama sauti au picha hazikuwa halisi na ziliigizwa kwa kuwa ilikuwa imeunganishwa na mfumo maalumu wa intelijensia ya kidijitali kwa ajili ya kubaini mambo mbalimbali ya uhalifu wa kimtandao.

Naibu Kamishna Mamboleo alishusha pumzi za ndani kwa ndani, alikuwa amechanganyikiwa kwani video ile ilikuwa na sauti na picha zilizowahusisha watu wawili walioheshimika sana nchini: Kamishna Omalla, Mkuu wa Kamisheni ya Intelijensia wa Jeshi la Polisi na Mr. Oduya, bilionea mkubwa Afrika ambaye pia alikuwa akitajwa sana kumrithi Rais Yohana Funguo katika nafasi ya urais wa nchi.

Inaendelea...

NB: Litro 👩
 
Taxi - (157)

Aliichukua tena barua fupi iliyokuwa imeambatanishwa na ile CD, akaisoma kwa mara ya tatu. Bado ujumbe ulikuwa ni uleule, ujumbe mfupi lakini wenye uzito mkubwa, ikiwa imeandikwa kwa kompyuta:

Naibu Kamishna Mamboleo, pole sana na majukumu, naamini wewe na timu yako bado hamjafanikiwa kuwapata wahalifu japo naamini Inspekta Abel alishaanza kuujua ukweli, ndiyo maana wahalifu hao wakapanga kuyakatisha maisha yake.
Natumaini baada ya kuzisikiliza vyema sauti na kuitazama video hii fupi utabaini ni nani walio nyuma ya sakata la kuvamiwa Sammy na familia yake. Usijiulize video hii inahusianaje na tukio hilo au mimi nimeyabaini vipi haya, unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wahalifu papa wanatiwa mbaroni kisha nitakupa ushahidi mwingine mzito kuhusu mtandao wote wa uhalifu unaowahusisha baadhi ya askari wako wasio waaminifu ingawa wewe unawaamini. Pia usisahau kuwasiliana na IGP Solomon Zirro kwa taarifa zaidi.

Ni mimi raia mzalendo.


Naibu Kamishna Mamboleo alihisi mwili wake ukimtetemeka, akili yake ilijaribu kukataa kabisa kukubaliana na kile alichokuwa amekiona kwenye ile video, alichokuwa amekisikia toka kwenye ile CD na hata ujumbe ule aliousoma, akihisi labda alikuwa ndotoni. Hali ile ikafanya jasho jepesi lianze kumtoka usoni huku mapigo ya moyo wake yakianza kwenda mbio isivyo kawaida.

Alinyanyua simu ya mezani kwake mara mbili akitaka kumpigia simu Inspekta Jenerali wa Polisi, Solomon Zirro, lakini mar azote mbili alionesha kusita sana, hivyo akataka kwanza ajiridhishe kabla hajafanya chochote. Aliinyanyua simu kwa mara ya tatu na kubonyeza namba za katibu muhtasi wake, simu ikaita mara moja na kupokelewa. “Asia, nakuhitaji mara moja ofisini kwangu,” Naibu Kamishna Mamboleo alisema na kuirudisha simu sehemu yake.

Dakika iliyofuata katibu wake, Asia Bilali, mwanamama mwenye umbo kubwa la kuvutia likiwa limesheheni vema na kunesanesa, akiwa amevaa sare maalumu ya kazi aliingia na kusimama kwa ukakamavu mbele yake. Naibu Kamishna Mamboleo alimtazama Asia kwa makini kama aliyekuwa akiyatafuta maneno ya kumweleza. Aliinua ile bahasha iliyokuwa imehifadhi ile CD na kumwonesha Asia. “Ni nani aliyeileta hii bahasha?”

“Ililetwa na mwanamume mmoja anayetoka kampuni ya kusafirisha vifurushi ya Posta...” Asia alijibu huku akimtazama Naibu Kamishna Mamboleo kwa mshangao, kwani alikuwa ameulizwa swali lilelile kwa mara ya tatu tangu alipomkabidhi bosi wake ile bahasha.

Hata hivyo, kilichomshangaza zaidi Asia ni baada ya kumwona Naibu Kamishna Mamboleo akiwa na uso uliosawajika huku jasho jepesi likimtoka usoni.

“Kuna tatizo lolote, afande?” Asia aliuliza huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wa Naibu Kamishna Mamboleo akijaribu kuyasoma mawazo yake.

“Hakuna tatizo. Unaweza kwenda kuendelea na kazi,” Naibu Kamishna Mamboleo alimwambia Asia na kujiegemeza kwenye kiti. Asia alizidi kushangaa, hata hivyo alitoka na kumwacha bosi wake akiwa ametahayari. Mara simu ya meza kwa Naibu Kamishna Mamboleo ikaanza kuita kwa fujo. Naibu Kamishna Mamboleo aliitazama ile simu kwa wasiwasi kisha akanyanyua kiwambo cha simu na kupeleka sikioni.

“Naibu Kamishna Mamboleo, naongea na nani?” Naibu Kamishna Mamboleo alijitambulisha na kumuuliza mpigaji simu.
“IGP Zirro hapa, habari yako, Naibu Kamishna!” sauti kavu ya Solomon Zirro ilipenya kwenye ngoma ya sikio la Naibu Kamishna Mamboleo na kumfanya ahisi mwili wake ukizizima kama aliyepigwa na shoti ya umeme.

“Nzuri, afande!” Naibu Kamishna Mamboleo aliitikia salamu ile kwa sauti iliyotetemeka kidogo.

“Nakuhitaji ofisini kwangu haraka iwezekanavyo,” Solomon Zirro alisema na kukata simu.

Naibu Kamishna Mamboleo hakusubiri. Asubiri nini wakati alikwishajua kuwa hali haikuwa shwari kabisa! Aliinuka na kuchukua ile CD pamoja na barua yake, akatoka nje na kuelekea kwenye gari lake, alijipakia na kumtaka dereva wake ampeleke makao makuu ya polisi. Dereva alilitia gari moto na kufunga safari hiyo ya dharura hadi makao makuu ya polisi.

Naibu Kamishna Mamboleo aliteremka haraka na kuelekea ofisini kwa Solomon Zirro akimwacha dereva wake akitafuta sehemu ya kuliegesha gari lake. Naibu Kamishna Mamboleo alielekezwa kuingia katika chumba maalumu cha faragha. Humo aliwakuta Solomon Zirro na Kamishna Adili Mkwizu, Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, wakiwa wameketi wakitafakari.
Naibu Kamishna Mamboleo aliwasalimia kijeshi ingawa moyo wake ulikuwa ukidunda kwa hofu. Aliangalia kiti kilichokuwa tupu, akaketi.

“Umeshakutana na ujumbe huu?” Solomon Zirro alimuuliza Naibu Kamishna Mamboleo mara tu alipoketi huku akimsogezea CD kama ile aliyotoka kuitazama ofisini kwake ikiwa imeambatanishwa na barua fupi kama ile aliyokuwa nayo.

Naibu Kamishna Mamboleo aliitazama na kuitambua mara moja. Hakuwa na haja ya kuvipokea kwani na yeye alikuwa anavyo mkononi, alibetua kichwa chake kukubali huku akimwonesha IGP Solomon Zirro hata yeye alikuwa amepelekewa ofisini kwake.

“Ujumbe umeshanifikia, afande,” Naibu Kamishna Mamboleo alisema na kushusha pumzi ndefu.

“Ulimwona mtu aliyeleta?” IGP Solomon Zirro aliuliza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Naibu Kamishna Mamboleo.

“Hapana, alimkabidhi katibu wangu kabla haijanifikia,” Naibu Kamishna Mamboleo alijibu na kumeza mate kutowesha koo lake lililoanza kukauka.

“Unasemaje kuhusu kilichomo ndani yake, kina ukweli wowote?” Solomon Zirro aliuliza tena huku akizidi kumkazia macho Naibu Kamishna Mamboleo.

“Sina shaka kabisa, afande, kuwa niliyoyasikia na kuyashuhudia yote ni halisi kabisa.”

“Hata sisi tumebaini hivyo. Hata hivyo, tunajiuliza, ni nani aliyerekodi matukio haya na kwa nini alikaa nayo siku zote hizo!” Solomon Zirro alisema na kumtupia jicho Kamishna Mkwizu kisha akashusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Ni dhahiri kuwa mtu aliyerekodi matukio haya anayajua mengi kuhusu huu uhalifu unaoendelea sasa na pengine yupo hatua zaidi ya moja mbele ya jeshi la polisi. Kilichotushtua zaidi ni ushiriki wa Kamishna Omalla,” Solomon Zirro alisema na kuongeza. “Sasa nauona ugumu uliokuwa ukiupata katika kuumaliza uhalifu hapa jijini, maana mtu muhimu kama Kamishna Omalla anaposhiriki kwenye mambo haya ni rahisi sana kuingilia na kuvuruga upelelezi!”

Inaendelea...

NB: Litro 👩
 
Taxi - (158)

“Hata hivyo, kwa sasa naomba mambo haya yabaki kuwa siri kati yetu watatu, ingawa sina uhakika kama hakuna mwingine zaidi yetu anayejua kuhusu jambo hili. Nilichowaitia hapa ni kutaka twende kwa mheshimiwa Rais tukazungumze naye kuhusu jambo hili,” Solomon Zirro alisema kwa msisitizo.

* * * * *

Saa nane na dakika ishirini na tano mchana, Mr. Oduya alikuwa ameketi katika kiti chake kikubwa cha kiofisi, ofisini kwake katika jengo la makao makuu ya ofisi za The Splendid Group, barabara ya Bagamoyo. Alionekana kuwaza mbali sana na muda wote alikuwa akiitupia jicho saa yake ya mkononi.

Moyo wake ulikuwa ukimdunda kwa nguvu, kwa mara ya tatu sasa tangu alipoanza harakati zake wazo la kutaka kutoroka nchi lilizidi kupata nafasi akilini mwake, safari hii alijikuta akiwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa. Sasa alipanga kuondoka nchini na kwenda Canada, ambako angekaa huko hadi pale ambapo mambo yangeonesha kutulia.

Moyoni mwake, hofu ilikuwa kubwa ikitishia kuutawala moyo wake na sauti fulani ndani yake ilikuwa ikimweleza kuwa mambo yalikuwa yamekwenda mrama. Kwa mara ya kwanza tangu alipomfahamu Silas Polea, Mr. Oduya alijikuta akianza kumlaumu sana kijana huyo kwa kumwingiza katika matatizo makubwa, ambayo hakujua nini ingekuwa hatima yake. Hii ilitokana na kukaidi agizo lake la kuliteketeza lile gari la kizamani aina ya Cadillac DeVille.

Siku zote Silas alikuwa kijana mtiifu kwake na kila kazi aliyotumwa kuifanya aliifanya kwa uaminifu na umakini mkubwa, isipokuwa hii moja tu. Mr. Oduya hakuwa na shaka naye, hasa kwa kukumbuka mambo mengi aliyowahi kumfanyia. Hata hivyo, hofu kubwa ilishaanza kumshika baada ya kuona kuwa hadi muda ule alikuwa hajapokea taarifa zozote kuhusu Tunu. Si Silas, Robert Kamau wala Job aliyekuwa akipatikana kwenye simu! Ni hayo yaliyomtia mashaka ingawa aliamini kuwa siku ile ingeisha kwa furaha kubwa.

Aliichukua tena simu yake ya mkononi na kupiga namba ya Spoiler, bado sauti ilikuwa ileile kwamba namba hiyo ilikuwa haipatikani. Akashusha pumzi. Kabla hajajua afanye nini, mlango wa ofisi yake uligongwa mara moja na kufunguliwa, katibu muhtasi wake akaingia akiwa ameshika bahasha ya khaki yenye ukubwa wa wastani iliyobandikwa karatasi ndogo yenye maandishi ya Express Mail na ilikuwa na nembo ya Posta, akamkabidhi Mr. Oduya.

Mr. Oduya aliipokea kwa mashaka na kuitazama kwa makini. Hakujua kwa nini alikuwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa, labda kwa kuwa hadi muda ule hakuwa amepata taarifa zozote kuhusu watu wake.

“Nani kaileta hii?” Mr. Oduya alimuuliza katibu wake huku akiiangalia ile bahasha kwa makini.

“Imeletwa na kaka mmoja wa Posta.”

“Vyema,” Mr. Oduya alisema na kumruhusu katibu wake aondoke kurudi ofisini kwake, akaanza kuifungua harakaharaka na kutoa nakala moja ya CD iliyoambatanishwa na barua ambayo iliyavuta macho yake kwa hofu kubwa. Mr. Oduya aliyapitisha macho yake harakaharaka kuisoma ile barua. Ilikuwa imeandikwa hivi:

Mr. Oduya, sidhani kama bado una ndoto ya kuendelea na harakati zako chafu zenye kuleta maafa kwa watu wasio na hatia ili kuupata Urais wa nchi hii tukufu. Kama bado una ndoto hiyo nakushauri uachane nayo na ujitokeze kuomba radhi hadharani kisha ujikabidhi mwenyewe polisi kabla ya saa kumi jioni. Usipofanya hivyo hadi muda huo nitakusaidia kufanya hivyo ili kukuonesha kuwa sina mzaha. Si kwamba nakutisha, pengine itapendeza kama utaitazama kwanza video fupi ndani ya CD hiyo niliyokutumia na usikilize sauti zilizomo ili kubaini ni kwa kiasi gani ninaufahamu mtandao wako wote wa uhalifu, orodha yenu, picha zenu, maongezi yenu ya simu na harakati zenu chafu. Usijiulize nimewezaje kupata video hii na sauti zenu, kwani unaelewa fika uwezo wangu katika mambo ya kishushushu.

Tunu Michael.


Mr. Oduya aliirudia kuisoma barua ile mara tatu lakini bado asiyaamini yale aliyokuwa akiyasoma, alidhani labda huo ulikuwa mtego wa Tunu ili kumkamatisha. Hata hivyo, alihisi mwili wake wote ukitetemeka. Bila kusubiri aliichukua ile CD iliyoambatanishwa na ile barua na kuitumbukiza kwenye kompyuta yake.

Aliyoyashuhudia na kuyasikia yaliyafanya mapigo ya moyo wake yaende mbio isivyo kawaida na kijasho chembamba kikaanza kumtoka, hakuwa na uwezo wa kuendelea kukanusha kuwa Tunu aliyafahamu mengi kuhusu harakati zake chafu na asingesita kuchukua hatua kama alivyoahidi kwenye barua yake.

Akiwa bado amechanganyikiwa, moyo wake ukampasuka mara tu simu yake ya mkononi ilipoanza kuita kwa fujo, aliinyanyua na kuitazama kwa makini, ilikuwa namba ya Dk. Masanja. Mr. Oduya aliipokea haraka na kuipeleka sikioni.

“Hallo!” Mr. Oduya aliongea kwa sauti ya kutetemeka mara baada ya kuiweka kwenye sikio lake kiasi kwamba alianza kujishangaa.

“Vipi umesikia?” sauti ya wasiwasi ya Dk. Masanja ilisikika toka upande wa pili wa simu.

“Kusikia nini!” Mr. Oduya aliuliza kwa mshangao.

“Kilichompata rafiki yako, Kamishna Omalla. Amejipiga risasi ya kichwa ofisini kwake muda mfupi uliopita,” Dk. Masanja alisema kwa huzuni.

What! Ameji...” Mr. Oduya alitaka kusema lakini akahisi maneno yakikwama kooni. Donge lenye mchanganyiko wa hasira na huzuni lilimkaba kooni na kumfanya ahisi koo lake likikauka ghafla huku nywele zikimsimama kichwani kwa hofu. “Hali yake inaendeleaje?” aliuliza huku akihisi moyo wake ukisitisha kazi yake kwa muda.

“Amekufa! Risasi imefumua kabisa kichwa chake...” Dk. Masanja alisema.

Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.

Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.

Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa ni bomu la kutegeshwa lililokuwa mbioni kulipuka.

Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.

Mambo bado ni 🔥🔥🔥 kwelikweli. Ili kujua mwisho wake, usichoke kufuatilia hadi mwisho...

NB: Litro 👩
 
Taxi - (158)

“Hata hivyo, kwa sasa naomba mambo haya yabaki kuwa siri kati yetu watatu, ingawa sina uhakika kama hakuna mwingine zaidi yetu anayejua kuhusu jambo hili. Nilichowaitia hapa ni kutaka twende kwa mheshimiwa Rais tukazungumze naye kuhusu jambo hili,” Solomon Zirro alisema kwa msisitizo.

* * * * *

Saa nane na dakika ishirini na tano mchana, Mr. Oduya alikuwa ameketi katika kiti chake kikubwa cha kiofisi, ofisini kwake katika jengo la makao makuu ya ofisi za The Splendid Group, barabara ya Bagamoyo. Alionekana kuwaza mbali sana na muda wote alikuwa akiitupia jicho saa yake ya mkononi.

Moyo wake ulikuwa ukimdunda kwa nguvu, kwa mara ya tatu sasa tangu alipoanza harakati zake wazo la kutaka kutoroka nchi lilizidi kupata nafasi akilini mwake, safari hii alijikuta akiwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa. Sasa alipanga kuondoka nchini na kwenda Canada, ambako angekaa huko hadi pale ambapo mambo yangeonesha kutulia.

Moyoni mwake, hofu ilikuwa kubwa ikitishia kuutawala moyo wake na sauti fulani ndani yake ilikuwa ikimweleza kuwa mambo yalikuwa yamekwenda mrama. Kwa mara ya kwanza tangu alipomfahamu Silas Polea, Mr. Oduya alijikuta akianza kumlaumu sana kijana huyo kwa kumwingiza katika matatizo makubwa, ambayo hakujua nini ingekuwa hatima yake. Hii ilitokana na kukaidi agizo lake la kuliteketeza lile gari la kizamani aina ya Cadillac DeVille.

Siku zote Silas alikuwa kijana mtiifu kwake na kila kazi aliyotumwa kuifanya aliifanya kwa uaminifu na umakini mkubwa, isipokuwa hii moja tu. Mr. Oduya hakuwa na shaka naye, hasa kwa kukumbuka mambo mengi aliyowahi kumfanyia. Hata hivyo, hofu kubwa ilishaanza kumshika baada ya kuona kuwa hadi muda ule alikuwa hajapokea taarifa zozote kuhusu Tunu. Si Silas, Robert Kamau wala Job aliyekuwa akipatikana kwenye simu! Ni hayo yaliyomtia mashaka ingawa aliamini kuwa siku ile ingeisha kwa furaha kubwa.

Aliichukua tena simu yake ya mkononi na kupiga namba ya Spoiler, bado sauti ilikuwa ileile kwamba namba hiyo ilikuwa haipatikani. Akashusha pumzi. Kabla hajajua afanye nini, mlango wa ofisi yake uligongwa mara moja na kufunguliwa, katibu muhtasi wake akaingia akiwa ameshika bahasha ya khaki yenye ukubwa wa wastani iliyobandikwa karatasi ndogo yenye maandishi ya Express Mail na ilikuwa na nembo ya Posta, akamkabidhi Mr. Oduya.

Mr. Oduya aliipokea kwa mashaka na kuitazama kwa makini. Hakujua kwa nini alikuwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa, labda kwa kuwa hadi muda ule hakuwa amepata taarifa zozote kuhusu watu wake.

“Nani kaileta hii?” Mr. Oduya alimuuliza katibu wake huku akiiangalia ile bahasha kwa makini.

“Imeletwa na kaka mmoja wa Posta.”

“Vyema,” Mr. Oduya alisema na kumruhusu katibu wake aondoke kurudi ofisini kwake, akaanza kuifungua harakaharaka na kutoa nakala moja ya CD iliyoambatanishwa na barua ambayo iliyavuta macho yake kwa hofu kubwa. Mr. Oduya aliyapitisha macho yake harakaharaka kuisoma ile barua. Ilikuwa imeandikwa hivi:

Mr. Oduya, sidhani kama bado una ndoto ya kuendelea na harakati zako chafu zenye kuleta maafa kwa watu wasio na hatia ili kuupata Urais wa nchi hii tukufu. Kama bado una ndoto hiyo nakushauri uachane nayo na ujitokeze kuomba radhi hadharani kisha ujikabidhi mwenyewe polisi kabla ya saa kumi jioni. Usipofanya hivyo hadi muda huo nitakusaidia kufanya hivyo ili kukuonesha kuwa sina mzaha. Si kwamba nakutisha, pengine itapendeza kama utaitazama kwanza video fupi ndani ya CD hiyo niliyokutumia na usikilize sauti zilizomo ili kubaini ni kwa kiasi gani ninaufahamu mtandao wako wote wa uhalifu, orodha yenu, picha zenu, maongezi yenu ya simu na harakati zenu chafu. Usijiulize nimewezaje kupata video hii na sauti zenu, kwani unaelewa fika uwezo wangu katika mambo ya kishushushu.

Tunu Michael.


Mr. Oduya aliirudia kuisoma barua ile mara tatu lakini bado asiyaamini yale aliyokuwa akiyasoma, alidhani labda huo ulikuwa mtego wa Tunu ili kumkamatisha. Hata hivyo, alihisi mwili wake wote ukitetemeka. Bila kusubiri aliichukua ile CD iliyoambatanishwa na ile barua na kuitumbukiza kwenye kompyuta yake.

Aliyoyashuhudia na kuyasikia yaliyafanya mapigo ya moyo wake yaende mbio isivyo kawaida na kijasho chembamba kikaanza kumtoka, hakuwa na uwezo wa kuendelea kukanusha kuwa Tunu aliyafahamu mengi kuhusu harakati zake chafu na asingesita kuchukua hatua kama alivyoahidi kwenye barua yake.

Akiwa bado amechanganyikiwa, moyo wake ukampasuka mara tu simu yake ya mkononi ilipoanza kuita kwa fujo, aliinyanyua na kuitazama kwa makini, ilikuwa namba ya Dk. Masanja. Mr. Oduya aliipokea haraka na kuipeleka sikioni.

“Hallo!” Mr. Oduya aliongea kwa sauti ya kutetemeka mara baada ya kuiweka kwenye sikio lake kiasi kwamba alianza kujishangaa.

“Vipi umesikia?” sauti ya wasiwasi ya Dk. Masanja ilisikika toka upande wa pili wa simu.

“Kusikia nini!” Mr. Oduya aliuliza kwa mshangao.

“Kilichompata rafiki yako, Kamishna Omalla. Amejipiga risasi ya kichwa ofisini kwake muda mfupi uliopita,” Dk. Masanja alisema kwa huzuni.

What! Ameji...” Mr. Oduya alitaka kusema lakini akahisi maneno yakikwama kooni. Donge lenye mchanganyiko wa hasira na huzuni lilimkaba kooni na kumfanya ahisi koo lake likikauka ghafla huku nywele zikimsimama kichwani kwa hofu. “Hali yake inaendeleaje?” aliuliza huku akihisi moyo wake ukisitisha kazi yake kwa muda.

“Amekufa! Risasi imefumua kabisa kichwa chake...” Dk. Masanja alisema.

Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.

Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.

Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa ni bomu la kutegeshwa lililokuwa mbioni kulipuka.

Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.

Mambo bado ni kwelikweli. Ili kujua mwisho wake, usichoke kufuatilia hadi mwisho...

NB: Litro
Mbio za sakafuni,barikiwa Bishop Hiluka
 
Taxi - (158)

“Hata hivyo, kwa sasa naomba mambo haya yabaki kuwa siri kati yetu watatu, ingawa sina uhakika kama hakuna mwingine zaidi yetu anayejua kuhusu jambo hili. Nilichowaitia hapa ni kutaka twende kwa mheshimiwa Rais tukazungumze naye kuhusu jambo hili,” Solomon Zirro alisema kwa msisitizo.

* * * * *

Saa nane na dakika ishirini na tano mchana, Mr. Oduya alikuwa ameketi katika kiti chake kikubwa cha kiofisi, ofisini kwake katika jengo la makao makuu ya ofisi za The Splendid Group, barabara ya Bagamoyo. Alionekana kuwaza mbali sana na muda wote alikuwa akiitupia jicho saa yake ya mkononi.

Moyo wake ulikuwa ukimdunda kwa nguvu, kwa mara ya tatu sasa tangu alipoanza harakati zake wazo la kutaka kutoroka nchi lilizidi kupata nafasi akilini mwake, safari hii alijikuta akiwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa. Sasa alipanga kuondoka nchini na kwenda Canada, ambako angekaa huko hadi pale ambapo mambo yangeonesha kutulia.

Moyoni mwake, hofu ilikuwa kubwa ikitishia kuutawala moyo wake na sauti fulani ndani yake ilikuwa ikimweleza kuwa mambo yalikuwa yamekwenda mrama. Kwa mara ya kwanza tangu alipomfahamu Silas Polea, Mr. Oduya alijikuta akianza kumlaumu sana kijana huyo kwa kumwingiza katika matatizo makubwa, ambayo hakujua nini ingekuwa hatima yake. Hii ilitokana na kukaidi agizo lake la kuliteketeza lile gari la kizamani aina ya Cadillac DeVille.

Siku zote Silas alikuwa kijana mtiifu kwake na kila kazi aliyotumwa kuifanya aliifanya kwa uaminifu na umakini mkubwa, isipokuwa hii moja tu. Mr. Oduya hakuwa na shaka naye, hasa kwa kukumbuka mambo mengi aliyowahi kumfanyia. Hata hivyo, hofu kubwa ilishaanza kumshika baada ya kuona kuwa hadi muda ule alikuwa hajapokea taarifa zozote kuhusu Tunu. Si Silas, Robert Kamau wala Job aliyekuwa akipatikana kwenye simu! Ni hayo yaliyomtia mashaka ingawa aliamini kuwa siku ile ingeisha kwa furaha kubwa.

Aliichukua tena simu yake ya mkononi na kupiga namba ya Spoiler, bado sauti ilikuwa ileile kwamba namba hiyo ilikuwa haipatikani. Akashusha pumzi. Kabla hajajua afanye nini, mlango wa ofisi yake uligongwa mara moja na kufunguliwa, katibu muhtasi wake akaingia akiwa ameshika bahasha ya khaki yenye ukubwa wa wastani iliyobandikwa karatasi ndogo yenye maandishi ya Express Mail na ilikuwa na nembo ya Posta, akamkabidhi Mr. Oduya.

Mr. Oduya aliipokea kwa mashaka na kuitazama kwa makini. Hakujua kwa nini alikuwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa, labda kwa kuwa hadi muda ule hakuwa amepata taarifa zozote kuhusu watu wake.

“Nani kaileta hii?” Mr. Oduya alimuuliza katibu wake huku akiiangalia ile bahasha kwa makini.

“Imeletwa na kaka mmoja wa Posta.”

“Vyema,” Mr. Oduya alisema na kumruhusu katibu wake aondoke kurudi ofisini kwake, akaanza kuifungua harakaharaka na kutoa nakala moja ya CD iliyoambatanishwa na barua ambayo iliyavuta macho yake kwa hofu kubwa. Mr. Oduya aliyapitisha macho yake harakaharaka kuisoma ile barua. Ilikuwa imeandikwa hivi:

Mr. Oduya, sidhani kama bado una ndoto ya kuendelea na harakati zako chafu zenye kuleta maafa kwa watu wasio na hatia ili kuupata Urais wa nchi hii tukufu. Kama bado una ndoto hiyo nakushauri uachane nayo na ujitokeze kuomba radhi hadharani kisha ujikabidhi mwenyewe polisi kabla ya saa kumi jioni. Usipofanya hivyo hadi muda huo nitakusaidia kufanya hivyo ili kukuonesha kuwa sina mzaha. Si kwamba nakutisha, pengine itapendeza kama utaitazama kwanza video fupi ndani ya CD hiyo niliyokutumia na usikilize sauti zilizomo ili kubaini ni kwa kiasi gani ninaufahamu mtandao wako wote wa uhalifu, orodha yenu, picha zenu, maongezi yenu ya simu na harakati zenu chafu. Usijiulize nimewezaje kupata video hii na sauti zenu, kwani unaelewa fika uwezo wangu katika mambo ya kishushushu.

Tunu Michael.


Mr. Oduya aliirudia kuisoma barua ile mara tatu lakini bado asiyaamini yale aliyokuwa akiyasoma, alidhani labda huo ulikuwa mtego wa Tunu ili kumkamatisha. Hata hivyo, alihisi mwili wake wote ukitetemeka. Bila kusubiri aliichukua ile CD iliyoambatanishwa na ile barua na kuitumbukiza kwenye kompyuta yake.

Aliyoyashuhudia na kuyasikia yaliyafanya mapigo ya moyo wake yaende mbio isivyo kawaida na kijasho chembamba kikaanza kumtoka, hakuwa na uwezo wa kuendelea kukanusha kuwa Tunu aliyafahamu mengi kuhusu harakati zake chafu na asingesita kuchukua hatua kama alivyoahidi kwenye barua yake.

Akiwa bado amechanganyikiwa, moyo wake ukampasuka mara tu simu yake ya mkononi ilipoanza kuita kwa fujo, aliinyanyua na kuitazama kwa makini, ilikuwa namba ya Dk. Masanja. Mr. Oduya aliipokea haraka na kuipeleka sikioni.

“Hallo!” Mr. Oduya aliongea kwa sauti ya kutetemeka mara baada ya kuiweka kwenye sikio lake kiasi kwamba alianza kujishangaa.

“Vipi umesikia?” sauti ya wasiwasi ya Dk. Masanja ilisikika toka upande wa pili wa simu.

“Kusikia nini!” Mr. Oduya aliuliza kwa mshangao.

“Kilichompata rafiki yako, Kamishna Omalla. Amejipiga risasi ya kichwa ofisini kwake muda mfupi uliopita,” Dk. Masanja alisema kwa huzuni.

What! Ameji...” Mr. Oduya alitaka kusema lakini akahisi maneno yakikwama kooni. Donge lenye mchanganyiko wa hasira na huzuni lilimkaba kooni na kumfanya ahisi koo lake likikauka ghafla huku nywele zikimsimama kichwani kwa hofu. “Hali yake inaendeleaje?” aliuliza huku akihisi moyo wake ukisitisha kazi yake kwa muda.

“Amekufa! Risasi imefumua kabisa kichwa chake...” Dk. Masanja alisema.

Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.

Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.

Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa ni bomu la kutegeshwa lililokuwa mbioni kulipuka.

Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.

Mambo bado ni 🔥🔥🔥 kwelikweli. Ili kujua mwisho wake, usichoke kufuatilia hadi mwisho...

NB: Litro 👩
We jamaa ni nomaaa
 
Taxi - (158)

“Hata hivyo, kwa sasa naomba mambo haya yabaki kuwa siri kati yetu watatu, ingawa sina uhakika kama hakuna mwingine zaidi yetu anayejua kuhusu jambo hili. Nilichowaitia hapa ni kutaka twende kwa mheshimiwa Rais tukazungumze naye kuhusu jambo hili,” Solomon Zirro alisema kwa msisitizo.

* * * * *

Saa nane na dakika ishirini na tano mchana, Mr. Oduya alikuwa ameketi katika kiti chake kikubwa cha kiofisi, ofisini kwake katika jengo la makao makuu ya ofisi za The Splendid Group, barabara ya Bagamoyo. Alionekana kuwaza mbali sana na muda wote alikuwa akiitupia jicho saa yake ya mkononi.

Moyo wake ulikuwa ukimdunda kwa nguvu, kwa mara ya tatu sasa tangu alipoanza harakati zake wazo la kutaka kutoroka nchi lilizidi kupata nafasi akilini mwake, safari hii alijikuta akiwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa. Sasa alipanga kuondoka nchini na kwenda Canada, ambako angekaa huko hadi pale ambapo mambo yangeonesha kutulia.

Moyoni mwake, hofu ilikuwa kubwa ikitishia kuutawala moyo wake na sauti fulani ndani yake ilikuwa ikimweleza kuwa mambo yalikuwa yamekwenda mrama. Kwa mara ya kwanza tangu alipomfahamu Silas Polea, Mr. Oduya alijikuta akianza kumlaumu sana kijana huyo kwa kumwingiza katika matatizo makubwa, ambayo hakujua nini ingekuwa hatima yake. Hii ilitokana na kukaidi agizo lake la kuliteketeza lile gari la kizamani aina ya Cadillac DeVille.

Siku zote Silas alikuwa kijana mtiifu kwake na kila kazi aliyotumwa kuifanya aliifanya kwa uaminifu na umakini mkubwa, isipokuwa hii moja tu. Mr. Oduya hakuwa na shaka naye, hasa kwa kukumbuka mambo mengi aliyowahi kumfanyia. Hata hivyo, hofu kubwa ilishaanza kumshika baada ya kuona kuwa hadi muda ule alikuwa hajapokea taarifa zozote kuhusu Tunu. Si Silas, Robert Kamau wala Job aliyekuwa akipatikana kwenye simu! Ni hayo yaliyomtia mashaka ingawa aliamini kuwa siku ile ingeisha kwa furaha kubwa.

Aliichukua tena simu yake ya mkononi na kupiga namba ya Spoiler, bado sauti ilikuwa ileile kwamba namba hiyo ilikuwa haipatikani. Akashusha pumzi. Kabla hajajua afanye nini, mlango wa ofisi yake uligongwa mara moja na kufunguliwa, katibu muhtasi wake akaingia akiwa ameshika bahasha ya khaki yenye ukubwa wa wastani iliyobandikwa karatasi ndogo yenye maandishi ya Express Mail na ilikuwa na nembo ya Posta, akamkabidhi Mr. Oduya.

Mr. Oduya aliipokea kwa mashaka na kuitazama kwa makini. Hakujua kwa nini alikuwa katika hali ya wasiwasi na mashaka makubwa, labda kwa kuwa hadi muda ule hakuwa amepata taarifa zozote kuhusu watu wake.

“Nani kaileta hii?” Mr. Oduya alimuuliza katibu wake huku akiiangalia ile bahasha kwa makini.

“Imeletwa na kaka mmoja wa Posta.”

“Vyema,” Mr. Oduya alisema na kumruhusu katibu wake aondoke kurudi ofisini kwake, akaanza kuifungua harakaharaka na kutoa nakala moja ya CD iliyoambatanishwa na barua ambayo iliyavuta macho yake kwa hofu kubwa. Mr. Oduya aliyapitisha macho yake harakaharaka kuisoma ile barua. Ilikuwa imeandikwa hivi:

Mr. Oduya, sidhani kama bado una ndoto ya kuendelea na harakati zako chafu zenye kuleta maafa kwa watu wasio na hatia ili kuupata Urais wa nchi hii tukufu. Kama bado una ndoto hiyo nakushauri uachane nayo na ujitokeze kuomba radhi hadharani kisha ujikabidhi mwenyewe polisi kabla ya saa kumi jioni. Usipofanya hivyo hadi muda huo nitakusaidia kufanya hivyo ili kukuonesha kuwa sina mzaha. Si kwamba nakutisha, pengine itapendeza kama utaitazama kwanza video fupi ndani ya CD hiyo niliyokutumia na usikilize sauti zilizomo ili kubaini ni kwa kiasi gani ninaufahamu mtandao wako wote wa uhalifu, orodha yenu, picha zenu, maongezi yenu ya simu na harakati zenu chafu. Usijiulize nimewezaje kupata video hii na sauti zenu, kwani unaelewa fika uwezo wangu katika mambo ya kishushushu.

Tunu Michael.


Mr. Oduya aliirudia kuisoma barua ile mara tatu lakini bado asiyaamini yale aliyokuwa akiyasoma, alidhani labda huo ulikuwa mtego wa Tunu ili kumkamatisha. Hata hivyo, alihisi mwili wake wote ukitetemeka. Bila kusubiri aliichukua ile CD iliyoambatanishwa na ile barua na kuitumbukiza kwenye kompyuta yake.

Aliyoyashuhudia na kuyasikia yaliyafanya mapigo ya moyo wake yaende mbio isivyo kawaida na kijasho chembamba kikaanza kumtoka, hakuwa na uwezo wa kuendelea kukanusha kuwa Tunu aliyafahamu mengi kuhusu harakati zake chafu na asingesita kuchukua hatua kama alivyoahidi kwenye barua yake.

Akiwa bado amechanganyikiwa, moyo wake ukampasuka mara tu simu yake ya mkononi ilipoanza kuita kwa fujo, aliinyanyua na kuitazama kwa makini, ilikuwa namba ya Dk. Masanja. Mr. Oduya aliipokea haraka na kuipeleka sikioni.

“Hallo!” Mr. Oduya aliongea kwa sauti ya kutetemeka mara baada ya kuiweka kwenye sikio lake kiasi kwamba alianza kujishangaa.

“Vipi umesikia?” sauti ya wasiwasi ya Dk. Masanja ilisikika toka upande wa pili wa simu.

“Kusikia nini!” Mr. Oduya aliuliza kwa mshangao.

“Kilichompata rafiki yako, Kamishna Omalla. Amejipiga risasi ya kichwa ofisini kwake muda mfupi uliopita,” Dk. Masanja alisema kwa huzuni.

What! Ameji...” Mr. Oduya alitaka kusema lakini akahisi maneno yakikwama kooni. Donge lenye mchanganyiko wa hasira na huzuni lilimkaba kooni na kumfanya ahisi koo lake likikauka ghafla huku nywele zikimsimama kichwani kwa hofu. “Hali yake inaendeleaje?” aliuliza huku akihisi moyo wake ukisitisha kazi yake kwa muda.

“Amekufa! Risasi imefumua kabisa kichwa chake...” Dk. Masanja alisema.

Mr. Oduya alihisi kama mwili wake ulikuwa ukicharangwa kwa visu vikali na kubanikwa katika moto mkubwa. Alihisi moto mkali sana ukitambaa kwenye mwili wake na ngozi yake ilikuwa inaungua na kumfanya kuhisi maumivu makali mno. Muda huohuo alihisi hasira kali zikiibuka ndani yake, chumba cha ofisi yake kilionekana kama kilichoshuka nyuzi kumi hivi na kuwa kifupi mno.

Mara simu yake ya mezani ikaanza kuita na kumzindua toka kwenye yale mawazo. Ndipo alipogundua kuwa ile simu ya mkononi ilikuwa bado ipo sikioni ingawa hakuwa akisikia tena kilichoongewa upande wa pili wa simu ile. Hakuweza kukumbuka ilichukua muda gani akiwa ameiweka ile simu sikioni huku mawazo yake yakiwa yamehama toka kwenye maongezi yake na Dk. Masanja hadi muda ule wakati simu ya mezani ilikuwa ikiita.

Hofu ilikuwa imemmeza kabisa, aliitazama ile simu ya mezani kwa wasiwasi huku akianza kuhisi jambo la hatari. Hata hivyo, hakutaka kuendelea kusubiri ile simu iendelee kuita zaidi kwani ilikuwa mbioni kukata baada ya kuita kwa muda mrefu. Hivyo akanyoosha mkono wake kivivuvivu ili kuipokea lakini kabla mkono haujaifikia ile simu ikakatika. Tukio lile likaiongeza hofu yake yake na hivyo akabaki akiikodolea macho ile simu kana kwamba lilikuwa ni bomu la kutegeshwa lililokuwa mbioni kulipuka.

Alianza kujiuliza, mpigaji wa simu ile angekuwa nani na angekuwa na shida gani muda ule, au ni yaleyale ya kupewa taarifa mbaya kuhusu Kamishna Omalla? Wakati akijiuliza mara ile simu ya mezani ikaanza kuita tena. Hakutaka iendelee kuita zaidi hivyo haraka akakinyakuwa kiwambo chake na kukiweka sikioni huku akiipa akili yake utulivu wa hali ya juu.

Mambo bado ni 🔥🔥🔥 kwelikweli. Ili kujua mwisho wake, usichoke kufuatilia hadi mwisho...

NB: Litro 👩
Ahsante mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom