Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,140
- 14,678
- Thread starter
- #141
Taxi - (50)
Sammy alimfungulia mlango wa abiria Pendo ili apande, kisha aliliingiza lile gari ndani ya uzio na kutulia ndani ya gari akiliacha liungurume taratibu. Baada ya dakika kama mbili alizima injini.
Alichomoa ufunguo na kuushika mkononi kisha aliteremka kutoka ndani ya lile gari akiwa kashika ufunguo wake na mkono mwingine alimshika mkono Pendo huku akitabasamu.
Winifrida aliendelea kumtazama Sammy kwa mshangao kisha akaligusa lile gari katika namna ya kulishangaa kabla hajageuka kumtazama Sammy.
“Kaka, hili gari la nani?” Winifrida alimuuliza Sammy kwa shauku.
“Kwani unalionaje! Zuri au baya?” Sammy alimtupia swali badala ya kumjibu.
Winifrida alikunja sura yake huku akilitazama lile gari kwa makini kwa namna ya kulikagua zaidi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kama aliyekuwa akitafuta jibu, kisha alifungua mlango wa mbele upande wa abiria na kuingia, akaketi kwenye siti ya abiria huku akiendelea kulitazama kwa mshangao.
“Unalionaje, zuri au baya?” Sammy aliuliza tena swali lile lile huku akiachia tabasamu.
Winifrida alimtazama na kunyanyua juu mabega yake huku akibetua midomo. “Sijui!”
“Basi na mimi sikwambii ni la nani,” Sammy alisema huku akiendelea kutabasamu.
“Ayi jamani, kaka!” Winifrida alilalama huku akimtazama Sammy kwa shauku ya kutaka kusikia kuwa ni gari lake. Sammy na Pendo wakaanza kucheka.
Joyce alikuwa amesikia muungurumo wa gari lakini aliamua kusubiri kwanza huku akitaraji kuona wageni wakiingia ndani lakini hakuwaona bali alikuwa akisikia wanaongea na kucheka. Aliamua kuchungulia nje kupitia mlango wa barazani uliokuwa umefunguliwa nusu, akamuona Sammy akiwa amemshika Pendo na wakati huo Winifrida alikuwa ameketi kwenye siti ndani ya gari.
Joyce aliwatazama kwa mshangao mkubwa asijue kilichokuwa kikiendelea pale nje ya nyumba. Hata hivyo, hakutoka nje bali alirudi ndani na kuendelea na shughuli yake.
Sammy alimshika Pendo akamwongoza kuelekea ndani huku wakimwacha Winifrida anaendelea kulikagua lile gari kama aliyekuwa akilifanyia matengenezo. Kwanza alivuta droo iliyokuwa kwenye dashibodi na kuanza kuchakurachakura akitafuta kilichomfaa. Kisha alianza kuchunguza hapa na pale, na baadaye aliinama kuchungulia chini ya dashibodi.
Hakuridhika, aliinama zaidi na kusukuma siti ya abiria huku akitazama chini kabisa ya siti, akaona kadi ndogo itumikayo kuhifadhi kumbukumbu kwenye simu maarufu kama memory card (Micro SD) iliyokuwa imepachikwa kwa ustadi mkubwa chini ya ile siti ya abiria.
Winifrida aliitoa ile kadi huku akiitazama kwa udadisi zaidi, alikunja sura yake akijaribu kufikiria. Alidhani labda Sammy au mtu mwingine yeyote alikuwa ameidondosha, lakini akajiuliza mbona kama ilioneka kama imefichwa!
Muda huo huo Sammy alitoka nje huku akimwangalia kwa makini. Winifrida alimuona na kuificha ile kadi. Alifungua mlango wa gari na kushuka huku akicheka, kisha akaelekea ndani na kumwacha Sammy akimsindikiza kwa macho hadi alipoingia ndani.
Sammy aliachia tabasamu na kubetua mabega yake juu huku akitingisha kichwa chake taratibu. Hakujua nini kilichokuwa kinaendelea kwenye akili ya Winifrida. Alifunga milango ya gari vizuri na kurejea ndani.
* * * * *
Ilikuwa saa moja jioni, Mr. Oduya alikuwa amewaacha ndugu wawili; Madame Norah na Zainab wameketi kitandani wakiongea kwa furaha na kusimuliana masaibu waliyopitia kwa kila mmoja wao hadi kufika hapo. Kwa kweli ilikuwa ni jioni ya kusisimua sana kwa ndugu wale wawili.
Aliyeanza ni Zainab aliyemsimulia kila kitu Madame Norah pasipo kuacha kitu, alisimulia tangu makuzi yake baada ya Madame Norah kupata ujauzito na kutorokea kusikojulikana, masomo yake hadi kuajiriwa Kilimanjaro Hotel alikokutana na Hemed Kimaro.
Hakuacha kitu jinsi mgogoro katika ndoa yao ulivyoanza na hatimaye kuingia katika mtego wa Mr. Oduya na mauaji ya Hemed, kisha alilazimika kwenda uhamishoni Canada, alikoanza maisha mapya akiitwa Suzanne Ross.
Muda wote Madame Norah alikuwa akimsikiliza kwa makini, kuna wakati alisisimkwa mwili na kuna wakati alihuzunika, hata hivyo kubwa zaidi ilikuwa kumpata mdogo wake akiwa mzima wa afya.
Madame Norah naye alimsimulia Zainab maisha aliyopitia, tangu alipomtelekeza mtoto wake nyumbani kwa Rafael Jengo kule Ngamiani Tanga na kutorokea jijini Dar es Salaam, maisha aliyoyaishi jijini Dar es Salaam na jinsi jina la Madame Norah lilivyopatikana kabla hajakutana na Karl Johan aliyempeleka nchini Sweden alikokutana na Andreas Gunnar.
Masimulizi kuhusu maisha ya ndugu wale wawili yalikuwa mfano wa filamu mbili za kusisimua sana, kila mmoja alikuwa akisisimkwa kusikia mapito ya mwingine.
“Sikutegemea kabisa kukutana na wewe tena, nilijua umeshakufa dada’angu,” Zainab alimwambia Madame Norah huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Hapana mdogo wangu, Mungu ni mwema japo maisha yangu yamekuwa ya huzuni sana, hasa kwa kuwa mama alikufa kabla hajanisamehe na mtoto pia nimemkosa. Bora hata ya kwako,” Madame Norah alijibu huku akishusha pumzi ndefu.
“Hata hivyo, suala la wewe kuhusishwa na kifo cha mumeo kabla haijaripotiwa kuwa umetoweka ni moja ya mambo yaliyoniumiza kichwa na kunifanya niishi maisha ya huzuni miaka yote hii nikiwa sijui kama uko hai au umekufa, nilihuzunika kuwapoteza wote, wewe na mama,” Madame Norah aliongeza huku akimtazama Zainab kwa huzuni.
“Kwa kweli mdogo wangu umepitia mambo makubwa sana,” Madame Norah aliongeza akisema kwa sauti tulivu huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wa Zainab.
“Sikufikii wewe, dada!” Zainab alisema huku akibetua mabega yake juu, na kuongeza, “Hivi una taarifa zozote za dada Zuena?”
“Zuena yupo Ghana, mambo yake si mabaya. Ameolewa na Dk. Aden Mafuru, Balozi wa Tanzania nchini Ghana,” Madame Norah alisema na kumfanya Zainab ashtuke.
“Huyo balozi ana uhusiano gani na huyu Mafuru, mwanasheria wa Mr. Oduya?” Zainab aliuliza kwa mshangao.
“Ni mapacha. Yule balozi ni mkubwa huyu mwanasheria ni mdogo,” Madame Norah alisema huku akijiweka sawa pale kitandani kisha akainua mkono wake kutazama saa yake ya mkononi.
“Kwa hiyo dada Zuena anaishi Ghana?” Zainab aliuliza tena kwa mshangao uliochanganyika na furaha.
Mambo yanazidi kunoga, tukutane tena kesho, hapa hapa ili kujua mwendelezo wa safari yetu ndefu ya kusisimua...
Sammy alimfungulia mlango wa abiria Pendo ili apande, kisha aliliingiza lile gari ndani ya uzio na kutulia ndani ya gari akiliacha liungurume taratibu. Baada ya dakika kama mbili alizima injini.
Alichomoa ufunguo na kuushika mkononi kisha aliteremka kutoka ndani ya lile gari akiwa kashika ufunguo wake na mkono mwingine alimshika mkono Pendo huku akitabasamu.
Winifrida aliendelea kumtazama Sammy kwa mshangao kisha akaligusa lile gari katika namna ya kulishangaa kabla hajageuka kumtazama Sammy.
“Kaka, hili gari la nani?” Winifrida alimuuliza Sammy kwa shauku.
“Kwani unalionaje! Zuri au baya?” Sammy alimtupia swali badala ya kumjibu.
Winifrida alikunja sura yake huku akilitazama lile gari kwa makini kwa namna ya kulikagua zaidi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani kama aliyekuwa akitafuta jibu, kisha alifungua mlango wa mbele upande wa abiria na kuingia, akaketi kwenye siti ya abiria huku akiendelea kulitazama kwa mshangao.
“Unalionaje, zuri au baya?” Sammy aliuliza tena swali lile lile huku akiachia tabasamu.
Winifrida alimtazama na kunyanyua juu mabega yake huku akibetua midomo. “Sijui!”
“Basi na mimi sikwambii ni la nani,” Sammy alisema huku akiendelea kutabasamu.
“Ayi jamani, kaka!” Winifrida alilalama huku akimtazama Sammy kwa shauku ya kutaka kusikia kuwa ni gari lake. Sammy na Pendo wakaanza kucheka.
Joyce alikuwa amesikia muungurumo wa gari lakini aliamua kusubiri kwanza huku akitaraji kuona wageni wakiingia ndani lakini hakuwaona bali alikuwa akisikia wanaongea na kucheka. Aliamua kuchungulia nje kupitia mlango wa barazani uliokuwa umefunguliwa nusu, akamuona Sammy akiwa amemshika Pendo na wakati huo Winifrida alikuwa ameketi kwenye siti ndani ya gari.
Joyce aliwatazama kwa mshangao mkubwa asijue kilichokuwa kikiendelea pale nje ya nyumba. Hata hivyo, hakutoka nje bali alirudi ndani na kuendelea na shughuli yake.
Sammy alimshika Pendo akamwongoza kuelekea ndani huku wakimwacha Winifrida anaendelea kulikagua lile gari kama aliyekuwa akilifanyia matengenezo. Kwanza alivuta droo iliyokuwa kwenye dashibodi na kuanza kuchakurachakura akitafuta kilichomfaa. Kisha alianza kuchunguza hapa na pale, na baadaye aliinama kuchungulia chini ya dashibodi.
Hakuridhika, aliinama zaidi na kusukuma siti ya abiria huku akitazama chini kabisa ya siti, akaona kadi ndogo itumikayo kuhifadhi kumbukumbu kwenye simu maarufu kama memory card (Micro SD) iliyokuwa imepachikwa kwa ustadi mkubwa chini ya ile siti ya abiria.
Winifrida aliitoa ile kadi huku akiitazama kwa udadisi zaidi, alikunja sura yake akijaribu kufikiria. Alidhani labda Sammy au mtu mwingine yeyote alikuwa ameidondosha, lakini akajiuliza mbona kama ilioneka kama imefichwa!
Muda huo huo Sammy alitoka nje huku akimwangalia kwa makini. Winifrida alimuona na kuificha ile kadi. Alifungua mlango wa gari na kushuka huku akicheka, kisha akaelekea ndani na kumwacha Sammy akimsindikiza kwa macho hadi alipoingia ndani.
Sammy aliachia tabasamu na kubetua mabega yake juu huku akitingisha kichwa chake taratibu. Hakujua nini kilichokuwa kinaendelea kwenye akili ya Winifrida. Alifunga milango ya gari vizuri na kurejea ndani.
* * * * *
Ilikuwa saa moja jioni, Mr. Oduya alikuwa amewaacha ndugu wawili; Madame Norah na Zainab wameketi kitandani wakiongea kwa furaha na kusimuliana masaibu waliyopitia kwa kila mmoja wao hadi kufika hapo. Kwa kweli ilikuwa ni jioni ya kusisimua sana kwa ndugu wale wawili.
Aliyeanza ni Zainab aliyemsimulia kila kitu Madame Norah pasipo kuacha kitu, alisimulia tangu makuzi yake baada ya Madame Norah kupata ujauzito na kutorokea kusikojulikana, masomo yake hadi kuajiriwa Kilimanjaro Hotel alikokutana na Hemed Kimaro.
Hakuacha kitu jinsi mgogoro katika ndoa yao ulivyoanza na hatimaye kuingia katika mtego wa Mr. Oduya na mauaji ya Hemed, kisha alilazimika kwenda uhamishoni Canada, alikoanza maisha mapya akiitwa Suzanne Ross.
Muda wote Madame Norah alikuwa akimsikiliza kwa makini, kuna wakati alisisimkwa mwili na kuna wakati alihuzunika, hata hivyo kubwa zaidi ilikuwa kumpata mdogo wake akiwa mzima wa afya.
Madame Norah naye alimsimulia Zainab maisha aliyopitia, tangu alipomtelekeza mtoto wake nyumbani kwa Rafael Jengo kule Ngamiani Tanga na kutorokea jijini Dar es Salaam, maisha aliyoyaishi jijini Dar es Salaam na jinsi jina la Madame Norah lilivyopatikana kabla hajakutana na Karl Johan aliyempeleka nchini Sweden alikokutana na Andreas Gunnar.
Masimulizi kuhusu maisha ya ndugu wale wawili yalikuwa mfano wa filamu mbili za kusisimua sana, kila mmoja alikuwa akisisimkwa kusikia mapito ya mwingine.
“Sikutegemea kabisa kukutana na wewe tena, nilijua umeshakufa dada’angu,” Zainab alimwambia Madame Norah huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Hapana mdogo wangu, Mungu ni mwema japo maisha yangu yamekuwa ya huzuni sana, hasa kwa kuwa mama alikufa kabla hajanisamehe na mtoto pia nimemkosa. Bora hata ya kwako,” Madame Norah alijibu huku akishusha pumzi ndefu.
“Hata hivyo, suala la wewe kuhusishwa na kifo cha mumeo kabla haijaripotiwa kuwa umetoweka ni moja ya mambo yaliyoniumiza kichwa na kunifanya niishi maisha ya huzuni miaka yote hii nikiwa sijui kama uko hai au umekufa, nilihuzunika kuwapoteza wote, wewe na mama,” Madame Norah aliongeza huku akimtazama Zainab kwa huzuni.
“Kwa kweli mdogo wangu umepitia mambo makubwa sana,” Madame Norah aliongeza akisema kwa sauti tulivu huku akiwa ameyatuliza macho yake kwenye uso wa Zainab.
“Sikufikii wewe, dada!” Zainab alisema huku akibetua mabega yake juu, na kuongeza, “Hivi una taarifa zozote za dada Zuena?”
“Zuena yupo Ghana, mambo yake si mabaya. Ameolewa na Dk. Aden Mafuru, Balozi wa Tanzania nchini Ghana,” Madame Norah alisema na kumfanya Zainab ashtuke.
“Huyo balozi ana uhusiano gani na huyu Mafuru, mwanasheria wa Mr. Oduya?” Zainab aliuliza kwa mshangao.
“Ni mapacha. Yule balozi ni mkubwa huyu mwanasheria ni mdogo,” Madame Norah alisema huku akijiweka sawa pale kitandani kisha akainua mkono wake kutazama saa yake ya mkononi.
“Kwa hiyo dada Zuena anaishi Ghana?” Zainab aliuliza tena kwa mshangao uliochanganyika na furaha.
Mambo yanazidi kunoga, tukutane tena kesho, hapa hapa ili kujua mwendelezo wa safari yetu ndefu ya kusisimua...