Stori ya kusisimua - Taxi

Taxi - (43)

Ilipoishia jana

“Nimemuona dada yangu mkubwa, unakumbuka niliwahi kukueleza kuhusu familia yangu na jinsi dada yetu mkubwa alivyotoroka baada ya kupata ujauzito wakati nikiwa nina miaka sita…”

“Ndiyo nakumbuka.”

“Leo nimemuona… I need to see her,” Zainab alisisitiza.

“Umemuona wapi? Naona sasa unatafuta matatizo na ikigundulika kuwa upo nchini huoni kama itatuletea sote matatizo!” Mr. Oduya aliongea huku uso wake ukionesha mashaka.

“Wala hakutakuwa na tatizo lolote. Nimemuona kwenye televisheni, ninachokuomba mume wangu, fanya vyovyote uwezavyo unikutanishe naye, hata kwa kumleta hapa, nahitaji sana kuongea naye.”

“Sasa nitampata wapi, na anaitwa nani?”

“Madame Norah…”

What?” Mr. Oduya alishtuka sana, akamkazia macho Zainab kwa mshangao. “Is Madame Norah your elder sister?” (Madame Norah ni dada yako mkubwa?)

Yes, she’s my sister, blood sister,” (Ndiyo, ni dada’angu wa damu) Zainab alisema huku akilengwa na machozi.

Sasa endelea...

Oh my God!” (Mungu wangu!) Mr. Oduya alisema huku akiwa haamini alichokisikia. Alimtumbulia macho Zainab kwa muda, akajikuta akiachia mdomo wake wazi kwa mshangao zaidi. “Ni kweli mnafanana, tena mnafanana sana!” alisema huku akiachia mluzi mdogo wa mshangao.

Kisha kilipita kitambo kirefu cha ukimya, walibaki wakitazamana kila mmoja akimezwa na ulimwengu wa tafakuri kabla Mr. Oduya hajachukua simu yake ya mkononi na kutafuta namba za Adam Mafuru. Alipozipata alipiga na kusikiliza.

“Mr. Mafuru,” Mr. Oduya aliita mara tu alipogundua kuwa Mafuru alikuwa amepokea simu. Uso wake ulikuwa na mikunjo.

Yes, Boss,” sauti ya Mafuru ilijibu kwa adabu.

“Naomba ufike hapa Paradise Club mara moja, kuna jambo muhimu sana unatakiwa kulifuatilia, it’s urgent please,” Mr. Oduya alisema huku uso wake uliondoa mikunjo, kisha ukaunda tabasamu pana.

Okay, Boss,” Mafuru alijibu. Mr. Oduya akakata simu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, aligeuka kumtazama Zainab huku akiendelea kutabasamu.

Don’t worry, my darling, kila kitu kitakwenda sawa,” Mr. Oduya alisema na kumfanya Zainab aruke kwa furaha na kumkumbatia.

Thank you, darling, thank you very much,” (Ahsante mpenzi, ahsante sana) Zainab alisema huku akimporomoshea Mr. Oduya mabusu mfululizo.

* * * * *

Saa nne na dakika arobaini asubuhi, Elli na Sammy walikuwa wanatoka ndani ya mgahawa wa kisasa wa Elli’s uliopo Ilala Sharif Shamba na kuingia ndani ya gari la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i la rangi nyeupe mali ya Elli, lililokuwa kwenye maegesho ya magari ya mgahawa ule.

Elli aliwasha gari na kuliondoa taratibu kutoka kwenye yale maegesho ya magari ya mgahawa wa Elli’s akazunguka na kuelekea kwenye geti kubwa la kutokea la jengo lile, akaliingiza barabarani huku akiendesha kwa umakini mkubwa. Ilikuwa safari ya kuelekea Kinondoni B.

Kutoka pale mgahawa wa Elli’s gari lilikata kona na kuingia upande wa kushoto likaifuata barabara ya Uhuru iliyokuwa na msongamano wa magari muda ule, hivyo Elli alilazimika kuendesha kwa mwendo mdogo.

Safari yao iliendelea huku wakiwa kimya, kila mmoja alikuwa akitafakari, walivuka eneo la Bungoni kisha wakayavuka majengo ya Kituo cha Amana Vijana, na mbele yake wakavuka vibanda vya wasusi wa Kimasai vilivyokuwa upande wao wa kushoto na kuingia upande huo huo wa kushoto wakiifuata barabara ya mtaa wa Mafao.

Kwa kuwa barabara ile haikuwa na msongamano Elli aliongeza mwendo akiyapita majengo ya ghorofa ya Shirika la Nyumba la Taifa eneo la Ilala na baada ya safari fupi hatimaye wakaja kukutana na barabara ya Kawawa.

Barabara ya Kawawa ilikuwa moja ya barabara kubwa na maarufu sana jijini Dar es Salaam iliyoanzia eneo la Veta Chang’ombe katika makutano ya barabara za Nyerere, Chang’ombe na Kawawa na kuishia katika eneo la Kinondoni Morocco kwenye makutano ya barabara za Ali Hassan Mwinyi, Mwai Kibaki, Bagamoyo na Kawawa.

Elli aliingia kushoto akaifuata barabara ile ya Kawawa kuelekea Magomeni. Muda wote Sammy alikuwa yupo kimya akiwaza mbali sana, muda wote macho yake yaliangalia nje wakati gari likipita eneo la Msimbazi Centre kisha likavuka eneo la Kigogo Sambusa na baadaye Kigogo Mbuyuni, kwenye mzunguko wa barabara za Kawawa na ile ya Kigogo.

Pilika pilika za wakazi wa jiji la Dar es Salaam zilikuwa zimeshamiri muda ule kwani eneo lile lilionekana kuwa na watu wengi, pikipiki na magari yaliyopishana kwenda sehemu mbalimbali zaa mji.

Walipovuka eneo la Kigogo Mbuyuni walianza kuteremsha bonde la Msimbazi kisha mbele kidogo Elli aliongeza mwendo ili kulipita lori la wazoa taka lililokuwa mbele yao. Kisha waliivuka barabara ya Mikumi upande wao wa kushoto huku wakipishana na magari mengi yaliyoingia katika barabara ile.

Baada ya safari fupi wakaanza kukivuka kituo cha daladala cha Magomeni Mikumi, Sammy akayatupa macho yake kutazama upande wake wa kulia, ng’ambo ya ile barabara ya Kawawa na kuiona yadi moja ya magari yaliyotumika, iliyokuwa na magari yasiyozidi ishirini yakiwa yameegeshwa kwenye uzio yakisubiri wanunuzi.

Sammy aliyatazama kwa makini yale magari na kuliona gari moja lenye muundo wa kizamani aina ya Cadillac DeVille jeupe. Moyo wake ukapiga paa! Aliendelea kulikodolea macho lile gari wakati Elli akivuka eneo lile kuelekea kwenye taa za kuongozea barabarani za Magomeni, kwenye makutano ya barabara za Kawawa na ile ya Morogoro.

Stop the car,” Sammy alisema ghafla huku akilikodolea macho lile gari na kumshtua Elli aliyegeuza shingo yake kumtazama kwa mshangao.

“Nimesema simamisha gari!” Sammy alisema tena, safari hii kwa sauti ya juu kidogo.

“Nini!” Elli aliuliza huku akikanyaga breki kwa nguvu pasipo kufikiri, gari likajivuta na kusota kwenye ile barabara pana huku likiyumba, bahati nzuri gari halikutoka nje ya barabara.

Muda huo huo walisikia sauti ya breki kali kutoka nyuma yao, dereva wa daladala linalofanya safari zake kati ya Gongolamboto na Masaki lililokuwa nyuma yao alikuwa akihangaika kukanyaga breki ya ghafla na kufanya gari lile liserereke na kusimama kando ya barabara.

Kwa sekunde chache ilitokea taharuki ndani ya lile daladala, abiria walitaharuki sana. Daladala liliposimama walianza kutoa lugha kali ya matusi kwa Elli, wengine waliishia kusonya tu na mmoja wao aliinua juu kidole chake cha kati kuonesha hasira zake.

Inaendelea...
 
Taxi - (44)

Elli hakuwajali, alilipeleka gari lake kando kabisa ya barabara kwenye barabara ndogo ya waenda kwa miguu na kuliegesha huku akimuomba msamaha dereva wa daladala aliyeonekana kuchukizwa na tukio lile. Eneo lile lilikuwa jirani kabisa na kituo cha mafuta cha Gapco.

Sammy aliteremka haraka na kuelekeza macho yake kuangalia kule kwenye yadi ya magari kulikokuwa na lile gari aina ya Cadillac DeVille, kisha alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kushika kiuno chake.

“Nimeiona gari ninayoitaka,” Sammy alimwambia Elli, bila kusubiri alianza kupiga hatua zake haraka kuelekea kule kwenye yadi ya magari, akavuka barabara ya Kawawa na kutokea upande wa pili wa barabara. Hapo hakuwaza kitu kingine chochote bali alichowaza ni jinsi ambavyo angemiliki lile gari. Elli alibaki kimya akimtazama Sammy kwa mashangao.

Elli aliwasha gari lake akaingia upande wa kile kituo cha mafuta na kulizungusha kisha akarudi tena barabara ya Kawawa na kukunja kuelekea upande wa kulia akimfuata Sammy. Alimkuta Sammy akiwa anaongea na kijana mmoja, mfanyakazi wa yadi ile ya magari.

Kabla hajajua wanaongea nini akamwona yule kijana akichukua funguo kisha akaanza kuondoka kumfuata Sammy ambaye tayari alikuwa amesimama akilitazama gari moja jeupe lenye muundo wa kizamani aina ya Cadillac DeVille. Elli alimfuata Sammy lakini kabla hajauliza chochote Sammy alimweleza kuwa alitaka kununua lile gari, Elli akashangaa sana!

Elli hakuwa na uhakika kama Sammy alikuwa ameushirikisha ubongo wake kabla hajafikia uamuzi wa kutaka kununua lile gari lenye muundo wa kizamani. Lakini Sammy alisisitiza kuwa alikuwa akilihitaji lile gari kwa sababu ya upekee wake.

“Kwanza ni gari lenye upekee, pili lina muundo wa kizamani na tatu ni zuri sana,” Sammy alisema na kuingia ndani ya lile gari.

“Na vipi kuhusu ubora wake? Usije ukanunua gari ukaliendesha mwezi mmoja tu kisha lianze kukuendesha wewe!” Elli aliuliza akiwa bado ana mashaka.

“Hili ni gari zima kabisa, ni kama jipya licha ya uzamani wake, kwa kuonesha hivyo tunampa garantii ya miezi sita, kama ataona lina matatizo ruksa kulirudisha,” alisema yule Mwarabu kwa kujiamini.

Sammy alitia ufunguo na kuwasha injini ya lile gari, gari likaunguruma bila shida yoyote. Sammy akapiga lesi huku akinesa nesa kwa mbwembwe na kuonekana kuridhika. Akaachia tabasamu.

* * * * *

Saa sita mchana Joyce alikuwa anawasili katika jumba la kifahari la Madame Norah lililozungukwa na ukuta mrefu wenye mfumo wa uhakika wa ulinzi na geti kubwa jeusi mbele yake. Jumba lile lilikuwa limejengwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi eneo la Mikocheni.

Toka kwa mbali uzuri wa jumba lile la ghorofa tatu ulionekana wazi, mandhari yake ilizungukwa na miti mirefu na mikubwa ya kivuli aina ya ‘Quercus virginiana’, kulikuwa na barabara ya lami yenye usafi wa hali ya juu iliyokuwa ikieleka katika jumba hilo na kupandwa miti ya kivuli iliyovutia na maua aina ya ‘lotus’.

Kulikuwa na ukimya mkubwa eneo hilo. Joyce alisimama nje ya lile geti kubwa jeusi kisha akabonyeza kitufe cha kengele na mara geti dogo kando ya lile geti kubwa jeusi likafunguliwa, mlinzi mmoja aliyekuwa wamevaa sare maalumu za kampuni binafsi ya ulinzi akachungulia na kumuona Joyce kisha akaachia tabasamu.

Alimsalimia kwa bashasha zote huku akimpisha aingie ndani. Hakumuuliza maswali yoyote kwa kuwa alimfahamu, kwani alikwishafika hapo mara mbili kabla ya siku ile na tayari walikuwa na taarifa kuwa angefika siku hiyo.

Joyce alipoingia ndani ya ule uzio walinzi wawili waliokuwa katika kibanda cha walinzi upande wa kulia wa lile geti walimsimamisha, mmoja wao alichukua kifaa maalumu cha kukagulia akamkagua kuona kama alikuwa na silaha yoyote na alipohakikisha kwamba hakuwa na silaha yoyote wakamruhusu aendelee na safari yake.

Joyce alipiga hatua zake taratibu kuelekea kwenye baraza kubwa ya mbele iliyokuwa na mlango mkubwa wa kuingilia ndani ya lile jumba, alikuwa akikatiza katikati ya bustani nzuri ya maua ya kupendeza aina ya ‘lotus’ na katikati ya bustani ile kulitengenezwa njia nzuri ya kutembea kwa miguu kwa vitofali vidogo vinavyovutia.

Kabla hajafika kwenye ile baraza kubwa ya mbele iliyokuwa imepangwa seti moja ya makochi meusi ya sofa alimuona Madame Norah akitoka ndani ya lile jumba akiwa ameongozana na msichana mmoja aliyekadiriwa kuwa na miaka kati ya ishirini na sita na ishirini na nane.

Alikuwa msichana mrefu na mrembo hasa, alikuwa na nywele nyingi nyeusi za kibantu zisizotiwa dawa, begani alitundika mkoba mzuri wa kike wa rangi ya pundamilia uliogharimu fedha nyingi.

Alikuwa amevaa suruali ya jeans ya rangi ya bluu, blauzi nyekundu ya mikono mirefu na viatu vyekundu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio. Mkononi alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe.

Madame Norah alikuwa amemuona Joyce wakati akiingia, hivyo aliachia tabasamu na kumpokea kwa bashasha zote.

“Hello Joy, karibu sana, binti’angu. Habari za huko utokako?” Madame Norah alimsalimia Joyce kwa bashasha huku akimkumbatia na kumbusu kwenye shavu.

“Nzuri tu, mama. Shikamoo!” Joyce alisema huku akiachia tabasamu.

“Marhaba, pole na majukumu,” Madame Norah aliitikia huku akimwachia Joyce na kusimama akimtazama kwa makini. Macho yake yaliweka kituo usoni kwake.

“Ahsante sana mama, vipi na wewe unaendeleaje?”

“Sijambo kabisa, mumeo na wajukuu hawajambo?” Madame Norah aliendelea kumuuliza Joyce huku akijihisi faraja kubwa sana kila alipokutana naye. Alimchukulia kama binti yake wa kumzaa.

“Wote hawajambo, mama…” Joyce alijibu huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani, kisha kikatokea kitambo kifupi cha ukimya kila mmoja akimwangalia mwenziwe kwa namna iliyokosa tafsiri, ilikuwa kama mzazi na bintiye waliopotezana muda mrefu na sasa walikuwa wanaonana kwa mara ya kwanza.

Muda wote yule msichana aliyeambatana na Madame Norah alikuwa amesimama kimya akiwatazama kwa zamu. Uso wake ulikuwa umepambwa na tabasamu pana.

“Nimefurahi sana kukuona tena, naomba mnifuate,” Madame Norah alivunja ukimya huku akiwaashiria Joyce na yule msichana wamfuate.

Wote watatu walielekea upande wa kulia wa lile jumba kulikokuwa na bustani nzuri ya kupumzika na bwawa kubwa la kuogelea lililokuwa limezungukwa na viti vizuri vya kujipumzisha chini ya miamvuli mikubwa ya kivuli.

“Joyce, kwanza kabisa ninakushukuru sana kwa kuacha shughuli zako na kuitika wito wangu, umekuwa unanipa heshima kubwa sana…” Madame Norah alisema baada ya wote kuketi kwenye viti, alikuwa anaonekana mtu mwenye furaha kubwa tofauti na siku nyingine.

“Nisingeweza kukosa kuja kuonana nawe, mama yangu, wewe umekuwa mtu muhimu sana kwangu katika kutimiza ndoto zangu,” Joyce alisema huku akishusha pumzi.

Inaendelea...
 
Taxi - (45)

“Sasa nimekuita ili nikukutanishe na mtu atakayekusaidia kwenye majukumu yako kama nilivyokuahidi…” Madame Norah alisita kidogo na kugeuza shingo yake kumtazama yule msichana mrembo aliyeambatana naye.

“Ni huyu hapa… anaitwa Nyaso Gilbert, ni binti mwanamkakati mzuri hasa, msomi wa Shahada ya Kwanza ya Sanaa katika Uchumi na Takwimu, naamini ataweza kusimamia vizuri program zako,” Madame Norah alimwambia Joyce.

Ooh, thank you, mam,” Joyce alisema huku akimkumbatia Madame Norah kwa upendo, kisha alimgeukia yule msichana. “Habari yako? Naona hata hatujasalimiana!” Joyce alisema kwa furaha huku akinyoosha mkono wake kumpa Nyaso.

“Nzuri tu dada’angu, nimefurahi sana kukutana na wewe maana Madame alikuwa anakusifia sana,” Nyaso alisema huku akinyoosha mkono wake na kukutanisha kiganja chake na kile cha Joyce. Wakasalimiana kwa bashasha zote huku wakifurahi.

Muda ule ule simu ya Madame Norah ilianza kuita, Madame Norah aliiangalia kwa makini na kuminya midomo yake huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani, kisha akaipokea.

“Hello, Mr. Mafuru,” Madame Norah alitamka mara baada ya kuiweka simu sikioni.

“Nipo hapa getini kwako,” sauti ya Mafuru ikasikika kutoka upande wa pili wa simu.

“Ooh umeshafika, waambie wakuruhusu, nipo huku bustanini,” Madame Norah alisema huku akijiinua kutoka kwenye kiti.

“Sasa Joyce, ngoja niwaache mpange mambo yenu, nimepata mgeni. Ila ukitaka kuondoka niambie ili nikupe dereva akuwahishe,” Madame Norah alisema huku akijiandaa kuondoka eneo lile.

“Sawa, mama,” Joyce alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Muda ule ule Mafuru alitokea na kusimama akiwaangalia kwa makini. Alikuwa amevaa suti ya kijivu na miwani myeusi na mkononi alibeba mkoba mdogo mweusi wa kiofisi.

“Habari zenu warembo?” Mafuru aliwasalimia huku akiachia tabasamu.

“Salama,” Joyce na Nyaso waliitikia kwa pamoja. Mafuru aliwatazama kwa makini, macho yake yakavutwa zaidi kumtazama Joyce. Alimtazama kwa kitambo hadi aliposhtuliwa na Madame Norah.

“Twende basi, unatazama watu hadi wanaona aibu!” Madame Norah alimwambia Mafuru kwa utani.

“Huyo ni binti yako, naona mnafanana sana!” Mafuru alimuuliza Madame Norah huku akielekeza kidole chake kwa Joyce.

“Kwani umekuja hapa kuzungumza na mimi au kupeleleza maisha ya watu wanaonihusu?” Madame Norah alimuuliza Mafuru akionekana kukerwa kidogo.

“Samahani! Sikukusudia kukuudhi,” Mafuru alisema kisha akaanza kumfuata Madame Norah aliyemuongoza kuelekea ofisini kwake ndani ya lile jengo huku wakiwaacha Joyce na Nyaso wameketi kwenye bustani wakipanga program zao.

“Hongera sana Madame, wewe ni mwanamke jasiri sana ambaye juhudi zako zinastahili kuungwa mkono, umeonesha ujasiri mkubwa kwa hiki ulichoamua kukifanya. Kwa hilo lazima nikupongeze,” Mafuru alimwambia Madame Norah wakati wakiingia kwenye ofisi binafsi ya Madame Norah.

“Ni wajibu wetu kurudisha sehemu fulani kwa jamii,” Madame Norah alisema huku akifungua mlango wa ofisini kwake na kumkaribisha Mafuru. Wakaingia na kuketi kwenye viti kwa mazungumzo.

“Uliponipigia simu kuomba kuniona nilishtuka sana, hadi sasa bado nina mshtuko na sijui unahitaji kuongea na mimi kuhusu nini!” Madame Norah alimwambia Mafuru maara baada ya kuketi.

“Kwanza kabisa naomba nikufikishie ujumbe wa Mr. Oduya kwako…” Mafuru alianza kuongea lakini akakatizwa.

“Mr. Oduya! Anataka nini kwangu huyo mzee?” Madame Norah alionekana kushtuka sana.

“Mbona umestuka sana, Madame, kwani Mr. Oduya hapaswi kukusalimia?” Mafuru aliuliza kwa sauti tulivu ya kusihi.

That old man is a monster… hata wewe sikuamini sana, nimekubali kuonana na wewe kwa vile tu pacha wako, Balozi Mafuru kamuoa mdogo wangu, vinginevyo sina ushirika na ninyi kabisa…” Madame Norah alisema na kushusha pumzi.

“Halafu umenishangaza sana kuniambia una ujumbe wangu kutoka kwa huyo mzee wako wakati mimi na yeye hatuna mazoea, nadhani lazima kuna jambo analitafuta kwangu, siyo bure,” Madame Norah alisema huku akikunja uso wake na kutengeneza matuta madogo.

“Watu hubadilika, Madame, hivyo usimhukumu mtu kwa aliyoyafanya jana wakati leo kabadilika… Mr. Oduya si mtu mbaya kama unavyomfikiria. Amenituma nikwambie kuwa anakupongeza sana kwa juhudi ulizozianzisha na anahitaji kuonana na wewe leo saa kumi na mbili jioni pale Paradise Club mjadili kuhusiana na hii project yako mpya. Ameguswa sana na anahitaji kuchangia…” Mafuru alisema na kumfanya Madame Norah amkate kauli.

“Kwa hiyo anataka kunitumia kama mtaji wake wa kisiasa baada ya kuona mambo yamekwama, siyo? Mimi na yeye wapi na wapi! Toka lini tukachangiana fedha kwenye masuala ya kijamii!” Madame Norah alizidi kushangaa.

“Mr. Oduya ni mtu wa kusaidia sana taasisi mbalimbali zinazofanya mambo makubwa kwa jamii, amekwisha saidia taasisi nyingi tu hadi sasa! Alipata taarifa zako kupitia runinga kuhusu lengo lako la kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga kituo na shule ya watoto wenye mahitaji maalumu, pamoja na makazi bora ya wazee… hujui tu hiki ni kitu alikuwa nacho siku nyingi na ameguswa kuona wewe pia una wazo kama lake, hivyo anataka kutoa mchango wake. Hakutaka kuja mwenyewe lakini amenituma nikwambie kwamba anahitaji kuonana nawe jioni ya leo,” Mafuru alisema huku akimkazia macho Madame Norah.

Kilipita kitambo kirefu cha ukimya, Madame Norah alionekana kuwaza sana, alikuwa njia panda ya ama akubali mwaliko au akatae.

“Sijajua hasa kwa nini atake kufanya hivyo sasa na si wakati mwingine wowote, kwani siku zote alikuwa hajui kuwa huwa ninasaidia makundi yenye mahitaji maalumu?” Madame Norah aliuliza huku akiyatuliza macho yake kwenye uso wa Mafuru.

“Hupaswi kuhofia, Madame, hakuna jambo lolote baya ingawa ni kweli kama ulivyosema kwamba wewe na yeye hamna mazoea ya karibu lakini naamini kuanzia sasa mtakuwa karibu zaidi, I’m here because I know something you don’t know,” (Nipo hapa kwa kuwa najua jambo usilolijua) Mafuru alimalizia kwa Kiingereza kuonesha msisitizo wake na kumfanya Madame Norah amtazame kwa mshangao Zaidi.

Madame Norah alitulia kwa sekunde chache akijaribu kuyatafakari maneno ya Mafuru pasipo kupata majibu.

Inaendelea...
 
Taxi - (46)

“Mpe nafasi naamini kukutana kwenu kutakuwa na faida kwenu wote na hili suala linahitaji utayari wako tu, hayo mengine yote yatakushangaza na kukusisimua zaidi! Kama uko tayari niambie nimpigie simu hapa hapa mbele yako, la kama unadhani hauko tayari pia niambie nimweleze sasa hivi,” Mafuru aliongeza huku macho yake yakiwa yameweka kituo kwenye uso wa Madame Norah.

Madame Norah alishusha pumzi za ndani kwa ndani, alikaa kimya kwa takriban dakika mbili akifikiria sana bila kupata majibu.

“Unaweza kunidokeza, ni mambo gani hayo ambayo unayajua lakini mimi siyajui?” hatimaye Madame Norah alivunja tena ukimya, alikuwa bado ana wasiwasi.

“Ni mambo mazito ambayo hayahitaji kuzungumzwa hapa na wala nisingeweza kukueleza kwenye simu. Ni wewe, yeye na mimi tu tunaopaswa kuendelea kuyajua kwa sasa, labda hadi hapo baadaye kama itahitajika,” Mafuru alisisitiza.

Okay, nipo tayari kuonana naye Paradise Club saa kumi na mbili jioni,” Madame Norah alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

* * * * *

Saa kumi jioni, Winifrida Kolimba alikuwa anatembea kwa maringo yaliyoonekana wazi. Hayakuwa maringo ya kutafuta kiki bali alijua wazi alivyokuwa mrembo na wengi walimchukulia kama malaika aliyekuwa ameshushwa duniani kimakosa, hivyo kuonesha maringo ilikuwa ni kichagizo tu cha jinsi alivyo.

Alikuwa na umbile dogo lililovutia mno na kuonekana wazi hata kama angevaa sare za shule, umbile lake lilimshawishi kila mwanamume aliyekamilika kumwangalia kwa uchu wa mahaba mazito. Ilikuwa vigumu sana kwa Winifrida kupita mbele ya mwanamume bila kukata shingo kumwangalia. Kiukweli alikuwa amezawadiwa urembo wa kutosha!

Kwa umbile lake na ile miondoko ya maringo alizidi kutoa tafsiri ya kuwa na ule uzuri usiomithilika, hasa kwa sababu ya weupe wake wa asili usiochanganywa na vipodozi vya aina yoyote na hivyo kuwafanya wanaume wakware wachanganyikiwe, pasipo kujali kama alikuwa mwanafunzi.

Jioni hiyo Winifrida alikuwa anatoka twisheni akiwa amevaa sketi ya rangi ya samawati, blauzi ya rangi ya pundamilia ya mikono mirefu na begi kubwa la madaftari alilokuwa amelibeba mgongoni, na alikuwa anatembea taratibu kando kando ya barabara iliyoelekea mtaani kwao eneo la Tabata Chang’ombe, jijini Dar es Salaam.

Wanafunzi wengine waliokuwa wameongozana naye walikuwa wakimkodolea macho wakati akitembea taratibu huku akionekana kutokuwa na haraka. Ni kweli hakuwa na haraka maana safari yake ilikuwa inaishia mtaa ule ule.

Mbele yake kulikuwa na wanafunzi wengine watatu wa kike walioonekana wakitembea kwa kujikongoja kutokana na uchovu. Wote walikuwa wamebeba mabegi makubwa yaliyowaelemea kwa uzito.

Winifrida alikuwa akiwacheka na kuwafanyia mzaha. Mara kwa mara walikuwa wakigeuka kumtazama kwa hasira lakini yeye aliendelea kuwafanyia mzaha.

Walionekana kumsubiri ili wampe ‘displini’ lakini yeye aling’amua na kusimama kupisha kwanza gari lipite kisha alivuka barabara kuwakwepa na kuelekea upande wa pili wa ile barabara, kwani alikuwa amefika usawa wa nyumbani kwao.

Wale wanafunzi walikonyezana kisha wakavuka barabara kuelekea upande wa pili wakiwa na lengo la kutaka kumkamata lakini Winifrida aligundua hila yao na kukimbilia ndani huku akiendelea kuwafanyia mzaha.

Alipoingia sebuleni, alijitupa kwenye sofa na kulibwaga begi lake juu ya sofa, kisha akajiegemeza kwa mgongo na kupeleka macho yake kuangalia juu ya dari huku akionekana kuwaza.

Mara simu yake iliyokuwa kwenye begi la madaftari ilianza kutoa mtetemo uliomshtua sana, aliangalia huku na kule kuhakikisha hakukuwa na mtu yeyote aliyeshtukia kisha aliinuka haraka, akachukua begi lake na kukimbilia chumbani kwake.

“Jacky, nilishakwambia usinipigie simu hadi nikubip… sasa hivi nipo nyumbani, tutaongea usiku,” Winifrida alisema kwa sauti ya kunong’ona mara tu alipoingia chumbani kwake, kisha aliikata ile simu na kuizima kabisa.

Alizungusha macho yake kukitazama kile chumba chake kwa makini, kilikuwa kikubwa kikiwa na kitanda kikubwa cha samadari cha futi sita kwa sita, cha mbao ngumu za mninga kikiwa na droo mbili kila upande na juu ya droo hizo kulikuwa na taa mbili zilizotoa mwanga hafifu.

Kilikuwa na kabati la nguo la ukutani na pembeni ya lile kabati kulikuwa na meza ya vipodozi yenye kioo kirefu cha kujitazama. Chumba pia kilikuwa na madirisha mawili mapana yaliyofunikwa kwa mapazia marefu yenye nakshi za michoro ya maua yaliyodariziwa vizuri na kuyafanya yapendeze.

Winifrida alijibwaga juu ya kitanda kilichokuwa kimetandikwa vizuri kwa shuka la rangi ya waridi lililofumwa maua katikati akionekana kuchoka, kisha akajilaza chali, miguu kaining’iniza sakafuni na kushusha pumzi. Sasa alionekana kujiwa na mawazo, aligaragara juu ya kitanda kile, kisha aliuchukua mmoja wa mito miwili iliyovikwa foronya rangi moja na ya lile shuka na kuukumbatia halafu akajilaza kifudifudi.

Hapo tena fikra zilianza kutembea kichwani mwake na kuaza kujiuliza vipi angeweza kuendelea kuvikabili vishawishi kutoka kwa wanaume wakware waliokuwa wakimwita kila alikopita? Na vipi angeweza kuyakabili mapenzi ya kijana Jackson yaliyoanza kumwingia moyoni na kuitawala akili yake ilhali yu bado mwanafunzi?

Alifikiria kwa kitambo kidogo huku fikra zikizidi kuranda na kupigana vikumbo ndani ya kichwa chake, mara aligutuka na kunyanyuka kutoka pale kitandani. Sasa mawazo yote aliyokuwa nayo yalipeperuka kwa muda na kuanza kuvua zile nguo alizovaa.

Alipogeuka alikikabili kile kioo kirefu cha kujitazama kilichopachikwa kwenye meza ya vipodozi, na kama kioo kile kilikuwa kikimtua, aliinuka na kukisogelea. Alianza kujianglia kwenye kioo namna alivyoumbika. Alijitazama na kujitazama tena, halafu akageuka na kujitazama huku na huku na alipohisi hajajifaidi bado, alikwenda kufunga mlango.

Alisimama mbele ya kioo akaendelea kuvua nguo zake na kubakiwa na chupi tu. Alijishika kiunoni kwa mikono yake na kujitazama tena huku na huku. Alijigeuza nyuma na kujiangalia matiti yake na kuyatomasatomasa huku akiyachezea.

Endelea kufuatilia stori hii hadi mwisho ili uyajue yote yaliyojificha ndani ya taxi...
 
Taxi - (47)

Ilipoishia jana

Winifrida alijibwaga juu ya kitanda kilichokuwa kimetandikwa vizuri kwa shuka la rangi ya waridi lililofumwa maua katikati akionekana kuchoka, kisha akajilaza chali, miguu kaining’iniza sakafuni na kushusha pumzi. Sasa alionekana kujiwa na mawazo, aligaragara juu ya kitanda kile, kisha aliuchukua mmoja wa mito miwili iliyovikwa foronya rangi moja na ya lile shuka na kuukumbatia halafu akajilaza kifudifudi.

Hapo tena fikra zilianza kutembea kichwani mwake na kuanza kujiuliza vipi angeweza kuendelea kuvikabili vishawishi kutoka kwa wanaume wakware waliokuwa wakimwita kila alikopita? Na vipi angeweza kuyakabili mapenzi ya kijana Jackson yaliyoanza kumwingia moyoni na kuitawala akili yake ilhali yu bado mwanafunzi?

Alifikiria kwa kitambo kidogo huku fikra zikizidi kuranda na kupigana vikumbo ndani ya kichwa chake, mara aligutuka na kunyanyuka kutoka pale kitandani. Sasa mawazo yote aliyokuwa nayo yalipeperuka kwa muda na kuanza kuvua zile nguo alizovaa.

Alipogeuka alikikabili kile kioo kirefu cha kujitazama kilichopachikwa kwenye meza ya vipodozi, na kama kioo kile kilikuwa kikimtua, aliinuka na kukisogelea. Alianza kujianglia kwenye kioo namna alivyoumbika. Alijitazama na kujitazama tena, halafu akageuka na kujitazama huku na huku na alipohisi hajajifaidi bado, alikwenda kufunga mlango.

Alisimama mbele ya kioo akaendelea kuvua nguo zake na kubakiwa na chupi tu. Alijishika kiunoni kwa mikono yake na kujitazama tena huku na huku. Alijigeuza nyuma na kujiangalia matiti yake na kuyatomasatomasa huku akiyachezea.

sasa endelea...

Alijigeuza tena mbele na nyuma na mara kwa ghafla, kama mtu aliyeshtuliwa, aliondoka mbele ya kioo na kufungua kabati la nguo, alitoa sketi fupi ya pundamilia na blauzi nyepesi nyeusi, akavaa haraka na kutoka.

* * * * *

Kwenye ukumbi wa kisasa wa chakula katika mgahawa wa Elli’s, Sammy na Elli walikuwa wameketi kwenye kona moja ukumbini wakinywa sharubati na kuongea. Sammy alikuwa na wasiwasi kuhusu namna ambavyo angemkabili mkewe kumweleza suala la kununua gari, kwa kuwa hakuwa amemshirikisha tangu mwanzo.

“Ukweli hata mimi najiuliza, utamwelezaje mkeo, kwamba hili gari umelipataje?” Elli alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.

“Hata sijui, maana ataniuliza kwa nini hatukushauriana kwanza kabla sijalinunua!” Sammy alisema huku akishusha pumzi.

“Kwa hiyo bado utaendelea kumficha kuhusu matatizo ya kazini kwako?” Elli alimuuliza Sammy huku akimkazia macho.

Sammy aliachia tabasamu, akashusha pumzi za ndani kwa ndani na kuzungusha macho yake mle ukumbini, aliwaangalia kwa muda wateja wachache waliokuwemo mle ndani muda huo, kisha akatoa leso mfukoni na kufuta paji la uso wake.

“Sidhani kama bado nahitaji kumficha ukweli, nimefikia uamuzi wa kumweleza kila kitu leo, natumai atanielewa,” Sammy alisema na kumeza mate kutowesha koo lake.

“Ni bora ufanya hivyo, maana hizi ni changamoto tu katika maisha na kila mtu humtokea, isitoshe mkeo ni mwelewa sana,” Elli alisema huku akibetua kichwa chake akionesha kukubaliana na Sammy.

“Kumficha mkeo ni kuruhusu matatizo zaidi yaibuke ndani ya ndoa yenu, hasa pale atakapokuja kujua kuwa ulimficha. Si hivyo tu, anaweza kunichukia hata mimi kwa kudhani nilikupotosha. Kwa hiyo jaribu kuweka mambo wazi ili mjadili na msonge mbele,” Elli alisisitiza na kumfanya Sammy ashushe pumzi.

“Sasa vipi kuhusu suala la vibali? Nataka gari lianze biashara mara moja.”

“Suala la vibali niachie mimi, hilo limo ndani ya uwezo wangu. Ninaye mtu kwenye mamlaka husika, ni ndani ya siku tatu tu kila kitu kitakuwa kimekamilika,” Elli alisema akimhakikishia Sammy. Na hapo tabasamu pana likachanua kwenye uso wa Sammy.

* * * * *

Saa kumi na mbili kamili Madame Norah aliwasili katika viunga vya Paradise Club akiwa ndani ya gari lake aina ya Mercedes Benz E-Class la rangi nyeusi. Aliingia baada ya kuvuka vizuizi vitatu vyenye ulinzi wa uhakika.

Alikuwa amevaa suti nadhifu ya kike ya rangi ya kijivu iliyokuwa imemkaa vyema na kumpendeza, begani alitundika mkoba mzuri wa nguo ya pundamilia uliomgharimu fedha nyingi na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio.

Mkono wa kushoto alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe na mkono wake wa kulia alivaa saa ghali ya kike aina ya Cartier La Dona iliyotengenezwa kwa dhahabu nyeupe ya karati 18, ikiwa na gerentii ya miaka hamsini.

Aliambatana na wanaume wawili wenye miraba minne, walinzi wake waliokuwa wamevaa suti maridadi nyeusi, miwani mikubwa myeusi iliyofunika macho yao na miguuni walikuwa wamevaa buti ngumu nyeusi za ngozi imara ya mamba.

Madame Norah na walinzi wake waliwasili na kupokewa na Mafuru aliyekuwa akiwasubiri muda wote katika viunga vya maegesho ya Paradise Club, kisha aliwaongoza kuelekea ghorofani kwa Mr. Oduya.

Kama kawaida, wale walinzi hawakuwaruhusu wapite hivi hivi bila kukaguliwa, japo walikuwa na taarifa zao, waliwakagua na kuhakikisha hawakuwa na silaha au kitu chochote hatarishi walichobeba, kisha waliwaruhusu wapite.

Mafuru aliwaongoza kuingia katika sebule kubwa walikomkuta Mr. Oduya akiongea na simu lakini mara tu alipowaona alisitisha mara moja maongezi na mtu aliyekuwa akiongea naye kwenye simu na kusimama kwa heshima kumlaki Madame Norah, huku uso wake ukipambwa na tabasamu la bashasha.

“Madame, karibu sana Paradise Club,” Mr. Oduya alisema huku akimpa mkono Madame Norah.

“Ahsante sana mheshimiwa Rais mtarajiwa,” Madame Norah alisema kwa utani na kuwafanya wote waangue kicheko.

“Mdomo wako uwe wa heri, na iwe kama usemavyo,” Mr. Oduya alisema huku akiendelea kucheka kwa furaha kisha aliwaelekeza wageni wake sehemu ya kuketi.

“Madame ni furaha yangu kukutana nawe siku ya leo na kabla ya yote
ninapenda kwanza kusema ahsante sana kwa kukubali mwaliko wangu wa kutaka kuonana nawe jioni hii,” Mr. Oduya aliongeza baada ya wote kuketi kitako.

“Kiukweli mwaliko wako umenishtua sana,” Madame Norah alisema huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.

“Najua, hata hivyo mimi ni nduguyo kabisa, tena ndugu wa damu…”

“Undugu huo veepe, mbona sikuelewi! Wewe Jaluo na mimi Mbondei wapi na wapi!” Madame Norah alisema huku akiendelea kumtazama Mr. Oduya kwa makini zaidi.

“Ni ndugu kwa kuwa wote ni Watanzania, hata hivyo kabla ya yote sijui mtatumia vinywaji gani?” Mr. Oduya aliuliza huku akiwatazama kwa zamu.

“Nadhani ungeeleza kwanza ulichoniitia, suala la vinywaji siyo lililonileta hapa,” Madame Norah alisema huku akionekana kuwa makini zaidi, hakuwa na muda wa kupoteza.

Okay, sitaki nichukue muda mrefu sana wa kuongea nawe… kwa kifupi nimefuatilia baadhi ya shughuli unazozifanya na nimejikuta nikiguswa sana. Hongera sana kwa kujitoa kusaidia jamii, ni wengi tunajaribu kufanya kama unavyofanya lakini wengi hatufanyi kwa kujitolea kama unavyofanya. Nimeguswa zaidi na hiki ulichoamua kukianzisha sasa…” Mr. Oduya alisema na kunyamaza kidogo. Madame Norah alibaki kimya akimsikiliza lakini akiwa makini kuliko simba jike.

Inaendelea...
 
Taxi - (47)

Ilipoishia jana

Winifrida alijibwaga juu ya kitanda kilichokuwa kimetandikwa vizuri kwa shuka la rangi ya waridi lililofumwa maua katikati akionekana kuchoka, kisha akajilaza chali, miguu kaining’iniza sakafuni na kushusha pumzi. Sasa alionekana kujiwa na mawazo, aligaragara juu ya kitanda kile, kisha aliuchukua mmoja wa mito miwili iliyovikwa foronya rangi moja na ya lile shuka na kuukumbatia halafu akajilaza kifudifudi.

Hapo tena fikra zilianza kutembea kichwani mwake na kuanza kujiuliza vipi angeweza kuendelea kuvikabili vishawishi kutoka kwa wanaume wakware waliokuwa wakimwita kila alikopita? Na vipi angeweza kuyakabili mapenzi ya kijana Jackson yaliyoanza kumwingia moyoni na kuitawala akili yake ilhali yu bado mwanafunzi?

Alifikiria kwa kitambo kidogo huku fikra zikizidi kuranda na kupigana vikumbo ndani ya kichwa chake, mara aligutuka na kunyanyuka kutoka pale kitandani. Sasa mawazo yote aliyokuwa nayo yalipeperuka kwa muda na kuanza kuvua zile nguo alizovaa.

Alipogeuka alikikabili kile kioo kirefu cha kujitazama kilichopachikwa kwenye meza ya vipodozi, na kama kioo kile kilikuwa kikimtua, aliinuka na kukisogelea. Alianza kujianglia kwenye kioo namna alivyoumbika. Alijitazama na kujitazama tena, halafu akageuka na kujitazama huku na huku na alipohisi hajajifaidi bado, alikwenda kufunga mlango.

Alisimama mbele ya kioo akaendelea kuvua nguo zake na kubakiwa na chupi tu. Alijishika kiunoni kwa mikono yake na kujitazama tena huku na huku. Alijigeuza nyuma na kujiangalia matiti yake na kuyatomasatomasa huku akiyachezea.

sasa endelea...

Alijigeuza tena mbele na nyuma na mara kwa ghafla, kama mtu aliyeshtuliwa, aliondoka mbele ya kioo na kufungua kabati la nguo, alitoa sketi fupi ya pundamilia na blauzi nyepesi nyeusi, akavaa haraka na kutoka.

* * * * *

Kwenye ukumbi wa kisasa wa chakula katika mgahawa wa Elli’s, Sammy na Elli walikuwa wameketi kwenye kona moja ukumbini wakinywa sharubati na kuongea. Sammy alikuwa na wasiwasi kuhusu namna ambavyo angemkabili mkewe kumweleza suala la kununua gari, kwa kuwa hakuwa amemshirikisha tangu mwanzo.

“Ukweli hata mimi najiuliza, utamwelezaje mkeo, kwamba hili gari umelipataje?” Elli alimuuliza Sammy huku akimtazama kwa makini.

“Hata sijui, maana ataniuliza kwa nini hatukushauriana kwanza kabla sijalinunua!” Sammy alisema huku akishusha pumzi.

“Kwa hiyo bado utaendelea kumficha kuhusu matatizo ya kazini kwako?” Elli alimuuliza Sammy huku akimkazia macho.

Sammy aliachia tabasamu, akashusha pumzi za ndani kwa ndani na kuzungusha macho yake mle ukumbini, aliwaangalia kwa muda wateja wachache waliokuwemo mle ndani muda huo, kisha akatoa leso mfukoni na kufuta paji la uso wake.

“Sidhani kama bado nahitaji kumficha ukweli, nimefikia uamuzi wa kumweleza kila kitu leo, natumai atanielewa,” Sammy alisema na kumeza mate kutowesha koo lake.

“Ni bora ufanya hivyo, maana hizi ni changamoto tu katika maisha na kila mtu humtokea, isitoshe mkeo ni mwelewa sana,” Elli alisema huku akibetua kichwa chake akionesha kukubaliana na Sammy.

“Kumficha mkeo ni kuruhusu matatizo zaidi yaibuke ndani ya ndoa yenu, hasa pale atakapokuja kujua kuwa ulimficha. Si hivyo tu, anaweza kunichukia hata mimi kwa kudhani nilikupotosha. Kwa hiyo jaribu kuweka mambo wazi ili mjadili na msonge mbele,” Elli alisisitiza na kumfanya Sammy ashushe pumzi.

“Sasa vipi kuhusu suala la vibali? Nataka gari lianze biashara mara moja.”

“Suala la vibali niachie mimi, hilo limo ndani ya uwezo wangu. Ninaye mtu kwenye mamlaka husika, ni ndani ya siku tatu tu kila kitu kitakuwa kimekamilika,” Elli alisema akimhakikishia Sammy. Na hapo tabasamu pana likachanua kwenye uso wa Sammy.

* * * * *

Saa kumi na mbili kamili Madame Norah aliwasili katika viunga vya Paradise Club akiwa ndani ya gari lake aina ya Mercedes Benz E-Class la rangi nyeusi. Aliingia baada ya kuvuka vizuizi vitatu vyenye ulinzi wa uhakika.

Alikuwa amevaa suti nadhifu ya kike ya rangi ya kijivu iliyokuwa imemkaa vyema na kumpendeza, begani alitundika mkoba mzuri wa nguo ya pundamilia uliomgharimu fedha nyingi na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio.

Mkono wa kushoto alikuwa amevaa bangili nyingi za pembe na mkono wake wa kulia alivaa saa ghali ya kike aina ya Cartier La Dona iliyotengenezwa kwa dhahabu nyeupe ya karati 18, ikiwa na gerentii ya miaka hamsini.

Aliambatana na wanaume wawili wenye miraba minne, walinzi wake waliokuwa wamevaa suti maridadi nyeusi, miwani mikubwa myeusi iliyofunika macho yao na miguuni walikuwa wamevaa buti ngumu nyeusi za ngozi imara ya mamba.

Madame Norah na walinzi wake waliwasili na kupokewa na Mafuru aliyekuwa akiwasubiri muda wote katika viunga vya maegesho ya Paradise Club, kisha aliwaongoza kuelekea ghorofani kwa Mr. Oduya.

Kama kawaida, wale walinzi hawakuwaruhusu wapite hivi hivi bila kukaguliwa, japo walikuwa na taarifa zao, waliwakagua na kuhakikisha hawakuwa na silaha au kitu chochote hatarishi walichobeba, kisha waliwaruhusu wapite.

Mafuru aliwaongoza kuingia katika sebule kubwa walikomkuta Mr. Oduya akiongea na simu lakini mara tu alipowaona alisitisha mara moja maongezi na mtu aliyekuwa akiongea naye kwenye simu na kusimama kwa heshima kumlaki Madame Norah, huku uso wake ukipambwa na tabasamu la bashasha.

“Madame, karibu sana Paradise Club,” Mr. Oduya alisema huku akimpa mkono Madame Norah.

“Ahsante sana mheshimiwa Rais mtarajiwa,” Madame Norah alisema kwa utani na kuwafanya wote waangue kicheko.

“Mdomo wako uwe wa heri, na iwe kama usemavyo,” Mr. Oduya alisema huku akiendelea kucheka kwa furaha kisha aliwaelekeza wageni wake sehemu ya kuketi.

“Madame ni furaha yangu kukutana nawe siku ya leo na kabla ya yote
ninapenda kwanza kusema ahsante sana kwa kukubali mwaliko wangu wa kutaka kuonana nawe jioni hii,” Mr. Oduya aliongeza baada ya wote kuketi kitako.

“Kiukweli mwaliko wako umenishtua sana,” Madame Norah alisema huku akimtazama Mr. Oduya kwa makini.

“Najua, hata hivyo mimi ni nduguyo kabisa, tena ndugu wa damu…”

“Undugu huo veepe, mbona sikuelewi! Wewe Jaluo na mimi Mbondei wapi na wapi!” Madame Norah alisema huku akiendelea kumtazama Mr. Oduya kwa makini zaidi.

“Ni ndugu kwa kuwa wote ni Watanzania, hata hivyo kabla ya yote sijui mtatumia vinywaji gani?” Mr. Oduya aliuliza huku akiwatazama kwa zamu.

“Nadhani ungeeleza kwanza ulichoniitia, suala la vinywaji siyo lililonileta hapa,” Madame Norah alisema huku akionekana kuwa makini zaidi, hakuwa na muda wa kupoteza.

Okay, sitaki nichukue muda mrefu sana wa kuongea nawe… kwa kifupi nimefuatilia baadhi ya shughuli unazozifanya na nimejikuta nikiguswa sana. Hongera sana kwa kujitoa kusaidia jamii, ni wengi tunajaribu kufanya kama unavyofanya lakini wengi hatufanyi kwa kujitolea kama unavyofanya. Nimeguswa zaidi na hiki ulichoamua kukianzisha sasa…” Mr. Oduya alisema na kunyamaza kidogo. Madame Norah alibaki kimya akimsikiliza lakini akiwa makini kuliko simba jike.

Inaendelea...

CC the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater Bigjahman moneytalk marybaby nipo2 ram kisukari Smart911 Madame S carbamazepine Astelia culture gal Prisoner of hope Mine eyes kuku mweus Thad hearly Shunie moneytalk Tumosa Mine eyes Kudo swahiba92 ludist Toyota escudo Clkey macson3 boga la kiangazi LEGE Smart911 Richard irakunda skfull popie Krizy Beat hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Mlenge Kacheda mjasiliamali Laki Si Pesa cocochanel kinusikwetu big jambo mludego Shupavu Kacheda mjasiliamali
 
Taxi - (48)

“Najua huamini hiki ninachosema, lakini sote lengo letu ni moja tu, kuisaidia jamii yetu ingawa ni kwa njia tofauti kidogo. Kwa hiyo ninataka tushirikiane katika suala hili ili wewe upate fedha za kusaidia wahitaji na mimi inisaidie katika kampeni yangu ya kuwania urais,” Mr. Oduya alisema kwa sauti tulivu.

“Hilo haliwezekani Mr. Oduya. Siwezi kuwa na ushirika na wewe,” Madame Norah alisema huku akitingisha kichwa chake taratibu.

“Kama unadhani hilo haliwezekani then you’re very wrong, my dear,” Mr. Oduya alisema huku akitabasamu.

I’m not wrong, Siku zote niko sahihi kwenye masuala yanayohusu mustakabari wangu,” Madame Norah alisema kwa kujiamini huku akiwa amekunja sura yake.

“Lakini hilo ni jambo la kwanza kuna jambo la pili litakalokusisimua zaidi, ninakwenda kukuonesha kitu ambacho you’ve been dying to see,” Mr. Oduya alisema na kuinuka huku akimtaka Madame Norah naye ainuke. Muda huo huo walinzi wa Madame Norah nao wakainuka wakiwa tayari kwa lolote. Mr. Oduya aliwageukia huku akiachia tabasamu.

“Mnaweza tu kusubiri hapa, she’ll be fine,” Mr. Oduya alisema lakini wale walinzi walionesha kutokukubaliana naye.

“Msijali, hawezi kunifanya kitu chochote kibaya,” Madame Norah aliwaambia walinzi wake, wakaonekana kumtii kisha alimfuata Mr. Oduya kuelekea chumbani huku wakiwaacha walinzi wake na Mafuru pale sebuleni. Mlango wa chumbani ulifunguliwa, wakaingia.

Madame Norah alisimama ghafla akiwa anashangaa, alikuwa anatazamana na mwanadada mrembo aliyekuwa ameketi kitandani huku machozi yakimbubujika machoni kwake utadhani mirija ya machozi ilikuwa imepasuka.

Madame Norah alimtazama kwa makini Zainab, alihisi kumfahamu ingawa hakujua walikutana wapi, aligeuka kumtazama Mr. Oduya huku akiendelea kujiuliza ni wapi alikutana na mrembo yule kwani sura yake haikuwa ngeni kabisa machoni kwake.

What is the meaning of this, Mr. Oduya?” (Hii maana yake nini, Oduya?) Madame Norah alimuuliza Mr. Oduya kwa mshangao akiwa haelewi kilichokuwa kikiendelea.

“Mi’ nilidhani ungefurahi baada ya kukutana na huyu mtu, kwani ulikuwa unaomba usiku na mchana ukutane naye, au siyo!” Mr. Oduya alimwambia Madame Norah huku akitabasamu.

“Ni nani, mbona kama…!” Madame Norah alitaka kusema huku akimwangalia Zainab kwa makini lakini hakumalizia sentensi yake kwani Zainab alishindwa kujizuia, alimrukia Madame Norah na kumkumbatia kwa nguvu huku akizidi kububujikwa na machozi.

“Dada Nuru!” Zainab alisema huku akilia kwa furaha na kuzidi kumng’ang’ania Madame Norah aliyekuwa bado amepigwa na butwaa.

“Kwa-ni wewe n-ni nani?” Madame Norah aliuliza huku akijaribu kujinasua kutoka kwenye mikono ya Zainab aliyeendelea kulia kwa uchungu huku akiwa hataki kumwachia.

“Mimi Zainab Semaya, mdogo wako!” Zainab alisema huku akilia.

Zainab who! Oh my God!” Madame Norah alimaka kwa mshangao mkubwa sana. Hakuwa ametegemea kabisa kuonana na Zainab baada ya miaka mingi kupita.

Madame Norah hakuweza kujizuia, donge la fadhaa lilimkaba kooni, alijikuta akisononeka sana rohoni, mara kikohozi kidogo kilimtoka na nyuma yake wimbi la machozi lilikuja mbio, alijikuta akilia sana huku akimkumbatia Zainab.

Kwa muda wa dakika kadhaa hali ndani ya chumba kile iligeuka kuwa sehemu ya vilio, wote walijikuta wakilia pasipo kupenda. Baada ya kitambo fulani Madame Norah alimwachia Zainab na kufuta machozi yake, kisha alimwangalia kwa makini.

“Kweli wewe ni Zainab, sura yako haijabadilika kabisa!” Madame Norah alisema huku akishusha pumzi ndefu. Zainab alibaki kimya, alikuwa anafuta machozi.

“Nadhani sasa niwaache, kwa vyovyote mtakuwa na mengi ya kuzungumza,” Mr. Oduya alisema huku akiachia tabasamu, kisha akaanza kupiga hatua kutoka, alipoufikia mlango aligeuka kumtazama Madame Norah.

“Nadhani sasa huna sababu ya kukataa kushirikiana na mimi,” alisema na kufungua mlango, akatoka na kuurudisha nyuma yake.

* * * * *

Winifrida alikuwa amesimama kwenye karo la kuoshea vyombo, alikuwa akisuuza vyombo viwili vitatu alivyolia chakula na kuweka mabaki ya vyakula kwenye chombo maalumu cha kuhifadhia uchafu. Alionekana kuwaza mbali sana.

Pendo alikuwa ananyata nyuma yake kwa tahadhari kubwa akitaka kumshtua lakini Winifrida alihisi uwepo wa mtu nyuma yake, aligeuka haraka lakini Pendo aliwahi kujificha huku akitabasamu.

Winifrida alipuuza na kuendelea kusuuza vyombo. Pendo alijitokeza tena na kuanza kunyata taratibu kumsogelea, Winifrida aligeuka haraka huku akikodoa macho yake kwa hofu na kumuona Pendo akiwa takriban hatua tatu nyuma yake.

“Mtu mwenyewe hujui hata kunyatia,” Winifrida alisema huku akiachia kicheko hafifu.

“Eeh umeogopa! Umeogopa!” Pendo alisema kwa sauti ya juu huku akicheka kisha aliondoka na kuelekea ndani akimwacha Winifrida anamalizia kusuuza vyombo huku akionekana kuwaza mbali.

Joyce alitokea na kusimama mlangoni, akamtazama Winifrida kwa makini. Macho yake yalikuwa yakikitazama zaidi kifua cha Winifrida aliyekuwa amevaa blauzi nyepesi nyeusi na sketi fupi ya pundamilia.

Blauzi ya Winifrida ilikuwa imeloa maji kidogo eneo la kifuani na kuzifanya chuchu zake zilizochomoza juu ya matiti yake magumu ya mviringo ndani ya blauzi nyepesi aliyovaa kiasi cha kuvuta hisia za watu zionekane waziwazi.

“Wee Winnie,” Joyce alimwita Winifrida na kumshtua sana.

Winifrida aliiachia bilauri aliyokuwa akiizuuza kwa mshtuko, ikaanguka sakafuni na kupasuka. Aligeuza shingo yake kutazama kule mlangoni ambako sauti ya Joyce ilitokea na macho yake yaligongana na macho ya Joyce aliyekuwa amesimama akimtazama kwa makini.

“Umenishtua sana, wifi. Nilisikia moyo umefanya, pah!” Winifrida alilalamika huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani. Aliyaondosha macho yake kwa aibu huku akiachia tabasamu la aibu.

“Kwa nini umeshtuka sana! Kwani ulikuwa unawaza nini?” Joyce alimuuliza Winifrida huku akimkazia macho.

“Aka! Nilikuwa siwazi chochote!” Winifrida alijitetea huku akionekana kutaharuki kidogo. Alimtazama wifi yake kwa jicho la wizi na kugundua kuwa alikuwa bado akimtazama kwa makini.

Inaendelea...
 
Taxi - (49)

“Kwani kuna nini, wifi?” Winifrida aliuliza huku uso wake ukionesha wasiwasi.

“Usihofu, wifi yangu, kama umemaliza kuosha vyombo njoo sebuleni, nataka tuongee mambo ya kawaida tu yanayokuhusu. Hatujawahi kukaa tukazungumza vizuri,” Joyce alisema kwa sauti tulivu ya upole huku akiachia tabasamu.

“Sawa, wifi,” Winifrida alisema huku akiendelea kuwa na wasiwasi, hakujua wifi yake alitaka kumwambia nini. Alikusanya vyombo vyake na kuelekea ndani.

Baada ya dakika chache, Winifrida na Joyce walikuwa wameketi sebuleni, peke yao tayari kwa mazungumzo. Joyce alikuwa amemuondoa Pendo na kumtaka akacheze nje.

“Sasa, Winnie, unafahamu kwamba hivi sasa wewe ni binti uliyepevuka,” Joyce alisema huku akimtazama kwa makini.

Uchangamfu aliokuwa nao Winifrida ulitoweka ghafla na akawa makini akionesha woga kiasi. Alikaa kimya, Joyce alimkazia macho kwa makini.

“Nadhani unaelewa?” Joyce alimuuliza huku akizidi kumkazia macho.

Winifrida alibaki kimya akiangalia viganja vyake alivyoviweka juu ya mapaja yake. Joyce aliiona hali ya Winifrida kwa jinsi alivyoingiwa na hofu, alitabasamu na kutafuta namna ya kuyaelekeza mazungumzo.

“Nimekwambia usihofu, wifi yangu, nataka nikwambie hivi, mwili wako sasa una mabadiliko makubwa sana. Umekua,” Joyce alisema na kunyamaza kidogo akiendelea kumtazama Winifrida kwa makini.

Winifrida alivuta pumzi ndefu na kifua chake kikapanda na kushuka. Alitabasamu kidogo kwa ahueni huku akimtupia jicho la wizi wifi yake.

“Najua umeshawahi kuona tofauti mwilini mwako, au siyo?” Joyce alimuuliza Winifrida kwa namna ya kubembeleza alipoona yupo kimya.

“Naziona, wifi,” Winifrida alijibu kwa sauti ya chini.

“Kama zipi?” Joyce aliuliza huku macho yake yakiweka kituo kwenye uso wa Winifrida.

“Wifi bwana!” Winifrida alisema kwa aibu huku akitazama sakafuni.

“Usiniogope, hapa tupo wawili tu, mimi na wewe, na wote ni wanawake. Huna sababu ya kunionea aibu, wifi yangu,” Joyce alisema kwa sauti tulivu ya upole.

“Sawa, wifi,” Winifrida alijibu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Sawa, tufanye kwamba umeziona hizo tofauti, je, unachukua hatua gani kuzikabili?” Joyce aliuliza tena kwa upole.

“Hatua?” Winifrida aliuliza kwa mshangao huku akimtazama Joyce kutaka ufafanuzi wa neno hilo.

“Labda niulize hivi, ni mambo gani unakumbana nayo kila siku unapokuwa shuleni au ukiwa njiani?” Joyce alijaribu kufafanua.

Winifrida alishusha tena pumzi ndefu za ndani kwa ndani, na taratibu kujiamini kukaanza kumrudia.

“Kama kufuatwa na wavulana, wananiita na kuniambia wananitaka.”

“Sasa hao wavulana unawachukuliaje, maana inaonekana ni wengi wanaokuita na kukutaka!” Joyce aliuliza huku akiachia tabasamu.

“Mimi wananikera tu, huwa siwajibu kitu,” Winifrida alisema huku akiukunja uso wake.

“Unayosema ni ya kweli, wifi?” Joyce alimuuliza akiwa kamkazia macho usoni.

“Kweli, wifi,” Winifrida alisema huku akipitisha kidole chake cha shahada shingoni na kukikung’uta hewani.

“Mbona hujawahi kuniambia?” Joyce alimuuliza tena huku akimkazia macho.

“Nilikuwa naogopa.”

“Uliogopa kunieleza? Kwa nini uniogope?” Joyce aliuliza na kumfanya Winifrida abaki kimya asijue la kusema. Alikuwa akinyonganyonga vidole vyake.

“Hakuna mvulana yeyote uliyewahi kumkubalia au hata aliyewahi kukushika shika kifuani na kukwambia una matiti mazuri?”

Winifrida alitingisha kichwa chake kukataa. Joyce alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu.

“Hebu angalia kifua chako, jinsi matiti yako yanavyochomoza juu ya blauzi na nguo nyingine unazovaa! Usipende kuvaa nguo nyepesi kama hivyo, mtoto wa kike unatakiwa kuusitiri mwili wako ili kuwapunguzia wavulana shauku,” Joyce alisema kwa sauti ya upole.

“Kama ulikuwa umeanza mchezo mbaya au ulifikiria kuuanza naomba uache kabisa, kazania masomo, wanaume ni walaghai tu, watakudanganya wanakupenda kumbe wanataka kukuchezea tu, na pengine wakuambukize magonjwa ya zinaa au ukimwi, nadhani unafahamu hilo. Pia kuna mimba, nadhani umenielewa vizuri wifi yangu,” Joyce alitoa nasaha zake.

Winifrida alibetua kichwa chake kukubali.

“Sawa, kuanzia leo anza kuusitiri mwili wako vizuri, usivae nguo kama hizi mbele ya kaka yako, si heshima. Inabidi sasa uwe unavaa sidiria nilizokununulia ili kusitiri matiti yako, na hivi vinguo vyako vya ajabu ajabu usivivae tena. Ni hayo tu wifi yangu,” Joyce alisema na kuinuka, akaelekea jikoni.

Winifrida alishusha pumzi ndefu za ahueni.

* * * * *

Saa kumi na mbili na nusu jioni, Sammy alikuwa akiendesha gari lake aina ya Cadillac DeVille akipita barabara iliyotoka Tabata Barakuda kuelekea nyumbani kwake Tabata Chang’ombe.

Aliiacha ile barabara kubwa ya lami na kuchepuka kuingia kushoto akiifuata barabara iliyoelekea nyumbani kwake, alizipita nyumba kadhaa za jirani na kufika mbele ya nyumba yake. Alikunja na kuingiza gari lake kwenye uwanja mpana wa mbele ya nyumba, akasimamisha gari mbele ya geti kubwa jeusi lililokuwa mbele ya ile nyumba yake na kupiga honi.

Baada ya kitambo kifupi geti dogo lililokuwa kwenye lile geti kubwa likafunguliwa nusu na muda huo huo Winifrida akiwa ameongozana na Pendo walichungulia nje na kuliona lile gari lakini hawakujua ni la nani.

Walibaki wakilitazama kwa makini kwa kitambo huku wakionekana kujiuliza maswali yaliyokosa majibu. Sammy aliendelea kutulia ndani ya gari lake akiwatazama kwa tabasamu pasipo kuwashtua. Pendo alilisogelea karibu lile gari na mara akamuona Sammy na kuruka kwa furaha.

“Baba! Baba!” Pendo aliita kwa nguvu na kumfanya Winifrida asogee karibu zaidi, akamtambua Sammy na kuachia yowe dogo la mshangao huku akibaki mdomo wazi.

“Ha! Kaka Sammy!” Winifrida alisema huku akifungua geti kubwa haraka kuruhusu lile gari liingie ndani ya uzio wa ile nyumba.

Inaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom