Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
- Thread starter
- #61
Bado kuna kikao kinaendelea sasa kati ya timu ya Balozi na Barrick wakikutana na Mhe.Ndesamburo na kikao kinaendelea kwa mujibu wa taarifa zilizonifikia hivi punde.
Bado kuna kikao kinaendelea sasa kati ya timu ya Balozi na Barrick wakikutana na Mhe.Ndesamburo na kikao kinaendelea kwa mujibu wa taarifa zilizonifikia hivi punde.
Huna haja ya kumpigia simu Tundu Lisu wala Shivji wala shirika lolote.Lobbying maana yake ni ushawishi and not anything illegal.Cha msingi ni kwa wabunge kuelewa kuwa huyo balozi anatetea maslahi ya waliomtuma hivyo basi na wao wasisahau maslahi ya waliowatuma.
Pili tuache kufikiria kuandamana and all that crap, tutafute njia za sisi pia kulobby kwenye mabunge ya nchi nyingine,hii ndio dunia tukilialia tu hakuna tutakachopata.Stand up send our ambassadors to lobby all around the world.
Hawa jamaa wamejipanga na ni jukumu letu pia kujipanga kwani la sivyo watatufunga bao la kisigino, kuna taarifa kuwa serikalini wamewaambia kwa waende wakawasiliane na wabunge kwani wao serikali hawana haraka ila bunge likiamua kuwa mapendekezo yapitishwe basi hawana budi kuchukua agizo la bunge ,ila kama bunge likiamua vinginevyo basi watafuata maagizo ya bunge.
Huna haja ya kumpigia simu Tundu Lisu wala Shivji wala shirika lolote.Lobbying maana yake ni ushawishi and not anything illegal.Cha msingi ni kwa wabunge kuelewa kuwa huyo balozi anatetea maslahi ya waliomtuma hivyo basi na wao wasisahau maslahi ya waliowatuma.
Hawa jamaa naambiwa kuwa wpo bize sana huko bungeni na wanakutana na kila mbunge,kinachotisha ni kuwa wanakutana na Mbunge mmoja mmoja sasa huenda huko ndio wanawaahidi kitu ama safari ama kamradi ka maji si unajua tena wabongo na mzungu?
Lazima kupiga kelele this time.
Hapo kuna kazi kubwa, inabidi tutumie Mugabeism kwa Wabunge wetu kutumia syle ya Mugabe liwalo na liwe!
Lakini pia ni ujumbe kwetu na kwa Wabunge kuwa Wawekezaji ndiyo wanaofaidi zaidi raslimali za nchi yetu kuliko sisi na ndo maana huyo Balozi ame-panic.
Wabunge kumbukeni hili:
"Watanzania Si Mabwege Tena" Dk Mwakyembe.
Wananchi tunafuatilia kwa ukaribu masuala ya mustakabali wa nchi yetu
Tatizo mikataba yote hiyo kuanzia energy mpaka madini imesha kuwa signed,sasa kuibadilisha lazima pande zote zikubaliane na kama tukiamua kutumia utemi kwa sababu ni madini yetu kumbukeni kuna consequence ambazo zinaweza kuwa mbaya kuliko,hapa tuna deal na mafia capitalist ambao its all about money...kwa ambao wame deal na wazungu wanaelewa nini maana ya mkataba kwao,huwezi leo uka sign hivi na kesho ukaja kulia bad deal,tumeumizwa sana nchi hii na wazungu kwa ajiri ya umbumbu wa kuingia mikataba tusioijua,kwa hiyo nikiona kinachoendelea TZ nacheka tuu maana najua tutapiga kelele tuu lakini mbavu wameshatubana na pa kutokea hakuna...dawa ni kutoingia hiyo mikataba tuu mpaka tubadilishe policy zetu,lakini tuliyoingia tunapoteza muda tuu labda tuombe negotiation nao ambacho hawa jamaa nawajua sio wabaya sana kwenye hilo na wanaweza kukubali ila kuwalazimisha hakuna kitu kama hicho...angalia IPTL ni 20 yrs na mpaka iishe na hakuna ujanja na juzi nasikia wametushtaki na serikali kuishia kuwalipa zaidi.
Koba,
Ukiangalia mifano ya Zambia na Congo hakuna cha pande zote kukubaliana.
Leo tukipata serikali makini isiyo ya CCM kuna uwezekano mkubwa wa mikataba hiyo kuwa abrogated kwa sababu halali kabisa, (ie: ilisainiwa kwa hongo, etc etc) Hakuna sababu ya kumshirikisha Barrick eti tujadiliane upya. Kwa mujibu wa Mzee Bomani, baadhi ya mikataba ililetwa nchini imeshaandikwa kabisa na hao wawekezaji na sisi tulichofanya ni kuweka saini tu. Sasa mikataba kama hiyo haina haja ya kukubaliana juu yake.
Hata kama bei ya dhahabu ni $1000 sisi hatutapata $30 ila ni 3% ya $300 ya bei wakati wa kusaini mikataba. hawaangalii bei kupanda. nadhani moja ya mapendekezo ya kamati itakuwa ni mrahaba kwenda sambamba na bei kupanda.
Kweli tutafute njia ya kutoburuzwa na hawa wazungu