UWEZO_WAKO
Member
- Nov 17, 2010
- 39
- 4
Na Lilian Lucas, Morogoro | Mwananchi
MKUU wa Mkoa mstaafu, Steven Mashishanga, amesema licha ya rais kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, angetakiwa kupunguza idadi ya wizara kufikia 15, ili kupunguza mzigo kwa Watanzania kuwahudumia.
Akizungumza nyumbani kwake jana, Mashishanga alisema rais amechelewa kutoa uamuzi licha ya kufahamu matatizo yaliyopo.
Mashishanga alisema rais kwa kuzingatia matatizo ya mfumko wa bei na uchumi, alitakiwa kupunguza idadi ya mawaziri kutokana na bajeti ya nchi kuwa finyu na angeweza kuongeza uwezo wa kuhudumia wananchi.
"Wakati wabunge wakijiandaa kwenda kwenye bajeti, ni wakati mzuri na mwafaka kwa rais wangu kupunguza idadi ya mawaziri, ili aweze kuhudumia Watanzania na angeona hali ya wananchi ilivyo asingekuwa na wizara zote hizi 30, ni nyingi kwa wakati tulionao," alisema.
Kuhusu CCM, Mashishanga alisema rais kama Mwenyekiti wa chama ana haja ya kuangalia kinavyofanya kazi hivi sasa, kwani kimekuwa kimya na huku kikijua fika matatizo yanayokikabili kwa ndani.
"Nashangaa chama changu kilivyokuwa kimya wakati wote! Kinatakiwa kujiangalia upya, ni hatari kama hakitajirekebisha wakati kinatakiwa kuwatetea wananchi kwa kila hali, kwani hakikujua kama kuna uvujaji wa mali? Kwa nini kilikaa kimya kisipojiangalia upya kuna hatari," alisema Mashishanga.
Pia, alipongeza wabunge walioonyesha uzalendo kuhakikisha mawaziri waliofanya vibaya kwenye wizara zao wanaondolewa na kuchukuliwa hatua, kwani bila kufanya hivyo mabadiliko hayo yasingefanyika.
Alisema licha ya rais kufanya mabadiliko hayo, aliwaomba Watanzania kutomlaumu badala yake waendelee kutoa ushauri bila kuchoka, huku akiwataka mawaziri walioteuliwa kutomwangusha.
MKUU wa Mkoa mstaafu, Steven Mashishanga, amesema licha ya rais kufanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri, angetakiwa kupunguza idadi ya wizara kufikia 15, ili kupunguza mzigo kwa Watanzania kuwahudumia.
Akizungumza nyumbani kwake jana, Mashishanga alisema rais amechelewa kutoa uamuzi licha ya kufahamu matatizo yaliyopo.
Mashishanga alisema rais kwa kuzingatia matatizo ya mfumko wa bei na uchumi, alitakiwa kupunguza idadi ya mawaziri kutokana na bajeti ya nchi kuwa finyu na angeweza kuongeza uwezo wa kuhudumia wananchi.
"Wakati wabunge wakijiandaa kwenda kwenye bajeti, ni wakati mzuri na mwafaka kwa rais wangu kupunguza idadi ya mawaziri, ili aweze kuhudumia Watanzania na angeona hali ya wananchi ilivyo asingekuwa na wizara zote hizi 30, ni nyingi kwa wakati tulionao," alisema.
Kuhusu CCM, Mashishanga alisema rais kama Mwenyekiti wa chama ana haja ya kuangalia kinavyofanya kazi hivi sasa, kwani kimekuwa kimya na huku kikijua fika matatizo yanayokikabili kwa ndani.
"Nashangaa chama changu kilivyokuwa kimya wakati wote! Kinatakiwa kujiangalia upya, ni hatari kama hakitajirekebisha wakati kinatakiwa kuwatetea wananchi kwa kila hali, kwani hakikujua kama kuna uvujaji wa mali? Kwa nini kilikaa kimya kisipojiangalia upya kuna hatari," alisema Mashishanga.
Pia, alipongeza wabunge walioonyesha uzalendo kuhakikisha mawaziri waliofanya vibaya kwenye wizara zao wanaondolewa na kuchukuliwa hatua, kwani bila kufanya hivyo mabadiliko hayo yasingefanyika.
Alisema licha ya rais kufanya mabadiliko hayo, aliwaomba Watanzania kutomlaumu badala yake waendelee kutoa ushauri bila kuchoka, huku akiwataka mawaziri walioteuliwa kutomwangusha.