Stereotype...

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,839
...Kumradhi 'wataoguswa ndipo', lakini na maswali yangu kadhaa;

...hivi ni kwanini watu wafupi 'wengi' wanakuwa wabishi, wakorofi, wagomvi?

...au ni mgongano tu wa mawazo?
 
...hivi kwanini watu wa pwani "wengi" wanapenda anasa, i.e kuchezesha ngoma, kuoa wake wengi, kucheza bao, kukaa vijiweni na wingi wa habari?

...au ni mgongano tu wa mawazo?
 
...hivi ni kwanini konda/utingo wanapowajaza abiria katika dala dala mpaka kupumua inakua shughuli hakuna anayethubutu kubishana nao?

mbaya zaidi mabasi ya mikoani; utingo/konda wanapowaamuru abiria wachuchumae, abiria wanatii bila hiyana 'wasijeonekana na trafiki! ...kwanini?


...au ni mgongano tu wa mawazo?
 

...hivi ni kwanini wanataaluma i.e maprofesa na madakitari wa mimea, binadamu, wanyama, uchumi, na wafanyabiashara 'wengi' wakubwa wanakimbilia Ubunge, haswa kwa kupitia CCM? kuna nini nasi tujiandae? au ndio ...'alalaye usimwamshe?'


au ni mgongano wa mawazo tu?
 

...hivi ni kwanini tuna serikali ya muungano, na serikali ya Zanzibar tu? Kwanini 'wengi' hawataki kuzungumzia muungano wa serikali moja, au angalau wa serikali tatu (ikiwemo ya bara?), bila kuleta porojo za gharama za uendeshaji?

...hivi 9/Dec 'kila mwaka' tunasherehekea uhuru wa nchi gani iwapo hakuna nchi inayoitwa Tanganyika?


...sijatumwa, ni mgongano tu wa mawazo!
 
...Kumradhi 'wataoguswa ndipo', lakini na maswali yangu kadhaa;

...hivi ni kwanini watu wafupi 'wengi' wanakuwa wabishi, wakorofi, wagomvi?

...au ni mgongano tu wa mawazo?

....wana complex ya kujisikia wao wako duni na kudharauliwa kutokana na ufupi wao kwa hiyo muda mwingi wanakuwa wanatumia kujionyesha kwamba sivyo kama watu wafikiriavyo...na wao wanajua na wana uwezo kama mtu yoyote yule mwenye urefu wa kawaida....in other words they are always out to prove something....
 
kazi ipo mwaka huu

wazee wakuchambua leteni majibu au ndo tupigie mstari kuwa ni mgongano wa mawazo????

...ila nina kaswali kangu hapa
kwa nini ukimuuliza mtanzania haujambo atakujibu sijabo hata kama anaumwa??
 

...hivi ni kwanini tuna serikali ya muungano, na serikali ya Zanzibar tu? Kwanini 'wengi' hawataki kuzungumzia muungano wa serikali moja, au angalau wa serikali tatu (ikiwemo ya bara?), bila kuleta porojo za gharama za uendeshaji?

...hivi 9/Dec 'kila mwaka' tunasherehekea uhuru wa nchi gani iwapo hakuna nchi inayoitwa Tanganyika?


...sijatumwa, ni mgongano tu wa mawazo!

hili Mtikila (kama sikosei)kuna kipindi alilivalia njuga sijui liliishia vipi.

Hiyo ya Dec 9, umeniamsha na mimi, ngoja nitafakari vizuri,,,
 

...hivi ni kwanini wanawake wabaya 'wengi wao' wanariiiiiinga?
 
...eti ni kweli kuna watu wanazaliwa 'tayari' wana genes za kuwa Gays, na lesbians? ...au 'eti' ndio Mw'Mungu alivyotaka wawe, kwahiyo wanastahili haki zote ikiwamo kuoana?
 
...hivi kweli unaamini WEWE umetokana na nyani au Sokwe? si kwamba ni zao la Adam na Hawa?... kama unaamini 'umetokana na sokwe', kwanini Sokwe hawaendelei na evolution? Mbona tunaona 'evolution' ya wadudu kama kipepeo ambao wana stage kama ; Egg >> larvae >> pupa >> Adult hiyo sio Evolution???

fikiria; Sperm + Egg >> Embryo >> mammal , hiyo haitoshi kuwa 'Evolution' wanayotaka tuamini ?


...au ni mgongano wa mawazo tu????
 

...hivi ni kwanini 'wengi' wasokuwa nacho, A.K.A masikini A.K.A 'mlalahoi' ufahari wake ni kuoa wake wengi na watoto wengiii (watano na kuendelea), wakati tajiri ufahari wake mtoto mmoja au wawili?


...mgongano wa mawazoo bila kuangalia itikadi/imani za dini
 

...hivi ni kweli 'ilituishi' tunahitaji ROHO, na sio UBONGO (unao programme shughuli za mwili mzima), maana mtu akiwa Brain dead anahitaji Life support machines kuishi, lakini wakati huo huo 'wenye imani' wanadai ROHO ipo (wapi mwilini?) na ikitoka ndio hurudi hivyo!?, ...au ndio 'tuamini tu'?


...au ni mgongano tu wa imani/mawazo, watu wa 'ROHO' wanavutia kwao na wana sayansi wanavutia kwao?
 
Mara nyingi warefu huwa wanakuwa wakimya sana tofauti na wafupi. Pia hii inaonesha kitu kile kile, kuwa wao wanaojiona tayari wako superior, hawana haja ya kujionesha tena, mwili unatosha.
 

...hivi ni kwanini 'wengi' wasokuwa nacho, A.K.A masikini A.K.A 'mlalahoi' ufahari wake ni kuoa wake wengi na watoto wengiii (watano na kuendelea), wakati tajiri ufahari wake mtoto mmoja au wawili?
...mgongano wa mawazoo bila kuangalia itikadi/imani za dini

Mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe!!
Muulize Che - Nkapa
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom