Jitihada
Senior Member
- Feb 6, 2011
- 156
- 10
Habari zenu wanajamvi? Kwanza poleni kwa makali ya mgao unaoendelea hivi sasa na bila ya kuwa na dalili ya makali ya mgao kupungua achilia mbali kuisha kabisa maana hata wakubwa wanalijua hilo! Ok, sasa leo naomba kujua hatua za kisheria za kuzichukua endapo vitu vyangu vya umeme vikaungua kwasababu ya mgao wa umeme, Maana hali ya mgao inaelekea kubaya, tanesco wamekuwa wakikata na kuurudisha umeme mara kwa mara tena kwa mda mfupimfupi na tayari washaniunguzia vyombo vyangu vya umeme, friji moja, TV moja pamoja na pasi. Nawasilisha hoja.