Stephen Hawking's Final Book Says There's 'No Possibility' of God in Our Universe

Swali zuri. Suala la watu kujitenga au kuhitilafiana ni kutokana na ujinga,mataminio ya nafsi na ujuaji.

Kila jambo lina chanzo,na ukisoma vizuri utakuta ya kuwa asili ya Mola wetu kuchagua miongoni mwa waja wake kuwa mitume au manabii ni baada ya waja kuanza kufanya shirki/ushirikina.

Binadamu tumeumbwa na utashi,uhuru wa kutenda na kuchagua na tukapewa nyenzo za kuupokea ukweli. Huu uhuru tuliopewa ndio tunautumia vibaya. Leo hii hakuna mtu anae lazimishwa kufanya uovu zaidi ya hiari yake mwenyewe,na kuna wakati mwanadamu anaweza kufanya jambk huku akijua kabisa jambo hili lina madhara lakini akafanya,hapa nani wa kumlaumu ? Kuuliza swali kwanini kuna madhara ni uvivu wa kufikiri na kujiuliza kwanini unafanya jambo ovu au lenye madhara ni matumizi mazuri sana ya akili.

Mitume wote walikuwa na imani moja,walikuja kutangaza wito kwa waja wote wamuabudu Mola mmoja na wampige vita mshirikina na wajitenge na taghuut. Hii ndio kauli ya mitume wote,hapa utaona ya imani ni moja,ila mitume walitofautiana sheria kutokana na mahitaji. Ndio maana sheria ya Mussa si ya Issa ,ya Issa si ya Daudi si ya Suleymaan na si ya Muhamman amani ya Allah iwe juu yao.

Nakomea hapa kufupisha maelezo,kama utakuwa na swaki kwa haya nikiyo kueleza utauliza.
kk
Mungu yupo na dini ya kweli ni matendo mema

Ila bado hatujaweza kuthibitisha uwepo wake , hilo usibishe dada !
 

Mistari ya Biblia inayosema dunia haizunguki.

1 Chronicles 16:30: "He has fixed the earth firm, immovable."

Psalm 93:1: "Thou hast fixed the earth immovable and firm ..."

Psalm 96:10: "He has fixed the earth firm, immovable ..."

Psalm 104:5: "Thou didst fix the earth on its foundation so that it never can be shaken."

Isaiah 45:18: "...who made the earth and fashioned it, and himself fixed it fast

Unaweza kutupa uthibitisho wa hiki unachosema?
Uthibitisho wa kipi ninachosema?

Uthibitisho gani?

Ili kitu kikubalike kwamba ni uthibitisho kwako, kinahitaji kukidhi vigezo gani?
 
Nacheka sana,huwezi kutofautisha kauli hizo mbili sababu zote zinaingia katika maana moja,kauli ya kwanza ni swali la kutaka kujua na kauli ya pili ni kuweka bayana au tamayizi au kuelezea na kukiri.

Sasa tatizo lipo kwako usie weza kutoa maana moja katika swali na kauli ya kukiri,hali ya kuwa viwili hivyo ni sawa.

Socrates Method sina haja ya kuijua,sababu kujua kwake na kutokuijua ni sawa. Naweza kukuuliza moja tu ambalo najua hutaweza kulijibu,achilia mbali kuhusu Socrates Method,lakini hapa nakuuliza swali,kwanini hutilii shaka uwepo wa Socrates wakati hujawahi kumuona zaidi ya kusikia habari zake ? Lakini je nikikuuliza swali unithibitishie kama Socrates aliwahi kuishi duniani unaweza kufanya hivyo ?

Nipo ....
amina sana NGUDU YANGU ..HAWA WATU NDIO HAPA TUNAWAKAMATA TUNAWAONA EMPTY KABISA...KUNA MMOJA ANAPINGA UWEPO WA YESU KUA ALIISHI ILA ANAKUBALI GALILEO ALIKUWEPO...HAHAHAHHAHA NIMEFURAHI SANA
 
Kitu cha pili fikiria hichi kitu

Tupo watu takribani , let us say kama ishirini kwenye majadiliano

Ni watu wa dini tofauti tofauti lakini katikati yetu kuna watu wawili hawaamini Mungu yupo

Kwa umoja wetu sisi watu kumi na nane wa dini tofaut tofaut si mwislamu si mkristo si mbudha si mnani yaan wote tukashirikiana kupinga wale watu wawili

Wale watu wawili wakaona isiwe tabu wakajitenga na sisi , tuliobaki tukaanza kuondoka kwenda sehemu

Katika maongezi yetu tukaanza kuwaponda wale jamaa , aah mafala sana wale hawaamini uwepo wa Mungu , kwa kweli tukawasema sana

Lakini mbudha akaibua hoja , hivi nyie wakristo na waislamu mungu wenu sio wa kweli ,, teh

Tukajitenga nae

Tukabaki wakristo na waislam , tukaanza kumponda mbudha , aaah yule jamaa ni multi orse jinga kabisa

Mara teh , sheikh akaibuka nyie mnaamini Allah

Wakristo wakaja juu , "we fala unasemaje

Kilichofuata ni mapigano ambayo hata hapa jukwaa la dini huwa tunayaona matusi kejeli , kati ya hizi dini mbili

Mara wakristo wakaenda njia yao huko walijitenga kinoma

Yaanu tukamkuta

Msabato

Mlokole

Mroma

Muanglican

Mpentecost

Mmoravian

Mluthet

Na wwngine wengi , ambao hawakuaminiana kabsa kuhusu mungu wanayemuabudu

Mara huku waislam nao wakajitenga

Nadhan unajua kuna makundi mangapi ya waislamu

Je unadhani , hilo la kujitenga linathababishwa na nini , kwa nini Mungu hakuamua kuwe na njia moja ya kumjua yeye

Usibishe hapa , unawakosoa sana wakristo jukwaa la dini

Je Mungu wao ni wauongo ?

Je wako ni wa kweli ?

Je tumwamini Mungu yupi ?

Kwa nini anajicontradict hivi

Kuna sehemu wanakula kitimoto

Mara huku hawali

Hapo ni kwa wakristo huku

Unadhani sababu ni ipi

Huo mtengano uliotokea kwa watu ishirini , je unaweza kuwa uthibitisho wa kwamba mungu yupo au hayupo ?!
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo, kungekuwa hakuna mtengano huu.

Mtengano huu unaonesha Mungu huyo hayupo, ni hadithi tu zimetungwa na watu.

Ndiyo maana kila utamaduni una hadithi yake tofauti.
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo, kungekuwa hakuna mtengano huu.

Mtengano huu unaonesha Mungu huyo hayupo, ni hadithi tu zimetungwa na watu.

Ndiyo maana kila utamaduni una hadithi yake tofauti.
Teh ....

Mi siwez kumthibitisha ...

Ila naamini yupo ...

Kuna wanasayansi wenzangu wa neuro hapa John Hopkins hawataki kuelewa kabisa story za Mungu kuwepo
 
Uwepo wa socrates unaweza kuthibitishwa

Unawezaje kuthibitisha uwepo wa Socrates ? Au unatumia nyenzo gani kuthibitisha uwepo wake ?
Lakini uwepo Wa Mungu kuthibitishwa ndo umeibua yote haya !!

Unafikiri ni sahihi kuwepo au kuibuka haya ? Je ushawahi kujiuliza ya kuwa wanao kana uwepo wa Muumba wameegemea misingi gani ? Je wako sahihi ?
Kiranga anataka athibitishiwe Mungu yupo , mimi naamini Mungu yupo ila siwezi kuthibitisha
Hapo ndipo wengi hatumuelewi kiranga na hatumsaidii sisi kama watu ambao tunaamini Mungu yupo

Tunamshambulia , na amekuwa victim

Kiranga hajawahi kutaka kuthibitishiwa uwepo wa Mungu ukipima katika mizani ya kielimu. Huwezi kuomba thabati ukianza na kukanusha,na kama angekuwa anataka kuthibitishiwa uwepo wa Mungu asingekuwa anakanusha mpaka leo. Kwa maana yeye ana imani yake tayari,ambayo alitakiwa kwanza athibitishe yeye kuwa Mungu yupo. Ajabu jambo asilolijua ni kuwa hiyo imani yake imejengeka katika ujinga,kwani siku zote swali lakini ni "Kama Mungu ni mjuzi wa yote,......... kwanini ameruhusu maouvu au majanga yatokee ?"

Naendelea ....
 
Unawezaje kuthibitisha uwepo wa Socrates ? Au unatumia nyenzo gani kuthibitisha uwepo wake ?


Unafikiri ni sahihi kuwepo au kuibuka haya ? Je ushawahi kujiuliza ya kuwa wanao kana uwepo wa Muumba wameegemea misingi gani ? Je wako sahihi ?


Kiranga hajawahi kutaka kuthibitishiwa uwepo wa Mungu ukipima katika mizani ya kielimu. Huwezi kuomba thabati ukianza na kukanusha,na kama angekuwa anataka kuthibitishiwa uwepo wa Mungu asingekuwa anakanusha mpaka leo. Kwa maana yeye ana imani yake tayari,ambayo alitakiwa kwanza athibitishe yeye kuwa Mungu yupo. Ajabu jambo asilolijua ni kuwa hiyo imani yake imejengeka katika ujinga,kwani siku zote swali lakini ni "Kama Mungu ni mjuzi wa yote,......... kwanini ameruhusu maouvu au majanga yatokee ?"

Naendelea ....
Kiranga njoo umjibu dada ako

Mi sielewi maswal yake
 
Teh ....

Mi siwez kumthibitisha ...

Ila naamini yupo ...

Kuna wanasayansi wenzangu wa neuro hapa John Hopkins hawataki kuelewa kabisa story za Mungu kuwepo
Kuamini unaruhusiwa kuamini lolote, hata lile ambalo halipo.

Na kifalsafa unaruhusiwa uhuru wa kuamini. Hili jambo halihitaji kwenda na fact. Ndiyo maana uhuru wa kuabudu upo katika katiba na Universal Declaration of Human Rights.

Kuna sababu hao wanasayansi wa Hopkins hawaamini habari za Mungu.

Ukiangalia nchi zenye maendeleo ya elimu kama Northern Europe utaona imani ya Mungu ni ndogo sana.

Halafu ukiangalia nchi zenye kiwango cha chini cha elimu rasmi huku kwetu Africa utaona watu wanasema imani ya Mungu iko juu sana.

Halafu ukiwaangalia hata hao wanaosema wanamuamini Mungu, ukiangalia matendo yao, utakuta kwa sehemu kubwa wanapiga soga tu, hawaishi kama watu wanaoamini kweli Mungu yupo. Kwa sababu hata kwa watu wanaosema wanaamini Mungu yupo, ni vigumu kuishi kama unaamini Mungu yupo wakati hayupo.

Ndiyo maana katika dunia hii, wanaoishi kwa maandiko ya huyo anayesemwa Mungu (ambayo yana contradiction kibao) ni wachache sana. Hata kama unaweza sheria za msingi tu kama kigezo.
 
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo, kungekuwa hakuna mtengano huu.

Huku ni kufikiri kitoto,ukisema hivyo ungekuwa wapi uhuru wa kuchagua na yangekuwa waoi matumizi ya akili ?

Lakini,Allah anaweka yaliyo bora na anajua kupangilia mambo na taratibu zake hazibadiliki.

Lakini swali kwako ambalo huwezi kulijibu,umejuaje hilo ?
Mtengano huu unaonesha Mungu huyo hayupo, ni hadithi tu zimetungwa na watu.

Lakini kielimu hapa hujaonyesha kama Mungu hayupo sababu majibu yalikutangulia kitambo sana kabla hujukiani kama utazaliwa.

Na kuishia kusema "...ni hadithi tu zimetungwa na watu." bila kuonyesha zilitungwa vipi na kwanini na kwa nani na umejuaje ? Huku nu kukimbia mjadala.
 
Kiranga njoo umjibu dada ako

Mi sielewi maswal yake
I swore off this calcified cretin.

Hana basic qualifications za kufanya mjadala nami.

Namuambia haelewi Socratic method ni nini, ananiambia hana haja ya kuelewa.

Hana hata utashi wa kuelewa asichoelewa, sasa nitajibizana naye ili iweje?

Nimemu ignore, hata anachoandika sikioni.
 
Kuamini unaruhusiwa kuamini lolote, hata lile ambalo halipo.

Na kifalsafa unaruhusiwa uhuru wa kuamini. Hili jambo halihitaji kwenda na fact. Ndiyo maana uhuru wa kuabudu upo katika katiba na Universal Declaration of Human Rights.

Kuna sababu hao wanasayansi wa Hopkins hawaamini habari za Mungu.

Ukiangalia nchi zenye maendeleo ya elimu kama Northern Europe utaona imani ya Mungu ni ndogo sana.

Halafu ukiangalia nchi zenye kiwango cha chini cha elimu rasmi huku kwetu Africa utaona watu wanasema imani ya Mungu iko juu sana.

Halafu ukiwaangalia hata hao wanaosema wanamuamini Mungu, ukiangalia matendo yao, utakuta kwa sehemu kubwa wanapiga soga tu, hawaishi kama watu wanaoamini kweli Mungu yupo. Kwa sababu hata kwa watu wanaosema wanaamini Mungu yupo, ni vigumu kuishi kama unaamini Mungu yupo wakati hayupo.

Ndiyo maana katika dunia hii, wanaoishi kwa maandiko ya hiyo anayesemwa Mungu (ambayo yana contradiction kibao) ni wachache sana. Hata kama unaweza sheria za msingi tu kama kigezo.
Mwanzon ni kama walkua wanantenga kutokana na misimam yangu ya dini

Ila nikaamua kuacha kuwa na misimamo , nisiwalazimishe waamini Mungu yupo

Urafiki ukarejea !

Wala nao hawanisumbui
 
I sweared off this calcified cretin.

Hana basic qualifications za kufanya mjadala nami.

Namuambia haelewi Socratic method ni nini, ananiambia hana haja ya kuelewa.

Hana hata utashi wa kuelewa asichoelewa, sasa nitajibizana naye ili iweje?

Nimemu ignore, hata anachoandika sikioni.
 
Mungu yupo na dini ya kweli ni matendo mema

Ila bado hatujaweza kuthibitisha uwepo wake , hilo usibishe dada !

Nacheka sana,kuniita mimi "dada" hakubadilishi ukweli na wanaume tuna lugha zetu,na katika wanaume kuna wanaume. Vipi ukitaka kunifedhehesha nini ? Nakupa udhuru na hivi ndivyo nilivyo mimi.

Huwezi kutenda mema bila kujua kwanini unatenda wema na unatenda wema kwa ajili ya nani ? Hapa ndipo wanatoka wote watendao wema huku wana imani potofu,nia batili na hapa wanatoka mabudha,wamajusi,waabudu mizimu,washirikina na mfano wao.
 
Nacheka sana,huwezi kutofautisha kauli hizo mbili sababu zote zinaingia katika maana moja,kauli ya kwanza ni swali la kutaka kujua na kauli ya pili ni kuweka bayana au tamayizi au kuelezea na kukiri.

Sasa tatizo lipo kwako usie weza kutoa maana moja katika swali na kauli ya kukiri,hali ya kuwa viwili hivyo ni sawa.

Socrates Method sina haja ya kuijua,sababu kujua kwake na kutokuijua ni sawa. Naweza kukuuliza moja tu ambalo najua hutaweza kulijibu,achilia mbali kuhusu Socrates Method,lakini hapa nakuuliza swali,kwanini hutilii shaka uwepo wa Socrates wakati hujawahi kumuona zaidi ya kusikia habari zake ? Lakini je nikikuuliza swali unithibitishie kama Socrates aliwahi kuishi duniani unaweza kufanya hivyo ?

Nipo ....

Mufti siku hizi unajengeka _Naona unajenga hoja kwa logic .....hatari sana

Ilabaki kidogo nidhani sio wewe..!?
 
Mwanzon ni kama walkua wanantenga kutokana na misimam yangu ya dini

Ila nikaamua kuacha kuwa na misimamo , nisiwalazimishe waamini Mungu yupo

Urafiki ukarejea !

Wala nao hawanisumbui
Rafiki ambaye atataka kunitenga kwa sababu ya tofauti za kifalsafa kuhusu dini, huyo hakufaa kuwa rafiki yangu tangu mwanzo.

Wajamaica wana msemo wao mmoja naishi kwa kuutumia maisha yangu yote.

Wanasema "Me no beg no friend". Siombelezi urafiki, unatokea tu naturally.

Mimi nina marafiki kuanzia ma Buddhist monks mpaka wachungaji.
 
Nacheka sana,kuniita mimi "dada" hakubadilishi ukweli na wanaume tuna lugha zetu,na katika wanaume kuna wanaume. Vipi ukitaka kunifedhehesha nini ? Nakupa udhuru na hivi ndivyo nilivyo mimi.

Huwezi kutenda mema bila kujua kwanini unatenda wema na unatenda wema kwa ajili ya nani ? Hapa ndipo wanatoka wote watendao wema huku wana imani potofu,nia batili na hapa wanatoka mabudha,wamajusi,waabudu mizimu,washirikina na mfano wao.
Sawa

Siku njema
 
I swore off this calcified cretin.

Hana basic qualifications za kufanya mjadala nami.

Namuambia haelewi Socratic method ni nini, ananiambia hana haja ya kuelewa.

Hana hata utashi wa kuelewa asichoelewa, sasa nitajibizana naye ili iweje?

Nimemu ignore, hata anachoandika sikioni.

Nacheka sana,usikimbie maswali nawajua vizuri sana,kama wakubwa zako walsindwa walishindwa ni muhali wewe kuweza,nimekuuliza maswali mangapi hujibu ?

Ajabu hata kanuni za mijadala huzijui,hakuna kanuni ya mijadala inayokutaka kukimbia maswali.

Socratic Method nilikwambia kuijua kwake na kutokuijua ni sawa,yaani hakunipunguzii chochote wala kuniongezea lolote,sasa wewe ndio ungetumia njia kujenga hoja yako,ajabu ukatolea mfano wa mwalimu na waanfunzi wake na ukasahau nimekuuliza swali katika muktadha gani. Hili ni tatizo la kukaririshwa kabla ya kuelewa,na umekuwa kama punda aliye bebeshwa mizigo ya vitabu na hafaidiki na vitabu hivyo.
 
Mkuu Kiranga na dmatemu na wengine mnaopinga uwepo was Mungu, hebu niambieni, mnachukuliaje Uchawi, Uganga, Elimu ya Nyota na Elimu ya majini?

Na je, nini chanzo cha uhai?
Define uchawi, Uganga, Elimu ya Nyota. Elimu ya majini.

Kwa sababu uchawi unaweza kuushangaa kumbe ni tricks saikolojia imechanganywa na kemia na baiolojia.

Uganga unaweza kuwa baiolojia na tricks za saikolojia.

Elimu ya Nyota unaweza kuwa tricks za saikolojia na unajimu.

Elimu ya majini inaweza kuwa sayansi ya ku navigate baharini, kwenye mito na maziwa ya maji.

Swali lako halina maana sana kama halina definition ya terms.

Hilo moja.

Halafu, kama kweli uchawi upo, kama unavyoaminika na wengi, watu wanaua wenzao kwa uchawi, huo ni ushahidi kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.

Angekuwepo, asingeruhusu uchawi au uovu wowote uwepo.
 

Similar Discussions

25 Reactions
Reply
Back
Top Bottom