Stephen Hawking's Final Book Says There's 'No Possibility' of God in Our Universe

Kwa nini unauliza swali lililolenga katika jibu fulani, wakati huna ushahidi wowote kwamba huko ulikolenga kwa swali lako ndiko kwenye jibu?

Kwa nini unauliza mtoto gani kaweka jani la muembe mlangoni kwako, wakati hujui jani la muembe limekuja vipi mlangoni mwako?

Unajuaje limewekwa na mtoto?

Hivi nje ya "nani" kuna nini chenye kuweza kubuni ? Hii ni lugha mzee,haikwepi kwani ilianza yenyewe kabla ya hizi fani.
 
Mpaka sasa nilichogundua nikwamba biblia na quaran ni vitabu vilivyoandikwa na watu wakijaribu kumuelezea mungu na makusudi yake ktk ulimwengu na viumbe vyake, ndio maana utaona Luna makosa mengi kama unavyobainisha kila siku,

Naomba unipe makosa mawili tu kutoka kwenye Qur'aan.
 
Joshua akisimamisha jua" jua linatembea? Au Dunia ndio inazunguka jua?
aliongea ivo ili ieleweke kitendo kilichofanyika sasa ULITAKA ASEME JUSHUA ALISIMAMISHA DUNIA WATU WASINGEWEZA ELEWA NN KILIFANYIKA... KWA MANENO MENGINE JUA LILIKUA HALIONEKANI LIKIZIMA..MBONA INAELEWEKA SANA..WEWE NA WAJOMBA RAFIK ZAKO MNAOPINGA NDIO MNAJICHANGANYA ....HAYO MANENO HATA MTOTO MDOGO AKISOMA ATAELEWA KUA JUA LILIGANGA....

BIBLIA HAITAFSIRI KISAYANSI KAMA NYIE MTAKAVYO ILI MKOSOE..ILA HUKUUNA NENO HATA MOJA KWENYE BIBLIA LITAKALOPITA HATA NUKTA...DUNIA NA VYOTE VITABIPA ILA SIO ILE HOLY BIBLE
 
Hata Galileo Galilei aliposema dunia inazunguka jua, na si kweli kwamba jua linazunguka dunia kama kanisa na Biblia inavyosema, aliambiwa kakufuru. Akafungiwa nyumbani kwake baada ya kuomba msamaha bila sababu ili tu asiuawe.

Biblia inasema Mungu ameisimamisha dunia, haizunguki. Hilo tu linatakiwa kukuonesha Biblia imeandikwa na watu, si Mungu. Tena watu ambao hawakuwa na elimu ya kujua dunia inazunguka.

Miaka 350 baadaye, kanisa katoliki limeomba msamaha na kusema Galileo alikuwa sawa.

Galileo alikuwa mbele zaidi ya kanisa katika kujua ukweli, kwa kutumia majaribio ya kisayansi.

Unaweza kuthibitisha Mungu yupo na habari za kuwapo huyo Mungu si hadithi za watu tu?

Habari ya kanisa kuomba radhi kwa kumhukumu Galileo kimakosa iliandikwa na The New York Times hapa chini.

Wengine mpaka leo tunahukumiwa kimakosa na wanadini kama alivyohukumiwa Galileo. Labda miaka 350 ijayo watu wataelewa ukweli.


Mistari ya Biblia inayosema dunia haizunguki.

1 Chronicles 16:30: "He has fixed the earth firm, immovable."

Psalm 93:1: "Thou hast fixed the earth immovable and firm ..."

Psalm 96:10: "He has fixed the earth firm, immovable ..."

Psalm 104:5: "Thou didst fix the earth on its foundation so that it never can be shaken."

Isaiah 45:18: "...who made the earth and fashioned it, and himself fixed it fast

Unaweza kutupa uthibitisho wa hiki unachosema?
 
Teh.....



Mi nshawahi wauliza dini ya kweli ni ipi uislam au ukristo

Huyo zurri alichonijibu , sure ni idiot

Naomba unikumbushe nilichokujibu ? Si unajua sisi binadamu tuna sahau sahau.

Sasa huyo mwenzako nimemuuliza maswali madogo lakini kwa kushindwa kwake kujibu "amepanic" kama amesingiziwa ufisadi.

Nimemuuliza swali dogo na wewe unaweza kumsaidia pia : Vipi hatilii shaka uwepo wa Socrates wakati hajawahi kumuona zaidi ya kusikia habari zake ? Je anaweza kunipa ushahidi kama huyo Socrates aliwahi kuishi hapa duniani ?

Hapa ndipo utaona tofauti yetu na nyinyi,sisi tunafikiria juu ya ukamilifu wa mambo lakini nyinyi mnaongozwa na dhana na wasi wasi tele.
 
Naomba unikumbushe nilichokujibu ? Si unajua sisi binadamu tuna sahau sahau.

Sasa huyo mwenzako nimemuuliza maswali madogo lakini kwa kushindwa kwake kujibu "amepanic" kama amesingiziwa ufisadi.

Nimemuuliza swali dogo na wewe unaweza kumsaidia pia : Vipi hatilii shaka uwepo wa Socrates wakati hajawahi kumuona zaidi ya kusikia habari zake ? Je anaweza kunipa ushahidi kama huyo Socrates aliwahi kuishi hapa duniani ?

Hapa ndipo utaona tofauti yetu na nyinyi,sisi tunafikiria juu ya ukamilifu wa mambo lakini nyinyi mnaongozwa na dhana na wasi wasi tele.
cha kwanza naamini Mungu yupo , usiniweke kundi moja na kiranga
Umenisikia ?!
 
Kuna kitu wengi humu hamjamuelewa KIRANGA. Anachofanya ndicho walichofanya wanafalisafa wengi wa karne za nyuma sana. Sidhani kama Kiranga anapinga Uwepo wa Mungu, nadhani anachotafuta ni UKWELI.'' IF YOU WANT TO KNOW THE TRUTH, YOU MUST DOUBT EVERYTHING, EVEN THE TRUTH MUST BE DOUBTED''. Asumption za wanafalsafa wa zamani ndizo zilizopelekea UGUNDUZI wa mambo mengi makubwa kwenye hii Dunia. Hata wapo waliohukumiwa kifo kwa kuambiwa wamekufuru lakini baadae ikagundulika Asumption zao zilikuwa ni Sahihi. ndio maana wenzetu wazungu wanafika mbali sana lakini sisi bado tunateswa na imani na mtu anapohoji anaonekana anakufuru. NINACHOAMINI MIMI HATA HAWA WANAOHOJI UWEPO WA MUNGU SIDHANI KAMA WANAMKOSEA MUNGU BALI MUNGU ANAPENDEZWA NAO KWAKUWA WANAUTAFUTA UKWELI ZAIDI NA KUTAKA KUMJUA
Unaweza kutaja hoja tu yenye kuonesha Kiranga anatafuta ukweli na si kwamba anapinga uwepo wa Mungu? Maana huyo jamaa anajua kabisa kuwa watu hawawezi kuthibitisha uwepo wa Mungu na pia anajua kuwa kabisa mtu kushindwa kuthibitisha kitu haifanyi hicho kitu kuwa hakipo kama kweli kipo kitakuwepo tu,ila yeye pamoja na hivyo bado hoja yake kubwa humu ni kudai uthibitisho kwa sababu anajua hutoweza kuthibitisha na ndiyo anaposema hakuna Mungu na ndiyo maana watu hawawezi kuthibitisha. Kwahiyo unaweza ukajadiliana naye ila akishaona mjadala unamshinda ndipo anapotumia silaha yake ya kutaka uthibitisho ili akunyamazishe.

Sasa huyu hayupo kutafuta ukweli bali yupo kiushindani katika kupinga uwepo wa Mungu na ndiyo maana anajaribu kuwafanya watu waone hakuna Mungu kisa uthibitisho wakati anajua hakuna anayesema kuna Mungu kwa sababu kuna uthibitisho.
 
Huyo Kiranga amekuwa muoga sana siku hizi,unatakiwa umshajiishe aache uoga na asiwe anakimbia maswali.
Kitu cha pili fikiria hichi kitu

Tupo watu takribani , let us say kama ishirini kwenye majadiliano

Ni watu wa dini tofauti tofauti lakini katikati yetu kuna watu wawili hawaamini Mungu yupo

Kwa umoja wetu sisi watu kumi na nane wa dini tofaut tofaut si mwislamu si mkristo si mbudha si mnani yaan wote tukashirikiana kupinga wale watu wawili

Wale watu wawili wakaona isiwe tabu wakajitenga na sisi , tuliobaki tukaanza kuondoka kwenda sehemu

Katika maongezi yetu tukaanza kuwaponda wale jamaa , aah mafala sana wale hawaamini uwepo wa Mungu , kwa kweli tukawasema sana

Lakini mbudha akaibua hoja , hivi nyie wakristo na waislamu mungu wenu sio wa kweli ,, teh

Tukajitenga nae

Tukabaki wakristo na waislam , tukaanza kumponda mbudha , aaah yule jamaa ni multi orse jinga kabisa

Mara teh , sheikh akaibuka nyie mnaamini Allah

Wakristo wakaja juu , "we fala unasemaje

Kilichofuata ni mapigano ambayo hata hapa jukwaa la dini huwa tunayaona matusi kejeli , kati ya hizi dini mbili

Mara wakristo wakaenda njia yao huko walijitenga kinoma

Yaanu tukamkuta

Msabato

Mlokole

Mroma

Muanglican

Mpentecost

Mmoravian

Mluthet

Na wwngine wengi , ambao hawakuaminiana kabsa kuhusu mungu wanayemuabudu

Mara huku waislam nao wakajitenga

Nadhan unajua kuna makundi mangapi ya waislamu

Je unadhani , hilo la kujitenga linathababishwa na nini , kwa nini Mungu hakuamua kuwe na njia moja ya kumjua yeye

Usibishe hapa , unawakosoa sana wakristo jukwaa la dini

Je Mungu wao ni wauongo ?

Je wako ni wa kweli ?

Je tumwamini Mungu yupi ?

Kwa nini anajicontradict hivi

Kuna sehemu wanakula kitimoto

Mara huku hawali

Hapo ni kwa wakristo huku

Unadhani sababu ni ipi

Huo mtengano uliotokea kwa watu ishirini , je unaweza kuwa uthibitisho wa kwamba mungu yupo au hayupo ?!
 
Safi,msaidie hayo maswali kujibu.
Uwepo wa socrates unaweza kuthibitishwa

Kama jinsi uwepo wa mtume mohammad na Yesu kristo unavyoweza kuthibitishwa

Lakini uwepo Wa Mungu kuthibitishwa ndo umeibua yote haya !!

Kiranga anataka athibitishiwe Mungu yupo , mimi naamini Mungu yupo ila siwezi kuthibitisha
Hapo ndipo wengi hatumuelewi kiranga na hatumsaidii sisi kama watu ambao tunaamini Mungu yupo

Tunamshambulia , na amekuwa victim
 
Je unadhani , hilo la kujitenga linathababishwa na nini , kwa nini Mungu hakuamua kuwe na njia moja ya kumjua yeye

Swali zuri. Suala la watu kujitenga au kuhitilafiana ni kutokana na ujinga,mataminio ya nafsi na ujuaji.

Kila jambo lina chanzo,na ukisoma vizuri utakuta ya kuwa asili ya Mola wetu kuchagua miongoni mwa waja wake kuwa mitume au manabii ni baada ya waja kuanza kufanya shirki/ushirikina.

Binadamu tumeumbwa na utashi,uhuru wa kutenda na kuchagua na tukapewa nyenzo za kuupokea ukweli. Huu uhuru tuliopewa ndio tunautumia vibaya. Leo hii hakuna mtu anae lazimishwa kufanya uovu zaidi ya hiari yake mwenyewe,na kuna wakati mwanadamu anaweza kufanya jambk huku akijua kabisa jambo hili lina madhara lakini akafanya,hapa nani wa kumlaumu ? Kuuliza swali kwanini kuna madhara ni uvivu wa kufikiri na kujiuliza kwanini unafanya jambo ovu au lenye madhara ni matumizi mazuri sana ya akili.

Mitume wote walikuwa na imani moja,walikuja kutangaza wito kwa waja wote wamuabudu Mola mmoja na wampige vita mshirikina na wajitenge na taghuut. Hii ndio kauli ya mitume wote,hapa utaona ya imani ni moja,ila mitume walitofautiana sheria kutokana na mahitaji. Ndio maana sheria ya Mussa si ya Issa ,ya Issa si ya Daudi si ya Suleymaan na si ya Muhamman amani ya Allah iwe juu yao.

Nakomea hapa kufupisha maelezo,kama utakuwa na swaki kwa haya nikiyo kueleza utauliza.
Usibishe hapa , unawakosoa sana wakristo jukwaa la dini
kk
 
Je Mungu wao ni wauongo ?

Je wako ni wa kweli ?

Je tumwamini Mungu yupi ?

Kwa nini anajicontradict hivi

Kuna sehemu wanakula kitimoto

Mara huku hawali

Hapo ni kwa wakristo huku

Unadhani sababu ni ipi

Huo mtengano uliotokea kwa watu ishirini , je unaweza kuwa uthibitisho wa kwamba mungu yupo au hayupo ?!

Haya maswali naomba nisiyajibu kwa kuzingatia adabu za mijadala,kwani tutakuwa tunatoka kwenye lengo na kuinajisi mada.

Tujikite kwenye mada hii kwanza,ukiwezekana haya maswali tutayajadili katika upweke wake.
 

Similar Discussions

25 Reactions
Reply
Back
Top Bottom