STEALTH (LOW OBSERVABLE) TECHNOLOGY | Teknolojia ya ndege kutoonekana/kutotambulika na rada (RADAR)

Kama nimeelewa vizuri, unakusudia hivi..
Unga wa mahindi na mahindi yenyewe..
Kwamba ukisaga mahindi utapata "unga mahindi/ugali" lakini haimaanishi mahindi Yana uwezo wa kuzalisha unga tu,lakini unga ni sehemu ndogo na moja tu ambayo inaweza zalishwa na mahindi..
Stealth bomber ni zao moja wapo la Stealth technology lakini wakati huo hio Stealth technology haiishii hapo bali ni pana zaidi..
Upo vizuri sana.
 
Nafikiri umekwisha kupata majibu ya swali lako kuhusiana na hilo. Labda pengine nami niongezee kidogo:

Bomber ni ndege ya kijeshi mahususi kwa ajili ya mashambulizi mazito na mepesi ya ardhini kutokea angani. Kwa maana ya kwamba ndege hizi hutumika katika kufanya mashambulizi katika mtindo wa kushusha ama kuangusha mabomu kutokea angani.

Bombers zimegawanyika hasa katika makundi mawili;

1) Strategic bombers
2) Tactical bombers

Strategic bombers:
Kundi hili hutumika katika majukumu ama missions za mbali (long-range) kwa ajili ya kuangusha mabomu katika maeneo ya kimkakati. Maeneo ama vituo vya kimkakati ni vile ambavyo ndio nyenzo ama msingi mkuu wa nchi katika kuendesha vita kama vile miundombinu za kiuchumi, viwanda n.k. ambavyo ndivyo chanzo cha rasilimali za kuiwezesha nchi kuingia vitani. Bombers hizi hufahamika zaidi kama 'heavy bombers' kutokana na uwezo wa kubeba idadi kubwa ya mabomu na kufanya mashambulizi mazito ardhini. Baadhi ya strategic bombers ni B-2 Spirit, B1B Lancer strategic bomber pamoja na Tupolev Tu-160 strategic bomber.

Tactical bombers:
Hizi ni mahususi katika kushambulia miundombinu muhimu za kijeshi. Yaani, vituo vinavyotumika na majeshi ya nchi pekee pamoja na zana zake; kambi za kijeshi, mifumo ya kijeshi ya ulinzi wa anga (air defense systems) n.k.

Dhumuni kuu la tactical bombers ni kudhoofisha miundombinu za kijeshi za adui ili asiweze kuingia vitani. Katika upande huu wa tactical, ni jeshi tu la adui ambalo ndilo hulengwa na mashambulizi tofauti na upande wa strategic. Bomber za aina hii hasa ni ndege ndogo kama vile fighters tofauti na zile za strategic. Mfano: Fighters kama vile; Sukhoi SU-34 pia ndege nyinginezo zenye uwezo wa kufanya majukumu mengi (multi-role); F-35 Lightning II, Eurofighter Typhoon, F-16 Fighting Falcon n.k.

Nihitimishe hapo kuhusu bombers.

Fighter ni ndege ya kijeshi mahususi hasa kwa mashambulizi ya anga kwa anga (air-to-air) ama juu kwa juu dhidi ya ndege zingine pia operesheni mbalimbali za anga. Sifa kuu ya ndege hizi ni kasi kubwa na uwezo wa kubadili badili uelekeo kwa lugha nyingine (maneuverability).

Hizi nazo zimegawanyika kimakundi kuendana na majukumu tofauti tofauti. Baadhi tu ya makundi hayo ni kama ifuatavyo:

1) Air Superiority. Hizi ni mahususi kwa ajili ya kuteka anga la adui na kuzishambulia angani ndege zingine. Mfano, F-22 Raptor. (Hizi ni za kibabe zaidi)

2) Fighter-bomber. Hizi ni kwaajili ya mashambulizi ya anga kwenda ardhini. Hizi hutumika hasa kama tactical bombers kwa ajili ya kushambulia miundombinu za majeshi ya adui kama nilivyoeleza hapo awali.

3) Interceptor. Hizi ni kwa ajili ya ulinzi. Zenyewe ni mahususi katika kuzuia ndege zingine kuvuka ama kuingia katika eneo fulani la anga.

4) Reconnaissance. Hizi ni kwaajili ya ukusanyaji wa taarifa muhimu kupitia anga. Hizi ni mahusui zaidi katika masuala ya kiintelijensia.

5) Multi-role. Hizi hufanya majukumu mengi. Maana yake ni kwamba, zina uwezo wa kutumika katika majukumu tofauti tofauti kuendana na operesheni mbalimbali za kijeshi. Zinaweza kufanya kazi kama air superiority fighter, bomber, interceptor n.k. Mfano; F-35 Lightning II.

Na kadhalika!
Naamini kila kitu umeweka clear kabisaaa.
 
Daaah MiG 21, J-7 bado tupo 2nd Gen
Hizo Mig-21 Fishbed sidhani kama ziko operational hapa Tanzania. Si ndio zile US walitutuhumu kuwatumia Wakorea (North) kutupatia parts zake. Tulizitumia tangu vita na Iddi Amin nadhani na yeye pia alikuwa nazo.
Hizo J-7G tulizonazo ni copycat ya Mig-21, kitu kilekile. Hata Nigeria wanazo.

Tanzania tunaweza afford angalau J-17 walizonazo Pakistan kutoka China. Hizo modern Mig, Sukhoi, Saab, F, etc tuwaachie Egypt, South Africa na Algeria.
 
Haya maandishi uliyoyaandika yamenisikitisha sana kwani ndiyo ukweli halisi kutuhusu. Lakini mkuu tulikosea wapi na nini kifanyike? Kama mpaka Circuit boards mpaka tuagize kweli? Aisee
Jibu la hili swali watu wenye exposure na nchi zinazoendelea/zilizoendelea kwa kasi wanalo.
Sisi tuna matatizo mengi mno, na hakuna wa kuyaondoa kirahisi. Watu wanaamini wanasiasa ndo wana shida kumbe sio wao tu, ni kwa vile wanaonekana. Jamii nzima matatizo matupu, nyuzi za mabilionea marehemu weusi walioacha mali zikagombewa na familia si unaziona kila siku. Mbona Waarabu na Wahindi hawana.
Civilization ndo inatangulia development yeyote including technological.
 
Hizo Mig-21 Fishbed sidhani kama ziko operational hapa Tanzania. Si ndio zile US walitutuhumu kuwatumia Wakorea (North) kutupatia parts zake. Tulizitumia tangu vita na Iddi Amin nadhani na yeye pia alikuwa nazo.
Hizo J-7G tulizonazo ni copycat ya Mig-21, kitu kilekile. Hata Nigeria wanazo.

Tanzania tunaweza afford angalau J-17 walizonazo Pakistan kutoka China. Hizo modern Mig, Sukhoi, Saab, F, etc tuwaachie Egypt, South Africa na Algeria.
Hakuna ulazima wa kununua hiyo midege kwa sasa hiyo pesa inabd tufufue kiwanda cha matair Arusha
 
Kwahiyo majadiliano yalifaa kuwa hii ni bomber na hii ni fighter badala ya hii ni bomber/fighter na hii ni Stealth
Majibu hayo hayana mahusiano ya moja kwa moja na mabishano yeyote bali yamelenga haswa katika zana hizo mbili (bomber & fighter) specifically, si nje ya hapo.

Unasema ilikuwa rahisi mabishano yangelenga kati ya fighter na bomber?

Mabishano yanaweza kutokea popote pale haijalishi ni hapo ama pengine. Pia, hayo mabishano yaliyokuwepo ni ya kawaida tu, naweza kuyaita majadiliano kama njia mojawapo ya kubadilishana mawazo kuhusiana na masuala haya na yafananayo.
 
Hizo Mig-21 Fishbed sidhani kama ziko operational hapa Tanzania. Si ndio zile US walitutuhumu kuwatumia Wakorea (North) kutupatia parts zake. Tulizitumia tangu vita na Iddi Amin nadhani na yeye pia alikuwa nazo.
Hizo J-7G tulizonazo ni copycat ya Mig-21, kitu kilekile. Hata Nigeria wanazo.

Tanzania tunaweza afford angalau J-17 walizonazo Pakistan kutoka China. Hizo modern Mig, Sukhoi, Saab, F, etc tuwaachie Egypt, South Africa na Algeria.
Sahihi kabisa lakini MiG21 Lancer unazingumziaje? Yani unataka kuniambia hata Mirage 2000 hatuwezi?
 
Radar tunaweza kina Ukraine, Iran, Turkey na wengine wasio giants kwenye tech wanatengeneza radar. Tatizo R & D utatumia gharama kubwa mno na muda mrefu. Na tukija pata, tutapata kama iliyotumika miaka 30 uko iliyopita. Pia tech yetu haibebani, yani hata kutengeneza processors, capacitors, emittters, batteries na vitu vingi mno hatujui. Nchi ambayo hamuwezi tengeneza brenda la juice hamuwezi tengeneza radar ndani ya miaka hata 20.


Haya hasa ndiyo maswala ya kujadili hapa na sio "stealth technology" au "low observable technology", teknolojia zilizotuzidi kimo, teknolojia rahisi hatuwezi huo ni msiba mkubwa kwetu.
 
Ni Mig-21 Fishbed (silaha zote za Urusi huwa zina NATO reporting names, Fishbed kwa hii).
Lancer ndo B1B, hawa Wamarekani hutoa majina ambayo ndo hutumika hivo hivo NATO. US military ni wazuri sana wa kutengeneza acronym, utakuta kifupisho kama THAAD, DARPA, OSINT, SIGINT, MANPAD, etc yani maneno matamu yanatamkika kabisa lakini ni vifupisho vya maelezo fulani. Sio unakuwa na vifupisho eti PCCB (bora ibaki TAKUKURU).

Hiyo Mirage 2000 za Dassault, Wafaransa ambao wametengeneza pia Rafale mojawapo ya 4+ generation fighter nzuri. Mirage 2000 ni nzuri sana lakini inaelekea mwisho wa utawala wake, tatizo la kumiliki silaha za zamani kuna muda utafika ukose spare parts (umeona nilipogusia 'tetesi' za North Korea kutupa parts za Mig-21). Silaha zinatakiwa kuwa serviceable. Mirage 2000 ni tangu 1978, sio zamani hata kidogo lakini kwa nini nimesema si best option?

•Tanzania tukinunua silaha, tukija kununua tena ni makumi ya miaka. Tafuta list ya vifaru tulivyonavyo uone vya mwaka gani. Sasa tukinunua ndege za 1970s kisha tunapanga kuishi nazo mpaka miaka 30 ijayo kweli zitakuwa na mashiko. Hizo Shenyang J-7G tulizipata around 2012 or 2014 lakini za zamani ingawa zina upgrades. Mirage wanazo India wanazitumia hasa kwenye ground attack.
Zipo ndege nyingi sana za 1970s muhimu kuwe na maintenance lakini tatizo moja kubwa kabisa, integration na silaha mpya utakosa.

•Mirage 2000 ni ya Wafaransa, hatuna mazoea ya kununua silaha kwao. Kuchanganya suppliers kuna shida zake hasa maintenance costs, kuoanisha mifumo ya silaha na training ingawa kuna faida pia.
•Muhimu kabisa kwa nini naona sio best option, operating costs za silaha za kizungu ni kubwa mno. Utauziwa e.g air-to-air missiles, spares kwa bei ndefu.
Mkuu mambo mengi nisichoshe watu na kuchanganya mada.
 
Ni Mig-21 Fishbed (silaha zote za Urusi huwa zina NATO reporting names, Fishbed kwa hii).
Lancer ndo B1B, hawa Wamarekani hutoa majina ambayo ndo hutumika hivo hivo NATO. US military ni wazuri sana wa kutengeneza acronym, utakuta kifupisho kama THAAD, DARPA, OSINT, SIGINT, MANPAD, etc yani maneno matamu yanatamkika kabisa lakini ni vifupisho vya maelezo fulani. Sio unakuwa na vifupisho eti PCCB (bora ibaki TAKUKURU).

Hiyo Mirage 2000 za Dassault, Wafaransa ambao wametengeneza pia Rafale mojawapo ya 4+ generation fighter nzuri. Mirage 2000 ni nzuri sana lakini inaelekea mwisho wa utawala wake, tatizo la kumiliki silaha za zamani kuna muda utafika ukose spare parts (umeona nilipogusia 'tetesi' za North Korea kutupa parts za Mig-21). Silaha zinatakiwa kuwa serviceable. Mirage 2000 ni tangu 1978, sio zamani hata kidogo lakini kwa nini nimesema si best option?

•Tanzania tukinunua silaha, tukija kununua tena ni makumi ya miaka. Tafuta list ya vifaru tulivyonavyo uone vya mwaka gani. Sasa tukinunua ndege za 1970s kisha tunapanga kuishi nazo mpaka miaka 30 ijayo kweli zitakuwa na mashiko. Hizo Shenyang J-7G tulizipata around 2012 or 2014 lakini za zamani ingawa zina upgrades. Mirage wanazo India wanazitumia hasa kwenye ground attack.
Zipo ndege nyingi sana za 1970s muhimu kuwe na maintenance lakini tatizo moja kubwa kabisa, integration na silaha mpya utakosa.

•Mirage 2000 ni ya Wafaransa, hatuna mazoea ya kununua silaha kwao. Kuchanganya suppliers kuna shida zake hasa maintenance costs, kuoanisha mifumo ya silaha na training ingawa kuna faida pia.
•Muhimu kabisa kwa nini naona sio best option, operating costs za silaha za kizungu ni kubwa mno. Utauziwa e.g air-to-air missiles, spares kwa bei ndefu.
Mkuu mambo mengi nisichoshe watu na kuchanganya mada.
Ina maana hata Uganda inatushinda kwa uchumi?
images%20(26).jpeg
 
Ina maana hata Uganda inatushinda kwa uchumi?View attachment 1502824
Hizo Su-30 ziko 6. Sijui katika groupings za jeshi ndege sita utaziweka group gani, squadron hazikai, wing hazikai, etc.
Kununua ndege na kuzioperate ni vitu viwili.
Unanunua utakachomudu tu, ukitafuta ndege walizokuwa nazo Indian Air force kwenye vita dhidi ya Pakistan utaona walishinda na ndege gani.
Israel alikuwa na silaha za kawaida lakini kumbe ndizo aliweza kumudu kufanyia training, Waarabu wakaja na silaha nzuri lakini training hawana kwa kuwa ni gharama wakawa wanashindwa mapigano.

Na hawanunui silaha kisa uchumi, wananunua kwa ajili ya ulinzi na wakilinganisha adui ana zana gani. Nchi kama Australia ina uchumi mzuri lakini haina mkazo sana kwenye usalama.
Egypt inanunua silaha nyingi sana kwa kuwa iko maeneo hatarishi, kama zingekuwa sababu za kiuchumi Nigeria na South Africa zingeizidi.
Switzerland ina uchumi lakini hainunui silaha kivile.

Sio hata silaha tu, nilikuwa natazama Bulgaria wana raia hawafiki 10M lakini wanajeshi 300,000. Sisi tuko 55M hata wanajeshi 50,000 hatuna.
Na ukumbuke Uganda ni nchi inayoongozwa kijeshi sijui niseme.
 
GTs na wadau wote wa JamiiForums kwa ujumla, habarini!

Kabla ya yote, niombe ukaribu wenu hapa katika hiki ninachokwenda kukiwasilisha kwenu. Natumai tutakuwa pamoja kuanzia mwanzo hadi mwisho katika uchambuzi wa kina kuhusiana na teknolojia ya stealth ambayo imekuwa ikisifika hasa katika masuala ya kijeshi kwa kuleta ufanisi mkubwa wa kufanya operesheni za kijeshi kwa kutumia zana zisizoweza kutambulika kirahisi na mifumo ya utambuzi kama vile rada.

Teknolojia ya stealth imekuwa na faida kubwa kwa mtumiaji hasa katika utekelezaji wa majukumu ama missions za kijeshi katika maeneo hatarishi yenye mifumo ya utambuzi (rada) ambapo mtumiaji wa teknolojia hii anaweza kufanikisha majukumu yake pasipo kugundulika kirahisi na upande wa pili ama upande adui. Nitaeleza kwa kina kuhusiana na teknolojia hii na vile jinsi inavyofanya kazi hivyo basi twende sambamba. Karibu!

Teknolojia ya STEALTH ama kwa maneno mengine LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY ni teknolojia ambayo hujumuisha mbinu mbalimbali za Kisayansi hususani Fizikia katika kuficha vitu ama kuvifanya visionekane ama kutambulika kirahisi na mifumo ya rada ama mifumo mingine ya utambuzi.

Teknolojia hii imekuwa ikifanyiwa kazi kwa takribani nusu karne sasa na imekuwa ikifanyika kwa usiri mkubwa sana. Usiri huu umekuwepo ili kuilinda teknolojia dhidi ya wizi na unyonyaji na pia kuzuia uvumbuzi wa teknolojia nyinginezo zitakazoweza kukabiliana na teknolojia hii ya stealth. Hivi sasa, teknolojia ya stealth ni mojawapo ya nyenzo muhimu katika uhandisi wa ndege, meli, makombora pamoja na zana nyinginezo za kijeshi.

Ndege za kijeshi kama vile B1-B Lancer, B-2 Spirit, F-22 Raptor, F-35 pamoja na F-117 kutoka nchini Marekani pamoja na Cheng-du J-20 kutoka nchini China ni baadhi tu ya ndege zitumiazo teknolojia hii ya stealth.

View attachment 1494819
View attachment 1494821
PICHA No.1: Ndege ya kijeshi ya mashambulizi mazito (bomber) aina ya B1-B Lancer yenye teknolojia ya stealth.
PICHA No.2: Ndege ya mashambulizi mazito, B-2 Spirit yenye teknolojia ya stealth.

Zana nyinginezo pia kama vile meli na makombora hutumia teknolojia hii. Mfano; meli, USS Zumwalt-class destroyer kutoka nchini Marekani na makombora kama vile AGM-158C LRASM.

View attachment 1494830
PICHA: USS Zumwalt-class destroyer yenye uwezo wa stealth.

Kabla hatujaelekea mbali zaidi kuhusiana na teknolojia hii ni vyema tukafahamu kwanza kuhusu mfumo maarufu unaotumika katika utambuzi, mfumo unaofahamika kama rada ama kwa lugha nyingine, RADAR.

RADAR ni kifupi cha RADIO DETECTION AND RANGING.
Rada ni mfumo wa kielektromagnetiki (electromagnetic) unaotumika katika utambuzi wa mahali penye vitu vinavyoakisi (reflecting objects). Mfano; ndege, watu, magari, nyumba na mazingira mengine ya asilia. Rada hufanya kazi kwa kutumia mawimbi ya kielektomagnetiki (electromagnetic waves) ambayo hutumwa katika mahali panatohitajika kwa utambuzi kisha huyakusanya tena mawimbi yaliyoakisiwa (reflected signals).

View attachment 1494869
View attachment 1495067
View attachment 1495077
View attachment 1495070
PICHA: Mifumo mbalimbali ya rada kwa ajili ya utambuzi.

Mfumo maalumu wa kusambaza mawimbi ya rada hujulikana kitaalamu kama TRANSMITTER na mfumo mwingine unaofanya kazi ya kuyakusanya mawimbi yaliyoakisiwa hujulikana kitaalamu kama RECEIVER. Katika mipangilio (configurations) ya mifumo ya rada, mtambo wa kuzambaza mawimbi ama signals (transmitter) pamoja na mtambo mahususi kwa ajili ya kuyanasa mawimbi (receiver) mara nyingi huwa katika mahali pa usawa.

Kwa maelezo mengine,

Radar uses the principle of sending a radar wave, which is a form of
electromagnetic radiation, in a desired direction with a transmitter, and then collecting the reflected signals from a target with a receiver.


Summary ya maelezo hayo ni katika michoro ifuatayo;

View attachment 1495062
View attachment 1494882
PICHA: Jinsi mfumo mzima wa rada ufanyavyo kazi. [Encyclopedia Britannica]

View attachment 1494933

Katika mchoro hapo ni jinsi ambavyo mawimbi husafirishwa kutoka katika transmitter ambapo mawimbi hayo (emitted wave) hugonga chombo kilichopo angani kisha huakisiwa (reflected) kurudi katika receiver ya rada ndipo taarifa hupokelewa kupitia screen maalumu (radar display).

Baada ya maelezo hayo mafupi, turejee sasa katika stealth ama low observable technology:

Teknolojia hii ya stealth hufanya kazi katika kupunguza kitu kinachofahamika kitaalamu kama, RADAR CROSS SECTION ama kwa kifupi RCS ambacho ni kipimo cha muonekano wa kitu pale kinapotazamwa kupitia rada.

Kwa maelezo mengine ya kitaalamu zaidi tunasema,

Radar cross section is a measure of the power that is returned or scattered in a given direction, normalized with respect to power density of the incident field.

Kwa maelezo mepesi ama rahisi kabisa, radar cross section ni kipimo cha muonekano (size) wa kitu pale kinapotazamwa kupitia mifumo ya rada uliopo mahali fulani.

Hapo awali nilisema kuwa, teknolojia ya stealh hutumika ili kupunguza kiwango cha radar cross section na hatimaye kukiwezesha chombo kutotambulika na rada. Ili kupunguza sasa hicho kiwango cha radar cross section, njia kuu mbili hutumika ambazo nitazitolea maelezo kwa kina:

1. Njia ya kwanza ni mtindo wa umbo la nje wa chombo. Kwa lugha nyingine SHAPING FEATURES.

View attachment 1494817

Hapo awali niligusia kitu hiki,
Katika mipangilio (configurations) ya mifumo ya rada, mtambo wa kuzambaza mawimbi ama signals (transmitter) pamoja na mtambo mahususi kwa ajili ya kuyanasa mawimbi (receiver) iko katika mahali pa usawa.

Chombo kilichopo angani mathalani ndege ya abiria inapopita karibu na eneo lenye mifumo ya rada, yale mawimbi (signals) yanayotoka katika transmitter ya rada hugonga chombo kilicho angani kisha chombo kile huakisi (reflect) mawimbi hayo. Mawimbi yaliyoakisiwa yanaporejea katika uelekeo wa mifumo ya rada, hunaswa na receiver ya rada.

Mawimbi yaliyoakisiwa na chombo kilicho angani yanaponaswa na receiver na kurejea katika radar, mahesabu ya kutambua umbali na mahali chombo kilipo hufanyika ndipo tunaposema kuwa chombo hicho kilicho angani kimetambulika ama kimeonekana na rada.

Sasa, ni kitu gani hutokea pale chombo kilicho angani kinapokuwa na teknolojia hii ya stealth?

View attachment 1495063
View attachment 1494829
PICHA: Ndege aina ya F-22 Raptor zenye teknolojia ya stealth.

Teknolojia ya stealth kupitia mtindo maalumu wa umbo la chombo husika huakisi mawimbi ya rada kuelekea upande mwingine tofauti na kule ambapo mifumo ya rada ipo. Kwa maana hiyo, mawimbi yaliyoakisiwa huelekea upande ambao receiver ya rada haiwezi kuyanasa hivyo hupelekea chombo kile kutoonekana katika rada.

Katika muundo wa nje wa ndege yeyote, sehemu zenye utambarare (flat/vertical surfaces) ni nyenzo muhimu katika kuakisi mawimbi ya rada upande uleule ambao mawimbi hayo hutokea ambapo ndipo penye uwepo wa receivers za rada hivyo kuzifanya rada kuweza kuyanasa mawimbi hayo kwa ufanisi mkubwa.

Wakati ambapo ndege hasa za kivita zinapoundwa viwandani, mitindo ama shapes mbalimbali huzingatiwa ili kuziwezesha kuakisi (reflect) mawimbi mahali ambapo receivers za rada hazitoweza kuyanasa. Kanuni mbalimbali za Kifizikia huzingatiwa hapa ili kufanikisha hili kwa ufanisi na ndio maana maumbo ama mionekano ya nje ya ndege hizi huwa tofauti sana na ndege zingine. Pia si ndege tu ila hata katika vyombo vingine kama vile meli, makombora n.k. hili pia hufanyika.

View attachment 1494826
View attachment 1494825
PICHA: Ndege za F-35 zikiwa katika hatua za undwaji wake.

Kinachofanyika kupitia teknolojia hii ya stealth ni kutoruhusu uwepo wa sehemu hizo zenye utambarare kwa kupandikiza ama kuweka pembe (angles) katika sehemu mbalimbali. Pembe hizo hufanya kazi ya kuyatawanya mawimbi ya rada ili kuyafanya yasiweze kurejea katika receivers za rada. Kutorejea kwa mawimbi hayo katika receivers za rada kama nilivyosema hapo awali huufanya mfumo wa rada kutotambua uwepo wa chombo hicho angani.

Picha ifuatayo unaweza kuona jinsi muundo wa ndege ya stealth ulivyo hususani umbo lenye pembe nyingi.

View attachment 1494827
View attachment 1494828

Picha ya kwanza ni ndege ya kijeshi aina ya F-117A na katika mchoro unaofuatia hapo ni jinsi umbo ama shape ya ndege hiyo (F-117A) ilivyoundwa ili kuweza kuyatawanya mawimbi ya rada yasiweze kurejea ama kunaswa na receivers za rada.

Baada ya maelezo haya juu ya njia ya kwanza ya kuweza kupunguza radar cross section, nitaishia hapa kwa sasa. Baki hapa kwa ajili ya sehemu ya pili. Asante na usisite kutoa maoni yako!


FRANC THE GREAT,
Semper magnas.
appreciation, ujasema tech hi wap
 
Ni Mig-21 Fishbed (silaha zote za Urusi huwa zina NATO reporting names, Fishbed kwa hii).
Lancer ndo B1B, hawa Wamarekani hutoa majina ambayo ndo hutumika hivo hivo NATO. US military ni wazuri sana wa kutengeneza acronym, utakuta kifupisho kama THAAD, DARPA, OSINT, SIGINT, MANPAD, etc yani maneno matamu yanatamkika kabisa lakini ni vifupisho vya maelezo fulani. Sio unakuwa na vifupisho eti PCCB (bora ibaki TAKUKURU).

Hiyo Mirage 2000 za Dassault, Wafaransa ambao wametengeneza pia Rafale mojawapo ya 4+ generation fighter nzuri. Mirage 2000 ni nzuri sana lakini inaelekea mwisho wa utawala wake, tatizo la kumiliki silaha za zamani kuna muda utafika ukose spare parts (umeona nilipogusia 'tetesi' za North Korea kutupa parts za Mig-21). Silaha zinatakiwa kuwa serviceable. Mirage 2000 ni tangu 1978, sio zamani hata kidogo lakini kwa nini nimesema si best option?

•Tanzania tukinunua silaha, tukija kununua tena ni makumi ya miaka. Tafuta list ya vifaru tulivyonavyo uone vya mwaka gani. Sasa tukinunua ndege za 1970s kisha tunapanga kuishi nazo mpaka miaka 30 ijayo kweli zitakuwa na mashiko. Hizo Shenyang J-7G tulizipata around 2012 or 2014 lakini za zamani ingawa zina upgrades. Mirage wanazo India wanazitumia hasa kwenye ground attack.
Zipo ndege nyingi sana za 1970s muhimu kuwe na maintenance lakini tatizo moja kubwa kabisa, integration na silaha mpya utakosa.

•Mirage 2000 ni ya Wafaransa, hatuna mazoea ya kununua silaha kwao. Kuchanganya suppliers kuna shida zake hasa maintenance costs, kuoanisha mifumo ya silaha na training ingawa kuna faida pia.
•Muhimu kabisa kwa nini naona sio best option, operating costs za silaha za kizungu ni kubwa mno. Utauziwa e.g air-to-air missiles, spares kwa bei ndefu.
Mkuu mambo mengi nisichoshe watu na kuchanganya mada.
Mkuu nilimaanisha hii kitu....

Elbit MiG-21 Lancer

The MiG-21 "Lancer" is not a new plane, but the name given to one of the modifications to the MiG-21 has modernized after the collapse of industries in the former Soviet Union. Once the USSR was over, many users of these planes were practically without assistance, or with limited assistance for only part of the aircraft. The MiG-21 "Lancer", the company modernized ELBIT of Israel, in cooperation with the Romanian industry is one of those versions.
 
Nilikusudia kuquote hapo juu
Pamoja sana, nipe kidogo maelezo ya Suppression of Enemy Air Defence (SEAD) na Destruction of Enemy Air Defence (DEAD) na Electronic Warfare (EW) katika habari za Air defence huwa kidogo vinanichanganya mkuu.
 
Hizo Su-30 ziko 6. Sijui katika groupings za jeshi ndege sita utaziweka group gani, squadron hazikai, wing hazikai, etc.
Kununua ndege na kuzioperate ni vitu viwili.
Unanunua utakachomudu tu, ukitafuta ndege walizokuwa nazo Indian Air force kwenye vita dhidi ya Pakistan utaona walishinda na ndege gani.
Israel alikuwa na silaha za kawaida lakini kumbe ndizo aliweza kumudu kufanyia training, Waarabu wakaja na silaha nzuri lakini training hawana kwa kuwa ni gharama wakawa wanashindwa mapigano.

Na hawanunui silaha kisa uchumi, wananunua kwa ajili ya ulinzi na wakilinganisha adui ana zana gani. Nchi kama Australia ina uchumi mzuri lakini haina mkazo sana kwenye usalama.
Egypt inanunua silaha nyingi sana kwa kuwa iko maeneo hatarishi, kama zingekuwa sababu za kiuchumi Nigeria na South Africa zingeizidi.
Switzerland ina uchumi lakini hainunui silaha kivile.

Sio hata silaha tu, nilikuwa natazama Bulgaria wana raia hawafiki 10M lakini wanajeshi 300,000. Sisi tuko 55M hata wanajeshi 50,000 hatuna.
Na ukumbuke Uganda ni nchi inayoongozwa kijeshi sijui niseme.
Kwa Africa ukiwa na SU-30 6 tu ni nyingi sana ndugu, yani unahesabika kuwa una jeshi la Anga bora.sisi wenyewe tuna F-7 (11) na F-6 (3) tu na bado tunatamba
 
Back
Top Bottom