STEALTH (LOW OBSERVABLE) TECHNOLOGY | Teknolojia ya ndege kutoonekana/kutotambulika na rada (RADAR)

B1B Lancer ni toleo la B1 lenye stealth technology zikiwemo radar absorbent materials katika parts mbalimbali.
B1B Lancer ni modification ya original type. Ni sawa useme Sukhoi Su-30 ni ya kawaida alafu Su-30MKI ni stealth. Ndege stealth ni from the prototype wanaamua iwe hivyo, sio wanamodify dege lililopo eti walifanye stealth.
Labda sema B1B inapunguza radar cross section kuliko original B1 lakini sio stealth. Yani hiyo inaonekana kwenye radar kuliko hata F-16, F-15, Mig-35, Jas-39 sasa unaiitaje stealth.
 
B1B Lancer ni modification ya original type. Ni sawa useme Sukhoi Su-30 ni ya kawaida alafu Su-30MKI ni stealth. Ndege stealth ni from the prototype wanaamua iwe hivyo, sio wanamodify dege lililopo eti walifanye stealth.
Labda sema B1B inapunguza radar cross section kuliko original B1 lakini sio stealth. Yani hiyo inaonekana kwenye radar kuliko hata F-16, F-15, Mig-35, Jas-39 sasa unaiitaje stealth.
Teknolojia ya stealth ni pana sana. Pia ni endelevu.

Hizo modification unazosema, nimekwisha kuzisema pia hapa. Na katika suala la hizo modifications,

1) Unamodify nini ama kitu gani?
2) Unamodify ili iweje?
3) Unatumia mbinu zipi?

Kama nilivyosema, teknolojia ya stealth ni muunganiko wa mbinu mbalimbali ambazo hutumika kupunguza radar cross section ya vitu mbalimbali. Kusudi lake ni kuvifanya visionekane kirahisi ama visitambulike na rada. Katika uchambuzi makini wa kiufundi kuhusu B1B Lancer, hizo mbinu zimetumika na zilifanyika kwa makusudi na sababu maalumu.

B1B Lancer ilitokana na kitu kinachoitwa 'redesign' . Yaani muundo wa B1 uliokuwepo ulibadilishwa kwa kuundwa na kuwekewa 'features' nyingine mbalimbali ambazo hazikuwepo hapo kabla, kuanzia muonekano mpaka katika utendaji kazi.

Pia, tukirejea katika ufafanuzi wa kile nilichokileta, zijazungumzia stealth fighters ama stealth bombers bali nimezungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.
 
Nakushukuru kwa kusoma pia kwa kuuliza swali zuri na la muhimu.

Dhumuni kubwa la stealth technology ni kupunguza kiwango cha radar cross section. Maana yake ni kwamba, stealth inaweka ugumu wa chombo kuwa detected na rada kwa kuzuia mawimbi ya rada yasiweze kuakisiwa kurudi katika rada. Lakini pamoja na hilo, kuna baadhi ya visababishi vinavyoweza kupelekea mawimbi ya rada kuakisiwa na kurudi kwenye rada pamoja na kuwa chombo kilichoakisi mawimbi hayo ni chombo stealth.

Kuna factors ama sababu mbalimbali ambazo zinaweza kupelekea stealth kuwa detected kwenye rada.

1) Sababu ya kwanza ni chombo chenyewe.
Kuna vyombo ambavyo vimewezeshwa kuwa na mchanganyiko wa mbinu mbalimbali ama kadha wa kadha za kuvipatia uwezo wa stealth. Pia, kuna baadhi ya vyombo kutokana na mahitaji na masuala mengine mbalimbali, vimepatiwa uwezo kidogo.

Baadhi ya vyombo hupatiwa uwezo kidogo wa stealth kutokana na mambo mbalimbali:

Kwanza ni gharama. Teknolojia ya stealth ni teknolojia yenye gharama kubwa na huhitaji rasilimali nyingi sana katika kuifanyia kazi ipasavyo. Hivyo katika baadhi ya vyombo, mbinu ya stealth mojawapo au baadhi ya mbinu chache hutumika. Kwa maana hiyo, katika viwango fulani vya kiutambuzi kupitia rada, kuna uwezekano wa chombo hicho kutambulika.

Pili ni katika masuala ya kiufundi. Katika suala la ku-design maumbo mbalimbali ya ndege ili yaendane na teknolojia ya stealth, kuna vitu mbalimbali lazima vizingatiwe. Umbo la nje la ndege ama chombo chochote cha anga lina mchango mkubwa sana katika upaaji na mwenendo wa chombo husika kwa ujumla pale kinapokuwa angani.

Hivyo, katika ku-design umbo litakaloweza kuendana na teknolojia ya stealth yaani, kuhakikisha kuwa umbo hilo linayatawanya mawimbi na si kuyaakisi kuelekea katika mifumo ya rada, ni lazima pia umbo hilo lizingatie masuala mengine ya anga ili chombo kiweze kuwa na mwenendo unaopaswa pale kiwapo angani. Kwa maana hiyo kuna zoezi la ku-balance hapo kati ya stealth na aerodynamics.

Kwa maana hiyo, wataalamu wanalazimika ku-limit baadhi ya vitu katika baadhi ya vyombo vya anga (si vyote) ili kuweka uwiano kati ya mambo hayo mawili. Kuhakikisha kuwa kwa kiasi chombo kiwe stealth na pia kiweze kusafiri katika viwango na mwenendo unaotakiwa kuendana na aina ya chombo husika. Kutokana na ku-limit ama kupunguza baadhi ya vitu hasa katika upande wa stealth, kunaweza kusababisha udhaifu fulani na kusababisha sasa chombo husika kutambulika kupitia viwango fulani vya kiutambuzi katika rada.

2) Sababu ya pili ni aina za rada zinazotumika.
Kuna baadhi ya rada zina uwezo wa ku-detect stealth lakini katika viwango fulani tena hasa umbali. Hapo awali nilisema kuwa stealth hukifanya chombo kuwa na radar cross section ndogo, kisiweze kuonekana kirahisi ama kutambulika na mifumo ya rada ama kwa maneno mengine, LOW OBSERVABLE.

Iko hivi,

Mifumo ya rada hufanya kazi katika viwango tofauti tofauti kuendana pia na kazi ama jukumu maalumu lililokusudiwa.

Katika viwango fulani vya rada, tunaweza ku-detect hata vitu vidogo zaidi vilivyopo angani kama vile njiwa. Lakini, mifumo hii ya rada hasa za ku-detect ndege za kivita na za kawaida hufanya kazi ya kuchuja (filtering) baadhi ya vitu hasa vile vidogo sana na kuvifanya visionekane katika mifumo hiyo kupitia software maalumu ili kusiwe na mkanganyiko katika utambuzi. Hilo lisipofanyika vizuri, kunaweza kupelekea utambuzi wa vitu vingine lukuki ama vingi sana kwa wakati mmoja katika eneo lengwa hatimaye kushindwa kubaini kile kilichokusudiwa.

Sasa hapo ndipo teknolojia ya stealth inapofaidika napo.

Kupitia teknolojia ya stealth, ndege kubwa kabisa iliyopo umbali fulani inaweza kupunguzwa radar cross section yake na kuwa na radar cross section kama ya njiwa ama chini ya hapo. Maana yake ni kwamba kiwango hicho kidogo cha radar cross section automatically kitachujwa na mifumo ya rada hatimaye kupelekea ndege hiyo kutotambulika kirahisi. Hivyo, katika viwango fulani vya rada, ndege yenye uwezo wa stealth inaweza kuonekana ama kujitokeza (appear) kwenye rada lakini isitambulike kutokana na mkanganyiko huo wa radar cross section.

Kingine kinachoambatana na hilo, mifumo ya rada inaweza kufanya kazi katika umbali fulani na si zaidi ya hapo. Kupitia viwango fulani vya stealth kuna uwezekano wa kupunguza hiyo range kwa kiasi kikubwa. Maana yake ni kwamba, mfumo wa rada unaweza kuwa na uwezo wa ku-detect vyombo vya anga katika umbali mathalani wa hadi kilometa 400 lakini kupitia teknolojia ya stealth, chombo kikaonekana ndani ya kilometa chache tu ya hizo kilometa 400. Hicho tayari ni kikwazo kwa rada, maana kama chombo kilichopo angani ni chombo cha adui, kinaweza kufanya tukio lolote lenye athari katika umbali mfupi tu na wa karibu ama 'within range' kabla ya kuonekana na rada. Hiyo ndio maana ya 'low observable'.

Asante!
Ukweli ni kwamba hii technology ni kwa Nchi kama zetu hizi, ila sio upeleke nchi kama Urusi yenye Rada tofauti tofauti zaidi ya 200 alafu utegemee utatoboa.utakufa mchana kweupe.
 
Teknolojia ya stealth ni pana sana. Pia ni endelevu.

Hizo modification unazosema, nimekwisha kuzisema pia hapa. Na katika suala la hizo modifications,

1) Unamodify nini ama kitu gani?
2) Unamodify ili iweje?
3) Unatumia mbinu zipi?

Kama nilivyosema, teknolojia ya stealth ni muunganiko wa mbinu mbalimbali ambazo hutumika kupunguza radar cross section ya vitu mbalimbali. Kusudi lake ni kuvifanya visionekane kirahisi ama visitambulike na rada. Katika uchambuzi makini wa kiufundi kuhusu B1B Lancer, hizo mbinu zimetumika na zilifanyika kwa makusudi na sababu maalumu.

B1B Lancer ilitokana na kitu kinachoitwa 'redesign' . Yaani muundo wa B1 uliokuwepo ulibadilishwa kwa kuundwa na kuwekewa 'features' nyingine mbalimbali ambazo hazikuwepo hapo kabla, kuanzia muonekano mpaka katika utendaji kazi.

Pia, tukirejea katika ufafanuzi wa kile nilichokileta, zijazungumzia stealth fighters ama stealth bombers bali nimezungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.
Point yangu ni ileile, Rockwell B1B Lancer sio stealth hata kidogo. Nimeona inaoneshwa ina radar cross section ya 1.02 square metre, pengine nimeona 0.72 sq metre na hivyo hatuwezi kuiita stealth.
Ndege kama HAL Tejas ina RCS ya 0.5 sq metre na haiitwi wala hawajawahi kukosea kuiita stealth.
Ingawa kuwa na RCS ndogo hivi kwa ukubwa wake ni jitihada kubwa lakini hakuifanyi iwe stealth. Iko low observable tu kulinganisha na bombers nyingine.
 
Ukweli ni kwamba hii technology ni kwa Nchi kama zetu hizi, ila sio upeleke nchi kama Urusi yenye Rada tofauti tofauti zaidi ya 200 alafu utegemee utatoboa.utakufa mchana kweupe.
Teknolojia hii ya stealth ni kwa yeyote mwenye uwezo wa kuwa nayo.

Stealth ni hitaji la majeshi mengi duniani. Kuanzia yule mwenye uwezo na hata yule asiye na uwezo wa kufanya hivyo na imekuwa hivyo tokea miaka mingi sana. Tangu enzi na enzi.

In fact, kuwa stealth ni NATURE ya binadamu yeyote.

Stealth haina tofauti na Privacy katika maisha ya kila siku. Kila mmoja wetu anapenda kufanya mambo yake fulani fulani kwa uhuru, bila bughudha wala usumbufu na bila wengine kujua ama kugundua kuwa anafanya kitu gani kwa wakati huo.

Kila mmoja huwa huru zaidi kufanya mambo mengi fulani fulani ambayo asingeweza kuyafanya in public ama mbele ya macho ya wengi. Ni jambo la kawaida kabisa ambalo lipo kwa kila aliye na akili timamu. Na katika stealth pia ni vivyo hivyo!

Hili ni hitaji la kila mtu.
Mataifa makubwa kijeshi; Marekani, China, Urusi uliyoitaja na mataifa mengineyo yamekuwa katika uwekezaji wa teknolojia hii ya stealth kwa muda mrefu sasa. Tofauti iliyopo hapo ni kwamba kila mmoja anafanya kuendana na uwezo wake.
 
Point yangu ni ileile, Rockwell B1B Lancer sio stealth hata kidogo. Nimeona inaoneshwa ina radar cross section ya 1.02 square metre, pengine nimeona 0.72 sq metre na hivyo hatuwezi kuiita stealth.
Ndege kama HAL Tejas ina RCS ya 0.5 sq metre na haiitwi wala hawajawahi kukosea kuiita stealth.
Ingawa kuwa na RCS ndogo hivi kwa ukubwa wake ni jitihada kubwa lakini hakuifanyi iwe stealth. Iko low observable tu kulinganisha na bombers nyingine.
Unaposema kuwa B1B Lancer "sio stealth hata kidogo" kisha hapohapo tena unasema "iko low observable", huoni utofauti hapo?

Nini maana ya STEALTH na nini maana ya LOW OBSERVABLE?

STEALTH ndio LOW OBSERVABLE.

Katika masuala ya kijeshi, stealth na low observable ni vitu vinavyofanana. Yaani ni vitu vyenye maana sawa, ama kwa kifupi ni kitu kilekile. Ndio maana teknolojia hii kwa ujumla wake hufahamika kama STEALTH TECHNOLOGY vilevile pia hufahamika kama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY. Yote ni sawa!
 
Unaposema kuwa B1B Lancer "sio stealth hata kidogo" kisha hapohapo tena unasema "iko low observable", huoni utofauti hapo?

Nini maana ya STEALTH na nini maana ya LOW OBSERVABLE?

STEALTH ndio LOW OBSERVABLE.

Katika masuala ya kijeshi, stealth na low observable ni vitu vinavyofanana. Yaani ni vitu vyenye maana sawa, ama kwa kifupi ni kitu kilekile. Ndio maana teknolojia hii kwa ujumla wake hufahamika kama STEALTH TECHNOLOGY vilevile pia hufahamika kama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY. Yote ni sawa!
Low observability inatokea wakitumia materials na tech kupunguza radar cross section kwa kiasi fulani. Stealth wanaanza tangu mwanzo kutengeneza shape ya kila eneo, engine maalumu, air intakes zake, wings na hata bomb bays. Ndio maana hata Su-57 haijakamilika kwa kuwa engine yake ya Izdeliye haijatengenezwa. Engine iliyopo inatumika kwenye Su-35 lakini sio kwa ajili ya stealth fighter hivo itafanya ndege ionekane kirahisi kwenye radar.

Hiyo B1B ina external hardpoints za kubebea mabomu sasa unaiitaje stealth. Ingawa hizi F-22 na J-20 zinaweza kubeba mabomu nje lakini kwenye situation hiyo hazichezi kama stealth. Hizo F-22 mission zake kadhaa inafanya ikiwa sio stealth kupunguza gharama za maintenance. Ni sawa uchukue ndege ya Airbus ya AirTanzania uweke radar absorbing materials kisha uiite stealth, si sahihi.
 
Low observability inatokea wakitumia materials na tech kupunguza radar cross section kwa kiasi fulani.
Nilisema hapo awali kwamba, teknolojia ya stealth ni pana sana. Pia ni endelevu.

Hiyo "low observability" unayoisema kutokana na kupunguza radar cross section ndio stealth yenyewe. Low observable ndio stealth hali kadhalika stealth ndio low observable.

Kitu kikishakuwa "low observable" kuliko umbo lake la kawaida, tayari hapo kuna utofauti. Na utofauti huo hauji hivihivi tu bali kuna processes ambazo zimefanyika kwa makusudi maalumu. Hizo processes ndio teknolojia yenyewe hiyo ambayo tunaiita STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY.

Unaposema kitu fulani "sio stealth hata kidogo" kisha hapohapo unasema kiko "low observable" ni contradiction. Unachanganya mambo.

Stealth wanaanza tangu mwanzo kutengeneza shape ya kila eneo, engine maalumu, air intakes zake, wings na hata bomb bays.
Haijalishi kuanzia mwanzo ama kuanzia katikati. Kuna mabadiliko mbalimbali kimipango yanayoweza kutokea kutokana na sababu kadha wa kadha zikiwemo za kisiasa. Kinachojalisha ni nyenzo, mbinu ama teknolojia inayotumika na ndicho kilichopo hapa.

Ni teknolojia gani imetumika kupunguza radar cross section katika B1B Lancer?

Nilisema hapo awali kwamba, B1B Lancer ilitokana na kitu kinachoitwa 'redesign' kimuundo na haiko kama B1 ya awali. B1 ya awali iliishia kwenye prototype, mradi ukafutiliwa mbali hata kwenye production haukuingia.

Kuna utofauti mkubwa sana kati ya hizo ndege mbili yaani, B1B pamoja na B1 ya awali, kuanzia shape, engines, inlets, wings, weapon bays n.k. Na zaidi ya hapo hata katika utendajikazi (performance) wa hizo ndege mbili ni tofauti kabisa.

Hiyo B1B ina external hardpoints za kubebea mabomu sasa unaiitaje stealth.
External hardpoints zipo katika ndege zenye uwezo wa stealth na hata zisizo na uwezo huo. Hata F-22 Raptor stealth fighter ina external hardpoints. Hizo external hardpoints huwa zinatumika katika missions maalumu na si mara zote.

Ni sawa uchukue ndege ya Airbus ya AirTanzania uweke radar absorbing materials kisha uiite stealth, si sahihi.
Mfano huo ulioutoa hauendani kabisa na kile kilichofanyika katika B1B Lancer. Ni dhahiri kuwa hufahamu ni nini kilifanyika katika B1B Lancer. Mfano wako huo umethibitisha hilo!

Nitarudia:
B1B Lancer ilitokana na kitu kinachoitwa 'redesign'. Muundo wa B1 uliokuwepo ulibadilishwa kwa kufanywa ama kuundwa upya kutokana na mabadiliko ya kimahitaji. Ninachozungumzia hapa ni muundo (design) na si 'end product' kama hiyo "Airbus ya Air Tanzania" uliyoisema.

Fahamu kwamba, tunapozungumzia teknolojia ya STEALTH ama LOW OBSERVABLE hatuzungumzii "stealth bombers" ama "stealth fighters" in particular...La Hasha!...bali tunaizungumzia teknolojia kama teknolojia. Tunazungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.

Baada ya kusema hayo, nikushukuru pia kwa mchango wako.
 
GTs na wadau wote wa JamiiForums kwa ujumla, habarini!

Kabla ya yote, niombe ukaribu wenu hapa katika hiki ninachokwenda kukiwasilisha kwenu. Natumai tutakuwa pamoja kuanzia mwanzo hadi mwisho katika uchambuzi wa kina kuhusiana na teknolojia ya stealth ambayo imekuwa ikisifika hasa katika masuala ya kijeshi kwa kuleta ufanisi mkubwa wa kufanya operesheni za kijeshi kwa kutumia zana zisizoweza kutambulika kirahisi na mifumo ya utambuzi kama vile rada.

Teknolojia ya stealth imekuwa na faida kubwa kwa mtumiaji hasa katika utekelezaji wa majukumu ama missions za kijeshi katika maeneo hatarishi yenye mifumo ya utambuzi (rada) ambapo mtumiaji wa teknolojia hii anaweza kufanikisha majukumu yake pasipo kugundulika kirahisi na upande wa pili ama upande adui. Nitaeleza kwa kina kuhusiana na teknolojia hii na vile jinsi inavyofanya kazi hivyo basi twende sambamba. Karibu!

Teknolojia ya STEALTH ama kwa maneno mengine LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY ni teknolojia ambayo hujumuisha mbinu mbalimbali za Kisayansi hususani Fizikia katika kuficha vitu ama kuvifanya visionekane ama kutambulika kirahisi na mifumo ya rada ama mifumo mingine ya utambuzi.

Teknolojia hii imekuwa ikifanyiwa kazi kwa takribani nusu karne sasa na imekuwa ikifanyika kwa usiri mkubwa sana. Usiri huu umekuwepo ili kuilinda teknolojia dhidi ya wizi na unyonyaji na pia kuzuia uvumbuzi wa teknolojia nyinginezo zitakazoweza kukabiliana na teknolojia hii ya stealth. Hivi sasa, teknolojia ya stealth ni mojawapo ya nyenzo muhimu katika uhandisi wa ndege, meli, makombora pamoja na zana nyinginezo za kijeshi.

Ndege za kijeshi kama vile B1-B Lancer, B-2 Spirit, F-22 Raptor, F-35 pamoja na F-117 kutoka nchini Marekani pamoja na Cheng-du J-20 kutoka nchini China ni baadhi tu ya ndege zitumiazo teknolojia hii ya stealth.

View attachment 1494819
View attachment 1494821
PICHA No.1: Ndege ya kijeshi ya mashambulizi mazito (bomber) aina ya B1-B Lancer yenye teknolojia ya stealth.
PICHA No.2: Ndege ya mashambulizi mazito, B-2 Spirit yenye teknolojia ya stealth.

Zana nyinginezo pia kama vile meli na makombora hutumia teknolojia hii. Mfano; meli, USS Zumwalt-class destroyer kutoka nchini Marekani na makombora kama vile AGM-158C LRASM.

View attachment 1494830
PICHA: USS Zumwalt-class destroyer yenye uwezo wa stealth.

Kabla hatujaelekea mbali zaidi kuhusiana na teknolojia hii ni vyema tukafahamu kwanza kuhusu mfumo maarufu unaotumika katika utambuzi, mfumo unaofahamika kama rada ama kwa lugha nyingine, RADAR.

RADAR ni kifupi cha RADIO DETECTION AND RANGING.
Rada ni mfumo wa kielektromagnetiki (electromagnetic) unaotumika katika utambuzi wa mahali penye vitu vinavyoakisi (reflecting objects). Mfano; ndege, watu, magari, nyumba na mazingira mengine ya asilia. Rada hufanya kazi kwa kutumia mawimbi ya kielektomagnetiki (electromagnetic waves) ambayo hutumwa katika mahali panatohitajika kwa utambuzi kisha huyakusanya tena mawimbi yaliyoakisiwa (reflected signals).

View attachment 1494869
View attachment 1495067
View attachment 1495077
View attachment 1495070
PICHA: Mifumo mbalimbali ya rada kwa ajili ya utambuzi.

Mfumo maalumu wa kusambaza mawimbi ya rada hujulikana kitaalamu kama TRANSMITTER na mfumo mwingine unaofanya kazi ya kuyakusanya mawimbi yaliyoakisiwa hujulikana kitaalamu kama RECEIVER. Katika mipangilio (configurations) ya mifumo ya rada, mtambo wa kuzambaza mawimbi ama signals (transmitter) pamoja na mtambo mahususi kwa ajili ya kuyanasa mawimbi (receiver) mara nyingi huwa katika mahali pa usawa.

Kwa maelezo mengine,

Radar uses the principle of sending a radar wave, which is a form of
electromagnetic radiation, in a desired direction with a transmitter, and then collecting the reflected signals from a target with a receiver.


Summary ya maelezo hayo ni katika michoro ifuatayo;

View attachment 1495062
View attachment 1494882
PICHA: Jinsi mfumo mzima wa rada ufanyavyo kazi. [Encyclopedia Britannica]

View attachment 1494933

Katika mchoro hapo ni jinsi ambavyo mawimbi husafirishwa kutoka katika transmitter ambapo mawimbi hayo (emitted wave) hugonga chombo kilichopo angani kisha huakisiwa (reflected) kurudi katika receiver ya rada ndipo taarifa hupokelewa kupitia screen maalumu (radar display).

Baada ya maelezo hayo mafupi, turejee sasa katika stealth ama low observable technology:

Teknolojia hii ya stealth hufanya kazi katika kupunguza kitu kinachofahamika kitaalamu kama, RADAR CROSS SECTION ama kwa kifupi RCS ambacho ni kipimo cha muonekano wa kitu pale kinapotazamwa kupitia rada.

Kwa maelezo mengine ya kitaalamu zaidi tunasema,

Radar cross section is a measure of the power that is returned or scattered in a given direction, normalized with respect to power density of the incident field.

Kwa maelezo mepesi ama rahisi kabisa, radar cross section ni kipimo cha muonekano (size) wa kitu pale kinapotazamwa kupitia mifumo ya rada uliopo mahali fulani.

Hapo awali nilisema kuwa, teknolojia ya stealh hutumika ili kupunguza kiwango cha radar cross section na hatimaye kukiwezesha chombo kutotambulika na rada. Ili kupunguza sasa hicho kiwango cha radar cross section, njia kuu mbili hutumika ambazo nitazitolea maelezo kwa kina:

1. Njia ya kwanza ni mtindo wa umbo la nje wa chombo. Kwa lugha nyingine SHAPING FEATURES.

View attachment 1494817

Hapo awali niligusia kitu hiki,
Katika mipangilio (configurations) ya mifumo ya rada, mtambo wa kuzambaza mawimbi ama signals (transmitter) pamoja na mtambo mahususi kwa ajili ya kuyanasa mawimbi (receiver) iko katika mahali pa usawa.

Chombo kilichopo angani mathalani ndege ya abiria inapopita karibu na eneo lenye mifumo ya rada, yale mawimbi (signals) yanayotoka katika transmitter ya rada hugonga chombo kilicho angani kisha chombo kile huakisi (reflect) mawimbi hayo. Mawimbi yaliyoakisiwa yanaporejea katika uelekeo wa mifumo ya rada, hunaswa na receiver ya rada.

Mawimbi yaliyoakisiwa na chombo kilicho angani yanaponaswa na receiver na kurejea katika radar, mahesabu ya kutambua umbali na mahali chombo kilipo hufanyika ndipo tunaposema kuwa chombo hicho kilicho angani kimetambulika ama kimeonekana na rada.

Sasa, ni kitu gani hutokea pale chombo kilicho angani kinapokuwa na teknolojia hii ya stealth?

View attachment 1495063
View attachment 1494829
PICHA: Ndege aina ya F-22 Raptor zenye teknolojia ya stealth.

Teknolojia ya stealth kupitia mtindo maalumu wa umbo la chombo husika huakisi mawimbi ya rada kuelekea upande mwingine tofauti na kule ambapo mifumo ya rada ipo. Kwa maana hiyo, mawimbi yaliyoakisiwa huelekea upande ambao receiver ya rada haiwezi kuyanasa hivyo hupelekea chombo kile kutoonekana katika rada.

Katika muundo wa nje wa ndege yeyote, sehemu zenye utambarare (flat/vertical surfaces) ni nyenzo muhimu katika kuakisi mawimbi ya rada upande uleule ambao mawimbi hayo hutokea ambapo ndipo penye uwepo wa receivers za rada hivyo kuzifanya rada kuweza kuyanasa mawimbi hayo kwa ufanisi mkubwa.

Wakati ambapo ndege hasa za kivita zinapoundwa viwandani, mitindo ama shapes mbalimbali huzingatiwa ili kuziwezesha kuakisi (reflect) mawimbi mahali ambapo receivers za rada hazitoweza kuyanasa. Kanuni mbalimbali za Kifizikia huzingatiwa hapa ili kufanikisha hili kwa ufanisi na ndio maana maumbo ama mionekano ya nje ya ndege hizi huwa tofauti sana na ndege zingine. Pia si ndege tu ila hata katika vyombo vingine kama vile meli, makombora n.k. hili pia hufanyika.

View attachment 1494826
View attachment 1494825
PICHA: Ndege za F-35 zikiwa katika hatua za undwaji wake.

Kinachofanyika kupitia teknolojia hii ya stealth ni kutoruhusu uwepo wa sehemu hizo zenye utambarare kwa kupandikiza ama kuweka pembe (angles) katika sehemu mbalimbali. Pembe hizo hufanya kazi ya kuyatawanya mawimbi ya rada ili kuyafanya yasiweze kurejea katika receivers za rada. Kutorejea kwa mawimbi hayo katika receivers za rada kama nilivyosema hapo awali huufanya mfumo wa rada kutotambua uwepo wa chombo hicho angani.

Picha ifuatayo unaweza kuona jinsi muundo wa ndege ya stealth ulivyo hususani umbo lenye pembe nyingi.

View attachment 1494827
View attachment 1494828

Picha ya kwanza ni ndege ya kijeshi aina ya F-117A na katika mchoro unaofuatia hapo ni jinsi umbo ama shape ya ndege hiyo (F-117A) ilivyoundwa ili kuweza kuyatawanya mawimbi ya rada yasiweze kurejea ama kunaswa na receivers za rada.

Baada ya maelezo haya juu ya njia ya kwanza ya kuweza kupunguza radar cross section, nitaishia hapa kwa sasa. Baki hapa kwa ajili ya sehemu ya pili. Asante na usisite kutoa maoni yako!


FRANC THE GREAT,
Semper magnas.
Kazi nzuri.
 
Nilisema hapo awali kwamba, teknolojia ya stealth ni pana sana. Pia ni endelevu.

Hiyo "low observability" unayoisema kutokana na kupunguza radar cross section ndio stealth yenyewe. Low observable ndio stealth hali kadhalika stealth ndio low observable.

Kitu kikishakuwa "low observable" kuliko umbo lake la kawaida, tayari hapo kuna utofauti. Na utofauti huo hauji hivihivi tu bali kuna processes ambazo zimefanyika kwa makusudi maalumu. Hizo processes ndio teknolojia yenyewe hiyo ambayo tunaiita STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY.

Unaposema kitu fulani "sio stealth hata kidogo" kisha hapohapo unasema kiko "low observable" ni contradiction. Unachanganya mambo.


Haijalishi kuanzia mwanzo ama kuanzia katikati. Kuna mabadiliko mbalimbali kimipango yanayoweza kutokea kutokana na sababu kadha wa kadha zikiwemo za kisiasa. Kinachojalisha ni nyenzo, mbinu ama teknolojia inayotumika na ndicho kilichopo hapa.

Ni teknolojia gani imetumika kupunguza radar cross section katika B1B Lancer?

Nilisema hapo awali kwamba, B1B Lancer ilitokana na kitu kinachoitwa 'redesign' kimuundo na haiko kama B1 ya awali. B1 ya awali iliishia kwenye prototype, mradi ukafutiliwa mbali hata kwenye production haukuingia.

Kuna utofauti mkubwa sana kati ya hizo ndege mbili yaani, B1B pamoja na B1 ya awali, kuanzia shape, engines, inlets, wings, weapon bays n.k. Na zaidi ya hapo hata katika utendajikazi (performance) wa hizo ndege mbili ni tofauti kabisa.


External hardpoints zipo katika ndege zenye uwezo wa stealth na hata zisizo na uwezo huo. Hata F-22 Raptor stealth fighter ina external hardpoints. Hizo external hardpoints huwa zinatumika katika missions maalumu na si mara zote.


Mfano huo ulioutoa hauendani kabisa na kile kilichofanyika katika B1B Lancer. Ni dhahiri kuwa hufahamu ni nini kilifanyika katika B1B Lancer. Mfano wako huo umethibitisha hilo!

Nitarudia:
B1B Lancer ilitokana na kitu kinachoitwa 'redesign'. Muundo wa B1 uliokuwepo ulibadilishwa kwa kufanywa ama kuundwa upya kutokana na mabadiliko ya kimahitaji. Ninachozungumzia hapa ni muundo (design) na si 'end product' kama hiyo "Airbus ya Air Tanzania" uliyoisema.

Fahamu kwamba, tunapozungumzia teknolojia ya STEALTH ama LOW OBSERVABLE hatuzungumzii "stealth bombers" ama "stealth fighters" in particular...La Hasha!...bali tunaizungumzia teknolojia kama teknolojia. Tunazungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.

Baada ya kusema hayo, nikushukuru pia kwa mchango wako.
Unaweza kuweka data za USAF zinazoonesha kuwa B1B Lancer ni stealth bomber. Yani uweke data za watengenezaji na wamiliki tuachane na za kwetu sisi mashabiki.
 
Unaweza kuweka data za USAF zinazoonesha kuwa B1B Lancer ni stealth bomber. Yani uweke data za watengenezaji na wamiliki tuachane na za kwetu sisi mashabiki.
Unarudia kosa lilelile!

Unachanganya kati ya "stealth bomber" na "stealth technology". Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Nilisema na ninarudia;
Tunapozungumzia teknolojia ya stealth ama low observable hatuzungumzii "stealth bombers" ama "stealth fighters" hasa, bali tunaizungumzia teknolojia yenyewe ya stealth. Tunazungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.

Stealth bombers ama stealth fighters ni 'end products' ama ni matokeo tu yanayotokana na teknolojia hii ya stealth ama low observable. Teknolojia ya stealth kwa ujumla wake ni pana sana.
 
Unarudia kosa lilelile!

Unachanganya kati ya "stealth bomber" na "stealth technology". Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Nilisema na ninarudia;
Tunapozungumzia teknolojia ya stealth ama low observable hatuzungumzii "stealth bombers" ama "stealth fighters" hasa, bali tunaizungumzia teknolojia yenyewe ya stealth. Tunazungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.

Stealth bombers ama stealth fighters ni 'end products' ama ni matokeo tu yanayotokana na teknolojia hii ya stealth ama low observable. Teknolojia ya stealth kwa ujumla wake ni pana sana.
Basi nauliza hivi, unaweza kuweka data zinazoonesha B1B Lancer ni stealth? Data zitoke USAF- operators au Boeing- manufacturer.
 
Unarudia kosa lilelile!

Unachanganya kati ya "stealth bomber" na "stealth technology". Hivyo ni vitu viwili tofauti.

Nilisema na ninarudia;
Tunapozungumzia teknolojia ya stealth ama low observable hatuzungumzii "stealth bombers" ama "stealth fighters" hasa, bali tunaizungumzia teknolojia yenyewe ya stealth. Tunazungumzia STEALTH ama LOW OBSERVABLE TECHNOLOGY kwa ujumla wake.

Stealth bombers ama stealth fighters ni 'end products' ama ni matokeo tu yanayotokana na teknolojia hii ya stealth ama low observable. Teknolojia ya stealth kwa ujumla wake ni pana sana.
Nimekukosoa kuiita B1B kuwa ni stealth, hii sio stealth. Sasa unanambiaje nachanganya kati ya stealth bomber na stealth technology? Kama bomber iko stealth simply tutasema stealth bomber. Hizo B-2 utasikia zinaitwa stealth kabisa bila kukwepa.
Bishana pia na Business Insider. Umeandika article nzuri lakini unabisha kitu wazi kabisa.
Kosa lingine unalofanya ni kuona "low observability" na "stealth" ni vitu sawa. Yani kwenye radar kuna tofauti kubwa mno katika hivyo vitu, huwezi kubeba B1B ikafanye mission ndani ya space ya Russia bila kufanya utangulizi wa kina B-2, F-22 au F-35.
IMG_20200706_191912.jpg
 
Russia’s Defense Ministry said on May 29 statement that “Su-27P and Su-30SM fighters from the air defense alert quick reaction forces of the Southern Military District were scrambled to intercept the targets.”

The crews of the Russian fighter jets approached the air targets within a safe distance and identified them as B-1B strategic aircraft, after which “the US bombers changed their flight course and flew away from the state border of Russia,” the statement runs.

The statement also claimed that the US strategic bombers over the Baltic and Black Seas “were timely uncovered” by the air defense alert quick reaction forces of the Western and Southern Military Districts. The B-1s were tracked by Russian radars at a considerable distance from Russia’s border.

>>> Ulishawahi kusikia B-2, F-22 au F-35 imekuwa intercepted? Turudi kwenye mada, kubali kuwa umekosea kuiita B1B Lancer ni stealth.
IMG_20200706_192955.jpg
 
Nimekukosoa kuiita B1B kuwa ni stealth, hii sio stealth. Sasa unanambiaje nachanganya kati ya stealth bomber na stealth technology? Kama bomber iko stealth simply tutasema stealth bomber. Hizo B-2 utasikia zinaitwa stealth kabisa bila kukwepa.
Bishana pia na Business Insider. Umeandika article nzuri lakini unabisha kitu wazi kabisa.
Kosa lingine unalofanya ni kuona "low observability" na "stealth" ni vitu sawa. Yani kwenye radar kuna tofauti kubwa mno katika hivyo vitu, huwezi kubeba B1B ikafanye mission ndani ya space ya Russia bila kufanya utangulizi wa kina B-2, F-22 au F-35.View attachment 1499300
Hii ndio raha ya ugomvi wa wasomi(GT), mtu unapata elimu ya buuure.

Sasa hapa assume majibizano yenu yangekua majukwaa kama ya celebrity au la siasa.

Sasa hivi tungekua tushajifunza mpaka matusi mapya.

Hongereni sana kwa majibizano(ugomvi) yenu wakuu
 
Nimekukosoa kuiita B1B kuwa ni stealth, hii sio stealth. Sasa unanambiaje nachanganya kati ya stealth bomber na stealth technology? Kama bomber iko stealth simply tutasema stealth bomber. Hizo B-2 utasikia zinaitwa stealth kabisa bila kukwepa.
Bishana pia na Business Insider. Umeandika article nzuri lakini unabisha kitu wazi kabisa.
Kosa lingine unalofanya ni kuona "low observability" na "stealth" ni vitu sawa. Yani kwenye radar kuna tofauti kubwa mno katika hivyo vitu, huwezi kubeba B1B ikafanye mission ndani ya space ya Russia bila kufanya utangulizi wa kina B-2, F-22 au F-35.View attachment 1499300
Ndio maana nikasema kwamba unachanganya. Stealth bomber na stealth technology ni vitu viwili tofauti. Moja ni product ya teknolojia huku nyingine ni teknolojia yenyewe in general na ina vitu vingi sana ndani yake.

Nilisema hapo awali kuwa teknolojia ya stealth ni pana sana na ni endelevu. Ukiyasoma maelezo yote niliyowasilisha hapa utapata kulifahamu vyema hilo.

Unaposema kitu ni "low observable" na wakati huohuo unasema "sio stealth hata kidogo" technically nikueleweje?

Unadhani ni kwanini stealth technology huitwa low observable technology?

Nikuulize maswali mengine mawili yaliyoko ndani ya mjadala:

1) Nini maana ya stealth?
2) Nini maana ya stealth technology?
 
Russia’s Defense Ministry said on May 29 statement that “Su-27P and Su-30SM fighters from the air defense alert quick reaction forces of the Southern Military District were scrambled to intercept the targets.”

The crews of the Russian fighter jets approached the air targets within a safe distance and identified them as B-1B strategic aircraft, after which “the US bombers changed their flight course and flew away from the state border of Russia,” the statement runs.

The statement also claimed that the US strategic bombers over the Baltic and Black Seas “were timely uncovered” by the air defense alert quick reaction forces of the Western and Southern Military Districts. The B-1s were tracked by Russian radars at a considerable distance from Russia’s border.

>>> Ulishawahi kusikia B-2, F-22 au F-35 imekuwa intercepted? Turudi kwenye mada, kubali kuwa umekosea kuiita B1B Lancer ni stealth.
View attachment 1499307
Unasema nimekosea.

Sawa! Let's assume nimekosea. Je, unaweza kunionesha mahali nilipokosea?
 
Back
Top Bottom