Stashangaa washabiki wa CCM na JK kufanya yafuatayo!!! SOMA NA TAKAFAKARI

kanyagio

JF-Expert Member
Dec 10, 2009
1,021
365
uchaguzi ndo huo umeisha na CCM kuingia madarakani kupitia kura za wananchi na pia kufanya ujanja maeneo kadhaa.

Kama kawaida yetu tutasahau haraka na maisha kuendelea na wananchi kuanza kulalamikia hali mbali ya maisha..

mimi sitashangaa yafuatayo kutokea:


  1. Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM kusikitishwa na uteuzi wa nafasi mbalimbali utakaofanywa na JK... utasikia wanasema du kawaweka maswahiba wake
  2. sitashangaa wananchi washabiki wa CCM kulalamikia rushwa kushamiri Tanzania .. kama kwamba walikosa mbadala wa kumweka uongozini kupambana na rushwa kwa umakini zaidi ..
  3. sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuanza kulalamikia hali ngumu ya maisha.. ngoja nitoe scenario moja: chadema wana sera ya elimu bure hadi kidato cha sita (6) kama si chuo kikuu. lakini sitashangaa walioinyima kura Chadema kuanza kuja kwako kukupigia magoti kuomba msaada wa kifedha ili apate ada ya kumpeleka mtoto sekondari.
  4. Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM waliokuwa wanavaa sare na kucheza kama hawana akili nzuri wakati wa mikutano ya kampeni kuendelea kuwa katika hali zao duni............ why? kwa sababu serikali imeshindwa kuwa visionary
  5. Sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuendelea kuishi katika nyumba za mbavu za mbwa (kama ile tuliyooneshwa wakati wa kampeni ikiwa na bango la JK) wakati wamekataa kumpigia kura Dr. Slaa aliyekuwa ameahidi kushusha bei ya saruji (cement) ili wananchi walio wengi waweze kujenga nyumba imara na bora
  6. sitashangaa wanachi mashabiki wa CCM kuendelea kulalamikia ukosefu wa dawa hospitalini..
  7. Sitashangaa wananchi mashambiki wa CCM kuendelea kulalamikia vitendo vya rushwa mahakamani na polisi
  8. sitashangaa wananchi na mashabiki wa CCM kuendelea kulalamikia utendaji mbovu wa idara mbalimbali za serikali (kumbuka jinsi Clouds walivyokuwa wanachambua utendaji mbovu wa idara mbalimbali e.g. EWURA, DAWASCO, TANESCO lakini wakawa vuvuzela wa CCM wakati wa uchaguzi)
  9. Sitashangaa wapenzi wa CCM kulalamikia mishahara wanayopata na wakati huo huo kulalamikia posho kubwa za viongozi
  10. sitashangaa watu hawa kuvaa ma- Tshirt, kofia na kanga 2015 kushangilia na kushabikia CCM wakati wa uchaguzi mwingine
kutokana na hili naomba tushirikiane pamoja kuzidi kutoa elimu ya uraia, ipo siku yatabadilika ... "YANA MWISHO" (nukuu toka kitabu cha KULI)
 
sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuanza kulalamikia hali ngumu ya maisha.. ngoja nitoe scenario moja: chadema wana sera ya elimu bure hadi kidato cha sita (6) kama si chuo kikuu. lakini sitashangaa walioinyima kura Chadema kuanza kuja kwako kukupigia magoti kuomba msaada wa kifedha ili apate ada ya kumpeleka mtoto sekondari.
Tatizo hapa ni kuwa hatujui hata kama kweli tuwalaumu hawa watu kwa sababu hatujui hata kama kweli walikipigia kura CCM au ni NEC imetupandikizia JK na askari wake wa kimamluki kutuongoza isivyo halali na kinyume cha sheria.......kutokana na mazingira haya siyo kosa kuwapigajeki jamaa hawa walalahoi wa CCM kwa sababu hata wao ni waathirika wa mfumo kandamizi wa CCM na JK wake...............
 
Kama vile ina mvuto flani hivi....ngoja niende ibadani nikirudi nitacomment
 
CHADEMA IMEKAMATA ARUSHA NA MWANZA, na pia manispaa nyengine.

Kwenye maeneo hayo, inaweza kusimamia sera zake.

TUONE KAMA ITAFANIKIWA kwenye Local Governments ilizokamata.

Utendaji unatakiwe uwe demonstrated sio maneno maneno.

uchaguzi ndo huo umeisha na CCM kuingia madarakani kupitia kura za wananchi na pia kufanya ujanja maeneo kadhaa.

Kama kawaida yetu tutasahau haraka na maisha kuendelea na wananchi kuanza kulalamikia hali mbali ya maisha..

mimi sitashangaa yafuatayo kutokea:


  1. Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM kusikitishwa na uteuzi wa nafasi mbalimbali utakaofanywa na JK... utasikia wanasema du kawaweka maswahiba wake
  2. sitashangaa wananchi washabiki wa CCM kulalamikia rushwa kushamiri Tanzania .. kama kwamba walikosa mbadala wa kumweka uongozini kupambana na rushwa kwa umakini zaidi ..
  3. sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuanza kulalamikia hali ngumu ya maisha.. ngoja nitoe scenario moja: chadema wana sera ya elimu bure hadi kidato cha sita (6) kama si chuo kikuu. lakini sitashangaa walioinyima kura Chadema kuanza kuja kwako kukupigia magoti kuomba msaada wa kifedha ili apate ada ya kumpeleka mtoto sekondari.
  4. Sitashangaa wananchi washabiki wa CCM waliokuwa wanavaa sare na kucheza kama hawana akili nzuri wakati wa mikutano ya kampeni kuendelea kuwa katika hali zao duni............ why? kwa sababu serikali imeshindwa kuwa visionary
  5. Sitashangaa wananchi mashabiki wa CCM kuendelea kuishi katika nyumba za mbavu za mbwa (kama ile tuliyooneshwa wakati wa kampeni ikiwa na bango la JK) wakati wamekataa kumpigia kura Dr. Slaa aliyekuwa ameahidi kushusha bei ya saruji (cement) ili wananchi walio wengi waweze kujenga nyumba imara na bora
  6. sitashangaa wanachi mashabiki wa CCM kuendelea kulalamikia ukosefu wa dawa hospitalini..
  7. Sitashangaa wananchi mashambiki wa CCM kuendelea kulalamikia vitendo vya rushwa mahakamani na polisi
  8. sitashangaa wananchi na mashabiki wa CCM kuendelea kulalamikia utendaji mbovu wa idara mbalimbali za serikali (kumbuka jinsi Clouds walivyokuwa wanachambua utendaji mbovu wa idara mbalimbali e.g. EWURA, DAWASCO, TANESCO lakini wakawa vuvuzela wa CCM wakati wa uchaguzi)
  9. Sitashangaa wapenzi wa CCM kulalamikia mishahara wanayopata na wakati huo huo kulalamikia posho kubwa za viongozi
  10. sitashangaa watu hawa kuvaa ma- Tshirt, kofia na kanga 2015 kushangilia na kushabikia CCM wakati wa uchaguzi mwingine
kutokana na hili naomba tushirikiane pamoja kuzidi kutoa elimu ya uraia, ipo siku yatabadilika ... "YANA MWISHO" (nukuu toka kitabu cha KULI)
 
Inasemekan watanzania ilimradi kuwe na amani tu hata wakila nyasi kwo sio tatizo, hata mafisadi watumie mabilioni kujinufaisha wao watanzania wala hawana wasi ili mradi amani ipo.
 
Mkuu uliyoandika ni ukweli mtupu kwa sababu umereflect tabia za Watanzania - Wachaguaji wabaya, walalamikaji wazuri. Yote uliyotaja tutayaona hivi punde.
 
Inasemekan watanzania ilimradi kuwe na amani tu hata wakila nyasi kwo sio tatizo, hata mafisadi watumie mabilioni kujinufaisha wao watanzania wala hawana wasi ili mradi amani ipo.

Ni kweli. Kinachosababisha haya kwa kiasi kikubwa ni Watanzania kuwa "watiifu mno" kwa viongozi wa dini, kila watakachoambiwa na viongozi hawa wanakitekeleza bila kujiuliza.
 
Unataka Chadema wademonstrate uwezo wao mara ngapi! Nenda kaangalie wilaya ya Karatu! Umeona mji wa Moshi ulivyo msafi na chadema inaongoza pale sasa linganisha na uchafu wa jiji lenu la DAR!!
 
Wewe unachotaka ni kwamba watu wafanye VURUGU na FUJO zisizo maana?

MWANZA MJINI, Ilemela na Nyamagana; wakati KURA zinahesabiwa; WANACHADEMA walifanya uharibifu wa mali; hivi huo ni uungwana? Kisa cha Vurugu hizo? Ni barua iliyochakachuliwa na Dk Slaa [Cheki thread ya Dk Slaa amechakachua Barua]. Do you really want people to demonstrate againstthe VOTE of MAJORITY?

Mahitaji ya maendeleo siku zote yatakuwepo, hata atawale nani hapa; hakuna atakaegeuza TZ pepo. Wananchi wamefanya chaguo lao; walipofanya hivyo walijua kuwa kuna wengine; bali waliamua kumchagua JK kwa kuwa waliona ndio best of the contestants.

Vyama vyote vimekubaliana na matokeo kasoro CHADEMA. sasa ni nani Un Democratic?

Please mates!

Ni kweli. Kinachosababisha haya kwa kiasi kikubwa ni Watanzania kuwa "watiifu mno" kwa viongozi wa dini, kila watakachoambiwa na viongozi hawa wanakitekeleza bila kujiuliza.
 
Mkuu washaanza kulalamika tayari. Je, hukuona taarifa ya habari TBC1 juzi saa 2 usiku? juu ya bei ya mfuko mmoja wa simenti kuuzwa Tshs 20,000= huko Songea?

Halafu mama Ishengoma (Kaimu RC) anawataka wafanyabuashara kushusha bei, nawao wakadinda!!

Maumivu ni kwetu sote Watanzania uwe CCM, CHADEMA, CUF, TLP, NCCR hapa ndo panaponifurahisha!!!!!!!!!
 
Wewe unachotaka ni kwamba watu wafanye VURUGU na FUJO zisizo maana?

MWANZA MJINI, Ilemela na Nyamagana; wakati KURA zinahesabiwa; WANACHADEMA walifanya uharibifu wa mali; hivi huo ni uungwana? Kisa cha Vurugu hizo? Ni barua iliyochakachuliwa na Dk Slaa [Cheki thread ya Dk Slaa amechakachua Barua]. Do you really want people to demonstrate againstthe VOTE of MAJORITY?

Mahitaji ya maendeleo siku zote yatakuwepo, hata atawale nani hapa; hakuna atakaegeuza TZ pepo. Wananchi wamefanya chaguo lao; walipofanya hivyo walijua kuwa kuna wengine; bali waliamua kumchagua JK kwa kuwa waliona ndio best of the contestants.

Vyama vyote vimekubaliana na matokeo kasoro CHADEMA. sasa ni nani Un Democratic?

Please mates!

Ulitaka watu waende nyumbani ili mumrudishe Masha mjengoni sio? Simply vurugu zimesababishwa na nec kutokana na shinikizo la chama tawala pale kuknkoonekana upinzani ni mkali. Walikuwa waaangalia possibility ya kuchakachua na ndio maana watu walikosa uvumilivu. Mbona majimbo ambayo ccm ilishinda majibu mara moja?? Ubungo, Kawe, Arusha, Segerea na mengine meeeengi eti ndio wanahesabu kura. Try to be realistic !!!!!
 
huu mtandao umevamiwa na mataahira ya ccm tafadhali nendeni mkae na genius wenu dr kikweche
 
CHADEMA IMEKAMATA ARUSHA NA MWANZA, na pia manispaa nyengine.

Kwenye maeneo hayo, inaweza kusimamia sera zake.

TUONE KAMA ITAFANIKIWA kwenye Local Governments ilizokamata.

Utendaji unatakiwe uwe demonstrated sio maneno maneno.
Si mara ya kwanza kwa chadema kushika uongozi wa manispaa na uzoefu unaonyesha ndio halmashauri pekee zilizofanya vizuri kuliko hizo zenu za ccm. Na ndio sababu zote hata ambazo mbunge katoka ccm bado zitabaki chini ya chadema. Subiri upate shule sio longo longo zenu.
 
Wewe unachotaka ni kwamba watu wafanye VURUGU na FUJO zisizo maana?

MWANZA MJINI, Ilemela na Nyamagana; wakati KURA zinahesabiwa; WANACHADEMA walifanya uharibifu wa mali; hivi huo ni uungwana? Kisa cha Vurugu hizo? Ni barua iliyochakachuliwa na Dk Slaa [Cheki thread ya Dk Slaa amechakachua Barua]. Do you really want people to demonstrate againstthe VOTE of MAJORITY?

Mahitaji ya maendeleo siku zote yatakuwepo, hata atawale nani hapa; hakuna atakaegeuza TZ pepo. Wananchi wamefanya chaguo lao; walipofanya hivyo walijua kuwa kuna wengine; bali waliamua kumchagua JK kwa kuwa waliona ndio best of the contestants.

Vyama vyote vimekubaliana na matokeo kasoro CHADEMA. sasa ni nani Un Democratic?

Please mates!
Basi wakamfungulie mashitaka ya kuchakachua barua mbona wanaogopa?
 
Makame ubongo wako ni mfu! Ntakusimulia kisa cha wakulima wawili wa mahindi;
''mulima1: yeye alipalilia shamba lake vizuri kuzuia magugu yasizoofishe mazao lakini akaghaili kulinda shamba lake lisivamiwe na ngedere matokeo yake ngedere walishambulia mazao yote.
Mkulima2. Yeye hakujihusisha sana na palizi ila alilinda shamba lake licvamiwe na ngedere, japo mazao hayakusitawi vizuri ila alifanikiwa kuvuna japo mazao kidogo kuliko mkulima wa kwanza'' makame, unajifananisha na yupi kati ya wakulima hawa?
 
Huyo makame kaniboa hadi nahc usingizi.hivi wewe unamiliki viwanda vingapi?au gari kumi na ngapi?unataka kujifanya unaipenda sana ccm ee?kuwa na watu 1000 kama wewe wenye mawazo hayo bora tuwe na nguruwe milion miamoja nchini.think bro kwanini tuendelee kuteseka kiasi hiki wakati kila kitu tunacho?acha kuundergrade ubongo wako makusudi huku hali halisi unaiona.
 
Arusha wamejiponza wenyewe,kwa sifa za kutaka mabadiko bila ya kuzisikiliza sera na kuzipembua ,wakafuata ushabiki na kumchagua mbuge hewa mwenye elimu ya darasa la 7,sasa sijui ni mabadiliko ya aina gani wanategemea kuletewa na mbunge huyo.
Tutegemee vituko toka mule mjengoni.
 
Huyo makame kaniboa hadi nahc usingizi.hivi wewe unamiliki viwanda vingapi?au gari kumi na ngapi?unataka kujifanya unaipenda sana ccm ee?kuwa na watu 1000 kama wewe wenye mawazo hayo bora tuwe na nguruwe milion miamoja nchini.think bro kwanini tuendelee kuteseka kiasi hiki wakati kila kitu tunacho?acha kuundergrade ubongo wako makusudi huku hali halisi unaiona.

Hata mimi sitashangaa. Na sitashangaa kama huyu Makame ndani ya JF anayetetea CCM na NEC akiwa ndo Lewis Makame mkurugenzi wa NEC au ndugu yake flani!!
 
Makame ubongo wako ni mfu! Ntakusimulia kisa cha wakulima wawili wa mahindi;
''mulima1: yeye alipalilia shamba lake vizuri kuzuia magugu yasizoofishe mazao lakini akaghaili kulinda shamba lake lisivamiwe na ngedere matokeo yake ngedere walishambulia mazao yote.
Mkulima2. Yeye hakujihusisha sana na palizi ila alilinda shamba lake licvamiwe na ngedere, japo mazao hayakusitawi vizuri ila alifanikiwa kuvuna japo mazao kidogo kuliko mkulima wa kwanza'' makame, unajifananisha na yupi kati ya wakulima hawa?

Unapoteza muda wako bure!!! Jaji Mstaafu Makame ni mzee sana!! Sidhani hata huwa naingia humu kusoma!!!

Keshajiishia...:doh:
 
Back
Top Bottom