Stashahada za Juu zafutwa

Kithuku

JF-Expert Member
Nov 19, 2006
1,395
208
Hii nayo ni usanii mtupu, jamaa wamebadilisha tu jina la "Advanced Diploma" kuwa "Higher Diploma", ati wanadai wamefuta kiwango hicho cha elimu! Usanii!

Stashahada za Juu zafutwa

na Salehe Mohamed

SERIKALI imefuta mfumo wa elimu wa stashahada ya juu (Advanced Diploma) nchini kutokana na kutoendana na vyuo vikuu vya Afrika Mashariki sambamba na kuboresha elimu ya juu inayotolewa na vyuo vikuu.
Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msolla, alitangaza uamuzi huo jana alipokuwa akifunga kongamano la wakuu wa vyuo vikuu na vitivo kwa nchi za Afrika Mashariki lililofanyika jijini Dar es Salaam, kwa wiki moja.

Alisema, kutokana na kufutwa kwa mfumo wa stashahada hiyo, wanafunzi wenye vyeti vya stashahada ya juu hawatoweza kuendelea na shahada ya uzamili (Masters) mpaka watakaposoma mwaka mmoja zaidi.

Msolla, alibainisha kuwa, mfumo huo ulitumika nchini pekee hali iliyochangia kutofautisha kati ya elimu ya Tanzania na nchi nyingine, lakini kutokana na makubaliano yaliyofikiwa na wakuu wa vyuo vikuu vya Afrika Mashariki, Tanzania imefuta kiwango hicho cha elimu ili kujenga wigo mpana zaidi wa elimu ya juu.

“Tumefuta mfumo huu, sababu kubwa ya kufanya hivi ni kuboresha elimu ya juu ili kuendana na nchi jirani ambazo hazina utaratibu tuliokuwa tukiutumia hapa nchini, hivyo kuanzia sasa hautambuliki,” alisema Professa Msolla.

Alisema, si kweli kuwa mwanafunzi aliyetunukiwa stashahada ya juu (Advance Diploma) ni sawa na aliyetunikiwa shahada (Degree), hivyo ni vema wananchi waelewe ukweli huo ili wasichanganye viwango hivyo vya kitaaluma.

Alibainisha kuwa, kutokana na kufutwa kwake, sasa utatumika mfumo mpya wa ‘higher diploma’ ambao pia haulingani na shahada.

Kuhusu kongamano hilo, alisema lengo lake ni kuweka mikakati ya kuhakikisha ubora na taaluma inayotolewa katika vyuo vyote vikuu vya Afrika Mashariki unalingana kwa lengo la kumpatia mhitimu ufahmu wa kutosha utakaomwezesha kukabiliana na changamoto za dunia.

Profesa Msolla pia alisema, anategemea kongamano hilo litatoka na njia muafaka za kuwabana watu wanaoghushi vyeti ili kujipatia kazi au kujiendeleza zaidi na elimu ya juu kwa kutumia vyeti hivyo.

Alisema, ni vema mamlaka husika za elimu ya juu kuangalia kwa ukaribu tatizo hilo linazidi kukua kila kukicha na kutafuta njia muafaka za kulidhibiti ili kuwa na wataalamu waliofanya juhudi za dhati walipokuwa wanasoma.

“Tanzania, Uganda na Kenya nina hakika zitakuwa mashahidi wazuri wa kukithiri kwa matumizi ya vyeti vya kughushi na kuvuja mitihani, ni changamoto kwetu kulitatua tatizo hili na ikiwezekana kulizuia kabisa kwani linatia aibu,” alisema Professa Msolla.

Hivi sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la wanafunzi wanaofaulu kupitia mpango wa Elimu katika Shule za Msingi na Sekondari (MMEM na MMES), hivyo ni vema vyuo vikuu vishiriki vijitahidi kutoa elimu bora ili vipande na kuwa vyuo vikuu na kuongeza nafasi za wanafunzi.

Naye Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Profesa Mayunga Nkunya, alisema takribani vyuo vyote vilivyohudhuria mkutano huo, vimeukubali mfumo wa kuhakiki ubora wa elimu na tayari vimeanza kuutumia.

“Malengo tuliyojiwekea katika kongamano hili yamefikiwa, cha msingi tulitaka kujua ni hatua gani vyuo vikuu vitachukua kuhusiana na mfumo huu mpya ambao nina imani utasaidia sana kuboresha elimu,” alisema Profesa Nkunya.

Alisema wamekubaliana kuwa kila chuo kiweke utaratibu utakaohakikisha taaluma inayotolewa ni ya ustadi wa hali ya juu inayoendana na hadhi ya kimataifa.


Source: Tanzania Daima
 
sijaelewa kidogo hapo, kwa hiyo diploma na advance diploma zitakuwa hazipo na badala yake kutakuwa na higher diploma?
And hope maamuzi yatakuwa yamefanyiwa upembuzi yakinifu pamoja na kuangalia kukabiliana na athari zitakazojitokeza hapo baadae, na isije ikatokea tena tukaireverse system baadae.
 
Kuna wanafunzi melfu waliosoma IDM Mzumbe, IFM na Nyegezi wana shashahada mbali mbali toka vyuo hivyo na wamepata ajira kwa kutumia vyeti hivyo, sasa leo wanaambiwa stashahada zao hazitambuliki! Kama kawaida ya waliokabidhiwa madaraka wameboronga kwa mara nyingine tena.
 
Sisi wenye background ya ualimu hatuhusiki na hilo. Kwetu kuna Certificate in Education (mwalimu wa Primary school), Dip.Ed (Secondary school), kisha zinaanza degree. Hatuna Adv.dip. Sasa watu wa accounts, hata mainjinia na madaktari wa binadamu wote kuna adv dip. Tena wa medicine huwa wananiacha hoi zaidi, wale wa Adv.Dip wanajiona kuwa wanaujua udaktari kuliko wenye degree! Huwa wanaitwa AMO, yaani wao na MD's haziivi kabisa, akikanyaga MD kwenye anga zao wanaungana wote kumpiga vita hadi atimue! Kuna jamaa zangu kadhaa madaktari waliniambia waliacha nafasi zao huko mikoani kutokana na mazingira kama haya, na wanasema hiyo ni mojawapo ya sababu ya hospitali nyingi tu za wilaya kuongozwa na hao AMO, wanawakimbiza MD's! Sijayaona haya kwenye education, labda ni kwa kuwa hatuna kada hiyo. Lakini sidhani kama kubadilisha tu jina na kuiita "Higher Diploma" kutasaidia chochote. Serikali inatakiwa kuwekeza nguvu zake katika kuhakikisha kuwa nafasi za elimu kwa kila kiwango zinapatikana kwa mwenye uwezo wa kiakili wa kiwango hicho, kwa hiyo wa university wapate nafasi, na wa hizo diploma na certificates pia nao wapate nafasi, kwani makundi yote haya yanategemeana katika utendaji kwenye kila sekta.
 
Sisi wenye background ya ualimu hatuhusiki na hilo. Kwetu kuna Certificate in Education (mwalimu wa Primary school), Dip.Ed (Secondary school), kisha zinaanza degree. Hatuna Adv.dip. Sasa watu wa accounts, hata mainjinia na madaktari wa binadamu wote kuna adv dip. Tena wa medicine huwa wananiacha hoi zaidi, wale wa Adv.Dip wanajiona kuwa wanaujua udaktari kuliko wenye degree! Huwa wanaitwa AMO, yaani wao na MD's haziivi kabisa, akikanyaga MD kwenye anga zao wanaungana wote kumpiga vita hadi atimue! Kuna jamaa zangu kadhaa madaktari waliniambia waliacha nafasi zao huko mikoani kutokana na mazingira kama haya, na wanasema hiyo ni mojawapo ya sababu ya hospitali nyingi tu za wilaya kuongozwa na hao AMO, wanawakimbiza MD's! Sijayaona haya kwenye education, labda ni kwa kuwa hatuna kada hiyo. Lakini sidhani kama kubadilisha tu jina na kuiita "Higher Diploma" kutasaidia chochote. Serikali inatakiwa kuwekeza nguvu zake katika kuhakikisha kuwa nafasi za elimu kwa kila kiwango zinapatikana kwa mwenye uwezo wa kiakili wa kiwango hicho, kwa hiyo wa university wapate nafasi, na wa hizo diploma na certificates pia nao wapate nafasi, kwani makundi yote haya yanategemeana katika utendaji kwenye kila sekta.



Kithuku:

Siku hizi universities ni viwanda vinavyofyatua graduates. Wanafunzi wote wenye wastani wa C za form 4 wanaweza kwenda university na kuondoka na digrii za nguvu sana. Hivi vyeti vya kawaida, diploma vinatupotezea muda tu.
 
Kithuku:

Siku hizi universities ni viwanda vinavyofyatua graduates. Wanafunzi wote wenye wastani wa C za form 4 wanaweza kwenda university na kuondoka na digrii za nguvu sana. Hivi vyeti vya kawaida, diploma vinatupotezea muda tu.

Kwa hakika mtu mwenye uwezo wa kupata wastani wa C katika mtihani wa form four anao uwezo pia wa kufika university na kufanya vizuri. Wastani wa C ya form four katika mfumo wa Tanzania ni sawa na points 21 ambazo ni Division 2, hao watu huwa wanakwenda form five, na wakiendelea na bidii hufika mbali hadi kwenye PhD. Pia baadhi ya universities za nje huwachukua hao na kuwapa pre-university course kwa mwaka mmoja tu, kisha wanaendelea na kozi ya degree kwa muda wa kawaida. Bila shaka nasi tunahitaji mifumo kama hii kuwaongezea watu wetu options za kusoma.
 
Nungwiiiii na Advanced diploma ya Mzumbe anatakiwa arudi tena shuleni kwi kwi kwiiii
 
Katika ilo Tangazo sijaona maelezo ya kina juu ya wale ambao tayari wana izo Ad Dip na wale ambao ndo wamekuwa enrolled wako vyuoni?
 
Alisema, kutokana na kufutwa kwa mfumo wa stashahada hiyo, wanafunzi wenye vyeti vya stashahada ya juu hawatoweza kuendelea na shahada ya uzamili (Masters) mpaka watakaposoma mwaka mmoja zaidi
.

Huu mwaka mmoja watapelekwa kusomea nini? Au ndo pre-masters course kama pre form one/form six??

Nafikiri serikali hapa itabidi itoe offer kwa wote waliosoma Adv. Diploma kupata huu mwaka mmoja wakiwa fully sponsored then kuendelea na masters wajilipie kwa sababu sioni kama kuna logic kubadilisha Adv. Dip kuwa Higher Diploma alafu wale wenye Adv. Dip wapewe mzigo mwingine wa kusoma mwaka mzima kabla ya masters....hii hainiingii akilini.

Yangu macho...
 
.

Huu mwaka mmoja watapelekwa kusomea nini? Au ndo pre-masters course kama pre form one/form six??

Nafikiri serikali hapa itabidi itoe offer kwa wote waliosoma Adv. Diploma kupata huu mwaka mmoja wakiwa fully sponsored then kuendelea na masters wajilipie kwa sababu sioni kama kuna logic kubadilisha Adv. Dip kuwa Higher Diploma alafu wale wenye Adv. Dip wapewe mzigo mwingine wa kusoma mwaka mzima kabla ya masters....hii hainiingii akilini.

Yangu macho...

Hizi ni siasa tu za ovyo, Msolla anaudhalilisha u-profesa wake! Profesa mzima (daktari wa mifugo) kuja na proposal ya kubadilisha jina la adv dip kuwa higher dip na kutudanganya itainua kiwango cha elimu, anajifananisha tu na wasiosoma, bora tu angejiuzulu akaanzishe kliniki ya kutibu punda na bata! Majina ya vyeti yanatofautiana dunia nzima, cha maana ni content ya kilichosomwa, depth yake na kwa baadhi ya taaluma, muda wa mazoezi, na si tu jina la hicho cheti. Nchi za Romania, Hungary, Ujerumani mashariki (zamani), digrii ya kwanza inaitwa "diploma", na inaeleweka hivyo, wakienda nchi nyingine hizo credentials zinakuwa evaluated na wanapata treatment ya mwenye digrii ya kwanza bila kulazimisha kubadili jina la hicho cheti. Kama shida ni kufananisha na nchi jirani, hakuna umuhimu wa kubadili tu jina na kuiita "higher diploma" badala ya "advanced diploma", mbona wao wasibadili zao? Wengine wana mfumo wa elimu ya 8-4-4, mbona siwasikii wakibadili ili wafanane na Tanzania na Uganda?

Wajua mtu akisoma harakaharaka hiyo taarifa ya Prof Dr (vet) Msolla atadhani hatua ya adv dip haipo tena, sasa watu wataenda university baada ya diploma (ama kubaki hapohapo), kumbe sivyo, bado ipo ila imebadilishwa tu jina, ati ni "higher diploma"! Uchuro mtupu!
 
Mimi sina la kuongea sanaaa, kwani nina hamu ya kuonana na wale wandugu waliokuwa wanadai kuwa digrii na advanced diploma ni sawa.

Hizi ni qualifications mbili tofauti kabisa. Hata kabla ya tukio la kufuta AD's, hiyo qualification ilikuwa haikubaliki kwenye shahada za pili, duniani kote. Yaani mwenye digrii akiomba admission kwa ajili ya masters degree, ataunga moja kwa moja labda tu iwe ni fani tofauti (kwa mfano mhasibu aende kutaka chukua masters ya madawa" ila hawa wandugu wengine walikuwa wanatakiwa kukamua post graduate diploma kwanza.

Sasa hata hiyo higher diploma nayo imedaiwa kutokuwa sawa na degree, which means, nayo itapaswa kupitia boda refu kwanza la post graduate then ndio waingie masters.

Hatudharau AD's but, wanapaswa kuelewa tofauti iliyopo baina yao na digrii.
 
Du hii kali, sasa wale ndugu zetu wa CBE, IFM, Mzumbe, TIA(enzi zile, DSA waliopata Masters kwa kutumia equivalent ya degree inakuwaje.Halafu na yule mdudu anaeitwa post graduate diploma naye ataendelea kuwepo? Maana yule alikuwa kwa ajili ya watu wa Advance Diploma. Sasa wakiisha itakuwaje?

Na huyo mdudu mpya anaeitwa Higer Diploma ndo nani. Mi nilivyoelewa hapo technical vyuo kama CBE, IFM, TIA ndo vinapelekwa kuzimu maana Certificate tu ndo sitakuwa dili.Sasa Certificate si hata Modern Commercial wanatoa?
 
Hizi ni siasa tu za ovyo, Msolla anaudhalilisha u-profesa wake! Profesa mzima (daktari wa mifugo) kuja na proposal ya kubadilisha jina la adv dip kuwa higher dip na kutudanganya itainua kiwango cha elimu, anajifananisha tu na wasiosoma, bora tu angejiuzulu akaanzishe kliniki ya kutibu punda na bata! Majina ya vyeti yanatofautiana dunia nzima, cha maana ni content ya kilichosomwa, depth yake na kwa baadhi ya taaluma, muda wa mazoezi, na si tu jina la hicho cheti. Nchi za Romania, Hungary, Ujerumani mashariki (zamani), digrii ya kwanza inaitwa "diploma", na inaeleweka hivyo, wakienda nchi nyingine hizo credentials zinakuwa evaluated na wanapata treatment ya mwenye digrii ya kwanza bila kulazimisha kubadili jina la hicho cheti. Kama shida ni kufananisha na nchi jirani, hakuna umuhimu wa kubadili tu jina na kuiita "higher diploma" badala ya "advanced diploma", mbona wao wasibadili zao? Wengine wana mfumo wa elimu ya 8-4-4, mbona siwasikii wakibadili ili wafanane na Tanzania na Uganda?

Wajua mtu akisoma harakaharaka hiyo taarifa ya Prof Dr (vet) Msolla atadhani hatua ya adv dip haipo tena, sasa watu wataenda university baada ya diploma (ama kubaki hapohapo), kumbe sivyo, bado ipo ila imebadilishwa tu jina, ati ni "higher diploma"! Uchuro mtupu!

Kithuku:

Ndio maana sisi watanzania ni mazezeta wa kutupwa. Kina siku tupo tayari kubadilika ili kufuata mfumo wa watu wengine. Lakini sijaona mataifa mengine yanakubalika hili yaende sawa na Tanzania.

Kwa nchi kama ya Tanzania, mafunzo ya miaka mitatu katika taasisi ya elimu ya juu kwa mwanafunzi yoyote aliyemaliza high school yakubalike kama digrii ya kwanza.
 
Mimi sina la kuongea sanaaa, kwani nina hamu ya kuonana na wale wandugu waliokuwa wanadai kuwa digrii na advanced diploma ni sawa.

Hizi ni qualifications mbili tofauti kabisa. Hata kabla ya tukio la kufuta AD's, hiyo qualification ilikuwa haikubaliki kwenye shahada za pili, duniani kote. Yaani mwenye digrii akiomba admission kwa ajili ya masters degree, ataunga moja kwa moja labda tu iwe ni fani tofauti (kwa mfano mhasibu aende kutaka chukua masters ya madawa" ila hawa wandugu wengine walikuwa wanatakiwa kukamua post graduate diploma kwanza.

Sasa hata hiyo higher diploma nayo imedaiwa kutokuwa sawa na degree, which means, nayo itapaswa kupitia boda refu kwanza la post graduate then ndio waingie masters.

Hatudharau AD's but, wanapaswa kuelewa tofauti iliyopo baina yao na digrii.


...acha kujitia aibu na unaonekana hujui kitu,nimeona wengi wenye hizo Advanced dipl. wanapata admission kwenye graduate school (England & US) tena shule za maana sio za uchochoroni kama ulizosoma wewe maana mtu aliyesoma hawezi kuongea huo utumbo wako (dont get me wrong sijasoma advanced diploma ila unachofanya to degrade Elimu za watu unaonekana ni limbukeni tuu)
 
ninaongeza kwa koba, elimu sio cheti bali ni ujuzi unaotoka nao... this is what is known as profession, na hii ni special art ambayo ni kwa wale tu waliobahatika kuipata, wale watakaojiingiza kwa bahati mbaya wataumbuka.

sasa wewe umesoma bicom miaka mitatu, huyu kasoma uchumi adv. diploma miaka mitatu, ikitokea wa adv. diploma akonyesha profession kubwa ya kuelewa mambo kuliko wewe wa degree, ana haki ya kukudharau licha ya makaratasi yako. nimeswema na nitasema daima.
 
Kuna wanafunzi melfu waliosoma IDM Mzumbe, IFM na Nyegezi wana shashahada mbali mbali toka vyuo hivyo na wamepata ajira kwa kutumia vyeti hivyo, sasa leo wanaambiwa stashahada zao hazitambuliki! Kama kawaida ya waliokabidhiwa madaraka wameboronga kwa mara nyingine tena.

Serikali lazima iwajibike kuwapa nafasi hawa wenzetu wenye advanced D ili kuweza kusoma huoo mwaka mmoja. Wakiishia kusema wanatakiwa wasome mwaka mmoja bila kutoa maelezo huo mwaka mmoja utasomwaje ni sawa na kuwatekeleza hawa wa Tanzania. Tukumbuke kwa upande mwingine takwimu zitazidi kuonyesha kuwa watanzania wenye Shahada ni wachache zaidi. Tutajikomboaje?

Moja ya njia za kufanya ni kuanzisha mitaala maalumu ya ku-upgrade hizi advanced Diploma na kuwe na Time limit!

Inaweza kuwa ni program ya miaka 3-5 kuhakikisha wote wenye dhambi ya advanced Diploma wanatubu. Vyuo vya kada husika viandae mitaala hiyo na kutoa hizo kozi kwneye vituo maalum bila kuathiri udahili (admissions) wa wanafunzi wa kawaida.

Serikali iwajibike kuwasomesha wasomi hawa au wjilipie ada wenyewe lakini wapewe discount.

Tukumbuke kila kitu kina gharama lakini faida bado ni ya Taifa.
 
...acha kujitia aibu na unaonekana hujui kitu,nimeona wengi wenye hizo Advanced dipl. wanapata admission kwenye graduate school (England & US) tena shule za maana sio za uchochoroni kama ulizosoma wewe maana mtu aliyesoma hawezi kuongea huo utumbo wako (dont get me wrong sijasoma advanced diploma ila unachofanya to degrade Elimu za watu unaonekana ni limbukeni tuu)

Ni kweli Koba, vyuo vya nje wana admission requirements tofauti kwa kila Masters degree. Inategemea masomo uliyosoma huko nyuma na credits ulizopata na sio jina la shahada au stashahada. Kama kozi unayotaka kusoma inahitaji mtu awe na background ya uchumi, takwimu, marekting, na mazagazaga mengine ambayo uliyapata kwa kutumia advanced Diploma, huwezi kukosa chuo kusoma masters. Kama ulipata degree say Bcom na kuna admission requirements za kozi husika umezikosa, Jina la degree yako halitakuokoa.
 
kama ni kendana na mfumo wa elimu ya Afrika Mashariki mbona Kenya mtu anatoka form 4 anaenda University?

Huu nao ni Ufisadi tu
 
Back
Top Bottom