Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Jamani mwenye kujua bei ya king'amuzi cha Azam nataka niachane kabisa na Star times.Kilichoniimpress wamekitoa.Kwa hiyo na mimi sina budi kujitoa.Ligi za Netherlands,Beligium na USA.Hizi ligi zimenifanya sasa hizi ligi ya uingereza sifuatilii kabisa.Kuna talents za kipekee sana.Kama saa hizi kuna bonge ya mechi USA MAJOR LEAGUE SOCCER,jana Samatta kanipita kushoto.Rangers vs Celtic wanipita kushoto.Wametoa vyote hivi kibabe tu.
Habari zenu wanaJamiiForums

Je una tatizo lolote unapotumia huduma zetu? Unaushauri wowote ili kuboresha huduma zetu?

Tafadhali tunaomba utumie thread hii, ili tukusaidie. Tafadhali tunaomba unapokuwa na tatizo ili tukusaidie kirahisi.

1. Utaje tatizo lako
2. Taja sehemu unayoishi
3. Pia kama unaweza tunaomba ututumie na namba yako ya smartcard!

STARTIMES tutajibu maoni, malalamiko na ushauri ule tu ambao utakuwa umejitosheleza na wenye nia ya kutusaidia kuboresha huduma zetu.

kumbuka namba zetu za huduma kwa wateja ni 0764700800 au 0677700800

Ahsanteni sana na karibuni nyote.
 
Hili ndiyo anguko la Startimes? Chanel za fox,tv1,cloudtv,national geographic wild,n.k zote mmefuta. Maana ya nini? Kama si ndiyo hatima yenu?
 
Niko Ubungo external, nina king'amuzi cha antena, napata chaneli zingine ila Upendo Tv inasema 'no service' tatizo nini? Niliwapigia customer service jma2 iliyopita wakasema watafanya uchunguzi kisha watanipigia. Hadi leo kimya.
 
hivi mnajisikiaje tunavyowauliza maswali hamtaki kutujibu ina maana mnatudharau? au mnaona bila startimes hatuwezi kuendelea na ving'amuzi vingine??? sio vizuri sasa mlianzisha uzi wa kazi gani kama hamna uwezo wa kutuhudumia kupitia hapa????
 
Niko Ubungo external, nina king'amuzi cha antena, napata chaneli zingine ila Upendo Tv inasema 'no service' tatizo nini? Niliwapigia customer service jma2 iliyopita wakasema watafanya uchunguzi kisha watanipigia. Hadi leo kimya.
Customers Care Ukiwakipigia Wana Dharau Bhalaa
Yaani Soon Wataona Wateja Hawalipi Isipokuwa Tutatazama Local

Yaani Shida
 
Hili ndiyo anguko la Startimes? Chanel za fox,tv1,cloudtv,national geographic wild,n.k zote mmefuta. Maana ya nini? Kama si ndiyo hatima yenu?
Niliwauliza Customers Care Wanasema Hizo Channels Zina Matatizo Ingawa Tunajua Ni Uongo, Watu Wengi Sana Wataacha Kulipa Ili Kampuni Ile Jeuri Yake

Hawaoni Ushindani Ulivyo Mkubwa
 
Back
Top Bottom