Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Unatumia kisimbuzi gani?
Ndg habari
Mimi nina kisimbuzi kile cha zamani lakini kwa bahati mbaya hakikusajiliwa hicho na kadi pia hailusajiliwa kina muda kama miaka 4 kipo ndani hakitumiki ivi majuzi nikatembelea ofisi zenu hapa Moshi ili kukisajili wakaniambia hawasajili visimbizi vipya kama nataka nitoe 62000 elfu ili wakisajili ikanibidi kuwasiliana na watoa huduma wenu wakanipa maelekezo jinsi ya kukisajili kwa simu lakini sikufanikiwa nikamsalimia simu nakuwafahamisha wakaniambia nitapigiwa simu mpaka sasa ni wiki ya 2 sijapigiwa simu
Je naweza kusaidikaje katika hili
 
Tuwasubir wahusika nami ni mdau kama wewe,visimbuzi vya zamani vilikuaje?
Ndg habari
Mimi nina kisimbuzi kile cha zamani lakini kwa bahati mbaya hakikusajiliwa hicho na kadi pia hailusajiliwa kina muda kama miaka 4 kipo ndani hakitumiki ivi majuzi nikatembelea ofisi zenu hapa Moshi ili kukisajili wakaniambia hawasajili visimbizi vipya kama nataka nitoe 62000 elfu ili wakisajili ikanibidi kuwasiliana na watoa huduma wenu wakanipa maelekezo jinsi ya kukisajili kwa simu lakini sikufanikiwa nikamsalimia simu nakuwafahamisha wakaniambia nitapigiwa simu mpaka sasa ni wiki ya 2 sijapigiwa simu
Je naweza kusaidikaje katika hili
 
Habar startimes, kinga'muzi changu ni cha antena nilipokuwa nakinunua pale ofisini kwenu buguruni malapa niliambiwa si lazima kulipia ili kuona local chanel hivyo toka mwaka 2014 nimekuwa nikikitumia bila shida yoyote. Sasa kwa sasa siwezi kukitumia mana kimekata frequency zote na nimejaribu kudilisha location ya antena bila mafanikio. Nikaamua niangalie setting zake mwisho nikakutana na ujumbe huu " pop will be offline from feb 15 due to chanel production stop" sasa nataka kujua tatizo ni nini hasa. Namba ya kadi ni 02035958208
 
Naomba msaada king'amuzi changu cha StarTime A/C.01819395449 Chanel ya ST SWAHILI inanigomea inataka pin code naomba msaada
 
Naomba msaada king'amuzi changu cha StarTime A/C.01819395449 Chanel ya ST SWAHILI inanigomea inataka pin code naomba msaada
IMG_20190610_184341.jpeg
 
Japo humu kwa sasa hawajibu malalamiko yawatu ila mimi niliamua kuwapigia kupitia namba zao izo walizoziweka apo juu kwn uzi na walinisaidia vzr tu
 
Hawa hawafai Serikali inasema lock channel bure lakini ukiishiwa kifurushi wanakata zote. Ukiwapigia simu wanaomba namba ya kisimbusi wanakwambia subiri dakika 5. Ndio nitolee hovyo kabisa hasa.
Hawafai kabisa wameiacha channel yao ya matangazo na TBC 1 pekee. Hao TBC sasa wanachokitangaza ni hatareee kazi kusifia vitu visivyojulikana
 
Habari zenu wanaJamiiForums

Je una tatizo lolote unapotumia huduma zetu? Unaushauri wowote ili kuboresha huduma zetu?

Tafadhali tunaomba utumie thread hii, ili tukusaidie. Tafadhali tunaomba unapokuwa na tatizo ili tukusaidie kirahisi.

1. Utaje tatizo lako
2. Taja sehemu unayoishi
3. Pia kama unaweza tunaomba ututumie na namba yako ya smartcard!

STARTIMES tutajibu maoni, malalamiko na ushauri ule tu ambao utakuwa umejitosheleza na wenye nia ya kutusaidia kuboresha huduma zetu.

kumbuka namba zetu za huduma kwa wateja ni 0764700800 au 0677700800

Ahsanteni sana na karibuni nyote.
Mimi Nilinunua Startimes Decoder ya Dish kwa sh. 69,000 bila dish lenyewe, nikaambiwa nitakuwa na offer ya mwezi mzima wa kuangalia channels. Ilipofika siku 14 wakakata, nikalalamika wakaniambia watanipa siku 14 lakini baada ya siku 4 Kikakata tena.
Maswali yangu.
1. Je niliponunua decoder ya Dish 69,000 je sikustaili kupata Dish?
2. Je kwa zile siku zangu za offer je sikustaili kupata fidia ya siku?
3. Mwisho kwenye mtandao wenu mmeweka number lakini uwa hazipokelewi ni voicemail muda wote

Mimi naishi Arusha Sombetini na hizi ndizo Decoder Card No. 02182927226
 
Hawa hawafai Serikali inasema lock channel bure lakini ukiishiwa kifurushi wanakata zote. Ukiwapigia simu wanaomba namba ya kisimbusi wanakwambia subiri dakika 5. Ndio nitolee hovyo kabisa hasa.
Wanadai ulipie 46 elfu ili uunganishwe milele,sijui kama serikali ya wanaonyongwa inafahamu utaratibu huu.

Kama wateja wenye dish ndio wanauziwa bei kubwa ,lengo ni lipi kuwabania hizo local chanel.

Ikumbukwe tu ving'amuzi vya antena ni vya mjini tu,sisi wa vijijini haki ya local chanel hatuna,tulipie!

Haki ya nani,tutajaza ving'amuzi ndani.
 
Hebu ninyi watu Wa startime saidieni hili suala la Bollywood Swahili kubadilisha lugha kwa baadhi ya tamthilia zake kuwa za kihindi tu na hakuna hata maandishi ya kiingerza ili angalau yasaidie watazamaji kuelewa! Na Kama kuna tatizo la kiufundi au lililo nje ya uwezo wenu tutaarifuni kupitia luninga kuliko kutuacha tukikodoa macho na hata kutokutazama TV !
 
Ndg habari
Mimi nina kisimbuzi kile cha zamani lakini kwa bahati mbaya hakikusajiliwa hicho na kadi pia hailusajiliwa kina muda kama miaka 4 kipo ndani hakitumiki ivi majuzi nikatembelea ofisi zenu hapa Moshi ili kukisajili wakaniambia hawasajili visimbizi vipya kama nataka nitoe 62000 elfu ili wakisajili ikanibidi kuwasiliana na watoa huduma wenu wakanipa maelekezo jinsi ya kukisajili kwa simu lakini sikufanikiwa nikamsalimia simu nakuwafahamisha wakaniambia nitapigiwa simu mpaka sasa ni wiki ya 2 sijapigiwa simu
Je naweza kusaidikaje katika hili
habari yako, tafadhari tupatie namba yako ya mawasiliano.
 
Back
Top Bottom