Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

Naomba kujua idadi ya vifurushi vyenu na gharama zake.


habari yako, gharama zetu zinategemea aina ya kisimbusi ulichonacho, gharama ni kama ifuatavyo

upload_2017-9-26_13-46-55.png
 
tumepata, hivi punde utapigiwa simu na watoa huduma wetu, ahsante kwa kuchagua startimes
Nashukuru, fundi amefika nyumbani na kuona decoder yangu alichosema dicoder ime collapse ninatakiwa kufika ofisini ili nifanyiwe backup kwenye kingamuzi kingine kwa gharama ya 32000.
Je zile channel local nilizokuwa nikiona nitaendelea kuona au nitakuwa nalipia?
 
Hivi startimes Tanzania hamna huduma ya malipo ya baada yani iwe kama umeme unaweka units na unatumia kutokana na matumizi yako.

Wekeni huduma ya units kwenye huduma zenu na ninawaambia ukweli mtapata sanaa wateja.
 
HIV kwa nini ulipiaji WA vingamz vyenu cku hz unasumbua sana?

Nina miez miwil mfululizo, nalipia ila Chanel hazshiki mpk kesho yake mfano Jana nimelipia sa 12:30 jion nikiwa na lengo LA kuwah kipind cha siri za familia lakin matokeo yake mpk sa a mbil naambiwa recharge wakat nimeshapat ujumbe WA uthibitisho kuwa nimelipia
Sasa tatizo nini?

Jitahdn kurekebisha hili
 
Yan najuta kuingia mkenge nikanunua ichi kishumbusi tangu jana nimelipia lakini bado akioneshi television yoyote ata zile radio zao za wapi uko aziongei yani ni msalaba mtupu kila mda ni kuscrach tuu yani ni matatizo matupu

Mwenye namba zao za huduma kwa wateja naomba anisaidie tafadhali ili niwapigie wakinizingua narudi dukani kuchukua azam

Sent using Jamii Forums mobile app

Kwa mlichonifanyia ctaki hata kuwaona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimenunua kifurushi cha mwezi tarehe 14/09/2017 kimeisha 25/09/2017 kabla mwezi haujaisha inakuaje iyo
Namba 020 3577 2752
 
mi ndo nimechoka na nyie jamani. unakaribia mwaka sasa nalipia ila channel hazifunguliwi hata! hivi nimeacha kulipia kimekaa tu kama pambo. najaribu kutafuta ofisi zenu hapa mbeya sizioni.
 
Nashukuru, fundi amefika nyumbani na kuona decoder yangu alichosema dicoder ime collapse ninatakiwa kufika ofisini ili nifanyiwe backup kwenye kingamuzi kingine kwa gharama ya 32000.
Je zile channel local nilizokuwa nikiona nitaendelea kuona au nitakuwa nalipia?


ndio utaendelea kupata chanel zako kama kawaida! tunashukuru kwa mrejesho
 
Hivi startimes Tanzania hamna huduma ya malipo ya baada yani iwe kama umeme unaweka units na unatumia kutokana na matumizi yako.

Wekeni huduma ya units kwenye huduma zenu na ninawaambia ukweli mtapata sanaa wateja.


tunashukuru kwa maoni yako, tutalifanyia kazi
 
mi ndo nimechoka na nyie jamani. unakaribia mwaka sasa nalipia ila channel hazifunguliwi hata! hivi nimeacha kulipia kimekaa tu kama pambo. najaribu kutafuta ofisi zenu hapa mbeya sizioni.

habari yako, tafadhari unapata ujumbe gani katika king'amuzi chako? ofis zetu za mbeya zipo mkabala na hospital ya aghakan Uwindini karibu na ofisi za halmashauri au shirika la posta
 
Jee kwa nn kama sijalipia siwezi kuona local channel kama clouds itv eatv na kama nipe sababu zenye mashiko laasivo nakitupa kisumbuzi chenu
 
HIV kwa nini ulipiaji WA vingamz vyenu cku hz unasumbua sana? Nina miez miwil mfululizo, nalipia ila Chanel hazshiki mpk kesho yake mfano Jana nimelipia sa 12:30 jion nikiwa na lengo LA kuwah kipind cha siri za familia lakin matokeo yake mpk sa a mbil naambiwa recharge wakat nimeshapat ujumbe WA uthibitisho kuwa nimelipia
Sasa tatizo nini? Jitahdn kurekebisha hili

habari yako, pole kwa usumbufu, ukishafanya malipo katika king'amuzi chetu, inakupasa usubiri si zaidi ya dk 15 kabla chaneli hazijaanza kuonyesha, endapo itachelewa basi kunakuwa na matatizo katika mifumo yetu, na tunakushauri ikitokea hivyo wasiliana na watoa huduma wetu moja kwa moja wafanye 'manual authorizations'
 
Jee kwa nn kama sijalipia siwezi kuona local channel kama clouds itv eatv na kama nipe sababu zenye mashiko laasivo nakitupa kisumbuzi chenu

habari yako, chanel hii ni local na huwa zinapatikana bure, isipokuwa pale tu kama ulinunua kile chenye bei maalum ambacho pia unaweza kubadilisha kadi na ukapata chanel zote za nyumbani bure
 
Mnacho bore ni hiki, Bollywood wanatoa movie nzuri sana kila siiku. Lakini nyie mnakomaa na movie zile zile,mara chamku,mara sikupendi mara hii unasema hii ya mwezi uliopita,nyingine ukiiona tu unasonya na kubadili chanel.

Mnakera sana tena sana,tunalipia lakini matufanya sisi mazuzu
 
habari yako, chanel hii ni local na huwa zinapatikana bure, isipokuwa pale tu kama ulinunua kile chenye bei maalum ambacho pia unaweza kubadilisha kadi na ukapata chanel zote za nyumbani bure

Safii sana na nielekezeni jinsi ya kufanya hivyo nipate local channel bure
 
Back
Top Bottom