Startimes Tanzania: Support thread (maswali, maoni na ushauri)

StarTimes Tanzania

JF-Expert Member
Jun 11, 2013
260
140
Habari zenu wanaJamiiForums

Je, una tatizo lolote unapotumia huduma zetu? Unaushauri wowote ili kuboresha huduma zetu?

Tafadhali tunaomba utumie thread hii, ili tukusaidie. Tafadhali tunaomba unapokuwa na tatizo ili tukusaidie kirahisi.

1. Utaje tatizo lako
2. Taja sehemu unayoishi
3. Pia kama unaweza tunaomba ututumie na namba yako ya smartcard!

STARTIMES tutajibu maoni, malalamiko na ushauri ule tu ambao utakuwa umejitosheleza na wenye nia ya kutusaidia kuboresha huduma zetu.

kumbuka namba zetu za huduma kwa wateja ni 0764700800 au 0677700800

Ahsanteni sana na karibuni nyote.
 
Last edited by a moderator:
Karibu sana JF StarTimes Tanzania
Mjibu mdau hapa.
Kwa muda wa zaidi ya wiki mbili kuna maeneo kadhaa hapa nchini pamoja na nyumbani kwangu, ambapo matangazo ya ITV & EATV (Startimes) yamekuwa yanakwama sana na kutoa picha mbaya na tena ni kuanzia saa 11 jioni hadi saa 5 usiku. Sasa ni hivi kwa upande wangu ninapoona matangazo ya ITV hayaonekani vizuri huwa ni bora nikazima TV kuliko kuangalia habari ya TBC.

Nawasilisha wakuu.
KILAKA.

Au bofya hapa
https://www.jamiiforums.com/habari-...2-itv-and-eatv-wanahujumiwa-na-startimes.html
 


Habari yako,

Ni kweli startimes tumepokea malalamiko mengi kuhusu tatizo hilo, na pia timu yetu ya wataalamu waligundua tatizo hilo, na tuligundua linasababishwa na muingiliano wa mawimbi kutoka kwa 'WiMAX operator' karibu na mitambo yetu.

Kwa kuwa sisi kama startimes hatukuwa na mamlaka juu ya 'operator huyo' tuliwasiliana na TCRA na wao kwa kushirikiana na wataalamu wetu wamekuwa wakifanya kazi kwa ukaribu kutatua tatizo.

Kwa kuwa chanzo cha tatizo kimeshajulikana kwa sasa wataalamu wetu kwa kushirikiana na TCRA wanafanyakazi kutatua tatizo na tunatumai hivi karibuni tatizo litarekebishwa . Tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa wateja wetu na umma kwa ujumla.
 
Mumjibu na huyu.
kitokana na kutoonekana vizuri kwa ITV katika kingamuzi cha STAR TIMES wakati wa taarifa ya habari katika maeneo mbalimbali nchini hususani mkoa wa DSM inasekana kuna taarifa za kukihujumu kituo hicho kikongwe nchini.Baadhi ya vingamuzi kama vile CONTINENTAL,DSTV,AZAM TV,EASY TV,wakati wa taarifa ya habari ITV inaonekana vizuri sana lakini kwa star times inakatika katika hovyo hadi watazamaji wa ITV wanashindwa kutazama taarifa za habari vizuri.mwandishi alipokwenda katika ofisi za sta times walimpoga chenga kwamba hawako tayari kuzungumzia hilo jambo,kama vile haitoshi mwandishi akamlazim kwenda katika mamlaka ya mawasiliano nchini TCRA prof. Mkoma alijibu ana wageni anawasubili.Hivyo katika kingamzi cha star times ITV inahujumiwa.
 
Karibuni sana Star media JF, Mjiandae kupongezwa pia kukosolewa na wanaokosoa wanawapenda kiasi cha kuwaambia udhaifu(holes) kwenye huduma zenu ili kesho muwe washindani bora kwenye soko lililojaa ushindani.

Karibuni uwanja huru.
 
Mie nimesahau nambari yangu ya siri, hivyo nikiingia pale setting nashindwa kupata access, msaada wenyu tafadhali


Habari yako

Tafadhali ingiza namba siri '0000' kisha ukiingia katika 'SETTING' nenda katika 'PARENTAL CONTROL' option na chagua 'OFF' kama ukiingiza hiyo PIN itakataa tafadhari tunaomba ufike katika ofisi zetu kwa msaada zaidi
 
Swali : Naomba kufaham bei ya king"amuzi chenu ni kiasi gani kwa sasa mana huku mtaani kila mtu anataja bei yake ?
 
Kuna jirani yangu hivi karibuni king"amuzi chake startimes kimeibwa achukue hatua gani licha ya kuwa amesharipoti polisi ?
 
Habari yako

Tafadhali ingiza namba siri '0000' kisha ukiingia katika 'SETTING' nenda katika 'PARENTAL CONTROL' option na chagua 'OFF' kama ukiingiza hiyo PIN itakataa tafadhari tunaomba ufike katika ofisi zetu kwa msaada zaidi
mkuu pole sana mimi nilikuwa na tatizo hadi nikahama nilifikiri ni eneo nililipo.Ila nawashukuru sana ITV kwa kuwa wameweza kunisemea tatizo langu nitaangalia leo kujua kama limeisha.

ushauri Mtumie nguvu nyingi kuzuia matatizo kutokea na msisubiri kuja kutatua tatizo.
 
Hellow startimes! king'amuz changu kinasumbua sana channel nyingi zina scratch especialy muda wa jioni nashindwa kuangalia TV kabisa tafadhali naomba msaada wenu npo maeneo ya mbagala na number ya smart card 02035351569
 
Swali : Naomba kufaham bei ya king"amuzi chenu ni kiasi gani kwa sasa mana huku mtaani kila mtu anataja bei yake ?

habari yako

tunaving'amuzi vya aina mbili, vinavyotumia antenna na vinavyotumia Dish

vinavyotumia Antena viko vya aina mbili

kuna vile ukinunua unafurahia chanel zaidi ya 75 mwezi mmoja kinauzwa tshs 59000
na kuna vile ukinunua unapata chanel 17 kwa muda wa miezi 7.5 vinauzwa tsh 34000 (kingamuzi na malipo humo humo)

vingamuzi vinavyotumia Dish

hivi vinauzwa TSHS 139000 pamoja na ufundi unapata na dishi lake
kama unadishi kinauzwa Tshs 96000

Ahsante
 
king'amuzi changu kinaonyesha NO SIGNAL toka jana, kwa hiyo siwezi kuona channel yoyote, nini tatizo na nifanyeje ku-solve?
 
Hellow startimes! king'amuz changu kinasumbua sana channel nyingi zina scratch especialy muda wa jioni nashindwa kuangalia TV kabisa tafadhali naomba msaada wenu npo maeneo ya mbagala na number ya smart card 02035351569


habari yako

Pole kwa tatizo, kama kinascratch ITV na EATV tafadhali usijali uwe na subira tatizo linatatuliwa hivi karibuni, lakini kama kinascratch chanel zote, tafadhali naomba wasiliana na fundi wetu wa mbagala aje akiangalie 0767634511 gharama za ufundi ni bure lakini utachangia kidogo gharama za Usafiri kwa fundi wetu '3000'

Ahsante
 
Back
Top Bottom