BabaMorgan
JF-Expert Member
- Dec 18, 2017
- 4,041
- 10,463
Tunaotumia kingamuzi cha startimes sasa tunajifunza lugha ya Kichina kupitia channel ya starswahili hongera kwa Wachina kutumia kampuni yao ya startimes kama jukwaa la kutangaza tamaduni zao pamoja na mafanikio yao.
Mataifa shindani kama USA yameendelea kushangazwa na kuongeza kwa ushawishi wa China Barani Afrika ukweli ni kuwa sababu zipo nyingi ila mojawapo ya sababu ni kingamuzi chao cha startimes kupitia channel zao kama CGTN na channel zao za kikanda kama StarSwahili na nyingine nyingi wanazoshirikiana nazo kama Channel Ten yenye vinasaba vya CCM.
Kupitia hizo channel tajwa hapo juu maudhui yake mengi yamekua ya kuisifu nchi ya China kupitia miradi yake iliyopo nchini China na Barani Afrika kama vile madaraja, viwanda, barabara na siasa za China huku wakituaminisha kuwa wao ndio marafiki wa kweli wanaojua shida zetu A to Z na wenyewe pekee ndio wanaoweza kuzitatua kwa kutuletea bidhaa Affordable kulinganisha na uchumi weru.
Pia wamekuwa wakitumia chombo chao kuwasuta wale wote wanaowashutumu vibaya juu ya siasa zake za ndani kukandamiza haki za raia wake mfano kama utotoni ushawahi kuishi na mlezi anayekutesa siku wakija wageni atakuvalisha nguo nzuri na atapika chakula kizuri na mwisho wa siku atakuita mbele ya wageni na kukuuliza namna gani unaishi naye kwa sababu ya hofu unakuta unamsifia na kuwaambia wageni kuwa una furahia kuishi naye ili hali si kweli.
Mwisho China wanastahili pongezi licha ya mapungufu yao ila wamedhihirishia dunia kuwa wameamua na wanaweza enzi za kutishiwa zilishapita.
From northern part of Tanzania.
Mataifa shindani kama USA yameendelea kushangazwa na kuongeza kwa ushawishi wa China Barani Afrika ukweli ni kuwa sababu zipo nyingi ila mojawapo ya sababu ni kingamuzi chao cha startimes kupitia channel zao kama CGTN na channel zao za kikanda kama StarSwahili na nyingine nyingi wanazoshirikiana nazo kama Channel Ten yenye vinasaba vya CCM.
Kupitia hizo channel tajwa hapo juu maudhui yake mengi yamekua ya kuisifu nchi ya China kupitia miradi yake iliyopo nchini China na Barani Afrika kama vile madaraja, viwanda, barabara na siasa za China huku wakituaminisha kuwa wao ndio marafiki wa kweli wanaojua shida zetu A to Z na wenyewe pekee ndio wanaoweza kuzitatua kwa kutuletea bidhaa Affordable kulinganisha na uchumi weru.
Pia wamekuwa wakitumia chombo chao kuwasuta wale wote wanaowashutumu vibaya juu ya siasa zake za ndani kukandamiza haki za raia wake mfano kama utotoni ushawahi kuishi na mlezi anayekutesa siku wakija wageni atakuvalisha nguo nzuri na atapika chakula kizuri na mwisho wa siku atakuita mbele ya wageni na kukuuliza namna gani unaishi naye kwa sababu ya hofu unakuta unamsifia na kuwaambia wageni kuwa una furahia kuishi naye ili hali si kweli.
Mwisho China wanastahili pongezi licha ya mapungufu yao ila wamedhihirishia dunia kuwa wameamua na wanaweza enzi za kutishiwa zilishapita.
From northern part of Tanzania.