Star tv na radio free acheni kufanya kazi kama radio ya chama cha ccm

obama sererea

Senior Member
Mar 13, 2012
101
37
Kwa hivi siku karibuni kituo cha television cha star tv na radio free ya jijini mwanza kimeonesha wazi wazi kuwa sasa kinafanya kazi zake kwa kutekeleza matakwa ya chama cha ccm,hii imeonekana kwenye baadhi ya vipindi vyake,kama vipindi vya kusoma magazeti asubui wamekuwa hawasomi magazeti kama tanzania daima na mengine yenye kukosoa serikali ya ccm,nawakumbusha ikumbuke umaarufu wake iliupata baada ya kuto mpendelea mtu kwenye habari zake,niwakumbushe majira sasa wako wapi na wametoka wapi,watanzania wanauwezo wa kuwapoteza mkawa kama radio uhuru
 
Umaarufu wenu unaweza kupotea kama upepo kutokana chama cha ccm mwanza kukosa mvuto kabisa
 
Umaarufu wenu unaweza kupotea kama upepo kutokana chama cha ccm mwanza kukosa mvuto kabisa
Leo Asubuhi wamenishangaza pia kwa kuondoa kipindi cha matukio kisa Kada wa chama Elnest Mabina ameuawa na wananchi huko kisesa hivyo issue hiyo ndo inge-make headline leo kwenye kipindi chao, wakaona bora waondoe kipindi cha matukio.
 
  • Thanks
Reactions: ram
Kumbe matukio ni kwa wananchi wa kawaida na wapinzani tu. Kada mkubwa kama huyu akiharibu kipindi kinapigwa chini.
 
kumbe star tv kama tbc siku hizi eeeeeeeh!!
ni vema nimelijua hili. kama vipi itv mpango mzima siku zote.............
 
Wasilaumiwe sana,kwa kuwa hicho kituo cha TV na Radio ni mali ya mwenyekiti wa chama mkoa,pia kwa wenyeji na makada wa chama mkoa hakuna asiye fahamu kuwa Marehem na mwenyekiti wa chama picha zilikuwa haziungi!Kwahiyo sijambo la kushangaza.
 
RFA na STAR ilikuwa wakati ule wa vijana kama Sam Kiama,Fredwaa, Deokaji Rahabu na wengineo waliokuwa wanafanya kazi kitaaluma bila kumwogopa mmiliki au kujikomba kwake. Nasikia Dialo hilo hakulitaka akataka kubaki na walamba miguu na ndio hao ambao wanasababisha kituo kinaenda chini na kukosa matangazo ya biashara yenye kuleta fedha sasa mishahara kwa manati.
Ukada ndio tatizo pale. Nasikia Mtangazaji Fred Fidelis aka Fredwaa alipata kusimamishwa kazi eti kwa kuangua kicheko baada ya kusikia Diallo ameanguka uchaguzi mkuu 2010.
 
Wanachonikera ni too much matangazo, kipindi cha watanzania tuongee magazeti kimekuwa cha matangazo tu, nusu saa nzima magazeti yanasomwa dk 10 tu, hata kama matangazo ndo yaingiza pesa katika media bado mnatakiwa kuwa na kiasi ktk kuyapokea hayo matangazo

Kwa hivi siku karibuni kituo cha television cha star tv na radio free ya jijini mwanza kimeonesha wazi wazi kuwa sasa kinafanya kazi zake kwa kutekeleza matakwa ya chama cha ccm,hii imeonekana kwenye baadhi ya vipindi vyake,kama vipindi vya kusoma magazeti asubui wamekuwa hawasomi magazeti kama tanzania daima na mengine yenye kukosoa serikali ya ccm,nawakumbusha ikumbuke umaarufu wake iliupata baada ya kuto mpendelea mtu kwenye habari zake,niwakumbushe majira sasa wako wapi na wametoka wapi,watanzania wanauwezo wa kuwapoteza mkawa kama radio uhuru
 
Umeona eeh....
Mi mwenyewe nimeshangaa sana, eti kutokana na sababu zisizozuilika lol!

Leo Asubuhi wamenishangaza pia kwa kuondoa kipindi cha matukio kisa Kada wa chama Elnest Mabina ameuawa na wananchi huko kisesa hivyo issue hiyo ndo inge-make headline leo kwenye kipindi chao, wakaona bora waondoe kipindi cha matukio.
 
Lakini kile ni kituo binafsi na zaidi ni cha cadre wa chama,mimi hata siwezi kuwalaumu sana kama ninavyowalaumu TBC.
 
no comment, sisi huku mtwara, star tv inazaidi ya miaka miwili haipatikaniki, rfa ina miezi kama mitatu haisikiki,sijui kilichovikumba vituo hivi, lakini ndiyo hivyo diallo lazima atetee unga ndani ya ccm, ukitaka kufanya biashara kwa mafanikio, unga mkono ccm, nukuu toka kauli ya waziri mkuu mstaafu fredrick sumaye
 
Kwa hivi siku karibuni kituo cha television cha star tv na radio free ya jijini mwanza kimeonesha wazi wazi kuwa sasa kinafanya kazi zake kwa kutekeleza matakwa ya chama cha ccm,hii imeonekana kwenye baadhi ya vipindi vyake,kama vipindi vya kusoma magazeti asubui wamekuwa hawasomi magazeti kama tanzania daima na mengine yenye kukosoa serikali ya ccm,nawakumbusha ikumbuke umaarufu wake iliupata baada ya kuto mpendelea mtu kwenye habari zake,niwakumbushe majira sasa wako wapi na wametoka wapi,watanzania wanauwezo wa kuwapoteza mkawa kama radio uhuru
Mimi huwa nafuatilia sana habari za ziara ya CCM mikoni utakuta magazeti mengi yanaripoti lakini hazitolewi kwenye Gazeti pendwa la Tanzania Daima, Pia Habari ya kupikwa (uzushi) ya Kapuya ilikuwa inachapishwa na gazeti moja tu la Tanzania Daina hadi kiu waliona ni uongo...ikabidi Global publisha wafuatilie wakaona ni uzanidiki.............Hivi ili habari zionekane nzuri ni lazima zielezee propaganda za CDM?Mbona suala la mitambo kuathiri mitambo ni la mara kwa mara du, hivi tu CDM haina dola ikiwa na dola si itawafunga waandishi wote wanaoandika tofauiti.............Haya makamanda........Pia Mkuu kwa nini Tanzania Daima hawajaandika ishu ya Slaa kuahidi kuhalalisha gongo au nao wanaacha kuripoti habari za chama au mhariri alizuiwa baada ya kuona kwamba jamaa alichemka.
 
Back
Top Bottom