Star TV na ITV kujitoa rasmi Startimes muda si mrefu!

bampami

JF-Expert Member
Nov 5, 2011
5,697
4,107
Habari nilizozipata, mda mfupi ulio pita ni kuwa mwanasheria wa continental ametuma barua ya kuitaarifu startimes kujitoa kwa startv rasmi startimes, na mda simrefu Itv nao wanatuma rasmi barua kama hiyohiyo, huk startimes mashop yote ya dar ya startimes yameambiwa yawataarifu wateja kuhusu kutoka kwa hizo channel mbili.

NTAENDELEA KUWA UPDATE.....

Source mimi mwenyewe toka maeneo ya hapa bamaga startimes, nimepata habari hizi nikiwa ndani ya duka lao mda huu..wakijadiliana watafanyaje???
Kwa masikitiko ni kwamba watu wote wenye ving'amuzi vya startimes hawataona tena matangazo ya star tv, sababu hazijatangazwa! Ila star times walitangaza kuwa star tv haitaonekana kwenye startimes je tatizo ni ni tunamuomba Yahaya Mohammed aje kutujuza kulikoni? Wamejitoa au wametolewa? Na kwa nini?


Ikumbukwe kuwa Dr.Nkoma alitoka povu akisistiza mabadiliko ya kutoka analogia kwenda digitali ni lazima yawepo kwa nguvu zote hata kama kuna changamoto nyingi.Kiasi waendeshaji vyombo vya habari walilalamika kupata hasara ya matangazo ya biashara; sababu watazamaji wamepungua kiasi kikubwa baadaya kuhamia digitali.Dr.nkoma alizidi kuuthibitishia umma wa kitanzania kuwa Tvs tano zikiwemo start tv, ITV, EATV,channel ten na TBC1 zitaonekana kwenye ving'amuzi vyote bila kujali mmiliki wake.Kuanzia jana STAR TV wamejitoa kingamuzi cha startimes huku kiongozi mkuu akitoka puvu kuwa haitatoka .kwahiyo TCRA watujuze, je tuwe na ving'amuzi vingapi kupata Tv zote.Na ,je watanzania wote wanaweza kununua vingamuzi vyote kama sasa ilivyojitokeza kupata star tv mpaka uwe na kinga'muzi cha continental?

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) itatoa Taarifa na Tamko la Kidhibiti (Regulatory Order) saa saba mchana Kwa saa za Africa Mashariki.

Aidha hakuna ukweli kwamba ITV na Watoa huduma wengine Wa Maudhui wanakusudia kujitoa katika Platform ya Star Media Tanzania Limited.

Hivi sasa kikao kinaendelea Kati ya Mamlaka na Watoa Huduma hao wawil na Maamuzi ya TCRA yatatangazwa saa saba mchana mbele ya vyombo vya Habari Mawasiliano Towers.

Msemaji Wa Mamlaka

Ni vizuri kuuelewa mfumo mpya Wa Utangazaji, Sheria na Kanuni zake badala ya kutoa kauli ambazo sio za ukweli na zenye nia ya kupotosha umma. Free to Air Channel zote ni Must Carry Kwa Multplex Operator Wote, yaani Agape Associates, Basic Transmission na Star Media Tanzania Limited Kwa mujibu Wa Sheria ya EPOCA, 2010 na Kanuni zake za 2011 kama ilivyoainishwa.

Kwa taarifa na Maelezo zaidi soma Sheia hiyo na Kanuni zake katika website ya TCRA www.tcra.go.tz.
 
Wajitoe haraka sana, startimes kazi imewashinda. Natamani kukitupa hiki kisi-MBUZI chao.
 
Kwanini wameamua kujitoa kwenye Startimes?

Hivi ni nani huwa anamlipa mwenzie ili channel yake iwepo hewani, ni startime au TV channel?
 
Bora maana nilikuwa nampango wa kununua

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hizo habari ni uongo na uzushi wa vijiweni!

Sheria ya mawasiliano kupitia TCRA inazitamka ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL 10 na EATV kama ni FTA yaani Free To Air channels na sio Pay TV.

Sheria inawataka wamiliki wote wa visimbuzi vyenye local license kuziweka kwenye list hizo channels bure bila walaji kulipia!

Wakuu endeleeni kuumiza macho kupitia visimbuzi vyenu!
 
Kwenye hiki king'amuzi cha kikulima cha Star Times kuna tangazo linapita kuwa Star TV wanataka kujitoa kwa Star Times,Sijui wanafikiria nini wakati coverage yao ni ndogo sana hasa kwa kupitia king'amuzi chao cha CONTINENTAL.
Nafikiri hawajajifunza kwa CLOUDS TV ambao walijifanya wanakimbia Star Times wakati hata watazamaji hawana,
Nafikiri wakae chini waangalie suala hili vizuri kabla ya kukurupuka.
 
Kila jambo hufanywa kufuatana na maslahi hivyo basi kama Star Tv wameona kwamba kwao ni hasara wana haki ya kujitoa
 
Siku hizi haina haja ya kuwa na Tv tena kwa maana masharti ni mengi
 
  • Thanks
Reactions: mja
Nimeliona hilo tangazo...ntatafuta king'amuzi kingine...startimes wanazingua na channl zisizo na viwango
 
Hizo habari ni uongo na uzushi wa vijiweni!

Sheria ya mawasiliano kupitia TCRA inazitamka ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL 10 na EATV kama ni FTA yaani Free To Air channels na sio Pay TV.

Sheria inawataka wamiliki wote wa visimbuzi vyenye local license kuziweka kwenye list hizo channels bure bila walaji kulipia!

Wakuu endeleeni kuumiza macho kupitia visimbuzi vyenu!

Tangazo linapita saiv kwenye tv, Star tv wanajitoa
 
Hizo habari ni uongo na uzushi wa vijiweni!

Sheria ya mawasiliano kupitia TCRA inazitamka ITV, TBC, STAR TV, CHANNEL 10 na EATV kama ni FTA yaani Free To Air channels na sio Pay TV.

Sheria inawataka wamiliki wote wa visimbuzi vyenye local license kuziweka kwenye list hizo channels bure bila walaji kulipia!

Wakuu endeleeni kuumiza macho kupitia visimbuzi vyenu!


Mkuu wewe ndio unaleta habari za vijiweni. Tayari tangazo la kujitoa kwa STAR TV linapita kwenye screen, wakisema

Ndugu mteja kutokana na matakwa ya STAR TV inatulazimu kuitoa katika orodha ya chaneli zetu. kwa maelezo zaidi piga STAR TV 0202503262. Samahani kwa usumbufu utakao jitokeza.

Jambo hili limekuja kipindi kizuri wakati watunga sheria wetu wakiwa kazini. Tuone basi kama hii ishu iaibuliwa bungeni.
 
Sasa tunaondoa maana halisi ya Digital coz inatakiwa mtu akiwa kwenye king'amuzi chochote apate Chanel zote muhimu!
 
Back
Top Bottom