Star Tv Mnachosha kwa kurudiarudia vipindi. Kwa nini?

SHIEKA

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,244
4,258
Mimi naitazama sana star tv. Hivi karibuni nimegundua kitu. Hawa wajamaa wana tabia ya kurudia vipindi fulani mara kwa mara. Kwa nfano: Kuna kipindi kinachohusu ugunduzi wa gari linaloendeshwa kwa nguvu za umeme huko uganda. Hiki kipindi kimerudiwa mpaka kinaniletea hasira ya kuzima tv kila kikitokea.Star tv, kwa nini marudio hayo? Pia kuna kipindi kinachohusu duma huko Namibia Kimerudiwa mpaka basi.
Halafu kero kuu ipo wakati wa taarifa ya habari usiku saa 2.Ukisikia wakisema tunapumzika kidogo ujue ni tangazo la Wajanja vodacom linakuja! Tangazo hili kwangu ni kero kubwa wakati wa taarifa ya habari.Yaani linakuwa ndo taarifa yenyewe ya habari! Star tv, ninajua mnafanya biashara kutunisha mguko wenu lakini msifanye hivo kwa gharama ya kuudfhi watazamahi kama mimi. Naomba mlishughulikie hili la tangazo za wajanja na marudio ya vipindi nilivyotaja.
 
Hahahahahaha!! Tangazo la wajanja!! Jaribu chanel zingne mkuu.
 
Halo GOOGLE! Channel nyingine zinaweka hilo tangazo la 'Wajanja', lakini sio kwa frequency na intensity ya Star tv! Naona kama vile star tv wanalipwa mkwanja mrefu zaidi kuweka hilo tangazo kwa jinsi wanavyolihusudu, pamoja na la lile la bia ya kwanza afrika mashariki!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom