Star TV: Mkutano wa hadhara wa Mwigulu Nchemba, leo tarehe 6 Disemba, 2014

Tema Mate

Senior Member
Dec 19, 2013
107
193
Hii leo Nibu Katibu Mkuu CCM BARA na Naibu waziri wa Fedha ambayea siku karibuni amebatizwa jina la SOKOINE Wa PILI atakuwa na Mkutamo wa hadhara Mkoani geita utakao Rushwa LIVE na Star tv kuanzia saa 8 mchana hii leo.

Mwigulu anakwenda kuzungumza na Watanzania kuhusu Mambo makubwa ambayo TAIFA letu linapitia,Utekelezaji wa Bajeti ya serikali na namna Mapapa wanavyopambana kukwamisha Mswada wa Kufuta Misamaha ya Kodi isiyo na tija kwa Taifa letu.
Mwigulu Nchemba anakwenda kuuelezea Umma kuhusu malengo na dhamira yake ya kusaidia wanyonge na Masiki,Vijana wasio na ajira na sakata la Matumizi mabaya ya fedha za Umma.

RUKSA kushare na Kuwatangazia jamaa na Watanzania wapenda Maendeleo.

Ni leo hii tar 06/12/2014 saa 8 kuelekea saa 9 Mchana kupitia Sta tv.
 
Huyo Mwigulu hana lolote, si alijidai kujikakamua pale bungeni Dodoma, eti waliojikwapulia fedha ya umma kwenye Escrow account, wawe wamezilipia kodi hizo pesa walizoiba, hadi ifikapo Desemba 30 mwaka huu.

Sasa si yeye mwenyewe amejionea jinsi huyo Singasinga wa IPTL alivyoivimbia serikali, na kutoa 'agizo' kutaka kamishina mkuu wa TRA, akamatwe na kufunguliwa mashitaka, ya kumdhalilisha yeye kuwa hajalipa kodi kwenye pesa aliyoikwapua kwenye akaunti ya Escrow, wakati amelipia kodi hayo mabilioni aliyoiba?!

Sasa itakuwa vyema kwenye kikao chake cha leo, aanze kwanza kulieleza hilo la Singasinga, jinsi anavyomvimbia na kugoma kulipa hiyo kodi, na jinsi alivyoiweka mfukoni serikali hii ya CCM!
 
Kwa mara ya kwanza tamsikiliza baada ya kusimama kidete kuwakandamizia mafisadi. Ila asiwepo Assampta yule mbuge wa Nkenge.
 
Hilo jina la sokoine wa II alipewa na nani mkuu? Leo itabidi nitafute muda niangalie koz bungeni alinifurahisha sana, lakini sasa aache habari zake za sijui nani kaiba mke wa furani, mara fulani kazaa na futani, Yeye aendelee kuwa mjenga hoja hata kama anapinga upinzani apinge kwa facts maana atleast yeye ndio kabakia mwenye akili CCM lakini sio kama wale wengine.
 
Ahakikishe pia anawaambia kutokana na wizi wa escrow katiba pendekezwa haifai kwakuwa inachochoe na kuwalinda wezi. Hapi kweli atakuwa amenikuna.
 
Ahakikishe pia anawaambia kutokana na wizi wa escrow katiba pendekezwa haifai kwakuwa inachochoe na kuwalinda wezi. Hapi kweli atakuwa amenikuna.
tatizo hawezi kusema kwa sababu hiyo katiba hata yeye amehusika kuipigia kura ya NDIYO ccm wote ni wanafiki sana.
 
Hilo jina la sokoine wa II alipewa na nani mkuu? Leo itabidi nitafute muda niangalie koz bungeni alinifurahisha sana, lakini sasa aache habari zake za sijui nani kaiba mke wa furani, mara fulani kazaa na futani, Yeye aendelee kuwa mjenga hoja hata kama anapinga upinzani apinge kwa facts maana atleast yeye ndio kabakia mwenye akili CCM lakini sio kama wale wengine.

daahhh hadi Kaka Shardcore umemkubali Mwigulu.Wallah Mwigulu ni Mashine,Jina la Sokoine amepewa na Watanzania
 
Muda mwingine ni bora ufunge hiyi Biashara ya Mayai naona Wateja wamekata,Saaa unapoteza hasira zako hapa
Mbona umepanic sana mkuu mwigulu ni mjomba yako huyu gaidi nani ataenda kumsikiliza labda wewe na ukoo wenu
 
Aende kupeleka maendeleo Iramba wanamngoja barabara zimesombwa na mvua zinazoendelea kunyesha
 
Back
Top Bottom