Napenda kuwapongeza star TV kwa ubunifu walionao kwa kupenda kuweka vipindi vizuri na vinavyoleta tija katika taifa letu. Jana kulikuwa na kipindi kizuri sana kuhusu mjadala wa KATIBA MPYA. Me napenda kuwashukuru na muendelee na moyo huo huo, Kwa upande wa MZA kulikuwa na YAHAYA MOHAMED na wanafunzi wawili kutoka SAUT, Upande wa Dar, kulikuwa na Mh Kafulila(NCCR), Mtatiro(Cuf) na Mwita Mwikabe(Chadema). Kweli kilitoa picha wananchi tunahitaji katiba mpya na mimi naomba hili liendelezwa na vituo vingine pia kama ITV na TBC, WASIONE HAYA maana hili swala si la chadema, wala dr slaa wala cuf wala nccr ni la wote. HATA TBC wasione haya.
Kweli STAR TV mmekomaa na mpo tayari kwa hilo na tumshukuru mh Antony Diallo kwa hilo.
Kweli STAR TV mmekomaa na mpo tayari kwa hilo na tumshukuru mh Antony Diallo kwa hilo.