Swizzy
JF-Expert Member
- Nov 4, 2016
- 773
- 511
Tangu jumatatu mpaka muda huu kingamuzi cha Star times kinaonesha channels zote for free (buree!!) hata kama hujalipia unaona tu.
Hii sio Mara ya kwanza kwa Star times kuachia chaneli zote bure kwa watazamaji wote hata ambao hawajalipia. Hii inafaida sana kwa watazamaji kwani mtazamaji/ mteja anaweza kuona hata chaneli zile za vifurushi vya bei kubwa.
Mwisho wa siku hiyo huduma ya kuangalia bure ikiisha kama mteja akivutiwa na vifurushi vya bei kubwa lazima atafanya juu chini alipie hata wale ambao huwa hawalipii kabisa watalipia kutokana na hizo huduma za bure ambazo star times huwa inazitoa kwa baadhi ya siku.
Ombi kwa DSTV, AZAM n.k na nyie muwe mnaachia vifurushi vyenu vyote bure kwa baadhi ya siku, ili sisi wateja tuangalie vinavyo tufaa maana tume zoea kulipia vifurushi vya bei ya chini kabisa hivyo vya bei kubwa tuna viogopa kweli hatujui hizo chaneli mlizo ziongeza kwenye hivyo vifurushi zina nini hadi kifurushi kinakuwa na bei kubwa. Tuna omba muige mfano kwa StarTimes.
Wenye ving'amuzi vya Star Times wacha tuendelee kufurahia huduma ya buree!!
....Ahsante nawasilisha....
Hii sio Mara ya kwanza kwa Star times kuachia chaneli zote bure kwa watazamaji wote hata ambao hawajalipia. Hii inafaida sana kwa watazamaji kwani mtazamaji/ mteja anaweza kuona hata chaneli zile za vifurushi vya bei kubwa.
Mwisho wa siku hiyo huduma ya kuangalia bure ikiisha kama mteja akivutiwa na vifurushi vya bei kubwa lazima atafanya juu chini alipie hata wale ambao huwa hawalipii kabisa watalipia kutokana na hizo huduma za bure ambazo star times huwa inazitoa kwa baadhi ya siku.
Ombi kwa DSTV, AZAM n.k na nyie muwe mnaachia vifurushi vyenu vyote bure kwa baadhi ya siku, ili sisi wateja tuangalie vinavyo tufaa maana tume zoea kulipia vifurushi vya bei ya chini kabisa hivyo vya bei kubwa tuna viogopa kweli hatujui hizo chaneli mlizo ziongeza kwenye hivyo vifurushi zina nini hadi kifurushi kinakuwa na bei kubwa. Tuna omba muige mfano kwa StarTimes.
Wenye ving'amuzi vya Star Times wacha tuendelee kufurahia huduma ya buree!!
....Ahsante nawasilisha....