TODAYS
JF-Expert Member
- Apr 30, 2014
- 13,745
- 21,196
Siasa za Afrika ni sawa na mti wenye majani mabichi yanayokufanya upende kwenda kukaa chini yake kwa sababu una kivuri kizuri ilihali chini kuna mchwa wanautafuna.
Nchini Uganda Rais anayesemwa na mpinzani wake kuwa ni dikteta Yoweli Museveni anafikilia kuwanyima haki wananchi wa Uganda kumchagua Rais wao, ambapo anafikilia bunge ndiyo liwe na uwezo wa kumchagua rais mpya.
Bila shaka anapanga kufanya hivi ili kuja kulazimisha mwanawe ndiye aje kuwa rais, huku akijua kuwa hawezi hata kupata kura za kutosha kutoka kwa wananchi.
Hawa ndiyo aina ya viongozi wa kiafrika.