Kwanini SSRA ikubali kuwalipa mafao wafanyakazi wa GGM na sio wafanyakazi wote ambao wako kwenye mifuko ya jamii?
>>>>>
Kumb. Na. CB.75/396/VOL.II/16 DATE: 30/07/ 2012
Meneja Mkuu,
Geita Gold Mining Ltd,
P.O.Box 532,
GEITA.
YAH: UFAFANUZI WA SSRA KWA WAFANYAKAZI WA MGODI WA GEITA
GOLD KUHUSU FAO LA KUJITOA
Tafadhali husika na kichwa cha habari hapo juu. Pamoja na kikao kilicho fanyika tarehe
25/07/2012 katika Mgodi wa Geita Gold na kuhudhuriwa na kiongozi wa Mamlaka ya
Usimamizi wa Sekta ya hifadhi ya Jamii (SSRA) na wafanyakazi wa Mgodi wa Geita
Kwanza kabisa tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kupata nafasi ya kutoa ufafanuzi
kuhusu kusitishwa kwa fao la kujitoa. Katika kikao hicho mliitaka Mamlaka kutoa majibu
ya hoja zenu. Hoja ambazo zimekuwa sababu za wafanyakazi kupinga Sheria inayozuia
kuwepo kwa fao la kujitoa:
Napenda kuwafahamisha kwamba hoja zote zilizotolewa ni za msingi sana na
zitatusaidia kuja kwenu mara mtakapotupangia ili kutoa ufafanuzi zaidi. Hata hivyo hoja
inayohitaji ufafanuzi wa haraka ni inayouliza; kutokana na hali na mazingira ya kazi je
wafanyakazi wa mgodi wenu wataendelea kupata fao la kujitoa baada ya marekebisho ya
Sheria? Jibu lake ni ndiyo. Kutokana na mazingira ya kazi na aina za mikataba
mliyokuwa nayo, mfanyakazi atakuwa na uhuru wa kuchagua kuendelea na pensheni au
kupewa fao la kujitoa. Kama mlivyofananuliwa na SSRA wakati wa kikao, wale wote
ambao waliingia mikataba kabla ya mabadiliko ya S heria watalipwa fao la kujitoa mara
mikataba yao itakapoiva. Wafanyakazi wapya watashuriwa kujiunga na Mfuko wa Akiba
unaruhusu wenye fao la kujitoa.
Kwa vile kwa mujibu wa Sheria, Mfuko wa msingi (mandatory Scheme) unaotoa fao la
kujitoa ni GEPF, Mamlaka itawashauri wafanyakazi wapya kujiunga na Mfuko huo. Hii ni
Barua zote za Kiofisi zitumwe kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka
Page 2
baada ya kutoa miongozo pamoja na kutoa elimu kwa kushirikisha Mifuko yote ili
wafanyakazi wa Mgodi wa Geita Gold waweze kuelewa aina za Mifuko na aina za mafao
ili kufanya maamuzi sahihi.
Vile vile kwa kuzingatia hali halisi na ugumu wa mazingira ya kazi za migodini, Mamlaka
itaangalia wakati wa kuandaa miongozo, uwezekano wa kuwa na skimu inayoendana na
mahitaji ya wafanyakazi hao katika Mifuko Mingine kama vile NSSF,PPF,LAPF na PSPF.
Hivyo tunachukua fursa hii kuwafahamisha kuwa wafanyakazi wa Mgodi wa Geita Gold
kwamba watalipwa mafao yao ya kujitoa mara mikataba yao itakapoiva na kuruhusiwa
kuchagua kujiunga na Mifuko ya Pensheni au Mfuko wa Akiba.
Shukrani za dhati kwa ushirikiano wenu.
Wenu,
MAMLAKA YA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA HIFADHI YA JAMII
Irene Isaka
MKURUGENZI MKUU
>>>>>
Kumb. Na. CB.75/396/VOL.II/16 DATE: 30/07/ 2012
Meneja Mkuu,
Geita Gold Mining Ltd,
P.O.Box 532,
GEITA.
YAH: UFAFANUZI WA SSRA KWA WAFANYAKAZI WA MGODI WA GEITA
GOLD KUHUSU FAO LA KUJITOA
Tafadhali husika na kichwa cha habari hapo juu. Pamoja na kikao kilicho fanyika tarehe
25/07/2012 katika Mgodi wa Geita Gold na kuhudhuriwa na kiongozi wa Mamlaka ya
Usimamizi wa Sekta ya hifadhi ya Jamii (SSRA) na wafanyakazi wa Mgodi wa Geita
Kwanza kabisa tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kupata nafasi ya kutoa ufafanuzi
kuhusu kusitishwa kwa fao la kujitoa. Katika kikao hicho mliitaka Mamlaka kutoa majibu
ya hoja zenu. Hoja ambazo zimekuwa sababu za wafanyakazi kupinga Sheria inayozuia
kuwepo kwa fao la kujitoa:
Napenda kuwafahamisha kwamba hoja zote zilizotolewa ni za msingi sana na
zitatusaidia kuja kwenu mara mtakapotupangia ili kutoa ufafanuzi zaidi. Hata hivyo hoja
inayohitaji ufafanuzi wa haraka ni inayouliza; kutokana na hali na mazingira ya kazi je
wafanyakazi wa mgodi wenu wataendelea kupata fao la kujitoa baada ya marekebisho ya
Sheria? Jibu lake ni ndiyo. Kutokana na mazingira ya kazi na aina za mikataba
mliyokuwa nayo, mfanyakazi atakuwa na uhuru wa kuchagua kuendelea na pensheni au
kupewa fao la kujitoa. Kama mlivyofananuliwa na SSRA wakati wa kikao, wale wote
ambao waliingia mikataba kabla ya mabadiliko ya S heria watalipwa fao la kujitoa mara
mikataba yao itakapoiva. Wafanyakazi wapya watashuriwa kujiunga na Mfuko wa Akiba
unaruhusu wenye fao la kujitoa.
Kwa vile kwa mujibu wa Sheria, Mfuko wa msingi (mandatory Scheme) unaotoa fao la
kujitoa ni GEPF, Mamlaka itawashauri wafanyakazi wapya kujiunga na Mfuko huo. Hii ni
Barua zote za Kiofisi zitumwe kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka
Page 2
baada ya kutoa miongozo pamoja na kutoa elimu kwa kushirikisha Mifuko yote ili
wafanyakazi wa Mgodi wa Geita Gold waweze kuelewa aina za Mifuko na aina za mafao
ili kufanya maamuzi sahihi.
Vile vile kwa kuzingatia hali halisi na ugumu wa mazingira ya kazi za migodini, Mamlaka
itaangalia wakati wa kuandaa miongozo, uwezekano wa kuwa na skimu inayoendana na
mahitaji ya wafanyakazi hao katika Mifuko Mingine kama vile NSSF,PPF,LAPF na PSPF.
Hivyo tunachukua fursa hii kuwafahamisha kuwa wafanyakazi wa Mgodi wa Geita Gold
kwamba watalipwa mafao yao ya kujitoa mara mikataba yao itakapoiva na kuruhusiwa
kuchagua kujiunga na Mifuko ya Pensheni au Mfuko wa Akiba.
Shukrani za dhati kwa ushirikiano wenu.
Wenu,
MAMLAKA YA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA HIFADHI YA JAMII
Irene Isaka
MKURUGENZI MKUU