SportPesa 2018 kufanyika Kenya

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Aug 12, 2011
7,140
14,678
nondi-edit-1.jpg


Michuano ijayo ya Kombe la Sport Pesa Super Cup, mwaka 2018, inatarajiwa kufanyika Kenya ikishirikisha timu nane za Kenya na Tanzania.

Mkurugenzi wa Utawala na Utekelezaji wa Sport Pesa inayodhamini michuano hiyo, Abbas Tarimba alisema jana wamefurahishwa na ushindani ulioonyeshwa na timu katika michuano ya mwaka huu iliyomalizika juzi kwa Gor Mahia ya Kenya kutwaa ubingwa huo.

Alisema pamoja na changamoto zilizojitokeza kwenye michuano hiyo, lengo lao la kuzinoa klabu kujiimarisha na ligi zao limefanikiwa na wanafurahi kuona hakuna malalamiko ya timu.

Hongera sana Gor Mahia, hongera Zedekiah Otieno (the team coach), hongera Kenya… muiwakilishe vema East africa on the coming match (July 13, 2017) against Everton…
 
I hpe wataleta kikosi cha kwanza...hawa waingereza wana tabia mbaya ya kuleta team B kuchuana na timu za kiafrika...
 
hata hvo simba sc na yanga sc walidharau sana haya mashandano, walichezesha timu B, na wacheji wa majaribio.
 
Mara nyingi huwa ni kutuondoshea aibu ya kuchabangwa mabao ishini mtungi!

Juzi ile siku Kenya wamecheza na Hull, unaona wangetia kikosi A tungenyukwa mabao sio chini ya thelathini.

Kudumisha urafiki kheri walete kikosi C
emoji23.png
emoji23.png
kuchabangwa mabao sio chini ya thelatini
emoji23.png
emoji23.png
dah!
emoji23.png
emoji23.png
ila ni ukweli, niliona wale wa Hull City Tigers walivyomenyana na sportpesa allstars wakanyukwa mabao na kushindwa ilhali wale wachezaji wa Hull walikuwa bado wachanga sana...kama teenagers vile...dah! sijui Everton team A inaweza ikawatendea unyama upi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom