Spika wa Bunge ana double standard?

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,427
85,872
Miezi michache alisimama mbele ya Bunge akidai kuwa CHADEMA kuna mfumo dume na kwamba yeye "anawaonea huruma na kuwaheshimu sana wanawake"

Leo hii, Spika yule yule, tena kwa udhalilishaji wa hali ya juu, kamtoa nje Mbunge wa CCM kwa kile kilichodaiwa kuwa "amevaa" nguo isiyo ya heshima.

Huyu Mbunge hakuwa anacheza dance, aliingia na kuketi, wala hakujitembeza mbele ya Bunge na "kuwatamanisha" wakware, iweje Ndugai ashindwe kutumia busara na kuamua kumdhalilisha kwa kiasi kile?

Hata hivyo, nimekumbuka wote ni CCM wanajuana wenyewe, "wakimalizana na sisi, watageukiana wenyewe kwa wenyewe"
 
Kitendo cha Ndugai kumtoa huyo dada bungeni kimenifanya niyajue mawazo yake, wakati wenzie wako busy kujenga hoja kuwasemea Watanzania matatizo yao, yeye yuko busy kuangalia maumbile ya watoto wa kike.
 
Hongera wabunge wa CCM

IMG-20210601-WA0049.jpg
 
Back
Top Bottom