Spika Tulia Ackson anapaswa awajibike kwa kujiuzulu, kutokana na kutamka kuwa anayemsema vibaya Rais Samia, anapaswa ashughulikiwe!

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Kwanza nieleze masikitiko yangu makubwa Sana kwa jinsi nilivyomsikia Spika Tulia Ackson akihamasisha machafuko, wakati akihutubia Umoja wa vijana wa CCM huko jijini Mbeya.

Kwa nchi inayoendeshwa kwa Demokrasia na yenye mfumo wa vyama vingi, ni jambo la kuskitisha Sana kwa matamko aliyoyatoa Spika wa Bunge letu Katika kikao cha UVCCM, kwa kuwataka vijana hao kuwa wasimvumilie mtu yoyote, aidha kutoka CCM au vyama vya upinzani, kuwa washughulike naye, atakayemsema vibaya Rais wetu Samia Suluhu Hassan!

Hayo maneno ni ya hatari Sana Katika nchi inayohubiri kudumisha amani kila siku.

Hivi kutoa "critical criticism" kwa kiongozi wa nchi, au kwa Spika wa Bunge, au hata kwa Mbunge yeyote, lengo likiwa kurekebisha mfumo ambao utauona siyo wa Haki, hivi kuna ubaya gani, Hadi Spika wetu atoe maneno ya vitisho vya kiasi hicho?

Katiba ya nchi yetu, ambayo ni sheria mama, Katika ibara ya 18(1) inatoa uhuru kwa kila mtanzania kutoa maoni yake.

Hivi Spika Tulia Ackson, anajaribu hata kupingana na Katiba ya nchi yetu, iliyotoa uhuru wa wananchi, kutoa maoni yao?

Hivi Spika Tulia Ackson, anajua kuwa kutokana na hayo matamko yake aliyoyatoa kwa huo Umoja wa vijana wa CCM, unaweza kuleta machafuko makubwa ya umwagaji damu nchini?🥺

Kutokana na maelezo hayo ningependa kumwomba Spika Tulia Ackson, ajiuzulu nafasi yake ya u-Spika wa Bunge Ili kuliepusha Taifa hili na machafuko ya umwagikaji damu

Mungu ibariki Tanzania
 
Na huyo ndo kiongozi unayetegemea aongoze mhimili wa kutengeneza sheria zitakazotoa haki kwa wananchi wote!!

Tanzania yangu nakulilia sana, ni wapi tulipokosea? Ni wapi waliotengeneza katiba yetu walipokosea? Ni lini walioshiba katika nchi hii watamuona mnyonge? Why wakishakalia hivyo viti wanasahau kila kitu?

Ipo siku Mungu aishie atakasirika, na nchi itaongozwa katika misingi ya haki kwa watu wote!!
 
Kwa nchi inayoendeshwa kwa Demokrasia na yenye mfumo wa vyama vingi, ni jambo la kuskitisha Sana kwa matamko aliyoyatoa Spika wa Bunge letu Katika kikao cha UVCCM, kwa kuwataka vijana hao kuwa wasimvumilie mtu yoyote, aidha kutoka CCM au vyama vya upinzani, kuwa washughulike naye!
Halina ubishi hilo. Mtu mzima, mama wa familia, mke wa mtu, ndugu wa ukoo,shemeji na mkwe wa ukoo,kiongozi wa mhimili wa serikali, msomi wa udaktari wa sheria ambaye hatujawahi kuona vyeti vyake vya matatizo ya afya ya akili kutamka hadharani ujinga ule ni dhahma kwa jamii ya wastaarabu. Maneno yale ndiyo hufanya wadharaulike na kutukanwa hovyo hadharani au mitandaoni.Aibu kubwa sana.
 
Kwanza nieleze masikitiko yangu makubwa Sana kwa jinsi nilivomsikia Spika Tulia Ackson akihamasisha machafuko, wakati akihutubia Umoja wa vijana wa CCM huko jijini Mbeya...
Hivi Spika Tulia Ackson, anajua kuwa kutokana na hayo matamko yake aliyoyatoa kwa huo Umoja wa vijana wa CCM, unaweza kuleta machafuko makubwa ya umwagaji damu nchini?

Kutokana na maelezo hayo ningependa kumwomba Spika Tulia Ackson, ajiuzulu nafasi yake ya u-Spika wa Bunge Ili kuliepusha Taifa hili na machafuko ya umwagikaji damu
 
Halina ubishi hilo.Mtu mzima,mama wa familia,mke wa mtu,ndugu wa ukoo,shemeji na mkwe wa ukoo,kiongozi wa mhimili wa serikal...
Kwa kweli hata Mimi nashangaa, kusikia kuwa huyo Spika Tulia Ackson, eti ana shahada ya PhD ya sheria!

Hivi inakuwaje kwa mwenye PhD ya sheria, asiweze hata kuzitafsiri sheria mama,

zilizomo kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania??🥺
 
Hivi Spika Tulia Ackson, anajua kuwa kutokana na hayo matamko yake aliyoyatoa kwa huo Umoja wa vijana wa CCM, unaweza kuleta machafuko makubwa ya umwagaji damu nchini?

Kutokana na maelezo hayo ningependa kumwomba Spika Tulia Ackson, ajiuzulu nafasi yake ya u-Spika wa Bunge Ili kuliepusha Taifa hili na machafuko ya umwagikaji damu
Naam.Amekosea mnoo!Ameongea kama mwanamke fulani wa hovyo(aliyelewa mipombe) na yupoyupo tu.Aibu sana.
 
Wakati mwingine tuwahurumie tu wanasiasa kama huyu!!?

UNAFIKIRI angesemaje!!??wakati anajua ni kwa Namna GANI kaingia Bungeni na uspika kaupataje!!

Acha ibaki ivo ivo!Mungu karidhia haya KUTOKEA kwa wakati HUU!!

TUSUBIRI mengine!
 

Mwenyewe akisoma huu uzi anacheka, haamini kama kuna kitu kinaitwa 'kujiuzulu', yaani unamwambia aruke kutoka kwenye V8?
Yaani ingekuwa kwenye nchi inayotekeleza kwa vitendo mfumo wa kidemokrasia wa vyama vingi na inayoendeshwa kwa mfumo wa sheria, alipaswa huyo Spika Tulia Ackson, ajiuzulu mara moja, Ili kuliepusha Taifa hili na aibu ya kutozingatia sheria tunazoapa kuzitii, kabla hatukabidhiwa majukumu hayo ya kitaifa
 
Na huyo ndo kiongozi unayetegemea aongoze mhimili wa kutengeneza sheria zitakazotoa haki kwa wananchi wote!!

Tanzania yangu nakulilia sana, ni wapi tulipokosea? Ni wapi waliotengeneza katiba yetu walipokosea? Ni lini walioshiba katika nchi hii watamuona mnyonge? Why wakishakalia hivyo viti wanasahau kila kitu?

Ipo siku Mungu aishie atakasirika, na nchi itaongozwa katika misingi ya haki kwa watu wote!!
Duh !! Hatari sana !
 
Kwanza nieleze masikitiko yangu makubwa Sana kwa jinsi nilivomsikia Spika Tulia Ackson akihamasisha machafuko, wakati akihutubia Umoja wa vijana wa CCM huko jijini Mbeya.

Kwa nchi inayoendeshwa kwa Demokrasia na yenye mfumo wa vyama vingi, ni jambo la kuskitisha Sana kwa matamko aliyoyatoa Spika wa Bunge letu Katika kikao cha UVCCM, kwa kuwataka vijana hao kuwa wasimvumilie mtu yoyote, aidha kutoka CCM au vyama vya upinzani, kuwa washughulike naye!

Hayo maneno ni ya hatari Sana Katika nchi inayohubiri kudumisha amani kila siku.

Hivi kutoa "critical criticism" kwa kiongozi wa nchi, au kwa Spika wa Bunge, au hata kwa Mbunge, lengo likiwa kurekebisha mfumo ambao utauona siyo wa Haki, hivi kuna ubaya gani, Hadi Spika wetu atoe maneno ya vitisho vya kiasi hicho?

Katiba ya nchi yetu, ambayo ni sheria mama, Katika ibara ya 18(1) inatoa uhuru kwa kila mtanzania kutoa maoni yake.

Hivi Spika Tulia Ackson, anajaribu hata kupingana na Katiba ya nchi yetu, iliyotoa uhuru wa wananchi, kutoa maoni yao?

Hivi Spika Tulia Ackson, anajua kuwa kutokana na hayo matamko yake aliyoyatoa kwa huo Umoja wa vijana wa CCM, unaweza kuleta machafuko makubwa ya umwagaji damu nchini?🥺

Kutokana na maelezo hayo ningependa kumwomba Spika Tulia Ackson, ajiuzulu nafasi yake ya u-Spika wa Bunge Ili kuliepusha Taifa hili na machafuko ya umwagikaji damu

Mungu ibariki Tanzania
Tulia omba Bwana akupe hekima.
 
Wakati mwingine tuwahurumie tu wanasiasa kama huyu!!?

UNAFIKIRI angesemaje!!??wakati anajua ni kwa Namna GANI kaingia Bungeni na uspika kaupataje!!

Acha ibaki ivo ivo!Mungu karidhia haya KUTOKEA kwa wakati HUU!!

TUSUBIRI mengine!
Neno "kuwahurumia" sidhani kama ni sahihi.Linaweza kuwa sawa ila si sahihi.Mtu mzima,mbele ya umma /hadharani anaanzaje kutoa maneno ya kijinga namna hiyo?Huko sasa ndiyo kujiona ni above the law.Tukijidai tunawahurumia ni kosa na laana kwa jamii.Watazoea na kuona ndiyo mtindo wa maisha.Kavimbiwa huyo.Likianzishwa timbwili mtaani ana uwezo wa kusimama na kujitetea nafsi yake?Akome kuwa na tabia mbaya kama mwanamke wa jalalani.Shame!
 
Hivi Spika Tulia Ackson, anajua kuwa kutokana na hayo matamko yake aliyoyatoa kwa huo Umoja wa vijana wa CCM, unaweza kuleta machafuko makubwa ya umwagaji damu nchini?

Kutokana na maelezo hayo ningependa kumwomba Spika Tulia Ackson, ajiuzulu nafasi yake ya u-Spika wa Bunge Ili kuliepusha Taifa hili na machafuko ya umwagikaji damu
Jamaa wenye akili finyu watajua wameshapewa green light ya kunyooka na wanaowaona hawapo upande wao !! Kauli za namna hii hazifai kabisa kwa mustakabali mwema wa Nchi !!
 
Neno "kuwahurumia" sidhani kama ni sahihi.Linaweza kuwa sawa ila si sahihi.Mtu mzima,mbele ya umma /hadharani anaanzaje kutoa maneno ya kijinga namna hiyo?Huko sasa ndiyo kujiona ni above the law.Tukijidai tunawahurumia ni kosa na laana kwa jamii.Watazoea na kuona ndiyo mtindo wa maisha.Kavimbiwa huyo.Likianzishwa timbwili mtaani ana uwezo wa kusimama na kujitetea nafsi yake?Akome kuwa na tabia mbaya kama mwanamke wa jalalani.Shame!
Muhimu aombe radhi na atolee ufafanuzi wa kauli ile !!
 
Back
Top Bottom