Spika Sitta na Usiri wa Mikataba na majibu ya serikali

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,921
31,161
2008-12-04 10:26:57
Na Mashaka Mgeta

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania, Samuel Sitta, amesema hakuna mantiki kwa waziri kusaini mkataba wa uchumi na biashara nje ya nchi na kufanya kuwa siri kwa umma.

Ingawa Spika Sitta hakumtaja moja kwa moja waziri aliyefanya hivyo, lakini kauli yake hiyo imekuja huku kukiwa na shutuma dhidi ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi kusaini kwa siri mkataba wa uwekezaji katika mgodi wa Buzwagi ambao unamilikiwa na kampuni ya Barrick, nchini Uingereza.

Sitta alisema hayo jana jioni katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Salaam wakati akizindua Mfuko Maalum wa kusaidia kujenga uwezo kwa wanahabari na vyombo wanavyofanyia kazi.

Alisema usiri unaofanyika katika kusaini mikataba hiyo, hautoi fursa iwapo umefanyika kwa maslahi ya umma au kwa kuiuza nchi.

``Kuna mantiki gani kwa waziri anakwenda ughaibuni kutuambia kuwa anakwenda kusaini mkataba wenye maslahi yetu wananchi na baadaye akirejea atuambie kuwa walichokubaliana ni siri, hata kwa wawakilishi wetu yaani wabunge,`` alisema Spika na kuhoji.

``Tutapimaje basi ikiwa maslahi ya nchi yamezingatiwa au mhusika kaenda kuiuza nchi,`` alizidi kuhoji.

Mwanzoni mwa mwaka huu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, aliibua mjadala mkubwa nchini baada ya kutoa siri za Karamagi kusaini mkataba nje ya nchi.

Zitto alitoa shutuma hizo katika hoja binafsi aliyowasilisha bungeni ambapo alidai kuwa, Karamagi alitumia madaraka vibaya kwa kusaini mkataba kinyume na agizo la Rais kwamba sheria za madini zipitiwe upya.

Hatua hiyo ya Zitto kutoa hoja hiyo bungeni, ilisababisha mbunge huyo kusimamishwa.

Hata hivyo, watu wa kada mbalimbali, walilaani kitendo cha kumsimamisha mbunge huyo kijana na machachari.

Spika alisema kuna makubaliano na serikali kwa waziri kumpatia Katibu wa Bunge mikataba yote ya maendeleo ambayo hivi sasa imetengewa masijala mahususi kwa ajili ya wabunge.

``Wanaoendeleza dhana ya usiri dhidi ya mwenye mali (mwananchi), wanalo jambo, wasakamwe ili waache mizengwe hiyo,`` alisema. Alisema usiri wa namna hiyo, ndio unasababisha wanahabari kuandika habari za kuhisi au kile wanachokiamini kuwa ni sahihi.

``Nawashauri wenzetu serikali kuweka utaratibu ulio wazi kwa kila wizara kuwa na dawati la taarifa ambapo wanahabari na wananchi wanaweza kupata habari za uhakika kuhusu utekelezaji wa majukumu yaliyo chini ya wizara hizo,`` alisema.

Alisema kumekuwapo na mvutano kati ya serikali na vyombo vya habari, hali iliyoko katika nchi nyingine zilizoendelea.

``Mivutano hii inatokana na haja ya wanahabari kufichua mambo ya hovyo yanayofanywa na serikali, na serikali kutokuwa tayari mambo yake kuanikwa kwa umma,`` alisema.

Alisema vyombo vinasaidia kufichua vitendo vinavyokwamisha maendeleo ya nchi kama vile ufisadi, rushwa katika utawala, matumizi mabaya ya madaraka, huduma mbovu kwa wananchi na ubadhirifu wa mali ya umma.

Alisema katika nchi nyingi masikini ikiwamo Tanzania, zina mifumo na sheria ambayo inakandamiza uhuru wa vyombo vya habari.

Alitoa mfano wa sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ya hapa nchini kwamba imepitwa na wakati.

``Natoa wito kwa serikali ya Tanzania kuharakisha kufikisha bungeni muswada wa sheria mpya ya habari itakayolingana na hali ya sasa,`` alisema.

Alisema katika miaka ya hivi karibuni kumekuwapo na vitendo, kauli na mitazamo ya baadhi ya watu inayoashiria mwelekeo wenye nia ya kuibomoa misingi iliyojengwa na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere kupitia baadhi ya vyombo vya habari.

Spika Sitta alisema vyombo vya habari hivyo vinaandika habari za uchonganishi, uzushi na hisia za chuki na utabaka.

``Hii ni tabia moja mbovu ambayo hutumiwa na waandishi wasio waadilifu kwa lengo la upotoshaji ili kujenga hoja juu ya upotoshaji wanaoufanya,``alisema Sitta.

Alisisitiza juu ya kauli yake aliyowahi kuitoa bungeni kwamba haki za binadamu za mtu mmoja mmoja ambaye kwa vitendo vyake anahujumu watu mamilioni, haziwezi kutazamwa bila kuzingatia haki za hao mamilioni.

Alisema ni wajibu wa nchi yoyote kuzingatia kwa haki za binadamu hazitoi mwanya wa kujenga tabaka la watu maalum ambao utaratibu wa kuwashughulikia unakuwa tofauti na watu wengine, ama walarushwa wakubwa wanaohujumu uchumi wa taifa kujisikia wana uhuru mpana wa kuendeleza maovu yao huku hali ya wengi ikididimia.

``Hali hii isipodhibitiwa mapema itauvunja umoja na utengemano wetu na kutuingiza kwenye migawanyiko, machafuko na hatimaye hata vita vya wenyewe kwa wenyewe,`` alisema Sitta.
SOURCE: Nipashe
 
Last edited by a moderator:
Sarakasi za Sitta zinatatiza kwelikweli. Kwa nini kauli zake za Agosti 2007 wakati wa sakata la Buzwagi zilikuwa tofauti na hizi anazotoa leo!
 
Huyu anajaribu kujificha kwenye kivuli chake,kipindi kile cha sakata la buzwagi alikuwa anamuogopa nani kuyasema haya.Lets wait,time will tell.
 
Huko CCM kila mtu lwake sasa. Wapinzani lale tu wakati huu ndo muda wa kunoa na kutoa makucha......
 
Yalikuwa maamuzi ya Bunge, siyo yeye. Mlitaka Bunge lifanye na kufuata anachokiamua yeye?
 
Sarakasi za Sitta zinatatiza kwelikweli. Kwa nini kauli zake za Agosti 2007 wakati wa sakata la Buzwagi zilikuwa tofauti na hizi anazotoa leo!

Use your brains brother or sister! Akiwa Bungeni, Sitta ni Spika na anaongozwa na Kanuni za Bunge! Akiwa kwenye hafla kama hiyo, Sitta haongozwi na kanuni za Bunge, yuko huru kusema lolote kama Mbunge! Msiwakatishe tamaa viongozi wetu wazuri kwa comments za kitoto na kihuni kama hizo. Nisamehe kwa kukasirika.
 
Huyu anajaribu kujificha kwenye kivuli chake,kipindi kile cha sakata la buzwagi alikuwa anamuogopa nani kuyasema haya.Lets wait,time will tell.

Huelewi? Alikuwa anaongozwa na Kanuni za Bunge! Nje ya Bunge, una uhuru wa kuongea nje ya kanuni! Ingawa mimi si mbunge, naamini Baba watatu umenielewa!
 
Huyu Spika Sitta mara nyingine ananichanganya kwani he does not seem to be consistent!! Mara kadhaa nimeamini kwa dhati kabisa kuwa huyu bwana ni principled na anachukia sana ufisadi la anatetea independence ya Judiciary;lakini matamko yake na apathy yake sometimes hayaendani na imani niliyokuwanayo kwa mfano juu ya independence of the judiciary, haiwezekani legislature ikawa independent of the executive wakati wabunge bado wanakaa kama wakurugenzi kwenye vyombo vya umma wanavyotakiwa kuvisimamia!! Serikali kupitia kwa waziri husika imekili bungeni kuwa kwa wabunge kuwa wajumbe wa mabodi ya mashirika ya umma ni against the principles of good governance.I expected Sitta kama mtu wa speed na viwango kama anavyotaka sisi tuamini angehakikisha kuwa wabunge wangesitishwa ujumbe wao mara moja hapo ndipo angeonyesha umakini.Unfortunately, nadhani elements of populism zinamfanya aogopekufanya kile ambacho kingelipa bunge uhuru wa kweli. Kuhusu ufisadi tukumbuke kuwa ni Sitta huyu huyu ndiye aliyetishia kumpeleka DR. Slaa polisi kwa kumtuhumu kughushi vielelezo vya EPA na hakuruhusu mjadala wa EPA bungeni. Hapa juzi rafiki yake Mramba alipopelekwa Lupango , akaja na mpya kuwa bunge lingekuja to his rescue ili masharti ya bail yake yalegezwe aweze kuhudhura bunge; huyu ni mtuhumiwa kwanini bunge liingilie utendaji wa mahakama??Spika ajue kwamba fisadi ni fisadi whether ni i rafiki zako Mungai na Mramba au mahasimu wako Lowassa na Karamagi, principles dictate that they are all cooked in the same pot and that is quality standard to me.
 
awamu hii tutaona mengi.....andaeni kalamu zenu kuandika!!!!
 
Sarakasi za Sitta zinatatiza kwelikweli. Kwa nini kauli zake za Agosti 2007 wakati wa sakata la Buzwagi zilikuwa tofauti na hizi anazotoa leo!

Angalau huyu amepiga sarakasi! Hata JK akipiga sarakasi tutamshangilia tu and that ís what we want from these people! Kosa ni kurudia kosa! I think he has taken the right position na aendelee kupiga kelele!
 
Hivi ni kwa nini walimsimamisha Zitto kwa kuibua hii issue. Na kama yeye alijua ni kosa, je alikuwa wapi kumsimikia bango huyo jamaa?? Naona dalili za mafarakano na mpasuko wa CCM.
 
Huyu Spika Sitta mara nyingine ananichanganya kwani he does not seem to be consistent!! Mara kadhaa nimeamini kwa dhati kabisa kuwa huyu bwana ni principled na anachukia sana ufisadi la anatetea independence ya Judiciary;lakini matamko yake na apathy yake sometimes hayaendani na imani niliyokuwanayo

- At least ni kiongozi pekee aliyemuambia wazi rais kuwa hotuba yake ya mwisho bungeni hasa kuhusu EPA was a nonesense! Unafikiri kukamatwa kwa kina Mramba hakuna anything to do na mashambulizi yake kwa hotuba ya rais?

- Kabla ya kutoa hizi hukumu tuwe tunaangalia mazingara ya kisiasa ambayo viongozi wetu wanafanyia kazi.
 
Field Marshall mkuu, mbona unachagua vipande unavyotaka na vingine vya umuhimu unaviacha? Contribution yangu imeangalia total picture na utendaji wa Sitta!! mbona hujacomment kuhusu independence ya legislature vis a vis wabunge kuwa wajumbe wa bodi na jinsi alivyomhandle DR. Slaa; mimi pia natoka Urambo but I am not partisan!!
 
Vichwa vya habari vingine vya jf very sensational! mtu hakutajwa hata jina lakini tunaambiwa "amemalizwa" kazi kweli kweli.....
 
Last edited:
Mimi siamini kama maneno ya upinzani dhidi ya mafisadi ninayosikia yanatolewa na Samwel Sitta huyu huyu ninayemfahamu. Labda wali intend kumsema Mrs wake.
Na hasa nikikumbuka kuona alivyokomalia issue ya EPA kuwa ni mambo ya mtandaoni na kutaka kum impeach Dr Slaa kwamba anatoa nyaraka za uongo? Tena alilisema kwenye luninga nikiwa naangalia hivi hivi.
Basi aje tena kwanza atuombe msamaha kwa kutupotosha wa tz. Au anadhani tumesahau?
Leo ni huyu huyu anayejifanya ana machungu na nchi hii dhidi ya mafisadi?!
Ama kweli kuwa uone viroja! Na hasa vya hawa wachumia tumbo kupitia sisiemu.
 
mimi siamini kama maneno ya upinzani dhidi ya mafisadi ninayosikia yanatolewa na samwel sitta huyu huyu ninayemfahamu. Labda wali intend kumsema mrs wake.
Na hasa nikikumbuka kuona alivyokomalia issue ya epa kuwa ni mambo ya mtandaoni na kutaka kum impeach dr slaa kwamba anatoa nyaraka za uongo? Tena alilisema kwenye luninga nikiwa naangalia hivi hivi.
Basi aje tena kwanza atuombe msamaha kwa kutupotosha wa tz. Au anadhani tumesahau?
Leo ni huyu huyu anayejifanya ana machungu na nchi hii dhidi ya mafisadi?!
Ama kweli kuwa uone viroja! Na hasa vya hawa wachumia tumbo kupitia sisiemu.


>>>>>>>>.............2010!!!
 
Ninamuamini Spika, maana bila yeye hivi vita vya mafisadi vingekua ndoto. Kila binadamu ana mapungufu yake!

Simuami na nasema simuamini spika Sitta kwa sababu anachofanya ni kusoma chuki zetu na kugundua kwamba vita tumeishinda na yeye anaelekea huko huko kama mmoja wa wapiganaji walioshinda, lakini katika vita hayumo kabisaaaaaa wala hajapigana na sidhani kama ana mpango wa kupigana.
Hasa nikikumbuka vita yake na Dr Slaa. Alitafuta kila namna bunge lisijadili ufisadi huu na akafanikiwa.
Maana Dr Slaa asingerudisha vita hii kwa wananchi, leo Jitu Pateli lingekuwa Kisutu?????
 
Back
Top Bottom