UramboTabora
Member
- Sep 11, 2008
- 49
- 2
na Prisca Nsemwa
Source: Tanzania Daima
MAASKOFU na wachungaji wa makanisa ya Pentekoste hapa nchini, wameandaa tuzo ya uongozi bora kwa ajili ya kumtunuku Spika wa Bunge, Samuel Sitta kwa kuuongoza vema mhimili huo tofauti na wakati mwingine wowote.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mchungaji William Mwamalanga, alisema wanatarajia kumpa Spika tuzo hiyo baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wake, hasa kwa namna anavyoliongoza Bunge.
Alisema, Spika Sitta amejitahidi kuliweka Bunge karibu na wananchi tofauti na miaka mingine ambapo chombo hicho kiliendeshwa kama kiini macho kwa wananchi, kwa vile mambo mengi yalifichwa.
Spika Sitta tuna kila sababu ya kumpa tuzo kwa kuwa ameweza kuliongoza Bunge ipasavyo, tofauti na miaka mingine yoyote, ndiyo maana baadhi ya viongozi mafisadi wanamchukia Sitta ni Spika bora, alisema Mwamalanga.
Mbali na hilo, maaskofu na wachungaji hao wamelaani kitendo cha Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kumlazimisha Spika huyo kujiuzulu na kutishia kumpora kadi ya uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwataka wajumbe wa NEC kumuomba radhi Sitta.
Mwamalanga, alisema kitendo walichofanya ni kuifahamisha jamii kuwa wanaendelea kuwakumbatia mafisadi kwa kuwa sababu zao za kumlazimisha ajiuzulu hazina msingi.
NEC ni kipofu na inataka kutuingiza shimoni, lakini kwa kuwa tuna macho, tutaendelea kusema, na chama hakiwezi kutupeleka mahala pabaya kwa sababu zao ambazo hazina msingi, alisema Mwamalanga.
Alisema, chama hicho kinamdhalilisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa baadhi ya wanachama wake wanakumbatia ufisadi. Chama legelege kinazaa vitu legelege, hatuwezi kunyamaza endapo anatokea mmoja wa kukiweka chama mahala pa kuridhisha na wengine wakamkataa na kumtaka ajiuzulu, NEC imetushangaza.
Rais awe mkali kwa viongozi wasio waadilifu, na ikiwezekana awapunguzie mishahara wasiofanya kazi ipasavyo kwakuwa viongozi wanaofanya kazi wanahesabika, mfano Spika Sitta na Magufuli, alisema. Naye Askofu Thomas Faida, alisema kuwa ujasiri wa Kikwete umepotea kwa kulea watu wachache ambao wapo kwa ajili ya manufaa yao, hivyo ni wakati wake wa kurudi kwa wananchi kulijenga taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mchungaji William Mwamalanga, alisema wanatarajia kumpa Spika tuzo hiyo baada ya kuridhishwa na utendaji kazi wake, hasa kwa namna anavyoliongoza Bunge.
Alisema, Spika Sitta amejitahidi kuliweka Bunge karibu na wananchi tofauti na miaka mingine ambapo chombo hicho kiliendeshwa kama kiini macho kwa wananchi, kwa vile mambo mengi yalifichwa.
Spika Sitta tuna kila sababu ya kumpa tuzo kwa kuwa ameweza kuliongoza Bunge ipasavyo, tofauti na miaka mingine yoyote, ndiyo maana baadhi ya viongozi mafisadi wanamchukia Sitta ni Spika bora, alisema Mwamalanga.
Mbali na hilo, maaskofu na wachungaji hao wamelaani kitendo cha Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kumlazimisha Spika huyo kujiuzulu na kutishia kumpora kadi ya uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwataka wajumbe wa NEC kumuomba radhi Sitta.
Mwamalanga, alisema kitendo walichofanya ni kuifahamisha jamii kuwa wanaendelea kuwakumbatia mafisadi kwa kuwa sababu zao za kumlazimisha ajiuzulu hazina msingi.
NEC ni kipofu na inataka kutuingiza shimoni, lakini kwa kuwa tuna macho, tutaendelea kusema, na chama hakiwezi kutupeleka mahala pabaya kwa sababu zao ambazo hazina msingi, alisema Mwamalanga.
Alisema, chama hicho kinamdhalilisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa baadhi ya wanachama wake wanakumbatia ufisadi. Chama legelege kinazaa vitu legelege, hatuwezi kunyamaza endapo anatokea mmoja wa kukiweka chama mahala pa kuridhisha na wengine wakamkataa na kumtaka ajiuzulu, NEC imetushangaza.
Rais awe mkali kwa viongozi wasio waadilifu, na ikiwezekana awapunguzie mishahara wasiofanya kazi ipasavyo kwakuwa viongozi wanaofanya kazi wanahesabika, mfano Spika Sitta na Magufuli, alisema. Naye Askofu Thomas Faida, alisema kuwa ujasiri wa Kikwete umepotea kwa kulea watu wachache ambao wapo kwa ajili ya manufaa yao, hivyo ni wakati wake wa kurudi kwa wananchi kulijenga taifa.
Source: Tanzania Daima