Spika Sitta: Kelele za Kingunge hazininyimi usingizi

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
Speaker%20Sitta.jpg



Na Sadick Mtulya

SPIKA wa Bunge Samuel Sitta amesema hoja za vigogo wa CCM akiwamo Kingunge Ngombale Mwiru kutaka ajiuzulu ni kelele ambazo haziwezi kumnyima usingizi.

Alisema wana-CCM hao ni wale waliopo kwenye kundi ambalo halipendezwi na msimamo wake bungeni kutokana na kuziba mianya yao ya kujipatia riziki kinyume na taratibu.

Spika Sitta aliliambia Mwananchi Jumapili jana kuwa kuondoka kwake madarakani kutatokana tu na mwongozo wa Katiba na sio hila wala fitina za watu.

Spika Sitta alisema hayo siku moja baada ya baadhi ya vigogo wa CCM kudai mbele ya kamati ya Rais Ali Hassan Mwinyi mjini Dodoma wiki hii kuwa mgawanyiko na uhasama uliojengeka miongoni mwa wabunge wa chama hicho tawala, umechochewa na Spika Sitta.

Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana katika mahojiano maalumu, Spika Sitta alifafanua kuwa kelele zinazopigwa sasa dhidi yake zinahusu maslahi binafsi ya kundi la watu wachache, akiwemo Kingunge na sio maslahi ya taifa.

“Yote mnayosikia na yatakayoendelea kuzungumzwa, ukiyafuatilia kwa makini utakuta ni kundi la watu wachache akiwemo huyo Kingunge; wanaohisi kuwa mwenendo wa Bunge ulivyo hivi sasa unaziba maslahi yao binafsi,” alisema Sitta.

Spika Sitta alisema pamoja na kelele hizo yeye bado ni Spika mahiri na kamwe hawezi kuyumbishwa na misimamo ya watu hao wachache wasiolitakia taifa mema.

Alisema kwa kuwa vigogo hao wana uhuru wa kidemokrasia wa kutoa hisia zao, hashangazwi na maneno yao ila akayafananisha na kelele.

"Maneno yao yote ni sawa na kelele, hivyo waendelee kupiga kelele tu. Mimi ni Spika ninayependwa na kukubalika na wabunge pamoja na wananchi, hivyo sitishiki na nipo imara kupambana hadi hatua ya mwisho," alisema Sitta.

Spika ambaye mara baada ya kuchaguliwa kukalia kiti hicho na kutangaza kuwa Bunge lake litaongozwa kwa viwango na kasi, alisema hatishiki na lolote kwa kuwa Bunge linakwenda vizuri na kwa viwango vinavyokubalika.

"Kutokana na hilo ndiyo maana Bunge hivi sasa linapendwa na wananchi na hata nchi wahisani wanalithamini," alifahamisha na kuongeza;

“Uimara wangu katika nafasi yangu ya uspika ndio unaolifanya Bunge lipendwe na wananchi hata nchi wahisani".

Jana baadhi ya vigogo wa CCM akiwamo Kingunge Ngombale Mwiru walikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari wakisema kuwa matatizo yanayoikabili CCM ni matokeo ya uongozi mbaya wa Sitta.

Sitta hivi karibuni alinusurika kunyang'anywa uanachama wa CCM katika kikao kilichopita cha NEC baada ya wanachama wanaodaiwa kuwa wafuasi wa watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kumtuhumu kuwa amekuwa akiendesha Bunge kibabe na upendeleo. Pia walidai kuwa staili ya Sitta kuingilia mijadala ndani ya Bunge na kushikamana na kundi moja la wabunge na kuingilia madaraka ya mihimili mingine ya dola, ni uvunjaji mkubwa wa misingi ya mgawanyo wa madaraka na kwamba imechangia kuleta mgawanyiko mkubwa miongoni mwao.
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.

Pasco
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.
Ndugu yuo got it very wrong, Speaker hawezi kupingana na mahakama?
hilo lazima ulielewe tena saana, hukumu yoyote inayotolewa na mahakama ni halali mpaka itakapotenguliwa na mahakama au mamlaka ya juu zaidi wenye mandate ya kufanya hivyo. mfano hili la Zombe hata Raisi kaliongelea lakini haimanishi anapingana na mahakama bali ni mtu kuona au kuzania haki haijatendeka.

Sasa ukija mazungumzo yaani vitu vilivyo nje ya ukumbi wa bunge au mahakama havina authority yoyote. Mfano Dr Sengondo Mvungi anapoongelea kitu, mimi au wewe au hata Jaji mkuu ikiwa ni nje ya eneo la mahakama litabaki ni neno au ushauri nk ambao yoyote yule anaweza kukubaliana nao au kutokubaliana nao. na ndio maana hata leo hii Raisi anaweza sema kitu, lakini wengine wakakipinga. Au AG anaweza kuwa na muono tofauti wa jambo la kisheria na mwanasheria mwingine hata awe Jaji Mkuu, lakini wakiingia mahakamani final say ni ya Judge.

Inabidi utofautishe mambo yanayo ongeleawa na watu kwenye semina, barabarani, warsha, kongamano, kwenye forums, blog nk na kile kinachoongelewa kwenye sehemu mahususi.

Mfano watu wanaona kwenye kesi ya Zombe haki haikutendeke, hizo zitaitwa kelele mpaka pale mahakama ya Juu au mamlaka zingine zitakapo liongelea suala hilo ndani ya mipaka yao.

Hili la serikali na Bunge bado serikali haijapeleka utekelezaji wake, hivyo huwezi kupinga kitu ambacho hakipo, ndio maana hata unapotaka kukata rufaa ni lazima uwe na uamuzi wa mahakama sau mwenendo wa kesi .

Na zaidi ya hapo si suala la Sitta kupinga au kukubali, bali hiyo report inatakiwa iwasilishwe na serikali kwa kamati husika na kusomwa bunge ili wabunge waridhie au la.
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Sijui ni nani anaendeleza hizi dhana ambazo hazielewi maana ya uhuru wa mihimili ya dola. Westminister system haufanani mahali pote duniani na unatofautiana kwa nchi na nchi. Na Tanzania hatujacopy mfumo ulivyo hasa bali tumeutengeneza kutufiti sisi.

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Spika hajawahi kuingilia uhuru wa mahakama kama ilivyo.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola.

In reality, Bunge linawakilisha nguvu kubwa zaidi ya Mahakama na Serikali. Ndicho chombo pekee kilichopewa madaraka ya kushauri na kusimamia serikali. Rais au Mahakama hawawezi kusimamia Bunge. Anachofanya Spika Sitta kimsingi ni kulipa Bunge nguvu yake hasa kwenye mfumo wa Westminister.


Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Kubishana na kupingana kwa nguvu ya hoja kati ya vyombo mbalimbali vya serikali ni jambo zuri na la msingi. Siyo makosa. Ni makosa pale ambapo Katiba inavunjwa.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Serikali ilitakiwa kutekeleza yale maazimio siyo "kuona hakuna hatia". Kwa serikali kuanzisha uchunguzi wake nje ya ule wa Bunge na kutoa adhabu au kuchukua hatua nje ya zile zilizopendekezwa na Bunge ni kutolitii Bunge. Serikali kama haikukubaliana na mapendekezo ya Bunge walitakiwa kuja na hoja Bungeni kuelezea ni kwa nini? Na walitakia hata kulazimisha kura kupigwa tena, kwani kisheria ni Bunge tu linaloweza kufuta maamuzi yake yenyewe!

Aliyelikoroga hili ni Pinda na JK kwani yalipotolewa maamuzi ya Bunge the next week yalitakiwa kutelezwa au waamue wote kujiuzulu! It is as simple as that. We can not try to have a democratic government without paying the price for it.
Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

It is not that simple. Bunge halina jukumu la kutunga sheria tu; lina jukumu la kuishauri serikali na kuisimamia na wakati wowote serikali inaenda kombo Bunge (ambalo ndilo wawakilishi wa Watanzania) wanawajibu wa kuirudisha kwenye njia. Na siyo tu hivi hivi bali hata ikibidi kuilazimisha serikali to resign au kumvua madaraka rais!

Rais hawezi kumvua madaraka Spika au kuwavua madaraka wabunge!

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza.

Si kweli; Bunge ndilo mtunga sheria. Ni lini Sitta amejaribu kutunga sheria? Kwenye hukumu hajahukumu yoyote anasimamia Bunge kuheshimiwa na siyo kutishiwa au kufanya kazi kwa huruma ya serikali.

Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia

Serikali ilipata wapi huo uamuzi wa kuona hakuna "hatia". Ina maana serikali inapingana na Bunge na tukikubali serikali ikiagizwa na Bunge kufanya kitu inaenda nje na tunachekelea basi tunakaribisha vurugu. Bunge likitenga fedha x kwenda kwenye mradi m na serikali ikaona ni vyema hizo x zienda kwenye mradi p Bunge halitakiwa kuuliza? Serikali ni lazima liiitii Bunge, period. Hawataki wavunje serikali yao twende kwenye uchaguzi mwingine. Ndio maana nchi nyingine kama Canada, Israel, Uingereza, ambazo pia zinafuata westminister system wanabadilisha serikali at any moment inaposhindikana na Mabunge yakaona umuhimu wa hivyo.

.
Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

That might be true; lakini bado kasimamia Bunge na uhuru wake. Ndio maana Hosea alilazimika kusitisha uchunguzi wake kwa sababu usingewezekana kisheria wakati Bunge linaendelea kama watu wachache walivyokuwa wanaamini.


Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.

I hope not kwani naweza kujikuta nimepull out all my hair.
 
Ndugu yuo got it very wrong, Speaker hawezi kupingana na mahakama?
hilo lazima ulielewe tena saana, hukumu yoyote inayotolewa na mahakama ni halali mpaka itakapotenguliwa na mahakama au mamlaka ya juu zaidi wenye mandate ya kufanya hivyo. mfano hili la Zombe hata Raisi kaliongelea lakini haimanishi anapingana na mahakama bali ni mtu kuona au kuzania haki haijatendeka.

well said.

Sasa ukija mazungumzo yaani vitu vilivyo nje ya ukumbi wa bunge au mahakama havina authority yoyote. Mfano Dr Sengondo Mvungi anapoongelea kitu, mimi au wewe au hata Jaji mkuu ikiwa ni nje ya eneo la mahakama litabaki ni neno au ushauri nk ambao yoyote yule anaweza kukubaliana nao au kutokubaliana nao. na ndio maana hata leo hii Raisi anaweza sema kitu, lakini wengine wakakipinga. Au AG anaweza kuwa na muono tofauti wa jambo la kisheria na mwanasheria mwingine hata awe Jaji Mkuu, lakini wakiingia mahakamani final say ni ya Judge.

exactly.. ndio maana wabunge hawaruhusiwi kuzungumzia mambo yaliyoko mahakamani wakiwa Bungeni; kwani hapo ndio kuingilia lakinii akiwa kilabuni na mshirika wake wanaweza kuyatolea maoni.
Inabidi utofautishe mambo yanayo ongeleawa na watu kwenye semina, barabarani, warsha, kongamano, kwenye forums, blog nk na kile kinachoongelewa kwenye sehemu mahususi.

very good.

Mfano watu wanaona kwenye kesi ya Zombe haki haikutendeke, hizo zitaitwa kelele mpaka pale mahakama ya Juu au mamlaka zingine zitakapo liongelea suala hilo ndani ya mipaka yao.

absolutely true.

Hili la serikali na Bunge bado serikali haijapeleka utekelezaji wake, hivyo huwezi kupinga kitu ambacho hakipo, ndio maana hata unapotaka kukata rufaa ni lazima uwe na uamuzi wa mahakama sau mwenendo wa kesi .
na zaidi ya hapo si suala la Sitta kupinga au kukubali, bali hiyo report inatakiwa iwasilishwe na serikali kwa kamati husika na kusomwa bunge ili wabunge waridhie au la.

exactly.. kwa sababu kinachosubiriwa Bungeni ni ripoti ya utekelezaji siyo taarifa ya uchunguzi mwingine wa kuona "kuna hatia au la" kama alivyofanya Pinda mara ya kwanza. Kama hawataki kutekeleza au hawakubaliani na maamuzi ya Bunge serikali inatakiwa kujiuzulu ili serikali itakayokuwa tayari kuteleza maamuzi ya Bunge iingie madarakani.
 
Man haka kazee kanadhani kuwa kataendelea kutufanya wajinga. Naona sasa kanaoneshwa wazi kuwa maslahi ya Taifa ni mbele ya kila kitu.

Kazee kanafiki sana, i thought ndio katakuwa Nyerere baada ya Nyerere original kutotoka, lakini ajabu sana kameonesha true colours. Porojo tu na kutete ujinga nadni ya CCM.
 
Jana baadhi ya vigogo wa CCM akiwamo Kingunge Ngombale Mwiru walikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari wakisema kuwa matatizo yanayoikabili CCM ni matokeo ya uongozi mbaya wa Sitta.

Sitta hivi karibuni alinusurika kunyang'anywa uanachama wa CCM katika kikao kilichopita cha NEC baada ya wanachama wanaodaiwa kuwa wafuasi wa watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi kumtuhumu kuwa amekuwa akiendesha Bunge kibabe na upendeleo. Pia walidai kuwa staili ya Sitta kuingilia mijadala ndani ya Bunge na kushikamana na kundi moja la wabunge na kuingilia madaraka ya mihimili mingine ya dola, ni uvunjaji mkubwa wa misingi ya mgawanyo wa madaraka na kwamba imechangia kuleta mgawanyiko mkubwa miongoni mwao.

Tatizo ni Sitta au ufisadi? Tatizo ni Sitta au mafisadi?
Pamoja na kuwa JK tumekuwa tunamuona kama ni kiongozi asiye na busara, lakini he proved us wrong alipokataa kumyang'anya kadi Sitta. Hiyo ni moja ya busara alizoonesha JK katika uongozi wake. Wanaoona tofauti ni mafisadi tu,
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.
.
Tunakushuru sana pasco kwa uchambuzi wako,ambao hauna ushabiki ndani yake.well done my man.
 
Sijui ni nani anaendeleza hizi dhana ambazo hazielewi maana ya uhuru wa mihimili ya dola. Westminister system haufanani mahali pote duniani na unatofautiana kwa nchi na nchi. Na Tanzania hatujacopy mfumo ulivyo hasa bali tumeutengeneza kutufiti sisi.



Spika hajawahi kuingilia uhuru wa mahakama kama ilivyo.



In reality, Bunge linawakilisha nguvu kubwa zaidi ya Mahakama na Serikali. Ndicho chombo pekee kilichopewa madaraka ya kushauri na kusimamia serikali. Rais au Mahakama hawawezi kusimamia Bunge. Anachofanya Spika Sitta kimsingi ni kulipa Bunge nguvu yake hasa kwenye mfumo wa Westminister.




Kubishana na kupingana kwa nguvu ya hoja kati ya vyombo mbalimbali vya serikali ni jambo zuri na la msingi. Siyo makosa. Ni makosa pale ambapo Katiba inavunjwa.



Serikali ilitakiwa kutekeleza yale maazimio siyo "kuona hakuna hatia". Kwa serikali kuanzisha uchunguzi wake nje ya ule wa Bunge na kutoa adhabu au kuchukua hatua nje ya zile zilizopendekezwa na Bunge ni kutolitii Bunge. Serikali kama haikukubaliana na mapendekezo ya Bunge walitakiwa kuja na hoja Bungeni kuelezea ni kwa nini? Na walitakia hata kulazimisha kura kupigwa tena, kwani kisheria ni Bunge tu linaloweza kufuta maamuzi yake yenyewe!

Aliyelikoroga hili ni Pinda na JK kwani yalipotolewa maamuzi ya Bunge the next week yalitakiwa kutelezwa au waamue wote kujiuzulu! It is as simple as that. We can not try to have a democratic government without paying the price for it.


It is not that simple. Bunge halina jukumu la kutunga sheria tu; lina jukumu la kuishauri serikali na kuisimamia na wakati wowote serikali inaenda kombo Bunge (ambalo ndilo wawakilishi wa Watanzania) wanawajibu wa kuirudisha kwenye njia. Na siyo tu hivi hivi bali hata ikibidi kuilazimisha serikali to resign au kumvua madaraka rais!

Rais hawezi kumvua madaraka Spika au kuwavua madaraka wabunge!



Si kweli; Bunge ndilo mtunga sheria. Ni lini Sitta amejaribu kutunga sheria? Kwenye hukumu hajahukumu yoyote anasimamia Bunge kuheshimiwa na siyo kutishiwa au kufanya kazi kwa huruma ya serikali.



Serikali ilipata wapi huo uamuzi wa kuona hakuna "hatia". Ina maana serikali inapingana na Bunge na tukikubali serikali ikiagizwa na Bunge kufanya kitu inaenda nje na tunachekelea basi tunakaribisha vurugu. Bunge likitenga fedha x kwenda kwenye mradi m na serikali ikaona ni vyema hizo x zienda kwenye mradi p Bunge halitakiwa kuuliza? Serikali ni lazima liiitii Bunge, period. Hawataki wavunje serikali yao twende kwenye uchaguzi mwingine. Ndio maana nchi nyingine kama Canada, Israel, Uingereza, ambazo pia zinafuata westminister system wanabadilisha serikali at any moment inaposhindikana na Mabunge yakaona umuhimu wa hivyo.

.

That might be true; lakini bado kasimamia Bunge na uhuru wake. Ndio maana Hosea alilazimika kusitisha uchunguzi wake kwa sababu usingewezekana kisheria wakati Bunge linaendelea kama watu wachache walivyokuwa wanaamini.




I hope not kwani naweza kujikuta nimepull out all my hair.
.

mwanakijiji sasa unazeeka vibaya.
 
Jamani hasira za kingunge ni pamoja na kunjang'anywa hiyo stend ya ubungo. hivi kwa nini wananchi wasiandamane kupinga uongozi wa Rais kikwete kama wafanyavyo nchi nyingine?
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.

"Mmeanza kuguswa,mtakoma mwaka huu mafisadi wote Sita Oyeeeeeeeeeee"
 
Tatizo ni Sitta au ufisadi? Tatizo ni Sitta au mafisadi?
Pamoja na kuwa JK tumekuwa tunamuona kama ni kiongozi asiye na busara, lakini he proved us wrong alipokataa kumyang'anya kadi Sitta. Hiyo ni moja ya busara alizoonesha JK katika uongozi wake. Wanaoona tofauti ni mafisadi tu,
Haikuw abusara kwa JK kwa kukataa kumnyang'anya card 6,alikuwa anjua what would happen by doing so,basically alilinda maslah ya urais wake,if he could do so,may be that would be the end of CCM,CCM could fall apart if he did that,thats why he didint do so
 
shida ya yote haya ni kukosa strong institutions in Tanzania, hii hupelekea kuwa na wabunge wasio na ubunge, mbaya zaidi tunaona hata raisi anakosa uraisi.

Poor TZ.
 
Kwa kusaidia mjadala ili uwe na afya zaidi, jee Kingunge alisema nini?

Alisema, Bunge la Tanzania linafuata mfumo wa Wenstminister wa Bunge la Uingereza unaoheshimu sana mipaka ya separation of powers baina ya mihimili mitatu ya dola, Bunge (The Legistlature), Serikali (The Executive) na Mahakama (The Judiciary).

Kingunge akamshambulia Spika Sitta kwa kuika mfumo huo na kuingilia uhuru wa Mahakama na Serikali huku akikikumbatia kikundi kinachoisulubu serikali huku yeye mwenywe akiingilia uhuru wa mahakama.

Swali ni jee tuhuma za Kingunge zina ukweli, au nao ni utetezi wa mafisadi.
Kwa maoni yangu ni kweli na mifano ipo. Spika Sitta amekuwa anapractice perliamentary supremacy over and above mihimili hii mingine miwili ya Dola. Amewahi kubishana na Jaji Mkuu wazi wazi kupinga uamuzi halali wa mahakama which is wrong.

Na katika maazimio 23 ya bunge kuhusu kamati ya Mwakiembe, anataka kuilazimisha serikali iyatekeleze kama yalivyo hata kama serikali inaona hakuna hatia, ndio maana Hosea bado yuko madarakani.

Lengo la separation of powers ni checks and balance kati ya mihimili hii kuzuia mmoja usiende kwenye extreme, Bunge litunge sheria, mahakama izitafsiri sheria hizo na serikali isaidie utekelezaji.

Sita amekuwa mtunga sheria, anataka kuhukumu kama kwenye Richmond, na kuilazimisha serikali kutekeleza. Kamati ya Bunge imeona kuna hatia Richmond, serikali meona hakuna hatia. Kikao hiki cha Bunge kilipanga kuisulubu tena serikali. Baada ya Sitta kusulubiwa kwenye kamati ya Mwinyi, sasa kaufyata ni heshina na adabu, mpaka kaliahirisha Bunge huku kuna ishu kibao muhimu kwa taifa.

Ili kuilinda heshima yake, Sitta lazima ataita press conference next week kutueleza kwa nini, na mkiona kimya, mjue Sitta kwisha habari yake, King Maker na timu yake in full control.

Huyu Pasco naye kwa kwenda chakani!... Unafanya makusudi kupotosha mambo au ndio matunda ya kufikia hoteli moja na Rostam Dodoma hayo?

Thank you Mwanakiji kwa kufafanua ukweli bayana, wenye macho wataona. Waganga njaa kina Pasco hawatakuja kuisha kwenye vi nchi masikini kama hivi, mpaka mwisho wa dunia.

Kina Kingunge na Pasco wanataka kutumia Ignorance ya watu on parliamentary systems wanatumia Half-Truths kutaka kulinda maslahi yao ya matumbo njaa!
 
Kwa wale msiomjua Kingunge, huyu babu ni manafiki saaaaana. Kuna wakati alikuwa anampotosha Mkapa, ndipo Nsa Kaisi akambwatukia mbele ya Mkapa na kumwambia " Mh Rais; huyu Mzee ni mnafiki na mwongo anakupotosha". Aliyasema haya wakiwa wote watatu, babu akanywea, natamani Mjeshi huyo (Nsa) arudishwe Ikulu akaokoe mambo
 
Sijui ni nani anaendeleza hizi dhana ambazo hazielewi maana ya uhuru wa mihimili ya dola. Westminister system haufanani mahali pote duniani na unatofautiana kwa nchi na nchi. Na Tanzania hatujacopy mfumo ulivyo hasa bali tumeutengeneza kutufiti sisi.



Spika hajawahi kuingilia uhuru wa mahakama kama ilivyo.



In reality, Bunge linawakilisha nguvu kubwa zaidi ya Mahakama na Serikali. Ndicho chombo pekee kilichopewa madaraka ya kushauri na kusimamia serikali. Rais au Mahakama hawawezi kusimamia Bunge. Anachofanya Spika Sitta kimsingi ni kulipa Bunge nguvu yake hasa kwenye mfumo wa Westminister.




Kubishana na kupingana kwa nguvu ya hoja kati ya vyombo mbalimbali vya serikali ni jambo zuri na la msingi. Siyo makosa. Ni makosa pale ambapo Katiba inavunjwa.



Serikali ilitakiwa kutekeleza yale maazimio siyo "kuona hakuna hatia". Kwa serikali kuanzisha uchunguzi wake nje ya ule wa Bunge na kutoa adhabu au kuchukua hatua nje ya zile zilizopendekezwa na Bunge ni kutolitii Bunge. Serikali kama haikukubaliana na mapendekezo ya Bunge walitakiwa kuja na hoja Bungeni kuelezea ni kwa nini? Na walitakia hata kulazimisha kura kupigwa tena, kwani kisheria ni Bunge tu linaloweza kufuta maamuzi yake yenyewe!

Aliyelikoroga hili ni Pinda na JK kwani yalipotolewa maamuzi ya Bunge the next week yalitakiwa kutelezwa au waamue wote kujiuzulu! It is as simple as that. We can not try to have a democratic government without paying the price for it.


It is not that simple. Bunge halina jukumu la kutunga sheria tu; lina jukumu la kuishauri serikali na kuisimamia na wakati wowote serikali inaenda kombo Bunge (ambalo ndilo wawakilishi wa Watanzania) wanawajibu wa kuirudisha kwenye njia. Na siyo tu hivi hivi bali hata ikibidi kuilazimisha serikali to resign au kumvua madaraka rais!

Rais hawezi kumvua madaraka Spika au kuwavua madaraka wabunge!



Si kweli; Bunge ndilo mtunga sheria. Ni lini Sitta amejaribu kutunga sheria? Kwenye hukumu hajahukumu yoyote anasimamia Bunge kuheshimiwa na siyo kutishiwa au kufanya kazi kwa huruma ya serikali.



Serikali ilipata wapi huo uamuzi wa kuona hakuna "hatia". Ina maana serikali inapingana na Bunge na tukikubali serikali ikiagizwa na Bunge kufanya kitu inaenda nje na tunachekelea basi tunakaribisha vurugu. Bunge likitenga fedha x kwenda kwenye mradi m na serikali ikaona ni vyema hizo x zienda kwenye mradi p Bunge halitakiwa kuuliza? Serikali ni lazima liiitii Bunge, period. Hawataki wavunje serikali yao twende kwenye uchaguzi mwingine. Ndio maana nchi nyingine kama Canada, Israel, Uingereza, ambazo pia zinafuata westminister system wanabadilisha serikali at any moment inaposhindikana na Mabunge yakaona umuhimu wa hivyo.

.

That might be true; lakini bado kasimamia Bunge na uhuru wake. Ndio maana Hosea alilazimika kusitisha uchunguzi wake kwa sababu usingewezekana kisheria wakati Bunge linaendelea kama watu wachache walivyokuwa wanaamini.




I hope not kwani naweza kujikuta nimepull out all my hair.


Mzee Kingunge amechukizwa na kitendo cha kunyang'anywa Ubungo Terminal!! Inaelekea huyu mzee hauelewi huo mfumo wa Westminister;sisi hapa tuna katiba ambayo ndiyo sheria yetu mama, Je Kingunge anaufahamu kuwa waingereza hawana KATIBA as such? Mzee akapunzike asiwe na wasiwasi atazikwa na bendera ya kijani!!
 
Hawa wazee wameongea mambo yao huko ndani ya vikao vyao, kwa nini wanajibizana kwenye magazeti? Hekima imewaishia kabisa?
 
Back
Top Bottom