Spika Sitta ameonyesha mfano, wengine wamuige

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Je, wale vibosile wenye hisa katika makampuni mbali mbali ya nje ikiwemo Barrick nao watatakiwa kutaja hisa ngapi walizonazo katika mahirika hayo!?

Spika Sitta ameonyesha mfano, wengine wamuige
David Azaria
HabariLeo; Monday,December 24, 2007 @00:02

SIKU kadhaa zilizopita Spika wa Bunge, Samuel Sitta, aliwatahadharisha wabunge kuwa mwaka huu atakuwa mkali na kuwachukulia hatua za kisheria wote watakaochelewesha kujaza na kurejesha fomu za kutaja mali na madeni yao ifikapo Desemba 31. Wakati Sitta akitoa tamko hilo bungeni, aliwataka wabunge wote kwenda kuchukua fomu hizo na kuzijaza haraka na kisha kuzirejesha kama inavyotakiwa.

Agizo la Sitta kwa wabunge wenzake limekuja siku chache tu baada ya kutangazwa kwa mabadiliko kwa Tume ya maadili ya viongozi na watumishi wa umma ambako sasa mali zote zitakazojazwa na viongozi wa serikali na wanasiasa zitahakikiwa na kuchunguzwa tofauti na zamani ambako walikuwa wakiziorodhesha tu.

Kwa hili Sitta anapaswa kupongezwa, lakini kikubwa hapa kinachotakiwa ni utekelezaji kwa sababu kuna maagizo mengi katika nchi hii ambayo yamekuwa yakitolewa na viongozi mbalimbali tena wa ngazi za juu serikalini, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida baada ya maagizo hayo kutolewa hakuna ufuatiliaji wala uhakiki kama kweli agizo limetekelezwa.

Watanzania watafurahi kama itakapofika Desemba 31, yaani Jumatatu ijayo, wabunge wote watakuwa wametekeleza agizo hilo vinginevyo wawajibike kwa kufuata kifungu cha 15(a) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kinachosema kwamba kuwa kiongozi wa umma atahesabika kuwa amekiuka maadili kwa kushindwa bila sababu za msingi kutoa tamko linalotakiwa au kutoa tamko la uongo katika kipengele chochote muhimu.

Tukumbuke kwamba kwa mujibu wa Katiba, Mbunge ambaye ni kiongozi wa umma anayewajibika na Sheria ya Maadili ya viongozi wa umma atakoma kuwa Mbunge ikiwa itathibitishwa kwamba amevunja masharti ya maadili ya viongozi wa umma. Sasa hapa ndipo Watanzania wanaposubiri kuona msimamo wa Sitta kama alivyosema Bungeni hivi karibuni.

Lakini suala hili isiwe tu kwa wabunge. Tunao watumishi wengi wa umma katika maeneo mbalimbali nchini ambao nao wanatakiwa kujaza fomu hizo na kutaja mali zao. Kwa hiyo kwa kuwa Spika Sitta ameanza kuonyesha njia kwa kuwabana wabunge wake ni vyema na viongozi wengine katika maeneo ya wakafuatilia katika kuhakikisha kwamba wanawabana wakuu wao wa idara katika kutaja fomu hizo.

Ni vyema Waziri Mkuu akawabana wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi watendaji wa manispaa, halmashauri za miji na wilaya katika kuhakikisha kwamba wanajaza fomu hizo ili ziweze kuchunguzwa na Tume ya maadili ya viongozi na watumishi wa umma. Na kwa kuwa mabadiliko sasa yamefanyika na kuwaruhusu hata wananchi kuhakiki mali zilizotajwa na viongozi katika fomu hizo, basi nao waweze kwenda kuhakiki na kuwafichua wale ambao wana tabia ya kuficha mali zao.

Serikali pekee haiwezi kuwajua mafisadi, wala Tasisisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) hawana uwezo huo, Polisi na hata asasi yoyote ambayo ingeundwa katika nchi hii ama hata kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kulichunguza hili haliwezi kupata mafanikio pasipo kuwashirikisha wananchi ambao ndiyo wanaoishi na viongozi hawa.

Kwa hiyo kufunguliwa kwa milango ya kuingia katika ofisi za Tume ya Maadili ya viongozi na watumishi wa umma kwa mtu yeyote yule kwa nia njema ya kuhakiki mali za kiongozi wake kama ameorodhesha ukweli ama amedanganya, ni moja ya ushirikishwaji wa wananchi katika Serikali yao na hii ni moja ya utekelezaji wa sera ya utawala bora. Hata hivyo, hayo yote hayatafanikiwa kama walio katika mamlaka hawatamuiga Spika Sitta katika kuwasisitizia walio chini yao kuhakikisha wanataja mali zao kabla ya Jumatatu ijayo.

Copyright @TSN 2006 All Rights Reserved
 
Sasa mbona hawajataja mali zake? Whats the point ya ku-declare halafu zisiwekwe public? This whole article is pointless na reeks of ushabiki.
 
Huo ni utumbo mtupu. Tanzania hatuna system ya kufuatilia mapato ya watu. Hivyo wanasiasa wengi wanamiliki mali zilizopo kwenye majina feki au zenye majina ya watoto wao au ndugu zao. Kuna watoto wana miaka miwili na tayari wanamiliki mamilioni hapo bongo.
 
Wanasifiana kwa kazi ambayo haijafanyika? Hii ni gimmick, hakuna jipya hapa. Kama Sitta ana nguvu basi atuambie Lowassa ana utajiri kiasi gani na kalipa kodi kiasi gani kwa mwaka 2007.
 
Wanasifiana kwa kazi ambayo haijafanyika? Hii ni gimmick, hakuna jipya hapa. Kama Sitta ana nguvu basi atuambie Lowassa ana utajiri kiasi gani na kalipa kodi kiasi gani kwa mwaka 2007.


Hivi hii ni siri?makampuni yake si yanajulikana? na yanafanya kazi za kihalali na kuajiri watu mpaka wafua nguo. TRA lazima ina rekodi za kulipa kodi. Mpaka kufua nguo tulete wawekezaji jamani? Unless kanuni za uongozi ziwe zinazuia viongozi kufungua vioski.
 
Pedro,

Tatizo ni kwamba the article is stupid, hailing the Speaker for his exemplary behavior is the centerpiece of the article, how come the declaration is not quantified?

How does the article make sense and help distinguish the speaker from the rest of the opack to a reader like me? To me, up to now, there is no apparent difference between the speaker who is supposed to have declared his property and the rest of the MPs!

Kama niko kwenye dial up connection inayonilipisha by the minute, the minutes taken to read the article are wasted.In terms of opportunity cost the time taken to read that article is wasted because an article that lacks substance is as good as none, sometimes even worse.
 
This is not the first time they say this. They have been doing so for years and nothing really happens, angesema atayafanyia kazi mambo ya maana na kuwa mkali kwa mambo ya maana zaidi ili iwe mfano, mengine hayo angetamka moja tu na wengine wangefuata!
 
Pedro,

Tatizo ni kwamba the article is stupid, hailing the Speaker for his exemplary behavior is the centerpiece of the article, how come the declaration is not quantified?

How does the article make sense and help distinguish the speaker from the rest of the opack to a reader like me? To me, up to now, there is no apparent difference between the speaker who is supposed to have declared his property and the rest of the MPs!

Kama niko kwenye dial up connection inayonilipisha by the minute, the minutes taken to read the article are wasted.In terms of opportunity cost the time taken to read that article is wasted because an article that lacks substance is as good as none, sometimes even worse.

Kusema la ukweli hata mimi hii topic nilikimbilia kufungua nikifikiri mfano aliouonyesha spika ni yeye mwenyewe kuwa mbunge wa kwanza kuweka mali zake wazi kwamba nina hiki nina kile, nina kuku wa kisasa mia mbili na kila mwezi wanazaliwa wengine nikiwauza pale hoteli mtakuja ninapata hela ya ziada ya kutanua kwa hiyo msifikiri ninakula hela zenu mkiniona ninanawiri au katika miaka yote hiyo utumishini nimejenga kakibanda pale Dar ni mali yangu lakini siishi pale fulani bin fulani kutoka botswana amekodi kwa mwezi ananipa vidola kadhaa etc... yaani kweli tuone kwamba vitu viko wazi na ni haki yake kuishi kifahari kwa sababu hakuwa mvivu wa kufikiri.

Badala yake nikakuta mikwara tu kama kawaida ya viongozi wa awamu hii.
 
sawa mtizamo wako ni mzuri lakini upande wangu mie sijaona maneno ayo yasikufanye uone mabadiliko yoyote ni siasa tu
 
Je, wale vibosile wenye hisa katika makampuni mbali mbali ya nje ikiwemo Barrick nao watatakiwa kutaja hisa ngapi walizonazo katika mahirika hayo!?

Spika Sitta ameonyesha mfano, wengine wamuige
David Azaria
HabariLeo; Monday,December 24, 2007 @00:02

SIKU kadhaa zilizopita Spika wa Bunge, Samuel Sitta, aliwatahadharisha wabunge kuwa mwaka huu atakuwa mkali na kuwachukulia hatua za kisheria wote watakaochelewesha kujaza na kurejesha fomu za kutaja mali na madeni yao ifikapo Desemba 31. Wakati Sitta akitoa tamko hilo bungeni, aliwataka wabunge wote kwenda kuchukua fomu hizo na kuzijaza haraka na kisha kuzirejesha kama inavyotakiwa.

Agizo la Sitta kwa wabunge wenzake limekuja siku chache tu baada ya kutangazwa kwa mabadiliko kwa Tume ya maadili ya viongozi na watumishi wa umma ambako sasa mali zote zitakazojazwa na viongozi wa serikali na wanasiasa zitahakikiwa na kuchunguzwa tofauti na zamani ambako walikuwa wakiziorodhesha tu.

Kwa hili Sitta anapaswa kupongezwa, lakini kikubwa hapa kinachotakiwa ni utekelezaji kwa sababu kuna maagizo mengi katika nchi hii ambayo yamekuwa yakitolewa na viongozi mbalimbali tena wa ngazi za juu serikalini, lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida baada ya maagizo hayo kutolewa hakuna ufuatiliaji wala uhakiki kama kweli agizo limetekelezwa.

Watanzania watafurahi kama itakapofika Desemba 31, yaani Jumatatu ijayo, wabunge wote watakuwa wametekeleza agizo hilo vinginevyo wawajibike kwa kufuata kifungu cha 15(a) cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, kinachosema kwamba kuwa kiongozi wa umma atahesabika kuwa amekiuka maadili kwa kushindwa bila sababu za msingi kutoa tamko linalotakiwa au kutoa tamko la uongo katika kipengele chochote muhimu.

Tukumbuke kwamba kwa mujibu wa Katiba, Mbunge ambaye ni kiongozi wa umma anayewajibika na Sheria ya Maadili ya viongozi wa umma atakoma kuwa Mbunge ikiwa itathibitishwa kwamba amevunja masharti ya maadili ya viongozi wa umma. Sasa hapa ndipo Watanzania wanaposubiri kuona msimamo wa Sitta kama alivyosema Bungeni hivi karibuni.

Lakini suala hili isiwe tu kwa wabunge. Tunao watumishi wengi wa umma katika maeneo mbalimbali nchini ambao nao wanatakiwa kujaza fomu hizo na kutaja mali zao. Kwa hiyo kwa kuwa Spika Sitta ameanza kuonyesha njia kwa kuwabana wabunge wake ni vyema na viongozi wengine katika maeneo ya wakafuatilia katika kuhakikisha kwamba wanawabana wakuu wao wa idara katika kutaja fomu hizo.

Ni vyema Waziri Mkuu akawabana wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi watendaji wa manispaa, halmashauri za miji na wilaya katika kuhakikisha kwamba wanajaza fomu hizo ili ziweze kuchunguzwa na Tume ya maadili ya viongozi na watumishi wa umma. Na kwa kuwa mabadiliko sasa yamefanyika na kuwaruhusu hata wananchi kuhakiki mali zilizotajwa na viongozi katika fomu hizo, basi nao waweze kwenda kuhakiki na kuwafichua wale ambao wana tabia ya kuficha mali zao.

Serikali pekee haiwezi kuwajua mafisadi, wala Tasisisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) hawana uwezo huo, Polisi na hata asasi yoyote ambayo ingeundwa katika nchi hii ama hata kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kulichunguza hili haliwezi kupata mafanikio pasipo kuwashirikisha wananchi ambao ndiyo wanaoishi na viongozi hawa.

Kwa hiyo kufunguliwa kwa milango ya kuingia katika ofisi za Tume ya Maadili ya viongozi na watumishi wa umma kwa mtu yeyote yule kwa nia njema ya kuhakiki mali za kiongozi wake kama ameorodhesha ukweli ama amedanganya, ni moja ya ushirikishwaji wa wananchi katika Serikali yao na hii ni moja ya utekelezaji wa sera ya utawala bora. Hata hivyo, hayo yote hayatafanikiwa kama walio katika mamlaka hawatamuiga Spika Sitta katika kuwasisitizia walio chini yao kuhakikisha wanataja mali zao kabla ya Jumatatu ijayo.

Copyright @TSN 2006 All Rights Reserved
Nikisomaga articles zako za nyuma Na za Sasa kwa jinsi unavyolamba miguu ya Lowassa nabaki kusitika sana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom