Spika ni mbumbumbu wa kanuni za Bunge?

Mwanamayu

JF-Expert Member
May 7, 2010
11,329
6,447
Wakati shughuli za Bunge zikiendelea tarehe 16/11/2010 wakati wa kumchagua naibu spika Spika, Anne Makinda, amekuwa akivunja kanuni za Bunge. Kwa kufanya hivyo ametupilia mbali kabisa kiapo chake cha pili: Kanuni alizovunja ni ya 5 (2) Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, na Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifu Spika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.

Wakati Mustapha Akuunay wa Chadema alipokuwa anaulizwa maswali wakati wa kuomba kura za unaibu spika, Eng. Manyanya aliuliza swali nje ya hoja na Mustapha akamwambia Spika kuwa Eng. Manyanya amevunja kanuni. Cha ajabu Anne Makinda alikuja juu na kwa jazba akamjibu "Mimi ndio ninasimamia kanuni na ndiye natakiwa kusema ni mheshimiwa yupi amevunja kanuni na sio wewe".

Sasa katika hali hii ni nani amevunja kanuni? Mustapha Akuunay au Spika? Je, Spika anaifahamu kanuni hii? Au Spika ana kanuni nyingine kichwani kwake ambazo ametungiwa na mafisadi kupewa na fisadi mkuu Rostam Aziz kule Njombe ambako walikutana naye

Kanuni ya pili ni 10 (4) Mbunge yeyote atakayechaguliwa kuwa Naibu Spika, kabla ya
kushika madaraka yake, ataapishwa na Spika
Kiapo cha Naibu Spika ambacho kitakuwa na maneno yafuatayo:- ....

Hapa Spika alikisahau kifungu hiki mpaka alipokumbushwa na Katibu wa Bunge kwani alishamwambia Ndugai akavae joho wakati joho linaonesha madaraka ya naibu spika na asingeweza kufanya hivyo bila kula kiapo kwanza. Sasa ni nani muda wote huu atakuwa anamkumbusha kanuni za Bunge? Sheria huwa aiangalii umbumbumbu wa mkosaji wa sheria wakati inatimizwa, sasa Anne Makinda ashughulikiwe kufuata kanuni za Bunge hasa namba 134 na ibara ya 84 (7) (d) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania toleo ya mwaka 2005.

Pia Anne Makinda amekiuka kiapo chake cha pili [kanuni ya 9(20)]kwa kuwa mkali sana au kuwa na jazba pale ambapo mbunge wa upinzani hasa Chadema anapoongea. Jazba kwa wapinzani na kwa upole kwa wale wa CCM ni dhahiri kutokuenda haki kwa wote

[“Mimi, Anne Semamba Makinda, naapa kwamba, nitaitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangu kama Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheo hicho nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuni za Bunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano na kwa

vyovyote vile sitatoa siri za Bunge. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”
]

Swali kwa wanawake wote Tanzania: je, Anne Semamba Makinda kwa haya anayoyafanya Bungeni mapema namna hii anawakilisha uwezo wenu wa kufanya kazi na jinsi mwanamke anatakiwa kuwa?
 
Ebu wenye magazeti andikeni hizi habari toka mtandaoni zionwe na watu wengi, ili hawa watu waogope maana yule mama hajui kitu kabisa
 
Ilishaandikwa hata kwenye vitabu vitakatifu kua ''KAENI NAO KWA AKILI''!!!!!!
 
Ninachowaomba wabunge wa upinzani wasitishwe na jazba za huyu mama, tena wawe wakali sana. Tofauti yenu na yeye ni kuwa yeye amevaa joho na nyie hamjavaa. Hawezi kuwafanya chochote nje ya kanuni. Kwanza mkimbana ndo atazidi kuchemka na kudhihirisha kuwa hicho cheo yeye binafsi hakiwezi. Hakiwezi kwa sababu yey binafsi ni mdhaifu sio kwa sababu yey ni mwanamke. Wapo wanawake wengi sana Tanzania wenye uwezo wa kuongoza bunge...
 
Hapo ndio unapoona mambo ya kupigiwa mapande! sidhani hata kama ali deserve kupata hiyo nafasi! mwe!! na kila siku zinapokwenda ndio populariy yake inapopungua kwa public ila itapanda kwa mafisadi wale walio mjengoni CCMs! na hii inanikumbusha about this quote of my fav!

The more you are talked about the less powerful you are.

Benjamin Disraeli (1804-1881) British politician and author.
 

Huyu mama amevamia fani za watu! Alidhani uspika ni kulipwa tu bila kusoma kanuni, siku chache tu ameshajidhihirisha kuwa hazijui kanuni. Kama kuna mtu aliona siku jina la Waziri mkuu lilipopelekwa bungeni, huyu mama alizuia swali la Lissu kwa muda, halafu akautumia muda wa kuhesabu kura kwa kuzipitia kanuni ili apate jibu. Alipokosa jibu akawa mkali! Yes, ukali na kufoka ndio silaha yake pekee iliyobaki, anajaribu kutishia waulizaji ili asiumbuke!
 
Huyu ni Anna au Anne naomba kupewa jibu. Hili jina la Anne limeanza baada ya kupata usipika au!!
 
Mimi kwakweli nilijisikia vibaya sana kama mwanamke,vilivyonifanya nijisikie vibaya ni mambo yafuatayo:
  • Wanawake mara nyingi tunaonekana kama watu wa kubebwa katika nafasi za juu kwasababu tunazozisababisha wenyewe kwa kuto tenda yale jamii kubwa inavyofikiria.Tundu Lissu alikuwa sahihi sana alichotakiwa kufanya ni kusitisha lile swali na Mhs Manyanya na kusonga mbele,watu wote wangempongeza na kuona ushupavu wake wa kiti kile.
  • Hasira na ukali mara nyingi inakuwa ni silaha ya watu wasiojua wajibu wao hivyo namshauri kama mama yangu na dada yangu aachane na hiyo silaha kabisa atende yaliyo sahihi.
  • tusikubali kutumika kunufaisha wengine tutakuwa tunajidhalilisha.
Namtakia kila la kheri mama yangu Anne Makinda,mwenyeezi mungu amuongoze atende haki.
Wakati shughuli za Bunge zikiendelea tarehe 16/11/2010 wakati wa kumchagua naibu spika Spika, Anne Makinda, amekuwa akivunja kanuni za Bunge. Kwa kufanya hivyo ametupilia mbali kabisa kiapo chake cha pili: Kanuni alizovunja ni ya 5 (2) Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, na Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifu Spika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.

Wakati Mustapha Akuunay wa Chadema alipokuwa anaulizwa maswali wakati wa kuomba kura za unaibu spika, Eng. Manyanya aliuliza swali nje ya hoja na Mustapha akamwambia Spika kuwa Eng. Manyanya amevunja kanuni. Cha ajabu Anne Makinda alikuja juu na kwa jazba akamjibu "Mimi ndio ninasimamia kanuni na ndiye natakiwa kusema ni mheshimiwa yupi amevunja kanuni na sio wewe".

Sasa katika hali hii ni nani amevunja kanuni? Mustapha Akuunay au Spika? Je, Spika anaifahamu kanuni hii? Au Spika ana kanuni nyingine kichwani kwake ambazo ametungiwa na mafisadi kupewa na fisadi mkuu Rostam Aziz kule Njombe ambako walikutana naye

Kanuni ya pili ni 10 (4) Mbunge yeyote atakayechaguliwa kuwa Naibu Spika, kabla ya

kushika madaraka yake, ataapishwa na Spika
Kiapo cha Naibu Spika ambacho kitakuwa na maneno yafuatayo:- ....

Hapa Spika alikisahau kifungu hiki mpaka alipokumbushwa na Katibu wa Bunge kwani alishamwambia Ndugai akavae joho wakati joho linaonesha madaraka ya naibu spika na asingeweza kufanya hivyo bila kula kiapo kwanza. Sasa ni nani muda wote huu atakuwa anamkumbusha kanuni za Bunge? Sheria huwa aiangalii umbumbumbu wa mkosaji wa sheria wakati inatimizwa, sasa Anne Makinda ashughulikiwe kufuata kanuni za Bunge hasa namba 134 na ibara ya 84 (7) (d) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania toleo ya mwaka 2005.

Pia Anne Makinda amekiuka kiapo chake cha pili [kanuni ya 9(20)]kwa kuwa mkali sana au kuwa na jazba pale ambapo mbunge wa upinzani hasa Chadema anapoongea. Jazba kwa wapinzani na kwa upole kwa wale wa CCM ni dhahiri kutokuenda haki kwa wote

[“Mimi, Anne Semamba Makinda, naapa kwamba, nitaitumikia vyema na kwa moyo thabiti Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kazi zangu kama Spika wa Bunge, na katika kutimiza wajibu wa cheo hicho nitawatendea haki watu wote kwa mujibu wa Katiba, Kanuni za Bunge na Sheria, Mila na Desturi za Jamhuri ya Muungano na kwa

vyovyote vile sitatoa siri za Bunge. Ewe Mwenyezi Mungu, nisaidie.”
]

Swali kwa wanawake wote Tanzania: je, Anne Semamba Makinda kwa haya anayoyafanya Bungeni mapema namna hii anawakilisha uwezo wenu wa kufanya kazi na jinsi mwanamke anatakiwa kuwa?


 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom