VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Amini nawaambieni, akina Halima Mdee (waliokuwa wanachama 19 wa CHADEMA na sasa wanatajwa kama Wabunge wa Viti Maalum) wanapata tabu na mateso makuu. Wanateswa na mioyo yao (kwamba wanaonekanaje mbele ya jamii kuitwa Wabunge huku wakiwa hawana chama chochote cha siasa kwasasa). Wamepoteza au kupunguza marafiki na kuongeza wanafiki; wamepunguza au kupoteza wanaowaamini na kuongeza wanaowatamani.
Huwa nazungumza nao. Huwa nateta nao. Huwa nawashauri. Wanachokisema kinaogofya kuliko chafya kwa ajili ya afya. Wanasema, wanashinikizwa kwa kulizwa kubaki Bungeni na Spika. Wanadai kuwa Spika anawaambia 'hawezi kurekebisha makosa yake kirahisi'. Anawaambia, kama ni mzigo wao waubebe yeye na NEC iliyompelekea majina kutoka 'kusikojulikana' kikatiba na kisheria. Wanasema kwa kuhema kuwa mara nyingi tu wamekuwa wakitaka kuachana na ubunge huo ambao nao wanauita feki ila hawawezi.
Tafadhali Spika Ndugai, waachie akina Halima Mdee. Kulazimisha kuwepo Bungeni si tu ni kinyume na katiba na sheria bali pia ni kinyume na ustaarabu wa kisiasa. Hata kama ni kufa na tai shingoni, tazama na hadhi na heshima ya akina Halima. Tazama wanavyonyooshewa vidole kama ngole; wanavyosemwa vibaya na wanavyoteswa na dhamira zao. Waachie wapate furaha yao; warudishe marafiki zao; wapambanie uanachama wao; wateuliwe na chama chao. Mateso yao yafike kikomo.
Kuwalazimisha akina Halima kuwa Wabunge 'wa upinzani' si sawa hata kidogo. Spika ulizungumzia utaratibu kama ulifuatwa au la ndani ya chama chao kuwafukuza uanachama. Ulijiridhisha kuhusu taratibu kama zilifuatwa katika kupatikana na kuteuliwa kwao? Hata kama unaona haya kwa kuwateua na kuwaapisha katika mkanganyiko na mgagaziko, muda wa kurekebisha bado unao. Ukiwaondoa Bungeni, macho yao yatalia ila mioyo yao itacheka.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Uyui, Tabora)
Huwa nazungumza nao. Huwa nateta nao. Huwa nawashauri. Wanachokisema kinaogofya kuliko chafya kwa ajili ya afya. Wanasema, wanashinikizwa kwa kulizwa kubaki Bungeni na Spika. Wanadai kuwa Spika anawaambia 'hawezi kurekebisha makosa yake kirahisi'. Anawaambia, kama ni mzigo wao waubebe yeye na NEC iliyompelekea majina kutoka 'kusikojulikana' kikatiba na kisheria. Wanasema kwa kuhema kuwa mara nyingi tu wamekuwa wakitaka kuachana na ubunge huo ambao nao wanauita feki ila hawawezi.
Tafadhali Spika Ndugai, waachie akina Halima Mdee. Kulazimisha kuwepo Bungeni si tu ni kinyume na katiba na sheria bali pia ni kinyume na ustaarabu wa kisiasa. Hata kama ni kufa na tai shingoni, tazama na hadhi na heshima ya akina Halima. Tazama wanavyonyooshewa vidole kama ngole; wanavyosemwa vibaya na wanavyoteswa na dhamira zao. Waachie wapate furaha yao; warudishe marafiki zao; wapambanie uanachama wao; wateuliwe na chama chao. Mateso yao yafike kikomo.
Kuwalazimisha akina Halima kuwa Wabunge 'wa upinzani' si sawa hata kidogo. Spika ulizungumzia utaratibu kama ulifuatwa au la ndani ya chama chao kuwafukuza uanachama. Ulijiridhisha kuhusu taratibu kama zilifuatwa katika kupatikana na kuteuliwa kwao? Hata kama unaona haya kwa kuwateua na kuwaapisha katika mkanganyiko na mgagaziko, muda wa kurekebisha bado unao. Ukiwaondoa Bungeni, macho yao yatalia ila mioyo yao itacheka.
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Uyui, Tabora)