Spika Ndugai, waonee huruma akina Halima Mdee. Jela uliyowaweka inawatesa na kuwatweza, ifike mahali uwaache

Ukweli Ndugai amekosea , na sasa kwa sababu wameshajitungia sheria ya kutokushtakiwa, basi anachofanya ni ulevi na ubabe wa madaraka.
Mkuu si kakosea tu bali anakidhalilisha kiti cha Uspika...Hiki kiti kina heshima yake bwana toka Uhuru enzi za kina Adam Sapi Mkwawa..ila kwa sasaaaa hiiiiii......
 
Amini nawaambieni, akina Halima Mdee (waliokuwa wanachama 19 wa CHADEMA na sasa wanatajwa kama Wabunge wa Viti Maalum) wanapata tabu na mateso makuu. Wanateswa na mioyo yao (kwamba wanaonekanaje mbele ya jamii kuitwa Wabunge huku wakiwa hawana chama chochote cha siasa kwasasa). Wamepoteza au kupunguza marafiki na kuongeza wanafiki; wamepunguza au kupoteza wanaowaamini na kuongeza wanaowatamani.

Huwa nazungumza nao. Huwa nateta nao. Huwa nawashauri. Wanachokisema kinaogofya kuliko chafya kwa ajili ya afya. Wanasema, wanashinikizwa kwa kulizwa kubaki Bungeni na Spika. Wanadai kuwa Spika anawaambia 'hawezi kurekebisha makosa yake kirahisi'. Anawaambia, kama ni mzigo wao waubebe yeye na NEC iliyompelekea majina kutoka 'kusikojulikana' kikatiba na kisheria. Wanasema kwa kuhema kuwa mara nyingi tu wamekuwa wakitaka kuachana na ubunge huo ambao nao wanauita feki ila hawawezi.

Tafadhali Spika Ndugai, waachie akina Halima Mdee. Kulazimisha kuwepo Bungeni si tu ni kinyume na katiba na sheria bali pia ni kinyume na ustaarabu wa kisiasa. Hata kama ni kufa na tai shingoni, tazama na hadhi na heshima ya akina Halima. Tazama wanavyonyooshewa vidole kama ngole; wanavyosemwa vibaya na wanavyoteswa na dhamira zao. Waachie wapate furaha yao; warudishe marafiki zao; wapambanie uanachama wao; wateuliwe na chama chao. Mateso yao yafike kikomo.

Kuwalazimisha akina Halima kuwa Wabunge 'wa upinzani' si sawa hata kidogo. Spika ulizungumzia utaratibu kama ulifuatwa au la ndani ya chama chao kuwafukuza uanachama. Ulijiridhisha kuhusu taratibu kama zilifuatwa katika kupatikana na kuteuliwa kwao? Hata kama unaona haya kwa kuwateua na kuwaapisha katika mkanganyiko na mgagaziko, muda wa kurekebisha bado unao. Ukiwaondoa Bungeni, macho yao yatalia ila mioyo yao itacheka.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Uyui, Tabora)
Hao ni watu wazima, wacha wajisemee wenyewe. Kwani unadhani hawajui cha halali, au cha haramu!?.
 
Lema na Lisu lini mnarudi Tanzania?

Walituaminisha wamekimbia nchi na kwenda kulelewa na wanaume wa kizungu kama wakimbizi kwa sababu hapa nchini walikuwa wanatishiwa maisha na mwendazake.

Sasa hivi mwendazake hayupo je ni lini mtaacha kuishi kwa kulelewa na wazungu Ulaya mrudi Tanzania kujenga nchi na kula kwa jasho lenu? Tunahoji haya kwa sababu tunaona mko kimyaaa.

Mkiendelea kukaa kimya watu watajua mlikimbia nchi kwa masilahi yenu na siyo kwa kutishiwa maisha na mwendazake. Kwanza wewe Lema ulilipa lile deni lako la million 400 lililosomwa na spika Ndugai bungeni?

Rudi ulipe madeni ya watu.

Na wewe mzee wa MIGA Lisu rudi hutawakuta Acacia uliokuwa unawatetea sana utakuta kampuni mpya ya madini inayoitwa TWIGA
Liangalie linaposti huku limekalia mpini
 
Amini nawaambieni, akina Halima Mdee (waliokuwa wanachama 19 wa CHADEMA na sasa wanatajwa kama Wabunge wa Viti Maalum) wanapata tabu na mateso makuu. Wanateswa na mioyo yao (kwamba wanaonekanaje mbele ya jamii kuitwa Wabunge huku wakiwa hawana chama chochote cha siasa kwasasa). Wamepoteza au kupunguza marafiki na kuongeza wanafiki; wamepunguza au kupoteza wanaowaamini na kuongeza wanaowatamani.

Huwa nazungumza nao. Huwa nateta nao. Huwa nawashauri. Wanachokisema kinaogofya kuliko chafya kwa ajili ya afya. Wanasema, wanashinikizwa kwa kulizwa kubaki Bungeni na Spika. Wanadai kuwa Spika anawaambia 'hawezi kurekebisha makosa yake kirahisi'. Anawaambia, kama ni mzigo wao waubebe yeye na NEC iliyompelekea majina kutoka 'kusikojulikana' kikatiba na kisheria. Wanasema kwa kuhema kuwa mara nyingi tu wamekuwa wakitaka kuachana na ubunge huo ambao nao wanauita feki ila hawawezi.

Tafadhali Spika Ndugai, waachie akina Halima Mdee. Kulazimisha kuwepo Bungeni si tu ni kinyume na katiba na sheria bali pia ni kinyume na ustaarabu wa kisiasa. Hata kama ni kufa na tai shingoni, tazama na hadhi na heshima ya akina Halima. Tazama wanavyonyooshewa vidole kama ngole; wanavyosemwa vibaya na wanavyoteswa na dhamira zao. Waachie wapate furaha yao; warudishe marafiki zao; wapambanie uanachama wao; wateuliwe na chama chao. Mateso yao yafike kikomo.

Kuwalazimisha akina Halima kuwa Wabunge 'wa upinzani' si sawa hata kidogo. Spika ulizungumzia utaratibu kama ulifuatwa au la ndani ya chama chao kuwafukuza uanachama. Ulijiridhisha kuhusu taratibu kama zilifuatwa katika kupatikana na kuteuliwa kwao? Hata kama unaona haya kwa kuwateua na kuwaapisha katika mkanganyiko na mgagaziko, muda wa kurekebisha bado unao. Ukiwaondoa Bungeni, macho yao yatalia ila mioyo yao itacheka.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Uyui, Tabora)
Usisahau kufika isikizya mzee tupatupa
 
Lema na Lisu lini mnarudi Tanzania?

Walituaminisha wamekimbia nchi na kwenda kulelewa na wanaume wa kizungu kama wakimbizi kwa sababu hapa nchini walikuwa wanatishiwa maisha na mwendazake.

Sasa hivi mwendazake hayupo je ni lini mtaacha kuishi kwa kulelewa na wazungu Ulaya mrudi Tanzania kujenga nchi na kula kwa jasho lenu? Tunahoji haya kwa sababu tunaona mko kimyaaa.

Mkiendelea kukaa kimya watu watajua mlikimbia nchi kwa masilahi yenu na siyo kwa kutishiwa maisha na mwendazake. Kwanza wewe Lema ulilipa lile deni lako la million 400 lililosomwa na spika Ndugai bungeni?

Rudi ulipe madeni ya watu.

Na wewe mzee wa MIGA Lisu rudi hutawakuta Acacia uliokuwa unawatetea sana utakuta kampuni mpya ya madini inayoitwa TWIGA
Unataka wakulale??
 
Screenshot_20210507-141919.png
 
Usiwatetee hao wanawake, Spika amewazuia nini kuondoka huko bungeni? hao ni walafi wa vyeo.
 
Amini nawaambieni, akina Halima Mdee (waliokuwa wanachama 19 wa CHADEMA na sasa wanatajwa kama Wabunge wa Viti Maalum) wanapata tabu na mateso makuu. Wanateswa na mioyo yao (kwamba wanaonekanaje mbele ya jamii kuitwa Wabunge huku wakiwa hawana chama chochote cha siasa kwasasa). Wamepoteza au kupunguza marafiki na kuongeza wanafiki; wamepunguza au kupoteza wanaowaamini na kuongeza wanaowatamani.

Huwa nazungumza nao. Huwa nateta nao. Huwa nawashauri. Wanachokisema kinaogofya kuliko chafya kwa ajili ya afya. Wanasema, wanashinikizwa kwa kulizwa kubaki Bungeni na Spika. Wanadai kuwa Spika anawaambia 'hawezi kurekebisha makosa yake kirahisi'. Anawaambia, kama ni mzigo wao waubebe yeye na NEC iliyompelekea majina kutoka 'kusikojulikana' kikatiba na kisheria. Wanasema kwa kuhema kuwa mara nyingi tu wamekuwa wakitaka kuachana na ubunge huo ambao nao wanauita feki ila hawawezi.

Tafadhali Spika Ndugai, waachie akina Halima Mdee. Kulazimisha kuwepo Bungeni si tu ni kinyume na katiba na sheria bali pia ni kinyume na ustaarabu wa kisiasa. Hata kama ni kufa na tai shingoni, tazama na hadhi na heshima ya akina Halima. Tazama wanavyonyooshewa vidole kama ngole; wanavyosemwa vibaya na wanavyoteswa na dhamira zao. Waachie wapate furaha yao; warudishe marafiki zao; wapambanie uanachama wao; wateuliwe na chama chao. Mateso yao yafike kikomo.

Kuwalazimisha akina Halima kuwa Wabunge 'wa upinzani' si sawa hata kidogo. Spika ulizungumzia utaratibu kama ulifuatwa au la ndani ya chama chao kuwafukuza uanachama. Ulijiridhisha kuhusu taratibu kama zilifuatwa katika kupatikana na kuteuliwa kwao? Hata kama unaona haya kwa kuwateua na kuwaapisha katika mkanganyiko na mgagaziko, muda wa kurekebisha bado unao. Ukiwaondoa Bungeni, macho yao yatalia ila mioyo yao itacheka.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Uyui, Tabora)
HALIMA hawezi pata bwana tena labda tu aendelee kugegedwa.
Hakuna mwanaume mwenye kutaka mwanamke muongo, anayepaya mali kwa dhuluma na muuaji.
NUSRAT HANJE ni muislam na eti amefunga, hii ni kufuru kwa allah
 
Hii ya Mdee &co ni ngumu sana kujisafisha, maana waliaminiwa sana na wananchi na chama pia. Wafanye maamuzi magumu. Wajiuzulu ubunge wao na wawaombe msamaha watanzania na chama. Watasamehewa.
 
Lema na Lisu lini mnarudi Tanzania?

Walituaminisha wamekimbia nchi na kwenda kulelewa na wanaume wa kizungu kama wakimbizi kwa sababu hapa nchini walikuwa wanatishiwa maisha na mwendazake.

Sasa hivi mwendazake hayupo je ni lini mtaacha kuishi kwa kulelewa na wazungu Ulaya mrudi Tanzania kujenga nchi na kula kwa jasho lenu? Tunahoji haya kwa sababu tunaona mko kimyaaa.

Mkiendelea kukaa kimya watu watajua mlikimbia nchi kwa masilahi yenu na siyo kwa kutishiwa maisha na mwendazake. Kwanza wewe Lema ulilipa lile deni lako la million 400 lililosomwa na spika Ndugai bungeni?

Rudi ulipe madeni ya watu.

Na wewe mzee wa MIGA Lisu rudi hutawakuta Acacia uliokuwa unawatetea sana utakuta kampuni mpya ya madini inayoitwa TWIGA
Anzisha andiko mahususi kuhusu hilo sio kwenye uzi huu
 
... mbona rahisi sana; wajiuzulu huo ubunge feki! As simple as that wanakuwa huru!
Spika anaweza akaomba barua za vikao vya familia na ukoo, na kama katiba za familia zao zilifuatwa, na kutaka kujua pia kama waliohudhuria vikao ni ndugu kweli.... atataka pia DNA zipimwe, na sahihi zao pia ziende kwa mchunguzi wa maandishi, kisha waje na barua ya hospitali ku-prove kwamba walikuwa na akili timamu, kisha waje na barua ya TAKUKURU kuprove kwamba hawajahongwa... in short hawezi kukosa visingizio.

Rejea ubunge wa mbunge wa Ndanda, na ubunge wa kina Lijualikali et al, wakati bunge lililopita linaisha.
 
Lema na Lisu lini mnarudi Tanzania?

Walituaminisha wamekimbia nchi na kwenda kulelewa na wanaume wa kizungu kama wakimbizi kwa sababu hapa nchini walikuwa wanatishiwa maisha na mwendazake.

Sasa hivi mwendazake hayupo je ni lini mtaacha kuishi kwa kulelewa na wazungu Ulaya mrudi Tanzania kujenga nchi na kula kwa jasho lenu? Tunahoji haya kwa sababu tunaona mko kimyaaa.

Mkiendelea kukaa kimya watu watajua mlikimbia nchi kwa masilahi yenu na siyo kwa kutishiwa maisha na mwendazake. Kwanza wewe Lema ulilipa lile deni lako la million 400 lililosomwa na spika Ndugai bungeni?

Rudi ulipe madeni ya watu.

Na wewe mzee wa MIGA Lisu rudi hutawakuta Acacia uliokuwa unawatetea sana utakuta kampuni mpya ya madini inayoitwa TWIGA
Unajifungua lini niandae zawadi?
 
Hili move lote la kichina liliasisiwa pale Lumumba, likapata baraka zote na Mwendazake pamoja na Spika - sasa Spika anaona kuwatema ni kumsaliti mwendazake !! patamu hapo.

Ila ningekuwa mimi ni mwana Covid-19, ningemtafuta Maza fasta nikamwambia kinaga ubaga mwanzo mwisho yaani episode loote lilivyokuwa then namwaga manyanga!! hela si kila kitu hapa duniani kuliko heshima na utu. Nasisitiza ni lazima umtafute maza ili ukishautema ubunge wao kesho na keshokutwa wasikusumbue sumbue kwamba hujalipa kodi tangu Uhuru 1961 wakati wewe umezaliwa miaka ya themanini, au umejenga nyumba yako kwenye chemchem ya gesi.

Halima alijijengea heshima kubwa sana nchini Tanzania, sidhani kuna mtoto wa miaka 5 hadi mzee wa miaka 100 Tanzania ambaye hamjui Halima. Sasa yote hayo yateketee kweli kisa tu kumfurahisha mwendazake na kundi lake dogo... hapana hapana. Halima tapika hilo kitu nafsi yako iwe huru..
Nasikia wao kwa wao hawaelewani.
 
Back
Top Bottom