Spika Ndugai: Wakurugenzi wa TARURA na RUWASA wanalipwa mishahara mikubwa kuliko Ma - DED yalivyo mambo ya ajabu

Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya.

Ndugai amesema hayo akimuunga mkono mbunge wa Gairo mh Shabiby aliyedai wakurugenzi wa Tarura na Ruwasa wamejigeuza miungu watu.

Ramadhan Kareem!
Tanzania kwenye ulipwaji wa mishahara kuna serikali nyingi.
 
Naona mkuu kama kapagawa hivi ....
Kabla ya kuwasema hao wakuu wenzao wangetaja ya kwao ilitujue kama tuna zika au kusafirisha.

hao n wataaluma waacheni walipwe hivyo hivyo tu....

Kwani maded ndio nani kwenye hii nchi?
Acha kutetea utopolo wewe!!!
Hivi hao Managers wana Utaalamu gani wa ajabu wa kulipwa mishahara mikubwa? Hivi unaziona barabara nyingi zilivo na viwango vya chini na miundo mbinu ya maji ilivo ya hovyo???
TARURA ilianzishwa na Jiwe ili kuwasaidia ndugu zake a.k.a Wanyonge kupata ajira za upigaji! TANROADS ilikuwa inatosha kabisa lakini kuna mambo ya kihuni tu yalikuwa yanaanzishwa kwa maslahi binafsi. Kazi za TANROADS zina ingiliwa na TARURA na TANROADS inaingilia kazi za TARURA...!!! This is just a management by Crisis!!!
Ni BORA TARURA IVUNJWE TUBAKI NA TANROADS peke yake inatosha sana.
 
Ccm si ndio waanzilishi wa kila kitu Happ bungeni anashangaa nini
 
Tanzania kwenye ulipwaji wa mishahara kuna serikali nyingi.
Hayati Jiwe alikuwa ameunda SERIKALI NDANI YA SERIKALI!!
Sukuma Gang from CHATO ndani ya Serikali ya CCM YA MAGUFULI. Tukisema Utawala huu wa A5 ulikuwa ni majanga mafisi wa Lumumba wanajifanya hawajui!! This time around sote tutaongea lugha moja tu!
 
Hayati Jiwe alikuwa ameunda SERIKALI NDANI YA SERIKALI!!
Sukuma Gang from CHATO ndani ya Serikali ya CCM YA MAGUFULI. Tukisema Utawala huu wa A5 ulikuwa ni majanga mafisi wa Lumumba wanajifanya hawajui!! This time around sote tutaongea lugha moja tu!
Ilikuwa serikali ya aina yake
 
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya.

Ndugai amesema hayo akimuunga mkono mbunge wa Gairo mh Shabiby aliyedai wakurugenzi wa Tarura na Ruwasa wamejigeuza miungu watu.

Ramadhan Kareem!
Mbona na Wabunge mnalipwa hivyo hivyo husemi?
 
Ilikuwa serikali ya aina yake
Halafu unashangaa mijitu kama kina Lusinde Kibajaj na Msukuma Kasheku (CLASS 7)wanasimama Bungeni kuunga mkono ujinga, ubazazi na uvuta bhang na Spika ati anatenga muda "maalumu " ili vichaa hao waongee kuwatukana CHADEMA na Wasomi wa kiwango cha Professors!?? Nonsense.
 
Kwa hiyo ndugai ni 'shujaa wa africa' kaitka matumizi makubwa ya hela ya umma kwa matibabu?😅😅😅
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) Prof. Assad alitimuliwa na Ndugai mara tu report yake CAG ya 19/20 ilipofichua Ufisadi huo wa matumizi ya Ndugai akiwa India kwa matibabu!!!
 
Halafu unashangaa mijitu kama kina Lusinde Kibajaj na Msukuma Kasheku (CLASS 7)wanasimama Bungeni kuunga mkono ujinga, ubazazi na uvuta bhang na Spika ati anatenga muda "maalumu " ili vichaa hao waongee kuwatukana CHADEMA na Wasomi wa kiwango cha Professors!?? Nonsense.
Kibajaji aombewa udaktari wa heshima!
 
Tanzania kwenye ulipwaji wa mishahara kuna serikali nyingi.
CCM ndiyo chanzo za hizi crisis kwenye nchi hii!
Siyo midhshara tu kuna maswala mengi sana yanayohusu Watumishi yamekaa zigzag! Mfano mwingine Mubashara ni mifuko ya Kijamii kwa Watumishi wa Umma na Serikali:
Leo Mwalimu akistaafu ngazi ya Certificate tu na mshahara wa kawaida ataondoka na zaidi ya Milioni 100 mpaka Milioni 150 .
Anastahafu mtumishi wa Umma ngazi ya Diploma au Degree kwa idadi ya miaka ya Utumishi ileile na mshahara mkubwa kuliko Mwalimu analipwa mafao ya milioni 30 mpaka 50 milioni!!
Wabunge wanakaa Bungeni miaka 5 tu wanapomaliza Bunge wanalipwa hata kabla ya Bunge kuvunjwa kati ya Milioni 270 mpaka Milioni 400 kutegemea na cheo alichokuwa nacho e.g. Waziri, Spika au N/Spika.
Tanzania ni nchi ya ajabu sana.
 
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya.

Ndugai amesema hayo akimuunga mkono mbunge wa Gairo mh Shabiby aliyedai wakurugenzi wa Tarura na Ruwasa wamejigeuza miungu watu.

Ramadhan Kareem!
Huyu nae ndumilakuwili mchumia tumbo, mbona hashangai Wabunge na maspika kulipwa mshahara mkubwa kuliko walimu. Kuna anaezidi kazi ya mwalimu? Hawa ndo walistahili mshahara mnono, lakini kwa Tanzania hizo ni ndoto
 
Back
Top Bottom