Spika Ndugai: Wakurugenzi wa TARURA na RUWASA wanalipwa mishahara mikubwa kuliko Ma - DED yalivyo mambo ya ajabu

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,506
141,230
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya.

Ndugai amesema hayo akimuunga mkono mbunge wa Gairo mh Shabiby aliyedai wakurugenzi wa Tarura na Ruwasa wamejigeuza miungu watu.

Ramadhan Kareem!
 
Kwani spika kwanini hajabadili Sheria za utumishi wa umma na mahusiano kazini?

Yeye spika angeongea na waziri husika muswada ungepitishwa tu .

Mbona Msukuma wa darasa la 7 analipwa pesa nyingi kuliko senior engineer wa Tanroads?

Huyu spika pumzi yake karibu itakatwa tu amfuate Meko muuni mwenzake
 
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya...
Natumai sheria zilioanzisha taasisi hizi zilipitishwa hapo hapo mjengoni, na mishahara yao haipangwi gizani kuna mamlaka zinaridhia na kupitisha. Mshangao kama huu ni wa kinafiki sana.

Acha na sie tushangae kama yeye!
 
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya..
Ndugai naona akili iko free fall!

Wakurugenzi hao wanahandle pesa na resources nyingi mno ambazo DED hawezi kuota kuzihandle.

Kwa mfano YEYE Ndugai ana handle wabunge wasiozidi 370 na wafanya kazi hawazidi 150.

Alipwe huo mshahara wa maDED , Hapo tutamwelewa.

(NB Humu JF kuna member alimshauri Ndugai anyamaze, yanayomtoka kinywani sasa hivi ni uvundo)
 
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya....
Mbona wakati mwendazake alikuwepo mlikuwa kimyaa!! kwani wameanza kulipwa namna hiyo majuzi baada ya msiba?

Ndugai kuna kitu unachokitafuta.
 
Spika Ndugai ameshangazwa na serikali kuwalipa mishahara mikubwa wakurugenzi wa mamlaka ya maji na ile ya barabara za vijijini ambayo ni zaidi ya mishahara wanayolipwa Wakurugenzi wa wilaya...
Anajua qualifications za kuwa Manager wa TARURA na RUWASA? maDED yaani Wakurugenzi wa Halmashauri wengi huteuliwa kwa hisani ya Rais hata kama hawana sifa stahiki.

NB: Mke wa Ndugai ni DED wa Bahi.
 
Huyu jamaa wasipomnyang'anya mic atakuja kutupa siri zake za ndani.
Mjadala wake auelekeze kwenye mishahara ya wabunge!

Unafiki na ufitini anaouonyesha ni wa kiwango cha juu SANA! Ni hatari kwa afya na usalama wa nchi!

Binafsi sifurahishwi na mishahara ya wabunge! Labda atueleze mshahara wa SPIKA ni ngapi, angependa upunguzwe kwa shs ngapi?

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Naona mkuu kama kapagawa hivi .

Kabla ya kuwasema hao wakuu wenzao wangetaja ya kwao ilitujue kama tuna zika au kusafirisha.

hao n wataaluma waacheni walipwe hivyo hivyo tu.

Kwani maded ndio nani kwenye hii nchi?
 
Back
Top Bottom