Spika Ndugai: Wabunge 19 waliofukuzwa CHADEMA wapo kwenye mikono salama

Leo Bungeni baada ya kipindi cha maswali na majibu, Spika wa Bunge Job Ndugai amesimama na kumkemea Nape Nauye, Mbunge wa Mtama ambaye hivi karibuni alitoa maoni yake binafsi kuwa wale wabunge 19 waliotimuliwa na CHADEMA sio wabunge halali.

Ndugai, akonekana mwenge wasiwasi na aliyepoteza mwelekeo akaanza kwa kujisifu kuwa yeye ni mzoefu, hivyo asipangiwe cha kufanya.

Ameenda mbali zaidi kwa kutaka kuonesha kuwa akina mama hao 19 wanaonewa na mfumo dume uliopo CHADEMA. Ndugai anasahau yeye na Profesa Lipumba walichowafanyia akina mama wa CUF walipovuliwa ubunge kwa kimemo cha Lipumba.

Mzee Ndugai atabaki katika historia kama SPIKA DHAIFU kuwahi kutokea. Tunazitaka Mamlaka za kulinda Katiba kuhakikisha KATIBA inalindwa.

Ikiwezekana kila NDUGAI atakapoonekana hadharani azomewe kwa aibu anayoiletea Taifa.

=======


Siku chache baada ya video kusambaa ikimuonesha Mbunge wa Mtama Nape Nnauye akichangia moja ya mjadala uliohusisha Wabunge 19 wa Viti Maalumu akiwaita (COVID 19) akidai kuwa wamefukuzwa na Chama na jambo hilo liheshimwa na kwa kuwa Katiba iko wazi kwamba hakutakiwi kuwa na watu wasio na chama ndani ya Bunge.

Spika wa Bunge, Job Ndugai amesimama Bungeni leo na kumuonya Mbunge Nape Nnauye na wabunge wengine kuwa makini na maneno wanayoyazungumza.

“Juzi mdogo wangu Nape yalimtoka maneno na yamezunguka sana kwa sababu ni mbunge, ikifika mahali mbunge na Spika mnapishana nadhani haipendezi, kwa hiyo sitapitia hoja zake kwa sababu ana uhuru lakini kitu kimoja hana uhuru kwa sababu ya kanuni ni kuwasema vibaya wabunge wenzake kanuni zinakataza hilo lazima nilikemee, aliwataja kwa majina ya mitaani huko ambayo kwa kweli alikosea sana na niliongea naye naamini aliteleza kwa hiyo sitamsimamisha hapa aseme chochote ninachoombeni waheshimiwa mmsamehe bure aliwakosea sana, tuchunge sana midomo yetu tunapodeal na binadamu wenzetu”-Spika Job Ndugai

C52928F3-EC31-4960-8D54-0057292E0E8C.jpeg
 
Back
Top Bottom