VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mbunge wa Momba, tena wa chama chetu cha CCM, amedhalilishwa Bungeni. Ametolewa nje ya Bunge kwa aibu kuu akiambiwa kuwa 'hajavaa vizuri'. Amri ya kutolewa nje kwa mwanamama huyo Mbunge wa Momba ilitolewa nawe Spika Job Ndugai. Ni baada ya kuombwa muongozo na Mbunge Ameir akidai kuwa mwanamama huyo amevaa suruali 'mbaya' na hivyo kutakiwa akavae 'vizuri'.
Kwakuwa Bunge ni uwanja wako wa kujidai kwa kumimina amri na shurti kama mashuti katika hali ya kutafuta kiki za kisiasa zisizo za kisasa, Mbunge wa Momba alitoka kwa aibu kubwa huku akitwezwa, akidhalilishwa na kubagazwa na kitendo hicho. Akarejea baadaye kuendelea na kikao cha Bunge akiwa amevalia sketi na blauzi ileile. Nje na ndani ya Bunge, baada ya tukio lile, Mbunge huyo hakuwa na amani moyoni mwake. Ameanikwa na kuchorwa kama mwanamke asiye na maadili.
CHADEMA waliposema na kusimamia uamuzi wao wa kuwafukuza uanachama akina Halima Mdee, ni wewe Spika Ndugai ndiye uliyekuwa ukisimama Bungeni mara kwa mara kuwakingia kifua. Ukijitamba kuwa akina Mdee wako mikono salama, umekuwa ukiuaminisha umma kuwa wewe ni mtetezi wa haki za Wabunge hasa wabunge wanawake. Tukio la Mbunge wa Momba limekuumbua na kukuanika.
Unamtoaje Mbunge kwa aibu Bungeni bila hata kujiridhisha? Haki yake ya kujieleza mbona hukumpa? Siasa huhitaji usanii ila wako huu umezidi. Unajichora kama mtetezi wa akina Mdee ambao wako Bungeni bila kuwa na chama chochote cha kisiasa kama Katiba inavyotaka huku ukimdhalilisha Mbunge wa chama chetu tena wa Jimbo la Momba. Filamu yako ya akina Mdee imebuma. Jitafakari!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Kwakuwa Bunge ni uwanja wako wa kujidai kwa kumimina amri na shurti kama mashuti katika hali ya kutafuta kiki za kisiasa zisizo za kisasa, Mbunge wa Momba alitoka kwa aibu kubwa huku akitwezwa, akidhalilishwa na kubagazwa na kitendo hicho. Akarejea baadaye kuendelea na kikao cha Bunge akiwa amevalia sketi na blauzi ileile. Nje na ndani ya Bunge, baada ya tukio lile, Mbunge huyo hakuwa na amani moyoni mwake. Ameanikwa na kuchorwa kama mwanamke asiye na maadili.
CHADEMA waliposema na kusimamia uamuzi wao wa kuwafukuza uanachama akina Halima Mdee, ni wewe Spika Ndugai ndiye uliyekuwa ukisimama Bungeni mara kwa mara kuwakingia kifua. Ukijitamba kuwa akina Mdee wako mikono salama, umekuwa ukiuaminisha umma kuwa wewe ni mtetezi wa haki za Wabunge hasa wabunge wanawake. Tukio la Mbunge wa Momba limekuumbua na kukuanika.
Unamtoaje Mbunge kwa aibu Bungeni bila hata kujiridhisha? Haki yake ya kujieleza mbona hukumpa? Siasa huhitaji usanii ila wako huu umezidi. Unajichora kama mtetezi wa akina Mdee ambao wako Bungeni bila kuwa na chama chochote cha kisiasa kama Katiba inavyotaka huku ukimdhalilisha Mbunge wa chama chetu tena wa Jimbo la Momba. Filamu yako ya akina Mdee imebuma. Jitafakari!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)