Spika Ndugai na Katibu wa Bunge wapelekwe Mahakamani kwa kutoiheshimu Katiba waliyoapa kuitetea

MtuHabari

JF-Expert Member
Oct 16, 2020
321
1,019
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
 
190876.jpg
 
Spika ana kinga ya kutokuishitakiwa, na hiyo kinga walijiwekea na wabunge wa ccm kuipitisha, ili spika aikanyage katiba vizuri.
 
Spika ana kinga ya kutokuishitakiwa, na hiyo kinga walijiwekea na wabunge wa ccm kuipitisha, ili spika aikanyage katiba vizuri.
Akiingia Lisu, say, watafungwa maana hatuwezi kukubali sheria ya kishenzi ya kulinda maovu. Tutaunda mahakama maalum nje ya mahakama hizi za sasa kushughulika na waasi hawa waliojiwekea sheria ya kujilinda ili wafanye maafa
 
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo APA kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa LA pili baada ya uhaini na mauaji....
Chadema ilitoa fursa ya waliofukuzwa kukata rufaa na kwa mantiki hiyo hukumu ya kamati kuu haikupelekwa kwa spika mpaka Baraza kuu litakapokaa na kuisikiliza rufaa ya wanachama 19.

Mpaka hapo mpira uko miguuni mwa Chadema,Baraza kuu litabariki maamuzi ya kamati kuu na kumuandikia spika au baraza kuu litawasamehe na kuwarudishia uanachama wao,NI suala la muda.

Mpaka sasa Ndugai yupo huru kufanya lolote na hao wabunge 19!

Ni kwa uelewa wangu!!
 
Chadema ilitoa fursa ya waliofukuzwa kukata rufaa na kwa mantiki hiyo hukumu ya kamati kuu haikupelekwa kwa spika mpaka Baraza kuu litakapokaa na kuisikiliza rufaa ya wanachama 19..
HUKUMU HAIKUPELEKWA! NANI MKWELI KATI YAKO NA NDUGAI ALIYESEMA ALIIPATA ILA AKAAHIDI KUWALINDA?
 
Nawaonea huruma sana wazee wajinga hawa! Hivi hawajihurumii wao na familia zao? Wanajua uchungu watakao pata watoto wao wakiona wazee wao wako jela kwa makosa ya kujitakia yasiyo na faida?
Mkuu una angalizo zuri, ila matamanio yako sio rahisi kufikiwa kwani ukija utawala mwingine watasema hawafukui makaburi.
 
Chadema ilitoa fursa ya waliofukuzwa kukata rufaa na kwa mantiki hiyo hukumu ya kamati kuu haikupelekwa kwa spika mpaka Baraza kuu litakapokaa na kuisikiliza rufaa ya wanachama 19....
Uko sawa, ila niambie hata mishipa ya fahamu hawana kuwa katiba inavunjwa?
 
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
Walishajiwekea kinga
 
Back
Top Bottom