Spika Ndugai: Mbowe alikuwa Ulaya sasa katumwa na watu wake anapotosha kuhusu ripoti ya CAG

Sasa amejuaje kama inapotoshwa wakati yeye hajaisoma, hajui chochote na hao wabunge wanaounda LAAC na PAC hawajaichambua?

Ndugai ni Speaker wa HOVYO sana kuwahi kutokea katika historia ya Bunge letu tukufu. Ameiharibu sana taswira ya Bunge na sasa kila zuzu yeyote anatamani kuingia kule
Kwa nini Mbowe aitolee uchambuzi wakati kisheria na anajua kabisa kwamba ni kamati za bunge PAC na LAAC ndio wanamamlaka ya kuichambua na kuiwakilisha kwetu kupitia bunge... Kama sio kutumwa ni nini?
 
Hatushangai kwa maelezo yake. Hebu fikiria mwizi wa kuku mwenye thamani ya shilingi 10,000 anafungwa miaka 10. Hawa Waheshimiwa wanakwiba shilingi 1,000,000 wanafungwa miezi sita na kifungo kuahirishwa hivyo wanatumikia jamii kwa kufagia hospitalini kwa wiki nne! "For Justice we better go to the Godfather" ...in Mario Bonasera's voice.
 
Sasa amejuaje kama inapotoshwa wakati yeye hajaisoma, hajui chochote na hao wabunge wanaounda LAAC na PAC hawajaichambua?

Ndugai ni Speaker wa HOVYO sana kuwahi kutokea katika historia ya Bunge letu tukufu. Ameiharibu sana taswira ya Bunge na sasa kila zuzu yeyote anatamani kuingia kule
Hao mazuzu ni pamoja na wale waliobobea katika kufufua misukule.
 
Spika wa Bunge Job Ndugai, amezitaka kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zichambue ripoti ya CAG na kuiwakilisha bungeni katika mkutano wa nne, kwa kuwa inapotoshwa huku akimtaja Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kuwa mmoja wapo

Spika wa Bunge Job Ndugai amezitaka kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zichambue ripoti ya Mdhibiti na Mkuguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) na kuiwakilisha bungeni katika mkutano wa nne badala ya mkutano wa tano, kwa kuwa inapotoshwa.

Akizungumza leo Jumatatu Aprili 12 2021, Ndugai huku akimtaja Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amedai kuwepo upotoshaji wa ripoti hiyo.

Kauli ya Spika imekuja siku moja baada ya Mbowe kuhutubia kupitia mitandao ya jamii, ambapo pamoja na mambo mengine alilituhumu Bunge kwa vitendo vya rushwa.

“Watu wanabeba tu mabilioni yameibiwa sasa huyo rafiki yangu Freeman Mbowe alikuwa Ulaya huko sasa katumwa na watu wake huko anapotosha mambo,” amesema.

Amesema sio watu wengi wenye uelewa wa kuchambua taarifa za kihasibu na hivyo kunaweza kukawa na ujenzi wa kituo cha afya wa Sh 500milioni lakini Sh 499milioni zimetumika vizuri kabisa.

Hata hivyo, amesema lakini kati ya fedha hizo Sh1milioni ikikosa kiambatanisho fulani ni kawaida wakaguzi wanahoji fungu zima la Sh 500milioni.

Amesema kwa hiyo unaposoma mtaani unaona sh 500 zimeibwa lakini kumbe pale ni Sh milioni moja ndio hazina risiti.

Amesema kamati hizo zitaanza mapema kuchambua ripoti hizo ili waangalie ratiba yao na kuwaelimisha watu kuhusiana na ripoti ya CAG ambayo ni taarifa nzuri lakini baadhi ya watu wanabeba na kupotosha tu.

Mwananchi
Ulikuwa wapi wakati wa msiba mkuu ?! Poleni sana

Odhis *
 
Ndugai yuko sahihi.

Mbowe amechambuliwa huko ulaya taarifa ya CAG akameza anakuja kujiropokea hapa Bongo.

Kwa tunaojua mambo ya kihasibu hatushangai na hua hatukurupukii taarifa ya CAG maana mkaguzi asipoelewa kitu basi hukibeba kama kilivyo kwenye report yake.

Ndio maana cases nyingi ambazo hua CAG anataja, watuhumiwa wakiitwa kwenye kamati za Bunge hua majibu yanatolewa na baadae zinaonekana hazina msingi.

Sasa Mbowe ametafsiriwa report na wazungu huko anakuja kujiropokea tu hapa.
Hivi wafikiri Mbowe ni mbumbumbu? hajui,,ana mda gani katika hilo bunge mpaka ashindwe kujua ,,na kumwambia amejiropokea huko ulaya.Hivi wewe bado una kichwa mgando?Au una fikiri Jiwe atarudi kwahiyo atakuona wa maana kukanusha?,,ukweli utabaki kuwa ukweli,juu ya Ripoti hiyo,,kama kuna madudu yataonekana,,kama hayapo pia tutayaona.Wacha tusubiri akina Babu Tale na Mwanaafuei waichambue,,,wakisaidiwa na Msukuma.
 
Spika wa Bunge Job Ndugai, amezitaka kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zichambue ripoti ya CAG na kuiwakilisha bungeni katika mkutano wa nne, kwa kuwa inapotoshwa huku akimtaja Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kuwa mmoja wapo

Spika wa Bunge Job Ndugai amezitaka kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zichambue ripoti ya Mdhibiti na Mkuguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) na kuiwakilisha bungeni katika mkutano wa nne badala ya mkutano wa tano, kwa kuwa inapotoshwa.

Akizungumza leo Jumatatu Aprili 12 2021, Ndugai huku akimtaja Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amedai kuwepo upotoshaji wa ripoti hiyo.

Kauli ya Spika imekuja siku moja baada ya Mbowe kuhutubia kupitia mitandao ya jamii, ambapo pamoja na mambo mengine alilituhumu Bunge kwa vitendo vya rushwa.

“Watu wanabeba tu mabilioni yameibiwa sasa huyo rafiki yangu Freeman Mbowe alikuwa Ulaya huko sasa katumwa na watu wake huko anapotosha mambo,” amesema.

Amesema sio watu wengi wenye uelewa wa kuchambua taarifa za kihasibu na hivyo kunaweza kukawa na ujenzi wa kituo cha afya wa Sh 500milioni lakini Sh 499milioni zimetumika vizuri kabisa.

Hata hivyo, amesema lakini kati ya fedha hizo Sh1milioni ikikosa kiambatanisho fulani ni kawaida wakaguzi wanahoji fungu zima la Sh 500milioni.

Amesema kwa hiyo unaposoma mtaani unaona sh 500 zimeibwa lakini kumbe pale ni Sh milioni moja ndio hazina risiti.

Amesema kamati hizo zitaanza mapema kuchambua ripoti hizo ili waangalie ratiba yao na kuwaelimisha watu kuhusiana na ripoti ya CAG ambayo ni taarifa nzuri lakini baadhi ya watu wanabeba na kupotosha tu.

Mwananchi
Mm nafikiri kuna tatizo hapa, aliyewakilisha ripoti ya wizi ni Mbowe au CAG? Kama ripoti ni ya uongo au tafsiri yake ina lengo la kuichafua serkali huyu si ndiye mwajiriwa wa serkali hiyo hiyo anayoitolea taarifa za wizi? Sasa hapa Mbowe anahusikaje? Namalizia kusema haya kwa hili analotueleza spika tunatakiwa tuwe na taaluma ya kihasibu kujua taarifa imepotoshwa.Si aitwe CAG awaeleze alikuwa na maana gani kuzungumzia upotevu na hasara nyingi za fedha alizozibainisha mle?Watanzania mbona tunageuzwa mazuzu na hawa wanaodhulumu kodi zetu kwa mabavu kupitia kwenye uchaguzi za kibabe?Mungu atoe uelekeo wa busara kwa Rais wetu.Mama nina imani naye anayo mwezi wa kuchambua wapiga dili hawa wanaopindisha pindisha sentensi ili tuendelee kupigwa.
 
Sasa amejuaje kama inapotoshwa wakati yeye hajaisoma, hajui chochote na hao wabunge wanaounda LAAC na PAC hawajaichambua?

Ndugai ni Speaker wa HOVYO sana kuwahi kutokea katika historia ya Bunge letu tukufu. Ameiharibu sana taswira ya Bunge na sasa kila zuzu yeyote anatamani kuingia kule
Mzee Ndungai pengine hutumia msuba kabla ya kuingia Bungeni
 
Nimesikiliza na kutazama hotuba yote ya @freemanmbowetz sikusikia sehemu yoyote akichambua taarifa ya CAG. Job Ndugai amedata? Kwanini amechanganyikiwa hivi? Anasema Mbowe alichambua taarifa ya CAG baada ya kutumwa na watu wake wa ulaya. Ndugai kachanganya Mbowe na Zitto? Nisaidienui mlio sikiliza Hotuba ya Mbowe.

Face with tears of joy
Ndungai hupiga msuba kabla ya kuingia Bungeni
 
Spika wa Bunge Job Ndugai, amezitaka kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zichambue ripoti ya CAG na kuiwakilisha bungeni katika mkutano wa nne, kwa kuwa inapotoshwa huku akimtaja Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe kuwa mmoja wapo

Spika wa Bunge Job Ndugai amezitaka kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) zichambue ripoti ya Mdhibiti na Mkuguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) na kuiwakilisha bungeni katika mkutano wa nne badala ya mkutano wa tano, kwa kuwa inapotoshwa.

Akizungumza leo Jumatatu Aprili 12 2021, Ndugai huku akimtaja Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amedai kuwepo upotoshaji wa ripoti hiyo.

Kauli ya Spika imekuja siku moja baada ya Mbowe kuhutubia kupitia mitandao ya jamii, ambapo pamoja na mambo mengine alilituhumu Bunge kwa vitendo vya rushwa.

“Watu wanabeba tu mabilioni yameibiwa sasa huyo rafiki yangu Freeman Mbowe alikuwa Ulaya huko sasa katumwa na watu wake huko anapotosha mambo,” amesema.

Amesema sio watu wengi wenye uelewa wa kuchambua taarifa za kihasibu na hivyo kunaweza kukawa na ujenzi wa kituo cha afya wa Sh 500milioni lakini Sh 499milioni zimetumika vizuri kabisa.

Hata hivyo, amesema lakini kati ya fedha hizo Sh1milioni ikikosa kiambatanisho fulani ni kawaida wakaguzi wanahoji fungu zima la Sh 500milioni.

Amesema kwa hiyo unaposoma mtaani unaona sh 500 zimeibwa lakini kumbe pale ni Sh milioni moja ndio hazina risiti.

Amesema kamati hizo zitaanza mapema kuchambua ripoti hizo ili waangalie ratiba yao na kuwaelimisha watu kuhusiana na ripoti ya CAG ambayo ni taarifa nzuri lakini baadhi ya watu wanabeba na kupotosha tu.

Mwananchi
Je! Katika kipindi cha miaka mitano 2016 hadi 2020 bunge liliweza kuchambua na kujadili kwa kina taarifa za CAG? Je! Bunge liliweza kuisimamia serikali au lilikuwa linaiunga mkono? Je! Kunapokuwa matumizi ya fedha nje ya bajeti maana yake ni nini? Tuangalie tulipojikwaa na kuanguka ili kesho tusirudie tena. Tanzania ni ya Watanzania wote ambao ni wazawa. Hakuna mzawa anaeitakia nchi mabaya. Yeyote anaesema mwenzake ni kibaraka wa mabeberu anastahili kuangaliwa kwa jicho la tahadhari. Tena ni wa kuogopwa kama ukoma.
 
Back
Top Bottom