Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Spika wa Bunge la Tanzania amesema Polisi wanakamata Watu hovyo wengine wenye heshima zao na wanajulikana wanakoishi lakini wanarundikwa tu Rumande bila ulazima wowote.
Ndugai amesema "inatakiwa tujifunze kwa Nchi za wengine ambapo Mtu huwa anaitwa kituoni na kufanyiwa mahojiano kisha kuruhusiwa kurudi nyumbani kwasababu anafahamika na hawezi kukimbia. Huku ukishakuwa Askari tunaona kuweka Watu ndani ni raha".
Ameongeza "Hiki kitu binafsi kinaniuma sana. Mtu anawekwa ndani wiki nzima au mwezi halafu baadae anakuja anaachiwa wakati shughuli zake nyingi zimeshasimama. Sheria nazo hata ukitoka huwezi kudai chochote, Waafrika hatuthaminiani".
Ndugai amesema "inatakiwa tujifunze kwa Nchi za wengine ambapo Mtu huwa anaitwa kituoni na kufanyiwa mahojiano kisha kuruhusiwa kurudi nyumbani kwasababu anafahamika na hawezi kukimbia. Huku ukishakuwa Askari tunaona kuweka Watu ndani ni raha".
Ameongeza "Hiki kitu binafsi kinaniuma sana. Mtu anawekwa ndani wiki nzima au mwezi halafu baadae anakuja anaachiwa wakati shughuli zake nyingi zimeshasimama. Sheria nazo hata ukitoka huwezi kudai chochote, Waafrika hatuthaminiani".