mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,050
- 4,904
Spika wa Bunge Job Ndugai amesema anakerwa na kada nne ambazo zinatukuza usomi wao mbele ya Watanzania wasiopenda kujikweza.
Amezitaja kada hizo ni wahasibu, wahandisi, mawakili na madaktari wa kusomea ambao amesema kila mtu anataka kuanza na kutukuza kisomo chake wakati si lazima iwe hivyo.
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo, Jumatano, Septemba 1, 2021 bungeni katika kipindi cha mjadala wa hoja za wabunge kuhusu muswada wa mabadiliko ya sheria mbalimbali uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Profesa Adelardus Kilangi.
Amesema anajua atashambuliwa na mawakili mitandaoni lakini anataka kujua iwapo hawaoni aibu kujiita ni wasomi wakati nchi ina wasomi wengine.
“Najua watanishambulia katika mitandao, ..ah lakini huo ndiyo ukweli nani asiyekuwa msomi katika nchi hii, au wengine hawajasoma, kwani hamuoni aibu fulani hivi kujiita wasomi wakati kuna wengine katika nchi hii wamesoma,” amehoji Ndugai.
Spika amesema; “kuna wakati nitahitaji mnishauri kuhusu hili la wanasheria kujiita wakili msomi, huu ni utaratibu fulani ulioanzishwa na wenzetu Waingereza wa kutukuza baadhi ya kada,’’
Ndugai amezitaja kada nne zinazompa shida na anawashangaa kuona wakitukuzwa kuliko wengine licha ya wengi kuwa ni wasomi.
Kada hizo ni wahasibu, wahandisi, mawakili na madaktari wa kusomea ambao amesema kila mtu anataka kuanza na kutukuza kisomo chake wakati siyo lazima iwe hivyo.
Kuhusu mawakili amehoji kama wakibaki na neno la wakili watapungukiwa kitu gani huku akiweka wazi kuwa neno msomi linawaongezea kitu gani kwa Watanzania wasiopenda kujikweza katika mambo mengine.
Kwa kada alizozitaja Spika, mawakili hujiita wakili msomi, wahasibu hupenda kuanza na neno CPA, wahandisi hutumia neno la ‘Engineer’ na waliosoma shahada za uzamivu (PhD) majina yao huanza na neno Dk
Amezitaja kada hizo ni wahasibu, wahandisi, mawakili na madaktari wa kusomea ambao amesema kila mtu anataka kuanza na kutukuza kisomo chake wakati si lazima iwe hivyo.
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo leo, Jumatano, Septemba 1, 2021 bungeni katika kipindi cha mjadala wa hoja za wabunge kuhusu muswada wa mabadiliko ya sheria mbalimbali uliowasilishwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali Profesa Adelardus Kilangi.
Amesema anajua atashambuliwa na mawakili mitandaoni lakini anataka kujua iwapo hawaoni aibu kujiita ni wasomi wakati nchi ina wasomi wengine.
“Najua watanishambulia katika mitandao, ..ah lakini huo ndiyo ukweli nani asiyekuwa msomi katika nchi hii, au wengine hawajasoma, kwani hamuoni aibu fulani hivi kujiita wasomi wakati kuna wengine katika nchi hii wamesoma,” amehoji Ndugai.
Spika amesema; “kuna wakati nitahitaji mnishauri kuhusu hili la wanasheria kujiita wakili msomi, huu ni utaratibu fulani ulioanzishwa na wenzetu Waingereza wa kutukuza baadhi ya kada,’’
Ndugai amezitaja kada nne zinazompa shida na anawashangaa kuona wakitukuzwa kuliko wengine licha ya wengi kuwa ni wasomi.
Kada hizo ni wahasibu, wahandisi, mawakili na madaktari wa kusomea ambao amesema kila mtu anataka kuanza na kutukuza kisomo chake wakati siyo lazima iwe hivyo.
Kuhusu mawakili amehoji kama wakibaki na neno la wakili watapungukiwa kitu gani huku akiweka wazi kuwa neno msomi linawaongezea kitu gani kwa Watanzania wasiopenda kujikweza katika mambo mengine.
Kwa kada alizozitaja Spika, mawakili hujiita wakili msomi, wahasibu hupenda kuanza na neno CPA, wahandisi hutumia neno la ‘Engineer’ na waliosoma shahada za uzamivu (PhD) majina yao huanza na neno Dk