Spika Ndugai awaapisha Humphrey Polepole na Riziki Lulida. Asema Bunge linawatambua Wabunge 19 wa Viti Maalum waliofutiwa uanachama CHADEMA

At Calvary

JF-Expert Member
Aug 22, 2018
4,513
3,552
Spika wa Bunge Job Ndugai leo November 30,2020 atawaapisha Wabunge wawili walioteuliwa na Rais Magufuli, Wabunge hao ni Humphrey Polepole ambaye ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM na Riziki Said aliyekuwa Mbunge Viti Maalum katika Bunge la 11 kupitia CUF.

Shughuli za uapisho zitafanyika katika Viwanja vya Bunge Jiji Dodoma saa 10:00 Jioni.

Ndugai.jpg

Spika Ndugai: Wako rafiki zetu ambao hivi karibuni wamejipambanua kwa kukejeli shughuli za bunge, niwatahadharishe na kuwakumbusha labda wamesahau kwamba ni jambo lisilokubaika kwa mtu yeyote kudharau shughuli za Bunge, kudhalilisha Bunge, kudhalilisha uongozi wa Bunge na hata kudhalilisha wabunge waliokwisha kuapishwa.

Kufikiri kwamba Bunge ni ukumbi wa Bunge peke yake ni fikra finyu sana. Kwa hiyo wabunge wote wa Bunge la 12 tuliowaapisha tunaendelea kuwatambua ni wabunge kamili ikiwa ni pamoja ni pamoja na wale 20 wa chama cha CHADEMA, kumi na tisa na yule mmoja aliechaguliwa ambae ni mheshimiwa Aida Khenan. Nashangaa wanawasonga hawa 19, yule mmoja wamemgwaya? Wakiweza wamfukuze basi lakini sisi tumeshamuapisha na tunamtambua kwamba ni mbunge wa Bunge la 12, hayo yanayoendelea huko yakwao.

Hebu waacheni wastaafu wetu wapumzike, tuwaache wapumzike wazee wetu wamefanya kazi nzuri iliyotukuka, mambo huku nyuma yao yanabadilika kwa hiyo mnapowafata wakati wao wana kumbukumbu zile za wakati ule na huku kuna mambo mapya yanaendelea mnataka kuwachonganisha wazee hawa na wananchi wa Tanzania na si haki.

Si vizuri baadhi ya vyombo vya habari mnaofanya namna hii, waacheni wazee wapumzike.

Kwa hiyo wale waliokuwa na wasiwasi wale wabunge 19, niwahakikishie wale ni wabunge kamili wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania na niwakumbushe wanahabari, kila mnapowatamka majina yao muanze na neno mheshimiwa.

Yupo rafiki yangu mmoja nimtaje tu jina, mheshimiwa Freeman Mbowe tulianza nae ubunge mwaka 2010, tunafahamiana vizuri japo alipigwa chini hapo katikati, mimi nimeendelea moja kwa moja. Mwenzangu alipigwa chini, mzoefu wa kuanguka kwenye chaguzi hizi wala sio mara ya kwanza.

Amesimama akaanza kuwatukana hadharani waheshimiwa wabunge hawa wanawake, kwa mtu mzima na mwanaume wa kitanzania uliyefundwa ni aibu kubwa kutukana wanawake hadharani, ningependa kuchukua nafasi kumuonya na kumkanya hadharani asione sifa katika jambo hilo.
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mbunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida.
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mBunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida
Polepole ni akili kubwa, huna mamlaka ya kuhoji uwezo wake. Ni wapi Katiba imetamka kwamba Mbunge wa kuteuliwa na Rais ni hadi pale Wabunge waliopo Bungeni watakosa sifa anazozitaka Rais?
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mBunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida
Ulitaka akuteue wewe?
 
Mi ningekuwa ndio Ndugai, hawa ningewaapishia kwenye Car Wash kabisa ili ma-CCM wenzangu yaseme "...Si mnaona tuliwaambia hakuna kifungu kilichovunjwa pale... eti Mbowe alikuwa anahoji akina Mdee kuapishwa garage, si mnaona akina Polepole hao wameapishiwa kwenye carwash!

Amini usiamini... kuwa mwana-CCM raha sana! Yaani huumizi kichwa!!!
 
Jamaa wana justify kwamba hata ile shughuli ya kina Mdee ilikuwa sawa!! kazi kweli kweli.

Spika anaweza kuwaapishwa wabunge hata kwenye uwanja wa nyumbani kwake kama ataona inafaa.
Mkuu ,
Tutazame kwa macho yote,
Je SIWA halitakuwepo Kama siku ile?
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mBunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida
Nimeamini kuwa wivu ni jambo baya sana. Halafu kuwa na adabu mpumbavu wewe, jaribu kuheshimu wakubwa wako, jinga kabisa.
 
Spika wa Bunge Job Ndugai leo November 30,2020 atawaapisha Wabunge wawili walioteuliwa na Rais Magufuli, Wabunge hao ni Humphrey Polepole ambaye ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM na Riziki Said aliyekuwa Mbunge Viti Maalum katika Bunge la 11 kupitia CUF.

Shughuli za uapisho zitafanyika katika Viwanja vya Bunge Jiji Dodoma saa 10:00 Jioni.
 
Nafasi kumi alizopewa Rais na Katiba ya JMT ni kama katika wabunge waliopo hakuna mtu ana sifa anazotaka lakini sio mBunge ndio anateua sasa huyu wetu anateua watu wa ovyoovyo ili kujaza makasuku kule mjengoni shida
Kuandika tu shida unaweza kuwa na constructive argument kweli wewe?
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom